“Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mkusanyiko 1996
NYAKATI za kale watu wa Yehova walisherehekea sherehe tatu kubwa kila mwaka. Vivyo hivyo, katika nyakati za kisasa watu wenye jina la Yehova hukutana mara tatu kila mwaka kwa ajili ya pindi za sherehe. Wao hufurahi kukusanyika kwa siku ya kusanyiko la pekee, kusanyiko la mzunguko la siku mbili, na mkusanyiko wa wilaya wa siku tatu au nne. Mwaka huu, kichwa cha mkusanyiko wa wilaya ni “Wajumbe wa Amani ya Kimungu.”
Kichwa hicho chafaa kama nini! Mungu wetu, Yehova, ni “Mungu wa amani,” ndiyo, “Mungu apaye amani.” Kiongozi wetu, Yesu Kristo, ni “Mkuu wa Amani,” na ujumbe ambao watumishi wa Yehova huleta ni ujumbe wa amani ya kimungu. (Wafilipi 4:9; Warumi 15:33; Isaya 9:6; Nahumu 1:15; linganisha NW.) Programu nzuri ya mkusanyiko imepangwa itakayotusaidia sote tuelewe kikamili zaidi umaana wa amani ya kimungu.
Mwaka huu katika Afrika Mashariki pekee, kutakuwako na mikusanyiko 22. Yamkini, kutakuwa na mkusanyiko karibu nawe. Kwa nini usiulize Mashahidi wa Yehova katika ujirani wako kuhusu wakati na mahali hasa mkusanyiko utakapofanywa kisha ufanye mipango ya kuhudhuria? Wote wanaopendezwa na amani ya kweli watapokea ukaribishaji mchangamfu.