Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 9/1 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Dhambi ya Asili Ilikuwa Nini?
    Amkeni!—1990
  • Dhambi ya Kwanza Ilikuwa Nini?
    Amkeni!—2006
  • Twaweza Kujifunza Kutokana na Wenzi Wawili wa Kwanza wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 9/1 kur. 23-24

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Mwanzo 3:22 wadokeza kwamba wengine mbinguni licha ya Yehova walikuwa na ujuzi wa pekee wa mema na mabaya. Je! ndivyo ilivyo?

Inaelekea kwamba, si Yehova peke yake, bali Mwanawe pekee pia alikuwa na ujuzi wa mema na mabaya katika maana inayoonyeshwa katika Mwanzo.

Baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi Yehova aliwahukumia. Kisha Mungu akasema: “Basi, huyu mtu ameliuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele.”​​—⁠Mwa. 3:22.

Wanadamu wawili wa kwanza hawakuwa kabisa bila ujuzi wa mema na mabaya. Mungu alikuwa amewambia kwamba lingekuwa kosa au vibaya kula matunda ya mti mmoja uliokatazwa; vivyo hivyo, kumtii Mungu lilikuwa jambo zuri. (Mwa. 2:16, 17) Kwa hiyo “ujuzi” hasa ulioonyeshwa na “mti wa ujuzi wa mema na mabaya” ulikuwa kujiamulia yaliyo mema na yaliyo mabaya. Kwa habari hii, Mtaalam T. J. Conant aliandika hivi: “Kwa kutojali mapenzi ya kimungu, na kwa kuamua na kutenda yake mwenyewe, mwanadamu alichagua kujijulia mwenyewe yaliyo mema na mabaya.” Ndiyo, Adamu na Hawa walikataa uamuzi wa Mungu wakaamua kujiwekea kanuni zao wenyewe za yaliyokuwa mema na yaliyokuwa mabaya.

Hata hivyo namna gani juu ya usemi wa Mungu, “mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya”?

Wengine wamefikiri kwamba hapa Mungu alikuwa akitumia wingi wa ukuu, kama vile mfalme mwanadamu anavyoweza kusema “Sisi hatukupendezwa” akijitaja yeye mwenyewe. Hata hivyo, kuna uwezekano mwingine unaoelekea kuungwa mkono zaidi na Maandiko.

Katika Mwanzo 1:26 Yehova alisema hivi: “Na tufanye mtu kwa mfano wetu.” Maandiko yanaelekeza kwenye uamuzi wa kwamba Mungu alikuwa akisema na Mwanawe pekee, ambaye baadaye alikuja duniani akawa Yesu. Huyu, yule Neno, alikuwa stadi wa kazi wa Mungu ambaye kupitia kwake vitu vingine vyote viliumbwa. (Yohana 1:1, 3; Kol. 1:15, 16; Mit. 8:22-31) Ulinganifu wa usemi wa Mwanzo 3:22 unaelekea kuonyesha kwamba Yehova alikuwa akisema kwa mara nyingine na yeye aliye msiri wake, Mwanawe pekee.

Ikiwa ndivyo ilivyo, ingeonyesha kwamba huyo Neno tayari alikuwa na “ujuzi wa mema na mabaya.” Kwa kushirikiana sana na Yehova kwa muda mrefu, bila shaka Mwana huyo alijifunza vizuri sana njia ya kufikiri pamoja na kanuni za Yehova. Kwa kuwa na hakika kabisa kwamba Mwanawe alikuwa amefahamiana na kushikamana kabisa nazo, inaweza kuwa kwamba Yehova alimpa ruhusa kadiri fulani pia ya kushughulika na mambo bila ya kumwuliza Baba kila wakati. Hivyo kwa kadiri hiyo, Mwana huyo angeweza na angekuwa na ruhusa ya kuamua yaliyokuwa mema na yaliyokuwa mabaya. Hata hivyo, hangekuwa akijiwekea kanuni ambayo ingepingana na ya Yehova.

Kwa habari ya Adamu na Hawa, kuja kwao kujua mema na mabaya kulihusu kuvunja amri ya Yehova na kukataa kanuni zake. Kwa kufanya hivyo walistahili kufa na walihukumiwa hivyo.

Katika tafsiri ya Kiingereza ya New World pamoja na tafsiri nyingine, Mwanzo 3:22 humalizikia kwa kistari hiki (​—⁠). Hiyo yaonyesha kwamba Mungu hakusema linalopaswa kufanywa. Mahali pake, maneno yake yanakoma nao mstari unaofuata unaeleza tendo lenyewe; akawafukuza Adamu na Hawa watoke katika bustani. Kwa hiyo kanuni yao ya kujitegemea ya mema na mabaya haikuwa kama ile ya Yehova na Mwanawe. Badala yake, iliwaongoza kwenye huzuni.​​—⁠Yer. 10:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki