Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 1/1 kur. 15-22
  • “Mchungaji Mwema” na “Kondoo Wengeni” Wake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mchungaji Mwema” na “Kondoo Wengeni” Wake
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “KONDOO WENGINE NINAO”
  • Zizi la Karibuni kwa Ajili ya “Kondoo Wengine”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Mchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Umati Mkubwa wa Waabudu wa Kweli—Umetoka Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 1/1 kur. 15-22

“Mchungaji Mwema” na “Kondoo Wengeni” Wake

“Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili, na hao nao imenipasa kuwaleta.”​—Yohana 10:16.

1. “Mchungaji mwema” anatofautianaje na “mtu wa mshahara”?

MCHUNGAJI mwema anatofautiana na mtu wa mshahara, ambaye huhangaikia tu mshahara atakaopata. Yesu alisema hivi: “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya. Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake.”​—Yohana 10:11-13.

2. (a) Kwa kusema kwamba “mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo,” Yesu alikuwa akitaja jambo gani kwa habari yake mwenyewe? (b) Uhai wa kibinadamu alioutoa Yesu ulitimiza kusudi gani kwa ujumla?

2 Huko nyuma katika Mashariki ya Kati kuchunga kondoo kondeni kulikuwa kazi yenye hatari. Twakumbuka namna kijana mchungaji Daudi alivyolazimika katika pindi moja kuwaua dubu na simba ili aokoe uhai wa kondoo wa Yese baba yake. (1 Sam. 17:34-36) Yesu alisema juu ya mbwa-mwitu wenye kuwala kondoo. Kumfukuza mbwa-mwitu kwaweza kumletea mchungaji hatari ya kuumizwa mwilini. Mchungaji mwema hawezi kukimbia ili ajiokoe kama vile anavyoweza kufanya mtu wa mshahara bali angewalinda kondoo na wanyama wala nyama. “Mchungaji mwema” hata angekuwa na nia ya ‘kuutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo’ ili asimpoteze hata mmoja. Kwa kuvuta fikira kwenye jambo hilo Yesu alikuwa akitabiri juu ya kifo chake akiwa nafsi ya kibinadamu kwa ajili ya “kondoo” wa Yehova. Lakini Yesu alikuwa na nia ya kuifikia sifa hii ya “mchungaji mwema.” Yehova Mungu, Baba yake wa kimbinguni, ambaye ndiye Mwenyeji wa “kondoo” wa kidunia, alikubali Mwanawe aitoe nafsi yake ya kibinadamu kwa ajili ya “kondoo” ambao Baba yake aliwapenda sana. “Nafsi” ya kibinadamu ya Yesu ilitolewa kama dhabihu ili kuwakomboa wanadamu kutokana na kifo, walichokuwa wamerithi kutoka kwa Adamu mwenye dhambi.

3. (a) Kulingana na Yohana 10:14, 15, Yesu alijifananisha na nini kuhusiana na Baba yake? (b) Ili Yesu aweze kushiriki ile ahadi ya Ibrahimu pamoja na lile “kundi dogo,” yeye alikuwa na nia ya kufanya nini?

3 Vilevile “mchungaji mwema” anakuwa na uhusiano wa karibu sana na kondoo mmoja mmoja wa kundi lake na kumpatia kila mmoja wao jina la kibinafsi ambalo katika hilo aweza kumwita aje kwake aipapase-papase kuionyesha aipenda au aitimizie mahitaji mengine. Akikumbuka sifa hii ya mchungaji wa Mashariki ya Kati, Yesu aliendelea kusema hivi: “Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi; kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.” (Yohana 10:14, 15) Yesu alijiona mwenyewe kuwa ‘kondoo” wa mfano. Yeye ndiye aliyekuwa “Mwana-Kondoo” wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu.” (Yohana 1:29) Katika kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo, yeye aitwa “Mwana-Kondoo” mara 28. Yesu alijiona kuwa ndiye aliyefananishwa na yule kondoo-mume ambaye mzee wa ukoo Ibrahimu alimtoa mahali pa mwanawe Isaka, ambaye Ibrahimu alikuwa ameonyesha nia ya kumtoa kama dhabihu kwa amri ya Yehova. (Mwa. 22:​1-13) Isaka aliipokea na kuipitisha kwa Yakobo ile ahadi aliyopewa Ibrahimu. Kama vile Isaka, Yesu aliirithi ahadi aliopewa Ibrahimu naye alikuwa na nia ya kutolewa awe dhabihu ili aweze kuishiriki ahadi hiyo pamoja na “kundi dogo” lake.

4. Je! Yesu ‘alinyakua’ hilo “kundi dogo” kutoka mkononi mwa Baba, naye Yesu alilionaje “kundi” hilo?

4 Kwa wazi, basi, Yesu alipendezwa sana na wokovu wa hilo “kundi dogo” lililomo katika “zizi la kondoo” la ule mpango wa Agano la Ibrahimu. Yeye aliwaona kuwa zawadi yenye bei kubwa sana kutoka kwa Baba yake wa kimbinguni. Kama vile alivyosema: “Kile alichonipa Baba yangu ni kitu kikubwa sana kuliko vitu vingine vyote, naye hakuna awezaye kuwapokonya kutoka katika mkono wa Baba.”​—Yohana 10:29, NW.

“KONDOO WENGINE NINAO”

5. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yesu alipendezwa na kuokoa zaidi ya wanadamu wenye mfano wa kondoo kwenye uzima wa kimbinguni?

5 Ijapokuwa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo huenda yasifikiri na kufundisha hivyo, Yesu anapendezwa na zaidi ya kuokoa viumbe vya kibinadamu kwenye uzima wa kimbinguni. Yesu alisema hivi: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; nao sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16) Sasa ni nani hao “kondoo wengine”?

6. (a) Makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yanafundisha nini juu ya “zizi hili” na “kondoo wengine”? (b) Mtajo wa Yesu juu ya Paradiso katika Luka 23:43 ZSB, na mfano Wake wa kondoo na mbuzi huonyesha nini?

6 Makanisa ya Jumuiya ya Wakristo wanadai kwamba “zizi” linalosemwa juu yake hapa na Yesu lingekuwa la Wakristo Wayahudi peke yao, hali “kondoo wengine” ni wale wanaokuwa Wakristo kutoka katika mataifa yasiyo ya Wayahudi; na kwamba wote Wayahudi wenye kuamini na watu wa Mataifa wenye kuamini wanakuwa “kundi moja” chini ya mchungaji mmoja” katika hilo zizi moja la kiroho. Walakini fundisho hilo halipatani na maandiko mengine ya Biblia yanayohusu habari hii. Ijapokuwa mtume Yohana hataji hivyo katika masimulizi yake ya Injili, Yesu alisema juu ya Paradiso ya kidunia chini ya ufalme wake naye alisema juu ya wengine kuwa walikuwa “kondoo“licha ya lile “kundi dogo” la warithi washirika wake wa kimbinguni. Wakati Yesu alipotoa unabii juu ya “ishara” ya kuwapo kwake ambako wakati huo bado kulikuwa kwa wakati ujao na ya mwisho wa taratibu ya mambo, aliumalizia, kulingana na masimulizi ya Mathayo, kwa mfano wa kondoo na mbuzi. “Kondoo” hao wangekuwa tofauti na “ndugu” za kiroho za Kristo, wanaofanyiwa mema na hao wenye mfano wa kondoo.​—Luka 23:43, ZSB; Mt. 24:3, NW; 25:31-46.

7. Ni kwa sababu gani Yohana angeweza kukumbuka mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi na kufahamu hesabu iliyomo katika “zizi hili”?

7 Mtume Yohana alifahamiana na mfano huo, kwa kuwa yeye na Yakobo ndugu yake na vilevile Petro na Andrea ndio waliomfanya Yesu atoe unabii huo kwa kumwuliza faraghani juu ya “ishara” hiyo, naye Yohana aliusikia unabii huo kwa ukamili. (Marko 13:3, 4) Kwa hiyo wakati alipoyaandika maneno ya Yesu juu ya “kondoo wengine” yawezekana awe alikumbuka mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi. Yeye ndiye mtume aliyekuwa mzee ambaye alipewa Ufunuo ulioonyesha kwamba yale makabila 12 ya Israeli wa kiroho yangekuwa na washiriki 144,000 tu. Kwa hiyo yeye alijua kwamba lile “zizi la kondoo” lililokuwamo lile “kundi dogo” lingetia ndani hesabu iliyo na kikomo ya wale wote ambao wangeokolewa.

8. Mtume Paulo anafananisha yale makabila 12 ya Israeli wa kiroho na nini kuhusiana na mti, na katika njia ya mfano, sehemu kuu za “mti” huo zilifananisha nini?

8 Katika Warumi sura ya 11, mtume Paulo anafananisha hayo makabila 12 ya Israeli wa kiroho na matawi ya mzeituni wa bustanini. Shina la mzeituni huo wa mfano lilifananisha mzee wa ukoo Ibrahimu, babu ya taifa la Israeli kwa habari ya mwili. Mti wenyewe ulifananisha wale wazee wengine wa ukoo waliofuata, Isaka Yakobo na wale wazee wa ukoo 12 walio kama vichwa vya yale makabila 12 ya taifa la asili la Israeli. (Matendo 7:8) Matawi yaliyokua kutokana na mti huo yalifananisha washiriki Wayahudi wa yale makabila 12 ya taifa la asili, la Israeli lenye kutahiriwa. Kwa wazi wao walikuwa warithi wa ahadi aliyopewa Ibrahimu kuhusiana na “uzao” ambao katika huo mataifa yote ya dunia yangejibarikia kwa habari ya kupata uzima wa milele. Kwa sababu hiyo Wayahudi wa asili wenye kutahiriwa ndio waliokuwa na nafasi ya kwanza ya kufanyiza huo ‘uzao wa Ibrahimu.’

9. Kwa asili, “matawi” hayo ya mfano yalikuwa nini, na kwa hiyo, ni nani aliyekuwa “shina” halisi, na ni nani aliyekuwa mti wenyewe?

9 Sasa twajua kwamba “uzao” huo ni wa kiroho, uzao unaozaliwa na Yehova Mungu ili uwe wana wake wa kiroho. Yeye ndiye aliyekuwa “shina” halisi la mzeituni huo wa kiroho. Mwanawe, Yesu Kristo, ndiye aliyekuwa mshiriki mkuu na wa maana wa “uzao” huo wa Yehova Mungu, Ibrahimu Mkuu Zaidi, na kwa hiyo Yesu Kristo alifananishwa na mti wenyewe wa mzeituni huo wa mfano. Kwa hiyo, “matawi” katika mti wa namna hiyo yangefananisha wanafunzi waaminifu waliopata kuwa warithi washirika pamoja naye wakiwa washiriki wadogo wa ule ‘uzao wa Ibrahimu’ wa kiroho. Kwa hiyo, basi, je! “matawi” hayo yalikuwa yasiyo na hesabu isiyo na kikomo?

10. Katika Warumi 11:​11-32, Paulo anaonyeshaje kwamba kungekuwako tu hesabu yenye kikomo ya “matawi” katika mzeituni huo wa mfano?

10 Mtume Paulo anaonyesha kwamba kungekuwako hesabu yenye kikomo ya “matawi” katika mzeituni huo wa kiroho. Namna gani hivyo? Kwa sababu yeye anataja kwamba wakati tawi mojalapo matawi ya asili linapokatwa, tawi jingine la asili halingekuwa mahali hapo katika mti huo. Badala yake, tawi kutoka katika mzeituni wa mwituni lingepandikizwa mahali pake. Kwa hiyo tawi hilo la mzeituni mwitu lililopandikizwa katika mti huo halingeongeza hesabu ya matawi katika mti huo. Hesabu ya matawi katika mti huo ingeendelea kuwa ile ile. Hivyo, wakati Waisraeli wa asili wenye kutahiriwa walipokatwa kutoka katika mti huo wa kiroho kwa kutomwamini na kumkataa Yesu Kristo akiwa Uzao Mkuu wa Ibrahimu Mkuu Zaidi, ndipo wale wasio Wayahudi au watu wa Mataifa walipopandikizwa mahali pa hayo “matawi” ya asili yaliyokatwa.​—Rum. 11:​11-32.

11. Katika Wagalatia 3:​26-29, Paulo anaonyeshaje kwamba wale waliomo katika zizi la Israeli wa kiroho hawangehesabiwa kuwa kama Wayahudi na Mataifa?

11 Kwa kufaa, basi, matawi hayo yaliyo katika mti wa Agano la Ibrahimu hayapaswi kuonwa kuwa Wayahudi wa asili na Mataifa wageni. Wote wapaswa kuonwa kuwa Israeli wa kiroho. Mtume Paulo ndiye anayetaja jambo hilo. Baada ya kuzungumza juu ya ahadi aliyopewa Ibrahimu na uzao wa Ibrahimu, yeye anaendelea kusema hivi: “Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. Hapana Myahudi wala [Mgiriki]. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.”​—Gal. 3:8, 16, 26-29.

12-14. (a) Katika Wagalatia 4:21-31, Paulo anawaelekeza Wakristo hao Wagalatia kwa nani akiwa mama yao wa kiroho? (b) Hivyo, je! Paulo anakazia hali yo yote ya Kiyahudi katika hilo ‘’kundi dogo” lililomo katika “zizi hili”?

12 Mtume Paulo aliandika barua hiyo kwa Wagalatia yapata miaka ya 50-52 W.K. Hiyo ilikuwa angaa miaka 17 baada ya Yehova kulitundika lile agano la Torati penye mti ambao katika huo Mwanawe Yesu Kristo alikuwa ametundikwa. Hata hivyo kulikuwako Wakristo fulani katika makundi ya Galatia waliotaka kujitia katika utumwa wa Sheria ya agano hilo la Torati lililopatanishwa na Musa katika Mlima Sinai Uarabuni. Katika kufanya hivyo walikuwa wakitaka kufuatana na Wayahudi waliokuwa wakipinga Ukristo walioshikamana na Yerusalemu wa kidunia na hekalu lenye kuonekana lililokuwa limejengwa hapo na Mfalme Herode Mkuu aliyejaribu kumfanya mtoto Yesu auawe. Yerusalemu huo ulikuwa umefananishwa na Hagar, kijakazi wa Ibrahimu nao ulikuwa kama mama kwa Wayahudi ambao walikuwa bado wanataka kuendelea katika utumwa wa torati ya Musa badala ya kumkubali Yesu Kristo akiwa Musa Mkuu Zaidi. Kwa hiyo, kuhusiana na jambo hilo, Paulo aliandika hivi:

13 “Lakini Yerusalemu ya juu mbinguni ni mji ulio huru, nao ni mama yetu. . . . Sasa, basi, ndugu zangu, ninyi ni watoto wa Mungu kutokana na ahadi yake, kama alivyokuwa Izaka. . . . Kwa hiyo, basi, ndugu, sisi si watoto wa mtumwa bali wa mama huru. Kristo alitupa uhuru akataka tubaki huru. Basi, simameni imara wala msikubali tena kuwa chini ya nira ya utumwa.”​—Gal. 4:21 mpaka 5:1, HNWW.

14 Isaka, mwana wa Ibrahimu, hakuwa Myahudi au Mwisraeli. Yeye, akiwa mwana wa Sara, mwanamke huru wa Ibrahimu, ndiye aliyekuwa baba ya Yakobo, aliyepewa jina Israeli na ambaye alipata kuwa baba ya Yuda. Wakristo waliomo katika lile “kundi dogo” katika “zizi hili” la Mchungaji Mwema Yesu Kristo wako kama Isaka kwa kuwa wao ni warithi wa ahadi aliyopewa Ibrahimu. Yerusalemu wa kimbinguni ndio mama yao wa kiroho, uliofananishwa na Sara mama ya Isaka Mwebrania, si Myahudi.

15, 16. Katika Yohana 10:16-18, je! Yesu anasema kwamba inampasa kuwaleta “kondoo wengine” kwenye “zizi” moja ili wawe na “mchungaji mmoja”?

15 Baada ya kuzungumza juu ya “zizi la kondoo” ambamo wanapatikana wale washiriki wa ‘uzao wa Ibrahimu’ wenye washiriki wengi, Yesu anaelekea upande mwingine aendeleapo kusema: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; nao hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja. Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.”​—Yohana 10:16-18.

16 Twaona kwamba Yesu hasemi kwamba ‘inampasa kuwaleta’ hao “kondoo wengine” katika “zizi hili.” Badala yake, yeye anasema kwamba “kutakuwako kundi moja,” kwa kuwa kutakuwako na yule “mchungaji mmoja” tu.

17. Ni jambo gani linaloweza kusemwa kwa sababu ya uhakika wa kwamba Yesu anazungumza juu ya “zizi hili” na kuendelea kwa utaratibu na bila kukatiza na mazungumzo juu ya “kondoo wengine,” lakini je! kwa lazima hilo linakuwa kweli?

17 Basi, kwa sababu Yesu anaingia kwa utaratibu sana kutoka mazungumzo yake juu ya “zizi hili” kwenye yale ya “kondoo wengine,” huenda msomaji akafikiri kwamba matendo hayo mawili yanafuatana upesi upesi, pasipo muda mrefu kupita kama vile karne nyingi za wakati. Vilevile, kwa sababu kama hiyo lazima Yesu awe anataja juu ya kuwaleta kwenye “zizi hili” wale watu wasio Wayahudi, watu wa Mataifa, kulingana na historia ya kupanuliwa kwa kundi la Kikristo katika siku za mitume. Kwa hiyo huenda mtu akakata maneno kwamba hapa Yesu hakuwa akitoa unabii wenye kufika mbali wa jambo litakalotukia wakati ujao ulio mbali. Walakini si lazima uamuzi wa namna hiyo uwe ndio sahihi. Hautofautishi kati ya “zizi hili” na “kundi moja.”​—Linganisha Ufunuo 7:8, 9.

18. Je! Yesu alikuwa na uwezo wa kutoa unabii wenye kufika wakati ujao ulio mbali, nako kubarikiwa kwa jamii zote za dunia walipaswa wangojee jambo gani lililopaswa kutukia kwanza?

18 Yesu alikuwa na kipawa cha kuweza kutoa njozi ya kiunabii na kwa hiyo aliweza kutoa mfano wake wa kondoo na mbuzi ijapokuwa ungetimizwa miaka 1,900 baadaye. Yeye ndiye aliyekuwa mshiriki mkuu wa ‘uzao wa Ibrahimu’ ulioahidiwa na kwa hiyo yeye alipendezwa sana kuona jamaa zote za mataifa ya kibinadamu zikiokolewa kwa kujibarikia milele kupitia kwa uzao huo. Baraka hiyo ilipaswa ingojee kukamilishwa kwa ule ‘uzao wa Ibrahimu’ wenye washiriki wengi 144,000 wakiwa chini yake. Jambo hilo lingechukua muda wa karne 19, kama vile mambo ya hakika ya historia yameonyesha. Ni kweli kwamba, hao wanaojibarikia wenyewe wangekuwa watu wa mfano wa kondoo kutoka katika jamaa za mataifa yote. Lakini wangekuwa “kondoo wengine,” kwa kuwa wao si wa “zizi hili” la warithi wa ahadi aliyopewa Ibrahimu. Kwa hiyo wao hawangekuwa Waisraeli wa kiroho, bali, kwa kulinganisha, wangekuwa watu wa Mataifa.

19. Kwa sababu ya yale yanayotangulia kutajwa katika Ufunuo, sura ya 7, ni nani walio washiriki wa “mkutano mkubwa” unaoelezwa katika Ufunuo 7:​9-17?

19 Kupatana kabisa na jambo hilo ni uhakika wa kwamba, baada ya mtume Yohana kuona yale makabila 12 ya Waisraeli wa kiroho yakitiwa muhuri, kama vile inavyoelezewa katika Ufunuo 7:​1-8, aliona ile njozi ya ule “mkutano mkubwa” usio na hesabu wa wale wasio Waisraeli wa kiroho na kwa hiyo ni wa wale “kondoo wengine.” Wao walionekana wakiwa wamesimama mbele ya kiti cha enzi cha kimungu nao walikuwa wakisema hivi: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.” Hao wanasemekana kuwa wanaokoka “ile dhiki iliyo kuu,” na kuanza kumtolea Yehova Mungu utumishi mtakatifu katika hekalu lake mchana na usiku. “Mchungaji mwema” anawapa hao “kondoo wengine” uangalizi wa upendo, kwa kuwa twasoma hivi: “Huyo Mwana-Kondoo . . . atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai.”​—Ufu. 7:9-17.

20. Ni wakati gani na mahali gani utimizo wa njozi ya “mkutano mkubwa” ilipoanza kutimizwa, kukiwako wonyesho gani?

20 Kupatana na utaratibu huo wa mambo kama vile unaovyoonyeshwa katika Ufunuo, sura ya 7, ilikuwa wakati wa masika ya mwaka 1935, miaka 20 tangu uanze “mwisho wa taratibu ya mambo” ulioanza katika mwaka 1914, kwamba maelezo juu ya njozi ya Ufunuo ya “mkutano mkubwa” yalitolewa. Jambo hilo lilitukia katika Mei 31, 1935, katika kusanyiko lililofanywa katika makao makuu ya United States ya Amerika. Wakati” wa pindi hiyo, J. F. Rutherford, aliyekuwa msimamizi wa Sosaiti, alitoa hotuba yake juu ya kichwa “Mkutano Mkubwa,” naye akaeleza namna ambavyo, jamii hiyo isivyokuwa jamii ya pili ya kimbinguni, bali ilikuwa jamii ya kidunia, wale “kondoo wengine” wa yule “mchungaji mwema.” Baadaye habari hiyo ilichapwa katika kurasa za gazeti la Mnara wa Mlinzi (Kiingereza). Ndipo kwa hakika “mchungaji mwema” alipoanza kuwaleta “kondoo wengine” wake nao wakaanza kusikia sauti yake na kumfuata, kwa kuwa katika siku iliyofuata maelezo hayo ya Ufunuo 7:​9-15 kulikuwako 840 walioonyesha wakf wao kwa Mungu kupitia kwa Kristo kwa ubatizo wa maji. Idadi kubwa ya hao ilionekana kuwa ya huo “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo.

21. (a) Kwa hiyo, licha ya lile “kundi dogo,” “mchungaji mwema” aliutoa uhai wake kwa ajili ya nani wengine? (b) Mchungaji huyo aliutwaaje uhai wake tena, nao huo ulikuwa wonyesho wa upendo wa nani?

21 “Mchungaji mwema” aliitoa “nafasi” yake kwa ajili ya hao “kondoo wengine” vilevile ambao si wa “zizi” la warithi wa ile ahadi aliyopewa Ibrahimu. Mtume Yohana, aliyekuwa mmoja wa ile jamii ya “uzao” wa Ibrahimu aliandika hivi: “Naye [Yesu Kristo] ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” (1 Yohana 2:1, 2) Yehova Mungu, Baba wa kimbinguni, alimpenda Mwanawe kwa kufanya jambo hilo. Kwa kuthamini jambo hilo, Yesu, yule “mchungaji mwema,” alisema hivi mbele ya wale waliomchukia kati ya Wayahudi: “Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.” (Yohana 10:17) Baba alionyesha upendo wake kwa huyo “mchungaji mwema” mwenye kujinyima kwa kumfufua kutoka kwa wafu katika siku ya tatu. Kwa njia hiyo Mwana wa Mungu akaipokea tena “nafsi” yake, walakini katika uzima wa kimbinguni.

22. Yajapokuwapo majaribio ya kuutwaa uhai wake, ni kwa sababu gani hakuna mwanadamu aliyeutwaa uhai wa Yesu wa kibinadamu, kufikia wakati aliposema maneno yaliyoandikwa katika Yohana 10:⁠18?

22 Kufikia wakati ambapo Yesu alizungumza juu ya “kondoo wengine” majaribio yalikuwa yamefanywa ya kumwua huyo “mchungaji mwema.” Walakini yeye hakuwa amefanya hata kidogo jambo ambalo lingemstahilisha kuuawa na wanadamu. Hiyo inaonyesha sababu gani akasema: “Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.”​—Yohana 10:⁠18.

23. Yesu aliutoa uhai wake wa kibinadamu kwa kupenda kwake mwenyewe wakati gani, na kwa sababu gani?

23 Miezi michache baadaye ukweli wa usemi huo ulitolewa. Katika usiku wa kusalitiwa kwake katika bustani ya Gethsemane, wakati mwanafunzi wake Petro alipojaribu kumlinda kwa upanga, Yesu alisema hivi: “Wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo [inavyopaswa kuwa]?” (Mt. 26:53, 54) Hivyo, baada ya kuwaachilia mitume wake wakimbie na kumwacha, Yesu alijitoa kwa kupenda kwake mwenyewe kwa kikundi cha watu kilichokuja kumkamata na kufanya jaribio la mwisho la kumfanya auawe. Kwa kufanya hivyo, Yesu hakuwa akitupa uhai wake.

24. Yesu alipokea kwa Baba yake mamlaka gani kamili kuhusiana na uhai wake, nalo jaribio la mwisho la kumzuia asitumie mamlaka hiyo lilishindwaje?

24 Yesu alikuwa na mamlaka kutoka kwa Baba yake wa kimbinguni ya kufuata mwendo huo, lakini aliachwa afanye hivyo kwa hiari yake. Mamlaka yake ya kuutwaa uhai wake tena kupitia kwa ufufuo ilitegemea nia yake ya kujitoa. Kwa sababu aliutoa uhai wake mpaka kufa, Baba yake wa kimbinguni alimpa mamlaka ya kuutwaa tena kutoka kwa Yeye peke yake awezaye kumwinua kutoka kwa wafu. Hakuna uweza mbinguni au duniani ambao ungeweza kuzuia mamlaka hiyo ya Yesu ya kuipokea tena “nafsi” yake, au uhai. Hivyo, muhuri wa liwali uliowekwa kwenye lile jiwe kubwa lililofunga njia ya kuingia kwenye kaburi alimozikwa baada ya kifo chake penye mti, haukuweza kumzuia Yesu asitumie mamlaka yake aliyopewa na Mungu katika siku ya tatu. Wala askari walinzi waliowekwa kaburini wawazuie wanafunzi wake wasiibe mwili uliokufa hawakuweza kumzuia.​—Mt. 27:62 mpaka 28:15.

25. Kwa kuwa Yesu hakuupoteza uhai wake wa kibinadamu kwa sababu ya kumwasi Mungu, aliupata ili aweze kuutumiaje kwa ajili ya wanadamu?

25 Kwa kweli, Yesu aliagizwa na Baba yake wa kimbinguni afanye hayo yote. Kwa hiyo, katika siku ya tatu ya kufa kwake, Yehova Mungu alitoa amri kwamba Mwanawe mtiifu ainuke kutoka kwa wafu na kupokea uhai tena, katika makao ya kiroho awe pamoja na Baba yake wa kimbinguni. Kwa kuwa hakuwa ameupoteza uhai wake kwa kutokumtii Mungu, alipokea vilevile haki na wenyeji wa uhai mkamilifu wa kibinadamu ili avitoe kwa Yehova Mungu katika hekalu lake la kimbinguni na kupatanisha dhambi ya ulimwengu wote.

26. (a) Hivyo, jamaa zote za dunia zilifunguliwa njia zifanye nini? (b) Sana sana, ni wakati gani “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Yesu walipoanza kujibarikia?

26 Hivyo, jamaa zote za mataifa ya ulimwengu zilifunguliwa njia ili ‘wajibarikie’ kupitia kwa Aliye Mkuu wa ‘uzao wa Ibrahimu.’ (Mwa. 12:1-3; 22:15-18) Ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa “Mchungaji Mwema” walianza ‘kujibarikia’ kupitia kwake walipojiweka wakf kwa Yehova Mungu kupitia kwake na kuonyesha wakf huo kwa ubatizo wa maji. Kisha waliisikiliza sauti ya Mchungaji Mwema na kumfuata, pamoja na mabaki watiwa mafuta wa uzao wa Ibrahimu. Mwanzo huo ulitukia sana sana katika kusanyiko la Washington (D.C.) la mwaka 1935. Tangu wakati huo mabaki watiwa mafuta wamewakaribisha “kondoo wengine” wote, na, kama alivyotabiri Yesu, limepata kuwapo “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja.”

27. Ni nani wengine licha ya “mkutano mkubwa” unaookoka “dhiki ile iliyo kuu” watakaokuwa sehemu ya “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema, na wakati gani?

27 Wakati wa utawala wa ile miaka elfu wa huyo “mchungaji mmoja,” Yesu Kristo aliyetawazwa, wafu wote wa wanadamu waliokombolewa watafufuliwa kutoka katika usingizi wao wa kifo nao watakuwa na nafasi ya ‘kujibarikia’ kwa kuwa sehemu ya “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema. Hiyo itatia ndani yule aliyekuwa “bawabu” hapo kwanza wa lile “zizi la kondoo” lililofananisha ule mpango wa Agano la Ibrahimu, yaani, Yohana Mbatizaji. (Yohana 10:1-3) Yesu atawaongoza wenye kutii kwenye “chemchemi za maji yenye uhai.” Ule “mkutano mkubwa” wa wale watakaookoka “dhiki ile iliyo kuu” inayokuja watakuwa baraka kwa mabilioni wenye kufufuliwa ili wajifaidi na hizo “chemchemi za maji yenye uhai.” (Ufu. 7:9-17) Wote wenye mfano wa kondoo wataweza kujiunga na “mkutano mkubwa” katika kusema: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.”​—Ufu. 7:10; 20:11-14.

—Kutoka The Watchtower July 15, 1980.

[Mchoro katika ukurasa wa 19]

(Ona mpangalio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Mpango wa Yehova kwa Ajili ya “Kondoo” Wake

(1) “Mchungaji mwema”: Yesu Kristo, anayeutoa uhai wake kwa ajili ya “kondoo”

(2) “Bawabu”: Yohana Mbatizaji, anayemjulisha “mchungaji” kwa “kondoo”

(3) “Zizi la kondoo”: Zizi la Ufalme la mpango wa Agano la Ibrahimu

(4) “Kondoo” waliomo katika zizi hili: “Kundi dogo,” kutoka kwa Wayahudi na Mataifa

(5) “Mlango wa kondoo”: Yesu

(6) “Mgeni,” “mwivi,” “mtu wa mshahara”: Waasi imani na wachungaji wa uongo

(7) “Kondoo wengine”: “Mkutano mkubwa” na wengine wanaorithi makao ya kidunia ya Ufalme

(Angalia pia “Mwara wa Mlinzi” (Kingereza) wa Mei 15, 1946, kur. 147-158)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki