Sababu Kwa Nini Matoleo ya Asali Hayakukubaliwa
Sheria ya Mungu kwa Israeli ilisema hivi: “Hamtateketeza chachu, wala asali iwayo yote, kuwa ni sadaka ya kusongezwa kwa [Yehova] kwa njia, ya moto” (Law. 2:11) Bila shaka namna ya asali inayotajwa hapa ni asali ya matunda, kwa kuwa asali ya namna hiyo, wala si asali ya nyuki, ingeweza kuitwa malimbuko. (Law. 2:12; 2 Nya. 31:5) Asali ya matunda ingeweza kuchachuka, na kwa hiyo, kwa kujaa ilikatazwa isitolewe kama sadaka madhabahuni.