Mfano wa Amani Waonyeshwa
Sifa ya Mashahidi wa Yehova ya kuwa na mwenendo mwema inajulikana vizuri sana. Huko Bombay, India, kusanyiko la Kikristo lilifanywa katika Jumba la Shanmukhananda kwa mara ya kwanza. Baraza ya Wadhamini ya jumba hilo ilifurahia sana kuona amani na utaratibu mzuri wa Mashahidi wa Yehova hata ikamwambia hivi mwangalizi wa kusanyiko: “Tumefurahia sana kusanyiko lenu. Hatujapata kuona hata kidogo namna yake. Ikiwa kila mtu angekuwa hivi hakungekuwa na uhitaji wa serikali. Mwaweza kuja hapa kila mwaka mkitaka.”