Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Ni nani hao “watakatifu” ambao Yehova alisema nao kwa njozi katika Zaburi 89:19?
Uchunguzi wa Zaburi 89 unafunua kwamba habari inayozungumzwa, inahusu agano la Ufalme. Mistari ya 19, 20 na 29 ya zaburi hii yasomwa hivi: “Ndipo ulipowaambia watakatifu wako kwa njozi, Ukasema, nimempa aliye hodari msaada; nimemtukuza aliyechaguliwa miongoni mwa watu. Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, nimempaka mafuta yangu matakatifu. .. . . Wazao wake nao nitawadumisha milele, na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu.”
Masimulizi ya 1 Mambo ya Nyakati 17 yanafunua kwamba ahadi ya nasaba ya kifalme yenye kuendelea katika nyumba ya Daudi ilifunuliwa Nathani kwa njozi. Mambo ya Nyakati cha Kwanza 17:15 kinatuambia hivi: “Kwa maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.” Kwa hiyo, “watakatifu” hao ni Nathani na Daudi, Daudi akipokea ufunuo huo wa kimungu kupitia kwa Nathani.