Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/1 kur. 17-22
  • Namna Yehova Anavyoongoza Watu Wake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Namna Yehova Anavyoongoza Watu Wake
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UONGOZI KWA HABARI YA KWELI ZA UFALME
  • KWELI KUHUSU WATU WA MATAIFA
  • UONGOZI KATIKA SIKU ZETU
  • ‘Nuru Imemeta kwa Ajili Wenye Haki’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Jinsi Huchaguliwa na Kuongozwa na Mungu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • ‘Ee Mungu, Utume Nuru Yako’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • “Mungu Hana Ubaguzi”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/1 kur. 17-22

Namna Yehova Anavyoongoza Watu Wake

“Kwa maana ndivyo alivyo Mungu, Mungu wetu, milele na milele yeye ndiye atakayetuongoza.”​—Zab. 48:14.

1. Biblia inaonyeshaje kwamba Yehova anawaongoza wale wampendao?

KWA karne zote zilizopita, Yehova ameongoza wale wanaompenda na wanaotaka kumtumikia. Mtunga zaburi huyu alikuwa mmoja wa hawa, kwa kuwa alimwomba Mungu hivi: “Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze [mimi].” (Zab. 43:3) Nabii Danieli alijua kwamba “yuko Mungu mbinguni afunuaye siri,” naye alitabiri kwamba katika wakati wetu, huu “wakati wa mwisho,” “maarifa [yaliyo sahihi] yataongezeka.” (Dan. 2:28; 12:4) Isaya vilevile alitabiri kwamba katika hizi “siku za mwisho” ibada ya kweli ‘ingewekwa imara’ na kwamba Yehova angeongoza watu wake: “Naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake.” Hivyo, mwaliko unaotolewa watu wote ni huu: “Njoni, twende katika nuru ya [Yehova].”​—Isa. 2:2-5.

2. Yehova anakumbuka jambo gani anapowaongoza watu wake katika kweli zake?

2 Kwa kweli Yehova anawaongozaje watu wake katika kweli zake? Jambo moja ni kwamba, yeye anakumbuka kwamba yeye aliwaumba wanadamu wakiwa na hiari. Hivyo, mtume Paulo alikubali “hiari” ya Filemoni. (Flm. 14) Kwa kuwa Mungu ndiye aliyeiumba hiari hii, yeye haipingi kwa kuwalazimisha watu waziamini kweli zake au watende kwa njia isiyopatana na hiari yao, wakitenda kama mashine. Kwa hiyo, katika wakati huu wa Kikristo, yeye anawasihi kwa upendo watu wenye mioyo yenye haki waje washirikiane na tengenezo lake lenye kibali yake kisha anawaongoza kwa upole kupitia kwa roho takatifu, na kwa Neno lake lililoongozwa naye na kwa tengenezo lake lenye kutoa kweli duniani.

3. Sana sana ni jambo gani la maana la kukumbuka juu ya namna Yehova huongoza watu wake?

3 Jambo jingine la kufikiriwa kuhusiana na uongozi wa Mungu kwa watu wake ni kwamba Mungu hutoa ufahamu wa kweli zake katika wakati wake mwenyewe, na katika njia yake mwenyewe. (Dan. 12:9) Tena, Yehova anawaongoza watu wake katika kweli hatua kwa hatua. Kwa kuwa ndiye aliyeiumba akili ya kibinadamu, Yehova anajua kwamba ‘chakula’ kidogo sana cha kiroho hakitaidumisha inavyofaa, lakini kingi mno kwa wakati mmoja kitakuwa kingi mno wanadamu wasiweze kukitumia chote. Katika Yohana 16:12 Yesu aliwaambia mitume wake waaminifu hivi: “Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa.” Kwa mfano, mtu atokapo kwenye chumba chenye giza ambamo amekuwa amefungiwa kwa muda mrefu, inakuwa vizuri zaidi akiletwa nuruni hatua kwa hatua. Nuru nyingi mno anapotoka tu yaweza kumshtua, hata labda kumdhuru. Vivyo hivyo kuna uhitaji wa kufunuliwa nuru ya kweli za Mungu hatua kwa hatua. Hii inalingana na yale yanayosemwa na mwenye hekima: “Njia ya wenye haki ni kama nuru ing’aayo, ikizidi kung’aa hata mchana mkamilifu.”​—Mt. 4:18.

4. (a) Yesu alionyesha jambo gani juu ya uhitaji wa kudhihirisha kweli hatua kwa hatua? (b) Kwa kuwa kweli za Yehova hudhihirishwa hatua kwa hatua, lazima watumishi wake wawe na nia ya kuwanya nini?

4 Yesu alijua vizuri sana kwamba njia ya Yehova ya kuzifunua kweli zake ni njia ya hatua kwa hatua. Aliwaambia mitume wake kwamba baadaye roho takatifu ya Mungu ingewaongoza kwenye kweli yote. (Yohana 16:12, 13) Na kwa kuwa kweli zilizokuwa zimetangulia kutolewa zingedhihirishwa wazi hatua kwa hatua, kungekuwako uhitaji unaolingana wa watumishi wa Mungu wasahihishe na kutengeneza upya maoni yao katika mambo mbalimbali ya Maandiko kama vile wakati ulivyozidi kusonga mbele.

UONGOZI KWA HABARI YA KWELI ZA UFALME

5, 6. Kwa habari ya ufalme wa Mungu, ni jambo gani huonyesha kwamba wanafunzi wa Yesu walikuwa na maoni yenye makosa?

5 Katika kuwaongoza Wakristo katika karne ya kwanza, Yehova hakuwadhihirishia kweli zote zilizohusiana na makusudi yake katika wakati mmoja. Kwa mfano, ebu fikiria fundisho kUu la Biblia, ufalme wa Mungu. Yesu alifundisha wafuasi wake kusali: “Ufalme wako uje.” (Mt. 6:10) Aliwahimiza: “Utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake.” (Mt. 6:33) Lakini je! katika muda wa miaka hiyo alipokuwa duniani wafuasi wake walifahamu mambo yote juu ya utawala wa Ufalme? Je! wangeweza kujibu maulizo yote kuuhusu kwa usahihi, kama vile: Ufalme wa Mungu ni nini? Ni nani watakaotawala ndani yake, nao watakuwa wangapi? Utakuja wakati gani? Utaifanyia dunia na wanadamu nini?

6 Kwamba wale waliokuwa wakizungumza na Yesu hawakuwa na maarifa hayo yote inaonyeshwa na ulizo walilomwuliza Yesu baada ya kufufuliwa kwake: “Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?” (Matendo 1:6) Badala ya kujibu kwa kuwaambia mambo yote yanayohusiana na utawala wa Ufalme, Yesu alitangaza hivi: “Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.” (Matendo 1:7) Sababu gani Yesu alishughulikia jambo hilo katika njia hiyo? Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa na maoni yaliyoimarika sana lakini yenye makosa kuhusu Ufalme. Waliamini kwamba Ufalme huo ungekuwa utawala wa kidunia ambao ungeupindua utawala wa Kirumi. Walakini kweli ilikuwa kwamba Ufalme huo ungekuwa wa kimbinguni, na kwamba wale waliochaguliwa watawale pamoja na Kristo wangetolewa duniani na kupelekwa mbinguni. (Ufu. 5:9, 10; 14:3; 20:4) Zaidi ya hayo, ulizo lao linaonyesha kwamba wao walitazamia kwamba Ufalme huo ungesimamishwa mara hiyo. Walakini haingekuwa hivyo, kwa kuwa mahali pake karne nyingi zingepita.

7. (a) Wajapokuwa na maoni yenye makosa juu ya Ufalme, Yesu alikuwa na maoni gani kuelekea hao wanafunzi? (b) Je! sisi tunafahamu kila jambo kuhusu utawala wa ufalme wa Mungu?

7 Ijapokuwa wanafunzi wake walikuwa na maoni yenye makosa, Yesu hakuwa hukumia kuwa wasiofaa na kuwatupilia mbali. Yeye, alijua kwamba kufahamu kwao kweli za Mungu kungekuwa kwa polepole, na kwamba roho takatifu ingewaongoza wafuasi wake hatua kwa hatua hivi kwamba katika wakati wake wangepata ufahamu ulio wazi. Mwishowe, wangepata ufahamu ulio kamili kuhusu utawala wa Ufalme. Walakini kwa wakati huo, Yesu alikazia katika akili za hao wafuasi wake wa kwanza kupendezwa kwingi mno na juhudi katika kuutafuta kwanza Ufalme, na kuwa na nia ya kutengeneza upya maoni yao juu yake. Kwa hiyo ijapokuwa walikuwa na maarifa sahihi ya kiasi tu ya kweli juu ya Ufalme, yale waliyojua yaliwawezesha ‘kuhimiza akilini mwao kuwapo kwa siku ya Yehova.’ (2 Pet. 3:12, NW) Leo, maarifa yetu juu ya utawala wa Ufalme wa Mungu, kuwa ni nini na yale utakayotimiza, ni ya juu zaidi, walakini si matimilifu kabisa.

KWELI KUHUSU WATU WA MATAIFA

8. Kulikuwa na gumu gani kuhusiana na Mataifa, na je! jambo hilo hata lilitajwa katika Pentekoste?

8 Ulizo jingine lililoonyesha namna ufa-hamu wa kweli ya Mungu ulivyo wa hatua kwa hatua ulihusiana na namna watu wa Mataifa wasio Wayahudi ambao walikuwa wamegeuka kuwa Wakristo tokea 36 W.K. na kuendelea walivyoonwa na wengine wa Wayahudi waliokuwa wamegeuka wakawa Wakristo. Kwa mfano, walipaswa watahiri, kama vile walivyokuwa Wayahudi wa asili? Je! jambo hilo hata lilitajwa katika 33 W.K. wakati roho takatifu ya Mungu ilipomiminwa katika Pentekoste? Hapana, kwa kuwa ijapokuwa kumiminwa huko kulithibisha kwamba Mungu alikuwa pamoja na wanafunzi hao na kwamba tangu hapo angeendelea kuwaongoza, haikuwapa kwa njia ya mwujiza maarifa yote juu ya kweli za Mungu. Hii inaweza kuonwa kutokana na uhakika wa kwamba ulizo la kutahiriwa halikuelezwa wazi kwa maamuzi yaliyowekwa na mitume na wazee waliokuwa Yerusalemu mpaka miaka 16 baada ya Pentekoste, katika mwaka 49 W.K.​—Matendo 16:4.

9-11. (a) Baada ya kufuata uongozi wa Yehova kwa miaka mingi, ni kwa sababu gani watumishi wa Yehova walikuwa katika hali bora zaidi ya kushughulika na gumu la kutahiriwa? (b) Maono aliyopewa Petro yalisaidiaje katika kurekebisha upya maoni katika ufahamu unaofaa wa kweli?

9 Katika muda wa miaka hiyo yote Yehova aliwaruhusu watu wake wapate kuona hasa namna alivyokuwa akiwatendea Mataifa. Katika njia hii, kuthamini kwao na kufahamu jambo hili kuliimarishwa. Hivyo, ulizo lilipotokea lililohitaji kuchukuliwa hatua yenye kuamua, watumishi wake walikuwa wametayarishwa vizuri wapate kulishughulikia kwa hekima na ufahamu. Ebu chukua kwa mfano, kutengeneza upya maoni ambako Petro alilazimika kufanya. Zaidi ya miaka mitatu baada ya Pentekoste, mtume Petro aliongozwa na roho takatifu asahihishe maoni yake juu ya watu wa Mataifa, ambao aliwaona kuwa najisi, wachafu.

10 Katika maono, Petro aliambiwa ale chakula kilichoonwa kuwa najisi (kichafu) katika torati ya Musa. Alipojibu kwa kushangaa kwamba yeye hali chakula kama hicho, sauti kutoka mbinguni ilimwambia kwamba kile ambacho Mungu ameita safi hakipaswi kuonwa tena kuwa najisi. Na katika wakati uo huo wajumbe wakaja kutoka kwa Mtaifa Kornelio. Kornelio alikuwa amewatuma wamwulize Petro aje nyumbani kwake amwambie juu ya makusudi ya Mungu. Lakini Petro alikuwa ndipo tu ameonyesha kushtushwa katika kula chakula najisi, na sasa alikuwa akiombwa aende katika nyumba ya Mtaifa, ambao vilevile aliwaona kuwa najisi! Anapaswa afanye nini? Roho takatifu iliongoza jibu hili: “Ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma.”​—Matendo 10:9-20.

11 Petro alifahamu maana yake. Maono juu ya Yehova kufanya kitu safi ambacho hapo kwanza kilionwa kuwa najisi hayakuhusu chakula peke yake, bali, la maana zaidi, yalihusu maoni ya Petro juu ya Mataifa. Akionyesha kwamba alifahamu, Petro alimwambia Kornelio pamoja na nyumba yake hivi: “Kwa sababu hiyo nalikuja nilipoitwa, nisikatae.” Ndipo roho takatifu ilipomiminwa juu ya nyumba hiyo ya Mtaifa, nao wakabatizwa. Roho takatifu ilikuwa imeonyesha kwamba sasa Mungu angewakubali Mataifa bila ya wao kutahiriwa.​—⁠Matendo 10:21-48.

12. (a) Ni gumu gani zaidi lililotokea kuhusiana na Mataifa. na lilitokea wakati gani? (b) Baraza kuu iliweza kutoa jibu lenye kukata maneno kwa msingi gani?

12 Lakini je! hilo liliwaridhisha Wayahudi wote waliogeuzwa kuwa Wakristo kwa habari ya Mataifa? Hapana. Kwa sababu miaka 13 baadaye, ulizo la kwamba iliwalazimu Mataifa kutahiriwa lilitokezwa na wengine wa Wayahudi wenye kutahiriwa waliokuja Antiokia, Shamu. (Matendo 15:1, 2) Kwa hiyo katika mwaka 49 W.K. mkutano ulipangwa pamoja na baraza kuu ya mitume na wanaume wengine wazee katika Yerusalemu. Katika kusanyiko hilo, Petro, Paulo na Barnaba walieleza yale ambayo Mungu alikuwa ametimiza kati ya Mataifa wasiotahiriwa ambao walikuwa wamehubiri. Baada ya kuchunguza namna Yehova alivyokuwa ameshughulika na watu hawa wa Mataifa kwa miaka mingi, wote walikubaliana na ushuhuda wa Maandiko Matakatifu, wakiutia nguvu ukweli wa kwamba haikuwa lazima Mataifa watahiriwe.

13. Wengine walionyeshaje kukosa kuthamini namna Yehova alivyokuwa akiwaongoza watu wake, na huenda kukawa kulikuwa na matokeo gani?

13 Si wafuasi wote wa Kristo waliokuwa na nia ya kusahihisha maoni ya kikale. Wengine walichukua masahihisho haya kama sababu ya kuacha kweli, mahali pa kuyaona kama ushuhuda wa uongozi wa Yehova kwa watu wake hatua kwa hatua. Kwa mfano, alipotoa mfano juu ya kula nyama ya mwili wake kwa njia ya mfano na kunywa damu yake, habari ya Biblia inasema kwamba “kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena.” (Yohana 6:53-66) Lo! namna huo ulivyokuwa ujinga! Kulikuwa kukosa namna gani kuthamini namna Yehova anavyowaongoza watu wake! Miaka 38 baadaye huenda wengine wao wali-pata hasara kubwa, kwa kuwa wale ambao hawakuendelea kutembea katika kweli iliyoendelea kufahamika waliyakataa maagizo ya Yesu ya kuukimbia Yerusalemu kabla haujaangamizwa. Hiyo iliwagharimu maisha zao, hali wale walio-endelea kumwacha Yehova awaongoze walikimbia wakasalimika.​—Luka 21:20-24.

UONGOZI KATIKA SIKU ZETU

14. Maoni yetu kuhusu kweli za msingi yamesahihishwa kadiri gani kwa muda wa karne moja iliyopita?

14 Tunapoangalia yale ambayo yamechapwa na tengenezo la Yehova katika kurasa za Mnara wa Mlinzi pamoja na vitabu vingine kwa muda wa karne iliyopita, tunapata chakula tele cha kiroho kifaacho. Mwanzoni mwa kipindi hiki, kweli za msingi za Biblia zilielezwa wazi wazi, nazo zimeendelea kuwa wazi mpaka hivi leo. Maoni yetu juu ya hell (moto wamateso), utatu, purgatori (matohara), nafsi, waliko wafu, ukombozi, ufufuo, mwisho wa dunia, Ufalme na mafundisho mengine ya maana yamekuwa na mabadiliko madogo sana katika muda huo wa miaka 100 moja. Kweli imeendelea kuwa kweli sikuzote. Hata ingawa kuifahamu kwetu kumetuhitaji tuyarekebishe maoni yetu mara kwa mara.​—Linganisha Yohana 16:13.

15. Je! kumekuwako uhitaji wa watumishi wa Yehova wa kisasa warekebishe upya maoni yao?

15 Yehova ameendelea kuongoza watu wake, hatua kwa hatua wazifahamu kweli zake, naye amefanya hivyo katika wakati wake mwenyewe na katika njia yake mwenyewe. Kwa sababu hiyo, katika wakati wa mapema sana katika karne iliyopita, Mashahidi wa Yehova wamefahamu kwamba lazima wawe na nia ya kubadilisha na kusahihisha maoni yao juu ya mafundisho, mazoea pamoja na mipango yao ya tengenezo ilipokuwa wazi kwamba roho ya Yehova ilikuwa ikiwaongoza wafanye marekebisho ya namna hiyo. Kama ilivyokubaliwa na Bryan Wilson katika gazeti New Society (Jamii Mpya) la tarehe ya Januari 26, 1978, ukurasa 183, Mashahidi wa Yehova “wamesema sikuzote kwamba kuendelea kujifunza Biblia kunaweza kuongoza kwenye maarifa makamilifu zaidi, na katika wa-kati uliopita makosa juu ya kufasiriwa kwa unabii yamekubaliwa.”

16. (a) Ni kwa sababu gani sana sana unabii wa Biblia ni sehemu inayohitaji kuwa na nia ya kurekebisha upya maoni? (b) Watumishi wa Yehova wameitikiaje habari juu ya “siku za mwisho,” nao wametegemezwaje?

16 Labda sehemu inayohitaji zaidi nia ya kurekebisha upya maoni ni ile inayohusu unabii wa Biblia. Unabii mwingi unatolewa kwa muhtasari tu. Kwa hiyo, imani inahitajiwa ili kungojea kutimizwa kwa mambo mengine mengi. (Ebr. 11:1) Mfano wa hili unahusiana na unabii wa Biblia unaoonyesha kwamba taratibu ya mambo iliyopo chini ya Shetani itaharibiwa na mahali pake kuchukuliwa na “mbingu mpya na dunia mpya.” (2 Pet. 3:13) Hata hivyo, sehemu nyingi kutosha za “ishara” yote ya mwisho unaokuja zimetolewa katika Biblia kuonyesha waziwazi kwamba wakati uliopo ndio “siku za mwisho,” “wakati wa mwisho.” (2 Tim. 3:1; Dan. 12:4) Hiyo imewachochea watumishi wa Mungu waongeze sana kazi ya kutimiza maneno ya Yesu: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mt. 24:14, NW) Wao wamefaulu katika kufanya hivyo na katika kuokoka kama tengenezo, vilevile katika kupata ufanisi wa kiroho yajapokuwapo mateso makali, vivyo hivyo wamefaulu katika kuvaa utu mpya katika ulimwengu huu mchafu. Huu wote ni ushuhuda wa kwamba kweli kweli Yehova amewategemeza.​—Isa. 54:17; Mt. 28:19, 20; Efe. 4:17-24.

17. Je! kutotimizwa kwa matazamio yetu ya mapema mno ya mambo kunamaanisha kwamba Yehova amebadilisha makusudi yake?

17 Lakini, je! katika hizi “siku za mwisho,” wengine wa watumishi wa Yehova wamekuwa na maoni yenye makosa katika wakati uliopita kuhusu mwisho au telos (Kigiriki) wa taratibu hii ya mambo? Ndiyo, wamekuwa nayo. Mengine ya maoni haya yalihusu urefu wa muda ambao ungepita kabla ya mwisho kuja. Kwa sababu ya kuwa na juhudi na shauku ya kuona jina, Neno na makusudi ya Yehova yakiondolewa lawama, na kwa kuwa na tamaa ya taratibu mpya, wengine wa watumishi wake wametazamia mambo kabla ya wakati wake katika nyakati nyingine. Hii inalingana na maoni waliyokuwa nayo wanafunzi kwamba ufalme wa Mungu ungejitokeza katika siku zao. (Matendo 1:6) Lakini kwa kuwa mambo yametazamiwa mapema mno kabla ya wakati wake na kwa hiyo yakakosa kutimizwa, hii yamaanisha kwamba huenda Mungu amebadili kusudi lake? Hata kidogo. “Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote,” asema Yehova. (Isa. 46:10) Hivyo, makusudi ya Yehova, na wakati wa kusimamisha taratibu mpya yenye haki umewekwa imara.

18. Ni kwa sababu gani ni jambo la maana kukaa katika “yale yaliyoandikwa”?

18 Bila shaka hii inakazia kwetu uhitaji wa kufikiria kwa uangalifu mambo yote ya hakika ya Maandiko, wala si kukazia mengine mpaka yanayaficha mengine. Kama vile Yesu mwenyewe alivyosema waziwazi: “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye.” (Mt. 24:36) Sikuzote kuna uhitaji wa kuangalia sana shauri la mtume Paulo la: “Kutokupita yale yaliyoandikwa.”​—1 Kor. 4:6.

19. Ijapokuwa maoni yamerekebishwa upya, ushuhuda unathibitishaje mwisho unaokaribia wa taratibu hii?

19 Ijapokuwa wengi wa Mashahidi wa Yehova wamelazimika kurekebisha upya maoni yao juu ya jambo hili, je! sisi tunaweza kukana kwamba sisi hatuko katika “wakati wa mwisho”? Bila shaka ushuhuda unaongezeka kila siku juu ya mwisho unaokuja wa hii taratibu ya mambo, tuonapo kuvunjika kwingi sana kwa matengenezo kama vile ndoa, jamaa, serikali na dini ya ulimwengu, pamoja na kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria na jeuri, pamoja na kutomheshimu Mungu kunakoendelea kuongezeka.​—⁠2 Tim. 3:​1-5.

20, 21. Wale wanaoendelea kutembea katika nuru ya Yehova yenye kuendelea watathawabishwaje?

20 Ijapokuwa wakati unaobaki wa hizi “siku za mwisho” haujulikani, jambo moja ni hakika. Wale wanaoendelea kutembea katika nuru ya Yehova inayoongezeka, nao wanakuwa na nia ya kurekebisha upya maoni yao, watakuwa kati ya mabaki ya watiwa mafuta na “mkutano mkubwa” ambao “wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu” na kuingia katika taratibu mpya ya Mungu yenye haki. (2 Pet. 3:​14, 15) “Huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga [huo mkutano mkubwa], na kuwaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atafuta machozi yote katika macho yao.”​—Ufu. 7:9-17.

21 Hivyo, wale wanaomtegemea Yehova kwa uongozi wanaweza kutazamia mbele kwa uhakika kusimamishwa kwa taratibu mpya ambayo katika hivyo, “asiye haki hatakuwapo.” Bali mahali pake, wapole na wenye kukubali mafundisho “watajifurahisha kwa wingi wa amani.”​—Zab. 37:10, 11, 29.

22. Watumishi wa Yehova wanaweza kuwa na uhakika gani sasa na kwa wakati ujao?

22 Kwa hiyo,”‏ kama vile imekuwa kwa muda huo wa miaka 100 iliyopita kwa habari ya tengenezo la watu wa Yehova la kisasa, sisi leo tuna hakika kwamba ndivyo vilevile itakavyokuwa katika muda unaobaki wa hizi siku za mwisho, “Ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele. Yeye ndiye atakayetuongoza.” (Zab. 48:14) Kisha, katika taratibu yake mpya, tunaweza tukiwa na uhakika uo huo, kutazamia mbele kwenye uongozi wa Yehova wenye kuendelea kwa watumishi wake kwa umilele wote, bila ya wao kufa hata kidogo, kwa kuwa “yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.” ​—⁠1 Yohana 2:17. ​—⁠Kutoka The Watchtower July 1, 1979.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki