Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 11/15 uku. 24
  • Daktari Anayethamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Daktari Anayethamini
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
    Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
  • Maswali ya Funzo la Kijitabu Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Damu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Heshima ya Kimungu kwa Uhai na Damu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 11/15 uku. 24

Daktari Anayethamini

TULIPOMTEMBELEA Dakt. M, tulimweleza kwamba sisi tu Mashahidi wa Yehova na kwamba tulikuwa na kitu tulichotaka kumpa. Alikuwa mwenye furaha akatukaribisha ndani mara moja, wakati wote huo alikuwa akituchekesha, akisema: “Lazima mlipe dola 15.00 mwingiapo ndani!” Tulimtolea kijitabu Blood tukamweleza kwamba tulikuwa tunatoa nakala moja kwa kila daktari, daktari wa kike na wakili ili wafahamiane zaidi na maoni ya Mashahidi na sababu hatukubali damu.

Daktari huyo alisema kwamba, ingawa alitumikia katika kikosi cha M.A.S.H. katika Korea na alikuwa ametia watu wengi damu mishipani, yeye aliamini kwamba kila mtu anapaswa kufanya uamuzi wake mwenyewe juu ya litakalofanywa na mwili wake. Vilevile alikubaliana na jambo la kumtibu “mwanadamu mzima,” kwa kuwa kutia mtu damu mishipani kwa nguvu kunaweza kutokeza matatizo (magumu) ya akili.

Baada ya kuzungumza naye Yohana 17:3, nilimtolea uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, nilieleza kwamba zitamsaidia ajue Biblia zaidi na namna Mungu atakavyoondolea wanadamu matatizo haya. Alikubali kuandikisha magazeti yote mawili, akisema: “naona kwamba haya yataniletea faida kubwa.”

Alieleza sababu ya kuwapenda Mashahidi wa Yehova. Wakati mmoja alivunjikiwa na gari lake akiwa katika barabara moja kuu ya Pennsylvania nayo motokaa nyingine ikaja kumsaidia. Watu hao, si kwamba tu walimsaidia kupeleka gari lake kwenye kituo cha mafuta, bali vilevile walikaa pale pale pamoja naye mpaka gari lake likatengezwa wakawa na hakika kwamba angeweza kuendelea na safari yake. Kabla ya kuondoka, walimwachia nakala za magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Hivyo akajua kwamba walikuwa Mashahidi wa Yehova. Alitaja mara kadha namna walivyomwonyesha fadhili nyingi wakijitaabisha ili wamsaidie.​—Imetolewa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki