Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 2/1 kur. 19-24
  • Utumishi Mtakatifu Katika Huu “Wakati wa Mwisho”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utumishi Mtakatifu Katika Huu “Wakati wa Mwisho”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NAMNA UNAVYOTOLEWA NA WAKATI GANI
  • Kutoa Utumishi Mtakatifu Usiku na Mchana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kuona Ubora wa Hazina ya Utumishi Mtakatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Wakristo Hupata Furaha Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kutoa Utumishi Mtakatifu Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 2/1 kur. 19-24

Utumishi Mtakatifu Katika Huu “Wakati wa Mwisho”

1.Tunajuaje kwamba tunaishi katika “wakati wa mwisho,” nalo andiko la Danieli 12:4 lasema nini juu yake?

KWA MSAADA wa unabii wa Biblia uliofunuliwa yatupasa tuone kwa urahisi kwamba tunaishi katika ule “wakati wa mwisho” uliotabiriwa. Kuhusiana na wakati huu wa hatari, unabii wa Danieli 12:4 wasema hivi: “Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno, na kukitia muhuri kitabu hicho, hata mpaka wakati wa mwisho; wengi watapiga mbio huku na huku, na maarifa yataongezeka.” (The Jewish Publication Society of America; Leeser) Tafsiri ya Septuagint ya Kigiriki yasomeka hivi: “Na wewe, Danieli, funga maneno hayo, na kutia kitabu hicho muhuri mpaka wakati wa mwisho; mpaka wengi wafundishwe, na maarifa kuongezeka.” (Bagster; Thomson; Vulgate ya Kilatini; Holy Bible from Ancient Eastern Manuscripts ya Lamsa) Ule “mkutano mkubwa” ambao umeelezwa katika kitabu cha mwisho cha Biblia umefaidika na hayo maarifa na ufahamu wa Biblia ulioongezeka.—Ufu. 7:9-17.

2. (a) Ni kwa sababu gani njia ambayo katika hiyo “mkutano mkubwa” watoa “utumishi mtakatifu” ni jambo la maana? (b) Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “kutumikia” linatofautianaje na neno linalotafsiriwa “utumishi mtakatifu”?

2 Tangu huu “mkutano mkubwa” uanze kukusanywa katika mwaka 1935 W.K., umekuwa ‘ukitoa . . . utumishi mtakatifu’ kwa Yehova Mungu. Namna unavyofanya hivyo ni jambo la maana sana. Kwa sababu gani? Kwa sababu katika usiku wa mwisho wa Yesu Kristo kuwa pamoja na mitume wake 11 waaminifu aliwaambia hivi: “Mimi nimesema nanyi mambo haya ili msikwazwe. Watu watawafukuza ninyi kutoka sinagogi. Kwa kweli, saa yaja wakati kila awauaye atafikiri amemtolea Mungu utumishi mtakatifu.” (Yohana 16:1, 2, NW) Badala ya “utumishi mtakatifu,” The Jerusalem Bible inasema “wajibu mtakatifu”; The Emphasised Bible ya Rotherham inasema “utumishi wa kimungu”; The New English Bible yasema “wajibu wa kidini.” Neno la Kigiriki cha asili linalotafsiriwa hivyo ni la·treiʹa. Namna ya kiarifa ya neno hilo la jina la Kigiriki ni la·treuʹein. Linatofautiana na neno la kiarifa cha Kigiriki di·a·ko·neinʹ, linalomaanisha “kuhudumu” ambalo latumiwa hata katika mambo ya vivi hivi, ya kawaida tu, mambo yasiyo matakatifu, kama vile katika Mathayo 8:15.

3. Ni kwa sababu gani Wayahudi walioshikamana na agano la Torati walifikiri kwamba hawangekuwa wakikosea kwa kumwua Yesu na kuwatesa wanafunzi wake?

3 Wakati mmoja Sauli wa Tarso, Asia Ndogo, alikuwa Myahudi aliyeongozwa vibaya na ambaye aliwatesa Wakristo mpaka alipogeuka kuwa Mkristo. Yeye alisema kuhusu Wayahudi wenzake “ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu [utumishi mtakatifu (la·treiʹa), NW], na ahadi zake; ambao mababu [Ibrahimu, Isaka na Yakobo] ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili.” (Rum. 9:4, 5) Kwa kuwa walishikamana na huo “utumishi mtakatifu” kama vile ulivyoonyeshwa katika agano la Torati, Wayahudi wasioamini walidhani kwamba hawangeweza kuwa wamekosea kwa kumtundika Yesu Kristo na kwa kuwatesa wanafunzi wake na hata kuwaua.

4. Paulo anausemaje utumishi wa makuhani katika vyumba vya hema, nao utendaji huo ulifananisha nini?

4 Kwa muda agano hilo la Torati lilipokuwa likitenda kazi, huo “utumishi mtakatifu” chini yalo ulikuwa na mahali pake, nao ulikubalika kwa Mungu. Kwa hiyo Paulo anautukuza asemapo: “Basi hata agano la kwanza lilikuwa na kawaida za ibada [utumishi mtakatifu (la·treiʹa), NW], na patakatifu pake, pa kidunia. Maana hema ilitengenezwa, ile ya kwanza mlimokuwa na kinara cha taa, na meza, na mikate ya Wonyesho; ndipo palipoitwa, Patakatifu. Na nyuma ya pazia la pili, ile hema iitwayo Patakatifu pa patakatifu. . . . Basi vitu hivi vikiisha kutengenezwa hivyo, makuhani huingia katika hema hiyo ya kwanza daima, wakiyatimiza mambo ya ibada [wakitoa utumishi mtakatifu (la·treiʹa), NW].” (Ebr. 9:1-6) Huo utumishi mtakatifu wa kisherehe ulihusiana na dhabihu zilizotolewa kwa ajili ya taifa la Israeli. Haukuhusu mambo ya watu ya kila siku. Kama vile mtume Paulo anavyoonyesha, “utumishi mtakatifu” huo wote chini ya agano la Torati ulikuwa wa mfano, ukifananisha mambo ya Kikristo.

5. Yale ambayo Paulo anawaambia Wakristo wafanye katika Warumi 12:1, je! ni jambo la kawaida, naye anayaitaje?

5 Kupatana na hilo, Paulo alisema hivi katika barua yake kwa Wakristo katika Rumi: “Kwa hiyo nawasihi kwa huruma za Mungu, ndugu, mtoe miili yenu dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu [la·treiʹa] pamoja na nguvu yenu ya akili. Na mwache kufanyizwa kulingana na mtindo wa taratibu hii ya mambo.” (Rum. 12:1, 2, NW) Kwa hiyo kufanya kwao jambo linalokuwa kama dhabihu, la kujinyima, lingekuwa jambo lisilo la kawaida, jambo ambalo kwa kawaida halifanywi na watu wasio Wakristo wa taratibu hii ya mambo ya kilimwengu.

6. Kwa kuingia katika agano la Torati kupitia kwa Musa, Waisraeli walijitia chini ya wajibu wa kufanya nini kwa Mungu, naye mfia-imani Stefano alisema nini juu ya jambo hilo?

6 Baada ya taifa la Israeli kukombolewa na nyumba ya utumwa katika Misri ya kale, walipewa namna ya utumishi mtakatifu wenye utaratibu wa kumtolea Mungu. Ni kama vile mfia-imani Mkristo Stefano alivyosema: “Na lile taifa watakaowafanya watumwa nitawahukumu mimi, alisema Mungu; na baada ya hayo watatoka, nao wataniabudu [watanitolea utumishi mtakatifu (la·treuʹein) NW] mahali hapa.” (Matendo 7:7) Kwa kuingia kwenye agano la Torati pamoja na Yehova Mungu kupitia kwa Musa akiwa mpatanishi wao, Waisraeli walijitia chini ya wajibu wa kumtolea Yeye utumishi mtakatifu. Baadaye wengi wa Waisraeli hao waliokuwa katika agano walichagua kuabudu miungu wengine. “Basi,” kama vile alivyoendelea kusema Stefano, “Mungu akaghairi, akawaacha ili waliabudu [walitolee utumishi mtakatifu (la·treuʹein), NW] jeshi la mbinguni, kama ilivyoandikwa katika chuo cha manabii, Je! mlinitolea mimi dhabihu na sadaka miaka arobaini katika jangwa, enyi nyumba ya Israeli?”—Matendo 7:42.

7. (a) Ili Wayahudi wafikie kwenye utimizo wa ahadi za Mungu, Paulo alisema kwamba walikuwa wakimtolea nini? (b) Kulingana na kile ambacho Wayahudi waliita madhehebu, mtume Paulo alikuwa akifanya nini kwa Mungu wa babu zake?

7 Ilikuwa miaka mingi baada ya Yehova Mungu kufuta agano lake la Torati pamoja na nyumba ya Israeli ya asili kwamba mtume Paulo alisema hivi katika kesi iliyosikilizwa na Mfalme Agripa katika Kaisaria: “Ahadi hiyo ndiyo ile ile inayotumainiwa na makabila kumi na mawili ya taifa letu, wakimtumikia [wakimtolea Mungu utumishi mtakatifu (la·treuʹein), NW] Mungu kwa [bidii] mchana usiku. Mheshimiwa Mfalme, Wayahudi wananishtaki kwa sababu ya tumaini hilo!” (Matendo 26:7, HNWW) Kwa sababu ya shtaka hilo Paulo aliweza kumwambia Feliki liwali Mrumi hivi mbele ya Wayahudi washtaki: “Ila neno hili naungama kwako ya kwamba kwa Njia ile ambayo waiita uzushi [madhehebu, NW], ndivyo ninavyomwabudu [ninavyomtolea utumishi mtakatifu (la·treuʹein), NW] Mungu wa baba zetu, nikiyaamini yote yanayopatana na torati na yaliyoandikwa katika vyuo vya manabii.”—Matendo 24:14; 28:22.

8. (a) Ni nini “madhehebu” hiyo ambayo kupatana nayo hata “mkutano mkubwa” wa leo wamwabudu Yehova? (b) Ni kwa sababu gani kuna hatari kubwa ya kutoa “utumishi mtakatifu” ulioongozwa vibaya, naye mtume Paulo alisema ni nini ulinzi wetu salama?

8 Iliyokuwa ikiitwa “madhehebu” ya uzushi ambayo kupatana na hiyo Paulo alikuwa akimwabudu Yehova kama Mungu ulikuwa Ukristo. (Matendo 11:26; 1 Pet. 4:16) Leo wale wa “mkutano mkubwa” wanakubali mbele ya watu wote kwamba wao ni mashahidi Wakristo wa Yehova, na kwa sababu hiyo ni lazima wawe waangalifu sana kuhusu namna wanavyojaribu kumtumikia Yehova katika njia takatifu. Tangu “wakati wa mwisho” uanze mwishoni mwa “majira ya Mataifa” katika mwaka 1914, miungu ya uongo na mabwana wa uongo wameongezeka. (Luka 21:24) Hata karne 19 zilizopita mtume Paulo aliona lazima ya kuwakumbusha hivi “Wakristo” katika mji mkuu wa Milki ya Kirumi: Waasi imani Wayahudi “waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu [kukitolea utumishi mtakatifu (la·treuʹein), NW] badala ya Muumba.” (Rum. 1:25) Alionyesha ni nini kilichokuwa kwake ulinzi salama juu ya utumishi mtakatifu ulioongozwa vibaya, aliposema: “Ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi; lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake; yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na sisi kwa yeye huyo.”—1 Kor. 8:5, 6.

NAMNA UNAVYOTOLEWA NA WAKATI GANI

9. Ni wakati gani ambapo jitihada za kumtolea Mungu “utumishi mtakatifu” kulingana na agano la Torati ya Musa zilipokuwa hazifai, na kwa sababu gani?

9 Kwa muda wa miaka 1,545 wakati ambapo agano la Torati lilipokuwa likitenda kazi katika taifa la Kiyahudi, kuanzia mwaka 1513 K.W.K. mpaka 33 W.K., Wayahudi waaminifu walimtolea Yehova Mungu kile kilichokuwa “utumishi mtakatifu” uliokubalika kwake. Lakini wakati agano hilo la Torati lilipoacha kufanya kazi wakati ambapo Yesu Kristo aliyetukuzwa alipopatanisha lile agano jipya mbinguni katika mwaka 33 W.K., agano la Torati ya Musa halikuwa tena njia ya kutolea utumishi mtakatifu anaoukubali Yehova, Mungu wa hilo agano jipya. (Ebr. 8:10-13) Ili utumishi wao wa kidini ukubaliwe na Yehova Mungu, iliwapasa Wayahudi wautoe kupitia kwa Mpatanishi aliye mkuu kuliko Musa, Yesu Kristo Mwana wa Mungu, aliye ‘uzao wa Ibrahimu.’ (Gal. 3:16) Jambo hilo lilipata kutajwa katika siku hiyo ya masika katika mwaka 2 K.W.K. wakati Zekaria kuhani Myahudi alipotangaza kwamba mwanawe wa umri wa siku nane apaswa kuitwa Yohana.

10. (a) Katika siku hiyo ya kumtahiri mwanawe, Zekaria alisema kwamba ni kusudi la Mungu kwamba watu Wake Wamtolee nini baada ya kukombolewa na adui zao? (b) Kwa ajili ya agano hilo lililofungamanishwa na kiapo, Yohana alikuja kuwa mtangulizi wa nani?

10 Kisha Zekaria aliyeongozwa na roho alisema juu ya kusudi la Mungu la “kuwatendea rehema baba zetu, na kulikumbuka agano lake takatifu; uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu, ya kwamba atatujalia sisi, tuokoke mikononi mwa adui zetu, na kumwabudu [kumtolea utumishi mtakatifu (la·treuʹein), NW] pasipo hofu, kwa utakatifu na kwa haki mbele zake siku zetu zote.” (Luka 1:59-75) Yohana mwana wa Zekaria alipata kuwa mtangulizi wa Yesu Kristo, aliyetumiwa na Mungu katika kutimiza agano alilofanya na Ibrahimu, akalithibitisha kwa kiapo kisichoweza kuvunjwa.—Mwa. 12:3; 22:15-18; Gal. 3:8, 16; Ebr. 6:13-17.

11. (a) “Mkutano mkubwa” unajitahidi kumtolea Mungu “utumishi mtakatifu” wapi leo? (b) 1 Wakorintho 10:31 linatokeza ulizo gani kuhusiana na huo “mkutano mkubwa”?

11 Kama watu waliokwisha barikiwa kupitia kwa agano la Ibrahimu, wale wa “mkutano mkubwa” wanajikuta wakiwa katika nyua za kidunia za “hekalu” la kiroho la Yehova nao wanatafuta kutoa utumishi mtakatifu pasipo hofu kwa Mungu wa Ibrahimu. Lakini namna gani? Ni kweli, maneno ya mtume Paulo katika 1 Wakorintho 10: 31 yanawapasa wale wa “mkutano mkubwa” pamoja na mabaki ya Waisraeli wa kiroho 144,000, yaani: “Mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”

12. Kwa sababu sisi tuna maono yaliyo tofauti na kwa sababu tunafanya mambo hayo ya kawaida chini ya jina la mashahidi Wakristo wa Yehova, je! kutenda hivyo kwenyewe kunafanya mambo hayo kuwa “utumishi mtakatifu,” au hapana?

12 Je! kwa maneno hayo mtume Paulo anamaanisha kwamba mambo yote tufanyayo sasa kama Wakristo yanakuwa “utumishi mtakatifu” (lat·reiʹa) kwa sababu ya sisi kuwa na maoni yaliyo tofauti juu ya mambo hayo? Sababu gani iwe hivyo? Wakati tunapokula, kunywa na kulala na kufanya mambo mengine ambayo wanadamu wengine wote wanalazimika kufanya ili waishi, kwa kweli tunatumikia nani? Ni sisi wenyewe, bila shaka. Ndiyo, sasa tufanyapo mambo hayo, twaufikiria utukufu wa Mungu. Kwa hiyo, hatuli kupita kiasi kadiri ya kuwa wagonjwa au walafi; hatunywi vileo kupita kiasi na kulewa; hatulali sana kwa kawaida kadiri ya kuwa wavivu. Walakini sasa tulapo, kunywa, na kulala chini ya jina la kidini la mashahidi Wakristo wa Yehova, sawasawa na wanavyofanya wanadamu wote chini ya majina yao ya kidini, je! jambo hilo lenyewe linageuza matendo hayo ya asili na ya lazima ya maisha ya wanadamu na kuwa “utumishi mtakatifu”? Hapana; sababu gani iwe hivyo?

13. Kwa sababu gani inakuwa tofauti wakati mashahidi watiwa mafuta wa Yehova wanapoadhimisha Chakula cha Bwana cha Jioni kila mwaka katika tarehe inayofaa?

13 Bila shaka, wakati mashahidi Wakristo wa Yehova ambao wametiwa mafuta kwa roho yake takatifu wanapoadhimisha Chakula cha Bwana cha Jioni au Chakula cha Jioni kila mwaka, kunakuwa na tofauti. Wakati huo kula kwao mkate usiotiwa chachu na kunywa divai nyekundu katika usiku wa masika wa Nisani 14 ni mambo wanayofanya wakiwa chini ya amri ya Yesu Kristo nayo yanakuwa na maana kubwa aliyoyapa. Kwa hiyo ni sehemu yenye maana sana ya “utumishi mtakatifu” wanaomtolea Mungu washiriki hao wa mwili wa kiroho wa Kristo.—1 Kor. 11:20-26; Mt. 26:26-30; Luka 22:19, 20.

14. Ni kwa sababu gani ni jambo linalofaa kufanya mambo yanayotajwa katika Warumi 13:1-7, na tufanyapo hivyo je! sisi tunatofautiana na raia wengine wa nchi wanaotii sheria?

14 Kwa upande mwingine wakati mashahidi Wakristo wote wa Yehova wafanyapo yale aliyowaagiza mtume Paulo kufanya katika Warumi 13:1-7, wanafanya tu yale wanayotakiwa kufanya raia wengine wote au wageni katika nchi fulani. Kwa kufaa twafanya hivyo kama watu wema na wenye utaratibu, nalo jambo hilo linatuepusha na matata kutokana na “mamlaka iliyo kuu.” Vilevile twafanya hivyo tukiwa na kusudi la juu zaidi, yaani, kuendelea kuwa na dhamiri njema na kuthamini yaliyo manyofu na yenye kufaa. Walakini kutenda kwetu sasa katika njia hiyo chini ya jina la mashahidi Wakristo wa Yehova hakugeuzi mara hiyo mwenendo wetu unaofaa kuwa ule “utumishi mtakatifu” wa Kimaandiko. Raia wengine wote wenye kutii sheria hufanya mambo ayo hayo, hata bila makusudi kama yale yale tunayokuwa nayo. Kwa hiyo tunatofautianaje katika mambo hayo?

15. Tunapovikataa vizuizi vinavyowekwa na wanadamu ili tusimtolee Yehova ibada, na hivyo tufanye yasiyofanywa na raia wengine wote, huo unakuwa utumishi wa namna gani, na kwa sababu gani?

15 Walakini, tuseme wenye mamlaka katika nchi wanatukataza tusiendelee na ibada yetu kama mashahidi Wakristo wa Yehova? Namna gani basi ikiwa sasa tunachukua maneno ya mitume wa Kristo: “Inatupasa kumtii Mungu kama mtawala kuliko wanadamu”? (Matendo 5:29, NW) Kuendelea kwetu kufanya yale ambayo hayafanywi na raia wengine wote, ili tutii yale ambayo Mungu anawaamuru mashahidi wake walio wakf na kubatizwa wafanye, hufanya yale tunayofanya yaendelee kuwa utumishi mtakatifu kwake. Hiyo inakuwa kweli hata ijapokuwa wenye mamlaka na raia wengine wa nchi huenda wakaliona kuwa jambo lililo kinyume cha sheria, na lenye kuvunja sheria.

16. Ni mfano gani wa huu ‘‘utumishi mtakatifu” ulio wa lazima unaotolewa katika Waebrania 10:23-25?

16 Kwa mfano, Neno la Mungu laamuru hivi: “Na tulishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke; maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu; tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.”—Ebr.10:23-25.

17. Ikiwa “mamlaka iliyo kuu” inasema tunafanya vibaya sana kwa sababu tunatii maagizo ya kimungu, je! hali ya kiroho ya mwendo wetu inageuzwa?

17 Bila shaka kutii kwetu kusihi huku kulikoongozwa na Mungu, hata tujapotaabika mikononi mwa wanadamu kwa sababu hiyo, ni utumishi mtakatifu uliotolewa kwa Mtu Aliye Mkuu Zaidi, Yehova Mungu. Acheni “mamlaka iliyo kuu” ya nchi iliyokasirishwa ikitaka, iseme kwa kusisitizia sheria kwamba utumishi huo ni mbaya sana.—2 Tim. 2:8-10.

18. “Tangazo la waziwazi la Tumaini letu” lahusu serikali gani, na hivyo jambo hilo lahusu maneno gani ya Yesu yenye amri?

18 Ungamo au ‘tangazo la waziwazi la tumaini letu’ lahusu ufalme wa Mungu wa Kimasihi utakaotawala kwa baraka ya jamaa zote za dunia. Kwa habari ya hilo ‘tangazo la waziwazi,’ Yesu alisema maneno hayo yenye kuamuru alipokuwa akitabiri juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo”: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho [tel’os] utakapokuja.” (Mt. 24:3, 14, NW) “Ninyi . . . watu watawapelekeni mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu, ili mpate kunishuhudia kwao. Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.”—Marko 13:4, 9, 10, HNWW.

19. Ni nani hasa wanaopaswa kutimiza maneno hayo ya kiunabii, nako kufanya hivyo kwao ni sehemu ya nini?

19 Ni nani watakaotimiza unabii huo ili wathibitishwe kuwa wa kweli? Ni wanafunzi walio wakf na kubatizwa wa Yeye aliyetoa unabii huo, yaani, Yesu Kristo, wale waliopewa unabii huo. Kuona wajibu wao na kushiriki katika utimizo wa unabii huo ni sehemu ya “utumishi mtakatifu” wasioweza kujiepusha nao.

20. Ili kuthibitisha kwamba lazima wanafunzi wake wafanye huu “utumishi mtakatifu.” Yesu alisema nini kwa wanafunzi wake mlimani katika Galilaya, na kwa hiyo wale wanaoishi wakati wa “mwisho wa taratibu ya mambo” lazima wafanye nini?

20 Ili kutia nguvu uhakika wa kwamba wanafunzi wake walipaswa kuufanya huu “utumishi mtakatifu,” Yesu aliyefufuliwa aliwatokea wanafunzi wake wapata 500 mlimani katika “Galilaya ya mataifa” akawaamuru hivi: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi. Na, tazama! mimi nipo pamoja na ninyi siku zote mpaka mwisho [syn·telʹi·a] wa taratibu ya mambo.” (Mt. 28:19, 20, NW; 4:15; 1 Kor. 15:6) Tangu mwisho wa “nyakati za Mataifa” katika mwaka 1914 tumekuwa tukiishi katika “mwisho wa taratibu ya mambo.” Kwa hiyo sisi sote wanafunzi walio wakf na kubatizwa wa Yesu Kristo aliyefufuliwa na kupewa mamlaka kamili, tumeamriwa tuufanye huu “utumishi matakatifu” aliotupa. Mpaka umalizike huu wakati wa “mwisho wa taratibu ya mambo” na lazima tufanye hivyo, pasipo kulegeza mkono kamwe.

21. (a) Wale watakaoruhusiwa kuingia kwenye Yerusalemu Mpya wa kimbinguni watapewa mapendeleo gani? (b) Wale wa “mkutano mkubwa” wanaoendelea kuwa waaminifu mpaka mwisho wa “dhiki ile iliyo kuu,” watapewa mapendeleo gani?

21 Kwa habari ya wale Waisraeli wa kiroho 144,000 wanaokubaliwa kuingia kwenye mji wa kimbinguni, ule Yerusalemu Mpya, inaandikwa hivi: “Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia [watamtolea utumishi mtakatifu (la·treuʹein), NW]; nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.” (Ufu. 22:3, 4) Na kwa habari ya wale waaminifu na watiifu walio washiriki wa lile “kundi kubwa” lisilohesabika, watabarikiwa kwa “wokovu” watoke kwenye “dhiki ile iliyo kuu” itakayoumaliza huu “wakati wa mwisho,” na wakiwa chini ya utawala ule wa miaka elfu wa Mwana-Kondoo wa Mungu wataendelea “kumtolea [Mungu] utumishi mtakatifu” katika nyua za kidunia za hekalu lake la kiroho. “Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”—Ufu, 7:9-17, NW.

—Kutoka The Watchtower Aug. 15, 1980.

[Picha katika ukurasa wa 21]

Kwa Wayahudi, utumishi mtakatifu ulihusiana sikuzote na ibada katika kulitii agano la Torati

[Picha katika ukurasa wa 22]

“Utumishi mtakatifu” unatia ndani kumtii Mungu chini ya mateso, kufanya tangazo la waziwazi la tumaini letu, kufundisha na kufanya wanafunzi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki