Mithali Yenye Hekima
“Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako, wala usiende nyumbani mwa ndugu [yako] siku ya msiba wako, afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.”—Mit. 27:10.
Mithali hii ya Biblia inakazia maana ya kuwa na rafiki ya kweli, na vilevile kuwa vivyo hivyo, sana sana katika wakati wa shida. Kwanza inasema juu ya kuwa rafiki wa namna hiyo. Katika siku ya msiba, ‘usiwaache’ au kuwakimbia wale ambao wamekuwa rafiki zako, au rafiki za jamaa yako. Hupaswi kuwa rafiki ya Wakati mambo yanapokuwa mazuri tu, anayejificha anapohitajiwa kweli kweli. Ufikirie pia, upande mwingine. Unapopatwa na uhitaji, mahali pa kusafiri umbali mrefu uiendee nyumba ya ndugu yako wa kimwili uone kama atakusaidia, ni vizuri zaidi kuwa na rafiki aliye karibu, na aliye na nia ya kukusaidia. Kama isemavyo mithali nyingine: “Yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.”—Mit. 18:24.