‘Tunalithamini Kweli Kweli’
KUTOKA sehemu nyingi za ulimwengu tuna-pokea barua kutoka kwa wasomaji wa wa Mlinzi. Mara nyingi barua hizi huwa za kuonyesha kuthamini kwao, nasi tungetaka kushiriki baadhi yazo pamoja nanyi.
Mara nyingi, wale wanaotuandikia wanakumbuka uongozi unaofaa ambao umetolewa na Mnara wa Mlinzi katika maisha zao. Mwanamke mmoja katika Uingereza anasema hivi: ‘Kweli ambazo nimejifunza kwa muda wa miaka mingi kutoka kwa Neno la Mungu zimenisaidia kubadili kabisa maoni yangu juu ya wakati ujao. Mahali pa kutokuwa na uhakika, sasa nina tumaini hakika katika Yehova na katika makusudi yake ya kusimamisha amani ya kweli na usalama kupitia kwa Mwanawe, Yesu Kristo.’ Naye mwanamume katika Ujeremani ambaye amekuwa akisoma gazeti hili kwa muda wa miaka 40 alikumbuka hivi: ‘Bila kichocheo kutoka katika Mnara wa Mlinzi singepata kamwe kuona maono yote ya moyoni yenye kina kirefu ya uradhi wa kweli yanayotokana na kufanya mapenzi ya Mungu. Ningekosa kuona hazina inayotolewa na mkono wa Yehova na ningetumia vibaya nguvu zangu.’
Mojawapo ya hazina hizo ambazo hesabu kubwa ya wasomaji wetu imepata kuona ni uongozi unaotolewa na Neno la Mungu kuhusu maisha ya Jamaa. Wanaandika hivi: ‘Mnara wa Mlinzi umenisaidia kuwa na ndoa yenye furaha. Mimi pamoja na mke wangu tunakumbushwa daima kwamba tunapaswa kufikiriana, kuwa wanyenyekevu, kukabili magumu yetu kwa upole na kwa kumtumaini Yehova.’ ‘Ulinisaidia kufa-hamu kutokana na Biblia kwamba kuoa wake wengi si jambo linalokubaliwa kati ya Wakristo nao ulinitia nguvu niwaruhusu wale wake wangu wa ziada waende zao na kushikamana na mke wangu wa kwanza. Kama matokeo, sasa ninaishi kwa furaha pamoja na jamaa yangu nami ninayo furaha ya kumtolea Yehova utumishi unaokubalika.’ ‘Kwa muda wa miaka 20 Mnara wa Mlinzi umeniwezesha kufundisha watoto wangu wafahamu yaliyo mema na yaliyo mabaya, ukanisaidia kuwa na hakika kwamba niliyokuwa nikisema yalikuwa yanafaa, kwamba yalipatana na maoni ya Mungu. Kwa kuwa tuliitumia Biblia, pamoja na Mnara wa Mlinzi,. katika kushughulika na magumu, hatukupata kamwe kuona uhusiano wa wazazi na watoto ukiharibika.’
Wengi wa wasomaji wetu wa Mnara wa Mlinzi walianza kufurahia kuusoma walipokuwa bado vijana. Mmoja kutoka Uingereza anaandika hivi: ‘Nilipojulishwa Mnara wa Mlinzi kwa mara ya kwanza, nilikuwa tineja (kijana wa miaka kati ya 13-19) aliyekuwa amekata tamaa. Nilijisikia kukosa usalama, nikawa nikizungumza kidogo sana na wazazi wangu, na nikawa nahitaji sana uongozi Mnara wa Mlinzi ulitosheleza uhitaji huo. Kwa kushikamana na Biblia kwa uaminifu, mara nyingi Mnara wa Mlinzi umechapa makala zenye kuchunguza na hata mara nyingine (kwangu mimi binafsi) zenye kuchoma mioyo sana juu ya kutumia kanuni za Biblia katika utu wetu sisi wenyewe. Namshukuru Yehova kwa msaada huo.’
Gazeti hili linatosheleza vilevile mahitaji ya wale ambao wameona siku nyingi katika maisha. Mjane mmoja aliuliza hivi: ‘Ningefanya nini bila kuwa na msaada wake? Namaanisha Mnara wa Mlinzi, bila shaka. Haujashindwa kamwe kunipa shauri lenye kufaa katika wakati wake juu ya magumu ninayokuwa nayo. Katika mwezi ule ule alipokufa mume wangu, ilitokea makala yenye kichwa “Huko Peke Yako Kamwe.” Lo! namna nilivyofarijiwa na kupata nguvu kutokana na makala hiyo pamoja na andiko lililozungumzwa, Zaburi 46. Tokea hapo, Mnara wa Mlinzi umenisaidia sana kujenga maisha mapya kama mtu aliye peke yake. Kupitia kwa mashauri yake nimepata kuona kwamba katika kuwafariji wengine waliokuwa na upweke, upweke wangu mimi umetoweka.’
Namna wasomaji wengi wa Mnara wa Mlinzi wanavyojisikia hupita zaidi sana kuwa na shukrani tu kwa ajili ya msaada uliyopokewa katika kushindana na ‘gumu fulani. Mwanamume mmoja katika Spania alisema hivi: ‘Katika karne hii ya 20 “iliyotiwa nuru” mara nyingi inakuwa vigumu sana kuona mambo katika maoni ya Mungu, katika maoni ya Bwana Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote, Yehova. Hata hivyo, Mnara wa Mlinzi umenisaidia kwa uaminifu kufanya lilo hilo katika muda wa miaka 30 iliyopita.’ Msomaji Mwitalia alifikia mkataa huu: ‘Namna ambavyo umetegemeza na kutetea mbele ya ulimwengu wote jina la Yehova, ukweli wa Neno lake, haki yake ya kutawala—hayo yote yamenionyesha kwamba umekuwa ndicho chombo ambacho Yehova ametumia kutoa nuru ya kiroho.’ Naye mwingine anaadika hivi: ‘Siku Mnara wa Mlinzi ulipofika nyumbani kwangu kwa mara ya kwanza, niliusoma, na mara hiyo dirisha ikafunguliwa kuelekea wakati ujao mzuri sana. Sikuzote nilikuwa nimefundishwa mambo kama vile kutokufa kwa nafsi, moto wa mateso na utatu. Walakini baada ya kusoma Mnara wa Mlinzi kwa saa moja, nilipaza sauti, ‘ nikasema, “Nimeipata kweli,” na sijaiacha.’