Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 1/1 kur. 14-19
  • Kuishi Sasa Katika Hiyo “Siku ya Mwisho” ya Ufufuo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuishi Sasa Katika Hiyo “Siku ya Mwisho” ya Ufufuo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Habari Zinazolingana
  • “Waliokufa Katika Kristo Watafufuliwa Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • “Ufufuo wa Kwanza”—Unaendelea Sasa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • “Roho ya Uhai Itokayo kwa Mungu Ikawaingia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Tumaini la Ufufuo Lina Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 1/1 kur. 14-19

Kuishi Sasa Katika Hiyo “Siku ya Mwisho” ya Ufufuo

1. Kwa makumi ya miaka kabla, ilidhaniwa kwamba kutukuzwa kwa mabaki ya Wakristo waliosalia kungetukia wakati gani, lakini je! yale yaliyotabiriwa katika 1 Wathesalonike 4:16, 17 yalitimizwa tangu wakati huo na kuendelea?

KWA KUWA “waliokufa katika Kristo” wanafufuliwa wakiwa na miili ya kiroho isiyoonekana kwa macho ya kibinadamu wakati wa hiyo “siku ya mwisho,” sisi wanadamu twapaswa kuenenda kwa imani, si kwa kuona, kwa habari ya kwamba unatukia hakika wakati huu. Twakumbuka kwamba kwa makumi machache ya miaka hesabu fulani yao walidhani kwamba kutukuzwa kwa washiriki wote waliosalia wa kundi la Kikristo kungetukia mwishoni mwa Majira ya Mataifa yapata Oktoba 1, 1914. (Luka 21:24) Walakini, hakuna jambo lo lote kama inavyosimuliwa katika 1 Wathesalonike 4:16, 17 ambalo lilitukia wakati wa tarehe hiyo. Mahali pake, vita ilitokea mbinguni, nao wale walioshindwa Shetani na mashetani zake, walipata kutelemshwa mbiombio kuelekea duniani. (Ufu. 12:7-13) Kwa kupendeza, hesabu fulani ya Wakristo waliozaliwa kwa roho waliokuwa hai na waliokuwa wakitenda kazi duniani katika mwaka 1914 wangalipo pamoja nasi katika mwili. Kwa wazi kulikuwa na kosa juu ya kuweka wakati wa “siku ya mwisho” ya kutukuzwa kwa kundi lililozaliwa kwa roho.

2, 3. Kutukuzwa kulikuwa kutukie wakati wa kipindi gani, na kwa hiyo ni ulizo gani linalotokea kuhusiana na utimizo wa 1 Wakorintho 15:50-57?

2 Hata hivyo, ‘kuwapo,’ au parousia, kusikoonekana kwa Yesu Kristo aliyetukuzwa kulianza mwishoni mwa Majira ya Mataifa katika mwaka 1914. Kwa hiyo kuanzia wakati huo na kuendelea ndicho kipindi cha wakati, wakati ambapo yaliyotabiriwa katika 1 Wathesalonike 4:16, 17 yanapaswa kutukia kuhusiana na Wakristo waliozaliwa kwa roho waliosalia, ili yalingane na “siku ya mwisho.”​—Yohana 6:54.

3 Kwa kufaa basi utimizo wa 1 Wakorintho 15:50-57 unaanza wakati gani? “Nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika. Angalieni, . nawaambia ninyi siri; hatutalala sote [wakati mwili wa kibinadamu unaoharibika unapokufa], lakini sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi [Wakristo kama Paulo] tutabadilika. Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa. Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda. Ku wapi, Ewe mauti, uchungu wako? Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati [ya Musa]. Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.”

4. Yesu alikufa wakati gani, na Danieli 9:24-27 lilikuwa limeonyeshaje hili?

4 Kwa habari ya kuhesabu wakati kulingana na Maandiko, twaweza kulinganisha matukio yanayolingana au yanayofanana. Kwa hiyo twauliza, Yesu Kristo mwenyewe alifufuliwa wakati gani ili apate kuwa ‘Kristo malimbuko’? Hii ilikuwa Jumapili, Nisani 16, ya mwaka 33 W.K. Siku mbili kabla, wakati wa Sikukuu ya Kupitwa, Nisani 14, alikuwa amening’inia juu ya mti mpaka akafa. Siku hiyo ya dhabihu ya Kristo ilikuwa wakati uliowekwa katika orodha ya matukio iliyoandikwa na Yehova na kuwekwa katika maandishi katika Danieli 9:24-27. Ilionyesha katikati ya juma hilo la mwisho la mfuatano wa “majuma sabini,” majuma ya miaka, si ya siku. Unabii wa Danieli ulitabiri kwamba wakati wa juma la miaka la mwisho au la 70 “[M]asihi atakatiliwa mbali, naye atakuwa hana kitu.” Walakini ni wakati gani, wakati wa juma hili la mwisho la miaka, lililoanza katika vuli ya mwaka 29 W.K.? Danieli 9:27 linajibu hivi: “Na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu.” Hivyo dhabihu za wanyama hazikuwa na ubora wo wote baada ya Yesu kufa.

5. Kuanza kwa “juma” la 70 la miaka kunahesabiwaje, nako kulionyeshwaje, na kulianzisha kipindi gani kwa Yerusalemu na taratibu ya Kiyahudi?

5 Kwa kuwa Yesu alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kama dhabihu Nisani 14, 33 W.K., “juma” hilo lilianza miaka mitatu na nusu mapema katika Tishri 15, mwaka 29 W.K. Hivyo, basi, ni tukio gani lililoonyesha kuanza kwa “juma” hilo la 70 la miaka? Yesu alikuwa Masihi, maana yake “Mtiwa Mafuta.” Ulikuwa wakati Yesu alipobatizwa na Yohana Mbatizaji. Muda mfupi baadaye, apate kuwa Mfalme wa Kimasihi juu ya watu wa Yehova. Wakati huo Yesu alikuwa na umri wa miaka 30. (Luka 3:21-23; 4:1-21) Hakika tukio hili lilionyesha kuanza kwa “wakati wa mwisho” kwa Yerusalemu na taratibu ya Kiyahudi ya dhabihu. Baadaye miaka isiyozidi 41, au katika kiangazi cha mwaka 70 W.K., Yerusalemu na hekalu lake zilifanywa ukiwa. Kama vile Danieli 9:26 lilivyotabiri: “Na watu wa mkuu [Jemadari Tito] atakayekuja [katika mwaka 70 W.K.] watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika [ya majeshi ya Kirumi], na hata mwisho ule vita vitakuwapo.”

6, 7. Ni nini kilichofuata mara tu baada ya kumalizika kwa Majira ya Mataifa katika mwaka 1914, na ni tangazo gani lililofanywa mbinguni wakati huo ambalo lilitimia kuhusiana na dunia yetu na wafu wayo?

6 Kwa kulingana, wakati Majira ya Mataifa yalipomalizika katika vuli ya mwaka 1914, “wakati wa mwisho” wa taratibu hii ya mambo ulianza. (Dan. 12:4) Upesi baada ya kumalizika kwa hayo Majira ya Mataifa mtiwa mafuta Yesu mbinguni aliwekwa kuwa Mfalme, Mrithi wa milele wa babu wake wa zamani, Mfalme Daudi wa Yerusalemu. Huko na wakati huo tangazo lililofuata baada ya kupigwa kwa baragumu ya saba lilitimizwa. Kuhusu hili twasoma hivi, katika Ufunuo 11:15-18:

7 “Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu [Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova] na wa Kristo wake, naye [Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova] atamiliki hata milele na milele. . . . Tunakushukuru wewe, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa sababu umeutwaa uweza wako ulio mkuu, na kumiliki. Na mataifa walikasirika, hasira yako nayo ikaja, na wakati ukaja wa kuhukumiwa waliokufa, na wa kuwapa thawabu yao watumwa wako manabii na watakatifu, na hao walichao jina lako, wadogo kwa wakubwa, na wa kuwaharibu hao waiharibuo nchi.”

8. (a) Mataifa yalimkasirikia nani na kwa sababu gani, na kwa kadiri gani? (b) Jambo hili lililinganaje na yaliyompata mtiwa mafuta Yesu wakati wa “nusu ya juma”?

8 Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ya mwaka 1914-1918 W.K., “mataifa walikasirika,” na wakaelekeza hasira yao juu ya watu waliojiweka wakf wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Sababu gani? Kwa sababu hawa walikuwa wakihubiri kumalizika kwa Majira ya Mataifa katika mwaka 1914 na kusimamishwa kamili kwa ufalme wa Kristo mbinguni. Hasira hii ya mataifa ilifikia upeo wake katika masika ya mwaka 1918, kwa wazi zaidi katika United States ya Amerika. Hii ilikuwa miaka mitatu na nusu tangu kumalizika kwa Majira ya Mataifa na kuwekwa kwa mtiwa mafuta Yesu kuwa Mfalme wa kimbinguni. Yaliyowapata watangazaji wa Ufalme duniani katika mwaka 1918 yanafanana sana na yale yaliyompata Yesu huko Yerusalemu wakati wa “nusu ya juma.” Kwa habari yake ufufuo wa wafu ulikuwa wa lazima. Kwa kufanana, katika mwaka 1918 watangazaji wa ufalme wake walipata pigo ambalo watesi wao walifikiria kuwa “pigo la mauti,” hata kwamba kutangazwa kwa Ufalme kukahitaji kuhuishwa, kufufuliwa.

9. (a) Kwa sababu gani kuhuishwa au kufufuliwa kwa mfano kwa watangazaji wa Ufalme wenye kuteswa kwenye utendaji kwa mara nyingine kusingekuwa ulinganifu wa kweli wa ufufuo wa Yesu Nisani 16, mwaka 33 W.K.? (b) ’Kunyakuliwa kwao ili kumlaki Bwana’ kusingeweza kutangulia kufufuliwa kwa nani kwa kiroho?

9 Kufufuliwa kwa Yesu katika Nisani 16, mwaka 33 W.K., kulikuwa kwa namna ya kiroho, kwenye makao ya kimbinguni, walakini kulikuwa kutoka kwa kaburi la kidunia. Kwa habari ya watangazaji wa Ufalme waliokuwa bado wangali katika mwili, kuhuishwa kwao kulikuwa kwenye utendaji wa kidunia, kuanza kuhubiri upya “habari njema hizi za ufalme” katika dunia yote inayokaliwa na watu “kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14, NW) Wakati ulikuwa bado kwa hao Wakristo waliozaliwa kwa roho kutukuzwa mbinguni, ‘kunyakuliwa katika mawingu, ili kumlaki Bwana hewani.’ Kupatwa kwao na jambo hili hakukuwa kumepangwa ‘kutangulie’ kufufuliwa kwa Wakristo ‘waliolala katika mauti katika Yesu’ mpaka kufikia mwaka 1918. Mahali pake, kama vile 1 Wathesalonike 4:14-17 linavyotaja, “waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.” Kwa kufaa, kufufuliwa kwao kwanza kungetangulia kuhuishwa au kurudishwa kwenye uzima kwa watangazaji wa Ufalme kwenye kazi zaidi wakiwa katika mwili duniani katika huu “wakati wa mwisho.” Kuhuishwa huku kulitukia katika masika ya mwaka 1919.

10. Ni ufufuo wa nani, nao ukiwa wakati gani, ungekuwa ulinganifu wa kweli wa ufufuo wa Yesu katika Nisani 16, mwaka 33 W.K.?

10 Kufufuliwa kwa kiroho kwa “waliokufa katika Kristo” katika masika ya mwaka 1918 miaka mitatu na nusu tangu kutawazwa kwa Kristo mwishoni mwa Majira ya Mataifa katika vuli ya mwaka 1914, kungelingana na ufufuo wake Yesu mwenyewe katika Nisani 16, mwaka 33 W.K., wakati wa “nusu ya juma.” (Dan. 9:27) Kwa njia hiyo ‘walifufuka kwanza.’ Kufufuliwa kwao ‘kulitangulia’ kufufuliwa kwa wale waliosalia mpaka ‘kuwapo,’ au parousia, kwa Kristo, na kuuawa kwa kuhubiri Ufalme.

11. Ni kipindi gani cha wakati kinachotokea kuhusiana na mashahidi wa Mungu wa kiunabii wa Ufunuo, sura ya 11, na je! kupanda kwao mbinguni kunafananisha utimizo wa 1 Wathesalonike 4:17?

11 Kipindi cha wakati kama icho hicho kinaonekana kuhusiana na mashahidi wa Mungu wa kiunabii wanaofananishwa katika Ufunuo, sura ya 11. Kulingana na Ufunuo 11:3-7, waliuawa baada ya kutoa unabii kwa siku 1,260, au miaka 3 1/2. Walakini wanafufuliwa: “Baada ya siku hizo tatu na nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama. Wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, Pandeni hata huku. Wakapanda mbinguni katika wingu, adui zao wakiwatazama.” (Ufu. 11:11, 12) Kwa unabii hii ilifananisha kuhuishwa kwa mabaki ya Wakristo waliozaliwa kwa roho katika utumishi wa Ufalme katika masika ya mwaka 1919. Kupanda kwao kwenye sifa ya kujulikana ulimwenguni pote hakukuwa kutimizwa kwa 1 Wathesalonike 4:17. Kuhusiana na hili, twakumbuka kwamba wale wanafunzi 120 wa Yesu hawakuhuishwa kwenye utendaji wa waziwazi katika Yerusalemu mpaka siku 51 baada ya kutundikwa na kuzikwa kwa Bwana wao, Yesu Kristo.

12. Kuhuishwa huko kwa mabaki ya kiroho kulitabiriwaje vilevile katika njozi iliyoandikwa katika Ezekieli 37:1-14?

12 Kuhuishwa huko kwa mabaki waliosalia vilevile kulitabiriwa katika Ezekieli 37:1-14. Hapo Yehova alimpa nabii Ezekieli njozi ya bonde lenye kujaa mifupa mikavu ya Waisraeli. Mifupa hiyo ilitengenezwa tena kuwa Waisraeli walio hai ambao walikuwa tayari kutoka katika uhamisho wao katika Babeli ya kipagani. Akieleza namna njozi hii ingetimizwa, Yehova alisema: “Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu [waliohamishwa katika Babeli], nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli. Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi [Yehova], nitakapoyafunua makaburi yenu, enyi watu wangu.”​—Eze. 37:12, 13.

13. Njozi hii ya bonde la mifupa mikavu ilitimizwaje katika nyakati za kisasa, na jambo hili lililinganaje na yale yaliyowapata wanafunzi wa Yesu baada ya yale yaliyotukia wakati wa “nusu ya juma”?

13 Katika utimizo wa kisasa wa njozi hiyo mabaki ya Waisraeli wa kiroho walihuishwa katika masika ya mwaka 1919 na walikombolewa kutoka Bebeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, na kutoka katika utiisho wa wapenzi wake wa kisiasa, kisheria na wa kijeshi waliofanya aliyowaamuru wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Inaelekea, kukiwa na maana ya kiunabii juu kuwekwa kwa wakati kwa kisasa kwa matukio, kuhuishwa kwa wanafunzi wake Yesu na kukombolewa kwao kutoka kwa taratibu ya mambo ya Kiyahudi yenye kuonea hakukutukia mpaka baada ya kufa na kuzikwa na kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu katika siku ya tatu, Nisani 16, mwaka 33 W.K. Huu ulikuwa muda mfupi baada ya “nusu ya juma” wakati Yesu alipotolewa dhabihu kama mkombozi wa jamii yote ya kibinadamu.

14. Mashahidi hawa wa kisasa wanaotenda kwa mara nyingine, waliohushwa ni wa jamii gani inayotajwa katika 1 Wathesalonike 4:15-17, nayo ile siku Yesu aliyoita “siku ya mwisho” ni yenye ‘furaha’ kwao namna gani?

14 Katika nyakati za kisasa, mabaki wa Israeli wa kiroho waliohuishwa, waliorudishwa kwenye utendaji kwa mara nyingine ambao waliianza kazi ya kutoa ushuhuda tena katika masika ya mwaka 1919 walikuwa wale ambao mtume Paulo aliwataja kuwa ‘sisi tulio hai, tuliosalia hata wakati wa kuwapo kwake Bwana.’ (1 The. 4:15) Wao wanatazamia, baada ya kumaliza kushuhudia Ufalme ulimwenguni pote kwa mara ya mwisho, kufa ‘katika umoja na Bwana’ na wakati wa kuwapo kwake. Wao wanakufa wakati wa hiyo “siku ya mwisho” ambayo katika hiyo, kama vile alivyosema Yesu, angewafufua kutoka kwa wafu wale wanafunzi waliopewa pendeleo la kula mwili wake na kunywa damu yake. Kwao hii inafananisha ‘kunyakuliwa’ ili kukutana naye, Bwana wao, “hewani.” Ufufuo huu wao wa mara moja kwenye uzima wa kimbinguni hauonekani kwa wanadamu wanaoachwa nyuma duniani, ni kana kwamba umezuiliwa na “mawingu.” Hakika, ‘ni wenye furaha,’ kwa sababu ‘wanakufa katika umoja na Bwana tangu sasa’ wakati wa ‘kuwapo kwa Bwana,’ pasipo kuhitaji kulala katika mauti katika kutazamia kuja kwake kwa pili.​—Ufu. 14:13; Yohana 6:53, 54; 1 Kor. 15:52, 53.

15. Ni wenzi wafanya kazi gani watakaokuwa karibu wakati mabaki waliosalia watakapoondoka mwishoni mwa “siku ya mwisho,” na kuachana huku huenda kukawa kwa namna gani?

15 “Mkutano mkubwa” wa Wakristo wenzao, utaachwa nyuma. Katika huu “wakati wa mwisho” na wakati wa ‘kuwapo kwa Bwana’ kusikoonekana wamekuwa wafanya kazi wenzi wa mabaki ya Waisraeli wa kiroho katika kutoa ushuhuda kwa mara ya mwisho kwa mataifa yote. Huu “mkutano mkubwa” unatazamia kuokoka “dhiki kuu” ambayo katika hiyo taratibu hii ya mambo ya ulimwengu itatoweka. (Ufu. 7:9,14) Hivyo watakuwapo wakati huo wenye furaha ufikapo, wakati ambapo yule wa mwisho wa mabaki ya Israeli wa kiroho ‘atakaponyakuliwa katika mawingu ili kumlaki Bwana hewani.’ (1 The. 4:17) Namna litakavyokuwa jambo la upendo kwa “mkutano mkubwa” utakaokuwa ukiishi katika siku hiyo ya mwisho ya ufufuo kuwaaga mabaki waliosalia wanapomaliza mwendo wao wa kidunia mwishoni mwa “siku ya mwisho”! (Yohana 53, 54) Huenda kuachana huku kusiwe rahisi, walakini kwaweza kuwa pamoja na kuonyeshana upendo kutoka moyoni kati ya wale wanaoondoka na wanaoachwa katika dunia ya paradiso. “Mkutano mkubwa” hautawaona tena.

16. Wajapoupoteza ushirika wa uso kwa uso wa nani, “mkutano mkubwa” utakuwa na furaha ya kuwakaribisha nani wenye kuingia kwenye dunia ya paradiso?

16 Ujapokuwa utapoteza uhusiano wa kimwili wa mabaki waliotukuzwa, “mkutano mkubwa” utafarijiwa na kundi kubwa la wakaaji wapya wa dunia iliyo paradiso. Hawa ni akina nani, nao wanatoka wapi? Ni wanadamu wale wengine waliokombolewa watakaofufuliwa kutoka katika nchi ya “adui wa mwisho,” kifo kilicholetwa na Adamu. (1 Kor. 15:26) Lo! namna itakavyokuwa furaha kwa “mkutano mkubwa” wakati huo kukutana na Ayubu, ndiyo, Ibrahimu, Isaka, Yakobo, Yohana Mbatizaji, aha, ndiyo, hata na watoto wachanga wa Bethlehemu waliotumwa kwenye makao ya wafu na adui wao, Herode Mkuu! Lo! namna itakavyokuwa furaha pia kukutana na rafiki tunaofahamu, “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema ambao hawakuiokoka “dhiki kuu” na kuingia moja kwa moja kwenye utawala wake wenye urefu wa miaka 1,000! (Ufu. 20:4, 6; Yohana 10:16) Je! washiriki wa mabaki watiwa mafuta watakaookoka “dhiki kuu” wataendelea kuishi katika Taratibu Mpya na kushuhudia kuanza kufufuliwa kwa wafu wa kidunia wakati wa “siku ya mwisho” yao? (Yohana 11:24) Maandiko hayaonyeshi kwa uhakika wo wote.

17. (a) Kuhusiana na kuvunwa kwa wafu wa kidunia, wale watakaofufuliwa wakati huo watakuwa nini kwa kulinganishwa na Kristo? (b) Ujapokuwa hauhitaji ufufuo kutoka kaburini, “mkutano mkubwa” utakuwa kama wale waliofufuliwa kwa habari gani, na ni hali gani yenye baraka itakayotokea mwishoni mwa utawala wa Kristo wa miaka elfu moja?

17 Wanadamu hao waliofufuliwa watavunwa kama mazao ya baadaye, ambayo Yesu Kristo aliyefufuliwa alikuwa ‘Kristo limbuko.’ (1 Kor. 15:20, 22, 23) Ujapokuwa hauhitaji ufufuo kutoka kaburini, “mkutano mkubwa” uliookoka utakuwa kama vile wale wafu waliofufuliwa, ukihitaji faida zaidi za dhabihu ya upatanisho ya Yesu Kristo. Matokeo yote ya kifo kilichorithiwa lazima yafutwe. Hakika, itakuwa baraka, mwishoni mwa utawala wa Kristo wa miaka 1,000, wakati, ‘adui wa mwisho mauti, atakapobatilishwa’ kwa wanadamu wote waliokombolewa na wenye kutii, kutia na “mkutano mkubwa” wa waokokaji wa dhiki. Kisha, kwa kufaa kabisa, Yehova Mungu atakuwa “yote katika wote.”​—1 Kor. 15:26, 28; Ufu. 1:18; 20:11-14.

—Kutoka The Watchtower June 15, 1978.

[Picha katika ukurasa wa 17]

Kuwakaribisha watu waliofufuliwa katika Paradiso

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki