Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 2/15 kur. 9-13
  • Ufufuo wa Uzima na Mwingine wa Hukumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufufuo wa Uzima na Mwingine wa Hukumu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “MKUTANO MKUBWA” NA UFUFUO
  • Siku ya Hukumu na Baada ya Hapo
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ule Ufalme na lile Tumaini la Ufufuo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Siku ya Hukumu Ni Nini?
    Amkeni!—2010
  • Hukumu Inayosawazisha Haki na Rehema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 2/15 kur. 9-13

Ufufuo wa Uzima na Mwingine wa Hukumu

1, 2. Sababu gani tangazo la Yesu la kwamba amepewa mamlaka ya kuhukumu si la ajabu sana lisiweze kuaminika?

KATIKA siku ‘iliyowekwa’ na Mungu, Mwanawe atatumia “zawadi ya uzima,” (Yohana 5:26, ZSB) Atawafufua wanadamu wafu ambao kwao dhabihu yake ya ukombozi inatumika. “Siku” hiyo itakuwa wakati wa hukumu, walakini haitakuwa ya saa 24. Kitakuwa kipindi cha miaka 1,000 iliyowekwa ya utawala wa Kristo. (Ufu. 20:4-6) Hukumu hiyo itamaanisha uzima kwa wengine na wengine watahukumiwa uharibifu. Je! hilo linasikika kuwa jambo lenye kustaajabisha kwetu leo wakati huu ambao hukumu zisizo za haki hutolewa kwa wingi sana nao wafuasi wengi sana wa dini huwa hawafahamu kabisa namna siku ya Mungu ya hukumu itakavyokuwa? Lilisikika kuwa jambo la kustaajabisha kwa Wayahudi wa siku za Yesu wenye kushika Sabato.

2 Kwa hiyo Yesu aliwaambia hivi: “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini watasikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu. Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo [kutoka kwa Baba Hakimu aliye Mkuu Zaidi] ndivyo nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.”​—Yohana 5:28-30.

3. Wale wanaotoka mautini kuingia uzimani ambao hawapatwi na hukumu yenye laana wanatofautianaje na wale ambao Yesu alisema juu yao katika Yohana 5:​28, 29, nao lazima wawe jamii ya watu gani?

3 Kabla ya Yesu kusema maneno hayo yaliyotajwa hapo juu, alisema, katika Yohana 5:24, 25, juu ya “wafu” wengine ambao “saa” yao ya kuwa hai ilikuwa imekwisha aanza. Hao waliotajwa walisemekana kuwa “wafu” hata hivyo hawakuwa “makaburini.” Walikuwa hata wakati huo wakisikia “neno” lililonenwa na Mwana wa Mungu nao walikuwa wakimwamini Yeye aliyemtuma. Kwa njia hiyo walikuwa wakitoka mautini na kuingia uzimani na kwa hiyo hawangepatwa na hukumu mbaya. Kwa sababu walikuwa wametoka mautini na kuingia uzimani, hao walioitii sauti ya Mwana wa Mungu walisemekana kuwa walikuwa wakiishi na kuwa na taraja la uzima wa milele. Lazima hawa wawe wale waliokuja kuwa warithi washirika wa kimbinguni pamoja na Yesu Kristo, yaani, wale 144,000 wanaopewa ufufuo katika makao ya kiroho wakawe pamoja naye katika Ufalme.

4. Mahali pa kuhukumiwa; warithi washirika wa Kristo 144,000 wanapewa mgawo gani?

4 Hawa warithi washirika wa Yesu Kristo 144,000, mahali pa kuhukumiwa, watakalia pamoja naye viti vya enzi vya hukumu. Ufunuo 20:4 husema “nao wakapewa [uwezo wa] hukumu.” Ufufuo wao unaitwa “ufufuo wa kwanza.” Kwa huo wanafufuliwa mara moja kwenye makao ya kimbinguni.​—Ufu. 20:6.

5. Kipindi cha hukumu ya kundi la Waisraeli wa kiroho kilianza wakati gani, naye Yesu alisema wangekuwa na pendeleo gani katika ufalme wake?

5 Kabla ya hapo kulikuwako kipindi cha hukumu kwa hao 144,000 walipokuwa duniani. Hii ilianza wakati kundi la Kikristo la Israeli wa kiroho lilipozaliwa katika siku ya Pentekoste ya mwaka 33 W.K. Kipindi hicho cha hukumu kinaendelea mpaka kumalizika kwa kundi hili la wana wa kiroho wa Mungu. (1 Pet. 4:14, 18) Kwa habari ya wakati wao ujao wenye utukufu, Yesu aliwaambia mitume wake waaminifu katika usiku wa Sikukuu ya Pentekoste ya mwaka 33 W.K. hivi: “Mimi naweka agano pamoja nanyi, kama vile Baba yangu ameweka agano pamoja nami, la ufalme, ili mpate kula na kunywa katika meza yangu katika ufalme, na kukalia viti vya enzi kuhukumu yale makabila kumi na mawili ya Israeli.” (Luka 22:​29, 30, NW) Kwa hiyo, mahali pa kuhukumiwa wakati wa utawala wa miaka elfu wa Kristo, wanashiriki pamoja naye kuhukumu wanadamu waliokombolewa.

6. Ili wanadamu wote kwa jumla wapate kuwa na wakati wa hukumu, kunahitajiwa kuwe na nini, nayo Hadeze itaharibiwaje?

6 Ili wanadamu waliokombolewa kwa jumla wawe na wakati wa kuhukumiwa hapa duniani kunahitajiwa kuwe na ufufuo wa “watu wote waliomo makaburini.” Katika kuthibitisha hilo, Yesu alisema, katika Yohana 5:28-30, kwamba “saa” ingekuja ambayo katika hiyo watu wote hawa wangesikia sauti yake na kuitika. Angewaita watoke makaburini yao, katika njia ile ile aliyomwita rafiki yake aliyekuwa kaburini katika Bethania: “Lazaro, njoo huku nje”! (Yohana 11:​43, 44) “Saa” hiyo ingekuja wakati wa utawala wa miaka 1,000 wa Yesu Kristo pamoja na wale 144,000 warithi washirika waliotukuzwa. (Ufu. 20:6, 11-14) Wakati wa utawala huo hadeze, au kaburi la kawaida la wanadamu, litaharibiwa kwa kuondolewa wanadamu wote waliokombolewa waliomo. Hiyo inamaanisha ufufuo!

7. Ni vikundi gani viwili vinavyotokea wakati huo na je! vinatokea mwanzoni mwa kipindi cha ufufuo?

7 Yesu alisema kwamba wakati huo vikundi viwili vingeonekana. Walakini, hii haitakuwa mwanzoni mwa kipindi hicho cha ufufuo, kwa kuwa wafu wote waliokombolewa hawatatoka makaburini wakati ule ule. Yesu alisema (1) juu ya “wale waliofanya mema” na (2) “wale waliotenda mabaya.” Hii haimaanishi namna watu mmoja mmoja waliofufuliwa watakavyokuwa mara tu baada ya kufufuliwa kutoka makaburini. Sababu gani tunasema hivyo?

8. (a) Kwa sababu “Mwana-kondoo wa Mungu” alikufa ili aichukue dhambi ya ulimwengu, wafufuliwapo kutoka katika wafu hawatapatwa na nini? (b) Hata hivyo, maisha yao ya mbele yatawahusuje, na kwa sababu gani?

8 Jambo la kuamulia namna wanadamu waliofufuliwa watakavyokuwa si namna walivyokuwa kabla ya kufa kwao. Ndivyo ilivyo, kwa sababu kifo chao kililipia dhambi zao. (Rum. 6:23) Vilevile, Yesu Kristo alikufa awe “Mwana-kondoo wa Mungu” ili ‘aichukue dhambi ya ulimwengu.’ (Yohana 1:29; 1 Yohana 2:2) Kwa hiyo wanadamu waliofufuliwa hawawezi kushtakiwa juu ya yale ‘aliyoyachukua.’ Kuhusu hilo, mtume Paulo aliandika: “Tusitumikie dhambi tena; kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.” (Rum. 6:​6, 7) Hivyo, kwa kufufuliwa. hakuna mwanadamu ye yote aliyekombolewa anayeingia katika ‘hatari maradufu,’ ya kuadhibiwa tena kwa sababu ya yale aliyoyatenda kabla ya kufa kwake. Kwa hiyo, jambo la kuamulia kwa wanadamu waliofufuliwa litakuwa, Watafanya nini tangu hapo na maisha zao, kwa kuwa sasa wamepewa mwanzo mpya chini ya ufalme wa Kristo wa miaka 1,000? Bila shaka, wakati wanapolala katika mauti utu wao haubadiliki. Kwa hiyo, yale waliyofanya au namna walivyoishi wakati wa taratibu hii mbovu ya mambo iliyopo yatakuwa na matokeo juu ya maelekeo yao au nia kuelekea ufalme wa Kristo.

9. Hao wanaopaswa hivyo na matokeo ya maisha yao ya mbeleni watakuwa na uwezekano wa kupatwa na matokeo gani mawili?

9 Ndiyo, namna ya maisha ya mbeleni waliyokuwa nayo itahusu matatizo (magumu) ya wale waliofufuliwa kwa habari ya kujipatanisha kwao na matakwa ya Ufalme juu ya haki na maendeleo yao ya kufikia uzima mkamilifu wa kibinadamu duniani. Wakati huo kutakuwa na uwezekano wa matokeo ya namna mbili. Kama alivyoonyesha Yesu katika Yohana 5:28, 29, watageukia ama mwendo wa kufanya mema au wageukie mwendo wa kutenda mabaya. Kukiwa na matokeo gani ya namna mbili?

10. Katika usemi “ufufuo wa uzima,” “uzima” unamaanisha nini?

10 Yesu alielekeza kwenye matokeo hayo aliposema juu ya “ufufuo wa uzima” na “ufufuo wa hukumu.” Kwa neno “uzima” katika habari hii, Yesu hakumaanisha uzima wa kadiri unaopatikana na wafu mmoja mmoja mara tu baada ya kutoka makaburini. Kama sivyo, si wafanya mema peke yao wangepata “ufufuo wa uzima,” bali vilevile watenda mabaya wangepata ufufuo wa namna hiyo, kwa sababu wao pia wangeanzia kwa kufanywa hai duniani. Kwa hiyo, “uzima” kama unavyotumiwa katika Yohana 5:29 unamaanisha uzima mkamilifu unaofikiwa na wengine mwishoni mwa utawala wa Kristo kwa sababu wameendelea kufanya mema katika kuutii ufalme na uhakimu wake.

11. Katika usemi “ufufuo wa hukumu,” “hukumu” inamaanisha nini?

11 Vivyo hivyo, “hukumu” inamaanisha matokeo kwa watu wengine mmoja mmoja ama wakati wa au mwishoni mwa “siku ya hukumu.” Katika Yohana 5:29 “hukumu” inakuwa kinyume cha “uzima.” Kwa hiyo inamaanisha hukumu yenye laana, kuwahukumia watenda mabaya uharibifu wa milele. Huu ni uharibifu wa nafsi na mwili katika Jehanum.​—Mt. 10:28.

12. Basi, ni matokeo gani mawili ya ufufuo chini ya ufalme wa Kristo, yanayowezekana kuwako baada ya mtu kufufuliwa?

12 Kwa hiyo kuna matokeo mawili ya ufufuo chini ya ufalme wa Kristo yatakayowezekana. Ama kupata uzima mkamilifu wa kibinadamu ama kupata hukumu ya kupoteza uzima wote. Kwa kufaa sana An American Translation inatafsiri Yohana 5:29 isomwe hivi: “watatoka [waingie] katika ufufuo na uzima, na . . . katika ufufuo wa hukumu.”

13, 14. (a) Yesu pamoja na mahakimu wake washirika wanasikia nini kabla ya kutoa hukumu? (b) Sababu gani hakuna uwezekano wa kuomba rufani kutokana na hukumu hiyo ya Kristo wakati huo wa miaka elfu?

13 Wakati wa hiyo miaka elfu wanadamu wote watahukumiwa kwa haki na Yesu Kristo pamoja na mahakimu wake washirika. Yesu alisema hivi: “Nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo.”​—Yohana 5:30.

14 Ayasikiayo Yesu kutoka kwa Hakimu Aliye Mkuu Zaidi, Yehova Mungu, anayatumia katika kutoa hukumu yake. Yeye atajipatanisha na yale maelezo ya kiunabii yanayomhusu akiwa hakimu ambayo Baba yake wa mbinguni alimwongoza Isaya aandike katika sura ya 11, mstari wa kwanza mpaka wa tano. Wakihukumu pamoja naye, mahakimu washirika 144,000 watamwiga Yesu Kristo. Katika njia hiyo hukumu ya Yehova ndivyo itakayokuwa ikitolewa, kwa kuwa Mwanawe Yesu Kristo atatafuta kufanya mapenzi ya Baba yake sikuzote, wala si mapenzi yake mwenyewe. Kwa hiyo, hakuna kuomba rufani katika mahakma kuu kutokana na hukumu hiyo iliyotolewa na Yesu Kristo. Hivyo, mwishoni mwa uhakimu wake wa miaka 1,000, ataweza kuutoa Ufalme kwa Hakimu Aliye Mkuu Zaidi, bila kuwa na hatia yo yote ya kutumia vibaya cheo chake. (1 Kor. 15:24-28) Kuanzia hapo Yehova Mungu atashughulika (atatenda) kwa habari ya jaribu la mwisho, lenye kuamua juu ya wanadamu wote aliokabidhiwa na Mwanawe.​—Ufu. 20:7-15.

“MKUTANO MKUBWA” NA UFUFUO

15. Katika kumwagiza Timotheo kwa Kristo Yesu atakayewahukumu walio hai na waliokufa, Paulo alikuwa akimaanisha “waliokufa” gani?

15 Siku ya hukumu inayokaribia ni jambo la kufikiriwa na wanadamu wote. (Matendo 17:30, 31) Akikubali hili, mtume Paulo alimwandikia Timotheo ambaye wakati mmoja alikuwa mmsionari mwenzake hivi: “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa. (1 Tim. 4:1) Kwa usemi “waliokufa,” Paulo anawataja “waliomo makaburini” na waliomo ‘makaburini yenye maji.’ Walakini ni nani wanaoitwa na Paulo “walio hai”?

16. Sana sana “walio hai” ni nani?

16 Wao watakuwa wale walioko duniani wakaoiokoka ile “dhiki kubwa” inayokuja na kufungiwa kwa Shetani Ibilisi na mashetani zake. Kwa hiyo watakuwa wangali hai duniani wakati utawala wa Kristo wa miaka 1,000 juu ya dunia uanzapo. Wale wanaokuwa raia zake wakati huo wakiwa na tumaini la uzima wa milele katika dunia ya paradiso ndio hasa wanaomaanishwa. Wengine wa mabaki wanaotazamia kuwa warithi washirika wa Kristo vilevile watakuwa wameokoka, walakini kama wataanza kuhukumu duniani kabla ya kuhamishwa na kuingizwa katika ufalme wa mbinguni tutangojea tuone. (1 The. 4:15-17; 2 Pet. 3:11-14) Walakini, “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo wataiokoka “dhiki kubwa,” pamoja na mabaki ya Waisraeli wa kiroho, na kuingia katika kipindi hicho cha miaka elfu wakiwa hai. Ufunuo 7:9-17 huthibitisha ukweli huu.

17. Tunajuaje kama wakaaji wa dunia wataangamizwa wote mwishoni mwa taratibu hii ya mambo?

17 Haya yote yanahakikisha kwamba wakaaji wa dunia hii yetu hawaangamizwi wote wakati wa mwisho kamili wa taratibu hii ya mambo. Kwa hiyo “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo ndio watakaokuwa “walio hai” watakaokuwapo siku ya hukumu ya miaka elfu ianzapo.

18. Jambo la ajabu kuhusu huu “mkutano mkubwa” wa waokokaji wa “dhiki” litakuwa jambo gani, na kwa sababu gani?

18 Jambo la ajabu kabisa kuhusu huu “mkutano mkubwa” wa waokokaji wa “dhiki” ni kwamba wao hawafufuliwi hata kidogo. Kwa kuwa hawajapata kufa hata kidogo na miili yao ya kibinadamu kuangamia, hawatakuwa na uhitaji wa kuitwa na Mfalme Yesu Kristo kutoka makaburini. Kwa sababu ya yale waliyowatendea mabaki watiwa mafuta wa ndugu za kiroho za Kristo wakati uliopita, hawa wenye mfano wa kondoo wamewekwa katika mkono wa kuume wenye kibali wa Mfalme, naye anawaambia hivi mwanzoni mwa utawala wake wa miaka elfu: “Njoni, [ninyi] mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu.” Kwa hiyo wataingizwa katika njia itakayowaelekeza katika kuupata uzima mkamilifu wa kibinadamu katika dunia ya paradiso. (Mt. 25:​31-46; Yohana 10:16) Pendeleo lao litakuwa kubwa kuwapo wakati “Mwana wa Adamu” anayetawala, Yesu Kristo, aanzapo kuwaita waliomo makaburini watoke katika ufufuo utakaowapa nafasi ya kupata uzima wa milele duniani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki