Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 3/1 kur. 4-10
  • Wazazi Wasio na Wenzi Wanashinda na Matatizo ya Ulimwengu wa Leo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazazi Wasio na Wenzi Wanashinda na Matatizo ya Ulimwengu wa Leo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UKRISTO WALETA FARAJA
  • KUSHINDANA NA UPWEKE
  • KUSHINDANA NA TAMAA ZA NGONO.
  • KUTUNZA NYUMBA NA KULEA WATOTO
  • SULUHISHO KAMILI—ILE TARATIBU MPYA
  • Familia za Mzazi Mmoja Zaweza Kufanikiwa!
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Je, Unawajali Wazazi Wasio na Wenzi wa Ndoa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je! Wewe Waweza Kusaidia Wajane na Yatima “Katika Shida Zao”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 3/1 kur. 4-10

Wazazi Wasio na Wenzi Wanashinda na Matatizo ya Ulimwengu wa Leo

“Mwanamke mjane kweli, asiye na mtu wa kumsaidia, amemwekea Mungu tumaini lake na huendelea kusali na kumwomba msaada usiku na mchana.”—1 Tim. 5:5, HNWW

1-3. (a) Mjane mmoja aliandika nini? (b) Je! kumekuwako na ongezeko la jamaa zenye wazazi wasio na wenzi, nayo ni yapi mengine ya matatizo yanayozipata jamaa hizo?

MIMI ni mjane wa miaka 28 na nina watoto wawili. Nimeshuka moyo sana kwa kuwa sitaki kulea watoto wangu bila baba. Inaelekea hata hakuna anayenijali. Najua hainipasi kuendelea kujisikia hivyo, lakini naweza kufanya nini?” Barua hii inaonyesha ombi la kawaida kutoka kwa watu fulani wanaoshindana na matatizo mengi—mzazi asiye na mwenzi.

2 Ripoti za ulimwenguni pote zinaonyesha ongezeko la haraka la jamaa zenye mzazi mmoja. Katika muda wa miaka 10 hesabu yazo imeongezeka karibu mara mbili katika United States, na katika Canada imekuwa zaidi ya mara mbili. Katika Australia na Uingereza ni kama sehemu moja kwa kumi ya jamaa zote. Inakadiriwa kwamba wawili kati ya kila watoto watano wanaoishi sasa katika United States watatumia sehemu fulani ya maisha yao katika jamaa zenye mzazi mmoja.

3 Kuna sababu nyingi za ongezeko hilo. Vita na misiba ya magari barabarani vimenyang’anya nyumba nyingi akina baba. Kadiri maisha ya jamaa yanavyoharibika, kuachwa na mwenzi, kutengana na talaka yamekuwa mambo ya kawaida. Akina mama wengine wasioolewa, wamechagua kulea watoto wao badala ya kutoa mimba au kuwatoa walelewe na watu wengine. Inamlazimu mzazi asiye na mwenzi ashindane na matatizo mengi. Upweke, kulea watoto, kutafuta riziki, tamaa ya ngono na kutunza nyumba ni baadhi ya matatizo hayo.

UKRISTO WALETA FARAJA

4. Ni hali gani za wakati wa karne ya kwanza zilizotokeza jamaa nyingi za wazazi wasio na wenzi?

4 Katika karne ya kwanza, wakati wa mwanzo-mwanzo wa Ukristo, uharibifu wa vita, magonjwa na kuharibika kwa adili vilevile kulitokeza idadi kubwa ya wajane na yatima. Nyakati nyingi talaka au kuachwa na mwenzi lilikuwa ndilo jambo la kawaida. Kwa kawaida watoto wachanga waliachiwa mama zao ambao sasa walilazimika kuwalea wakiwa peke yao. Ulimwengu wa Milki ya Kirumi ulikuwa jamii isiyo na huruma ambayo iliwadharau wanyonge. Kwa hiyo wajane walitendwa vibaya sana tena kwa ukatili. Wengine hata walilazimika kuwa makahaba ili wajipatie riziki.

5. Ukristo ulisaidia katika njia gani mbili?

5 Ukristo ulileta badiliko la kweli. Uliwahurumia wale wasiokuwa katika hali nzuri. Lakini hata zaidi ya hayo, kwa mafundisho yake, wazazi wasio na mwenzi walitiwa nguvu kiadili waachane na matendo maovu ya wakati huo. Badala ya kutokeza wanawake wasio na adabu, Ukristo ulitokeza wanawake waliojiweza, walio safi, waliopenda jamaa zao. Hata wasio Wakristo walitambua tofauti hiyo, kama vile mmoja wao alivyopaza sauti akasema: “Lo! Wakristo wana wanawake bora kama nini!”

6. Ni kanuni zipi za Kikristo zinazoweza kusaidia wazazi na wenzi, pamoja na Wakristo wote, washindane na mikazo ya leo?

6 Ni kanuni gani za Kikristo zilizosaidia? Mtume Paulo, katika kutoa shauri kuhusu wajane, alisema kwamba mjane aliye mfano mzuri “amemwekea Mungu tumaini lake na huendelea kusali na kumwomba msaada usiku na mchana.’ Alionyesha kwamba mjane ambaye umri wake umepita miaka 60 aweza kutiwa katika orodha ya walio wa kupewa msaada ikiwa, kati ya mambo mengine, ajitolea kufanya mambo mema.’ (1 Tim. 5:5, 9, 10, HNWW) Hapa, angaa kanuni tatu zaonekana wazi: (1) Mtumaini Mungu sasa na kutarajia tumaini la uzima wa milele aliouahidi; (2) endeleza uhusiano wa karibu wa kibinafsi pamoja na Mungu; (3) endelea kujitia katika kazi yenye kufaidi. Tutaona namna kanuni hizo tatu, zikitumiwa, zinavyoweza kusaidia kikweli si wazazi wasio na wenzi peke yao tu bali pia na Wakristo wote washindane na mikazo ya leo.

KUSHINDANA NA UPWEKE

7. (a) Ni kwa sababu gani sana sana upweke ni jambo gumu kwa wazazi wengine wasio na wenzi? (b) Kanuni inayopendekezwa katika 1 Timotheo 5:10 inaweza kusaidiaje?

7 Mzazi mmoja asiye na mwenzi alipumua, akasema hivi: “Ninapokuja nyumbani na kuziona kuta hizo nne, na sana sana baada ya watoto kwenda kulala, upweke unanishika kweli kweli.” Ndiyo, mara nyingi upweke ndilo tatizo kubwa zaidi linalowapata wazazi wasio na mwenzi. Ijapokuwa kukaribia watoto zaidi kunasaidia, wengi wanatamani sana ushirika wa watu wazima. Kuendelea kujishughulisha katika “mambo mema” [“kila kazi njema,” NW] ni suluhisho moja ambalo kwa muda mrefu limeonekana kuwa linaleta matokeo. Wajane Wakristo wa karne ya kwanza ‘waliwakaribisha wageni, wakaosha miguu ya watakatifu [kwa kuwatumikia kibinafsi] na kuwasaidia waliokuwa katika shida.’ (1 Tim. 5:10) Kwa kuona jambo hilo, mjane mmoja Mkristo wa kisasa wa miaka 68 alianza kutembelea wajane wengine waliokuwa jirani ‘pamoja na makao ya watu wazee-wazee wakati wo wote alipokuwa anajiona kuwa mpweke. Yeye alisema hivi: “Naona kwamba kwa kufanya ziara hizi, kufanya kazi zangu za nyumbani na kujiangalia kiroho, sina wakati wa kuwa mpweke.”

8. (a) Kwa nini kuhubiri Ufalme kunatusaidia kushinda upweke na kushuka moyo? (b) Je! kweli kunaleta matokeo?

8 Kuhubiri Ufalme ni “kazi njema” moja iliyoamriwa na Yesu ifanywe, kazi inayoweza kuondoa upweke na kushuka moyo. (Mt. 24:14; 28: 19, 20) Mzazi mmoja asiye na mwenzi aliyekuwa mpweke na mwenye kushuka moyo na ambaye alikuwa hashirikiani na watu alisihiwa na rafiki zake aanze kushiriki kazi ya kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba. Alifanya hivyo. Katika mlango wake wa kwanza alikaribishwa ndani na mwanamke aliyekuwa amelemaa vibaya sana, na hata hivyo alikuwa mchangamfu sana. Angewezaje kuwa mwenye furaha sana namna hiyo? “Ni kwa sababu nina maisha yangu, mpendwa wangu. Ninaishi,” ndilo lililokuwa jibu lake lenye furaha. Hilo likabadili sana maoni ya Shahidi huyo, ambaye aliwaza hivi: “Nina afya yangu, upendo wa kundi, watoto wawili wazuri, na zaidi, Yehova. Sababu gani nisiwe na furaha?” Kusaidia wengine kiroho kwaweza kutuzuia kuwa wenye kujifikiria tu na kujiachilia tuanze kujisikitikia. Kufundisha wengine kunaendeleza uhai wa tumaini letu na kulifanya upya; hivyo twaweza kuendelea ‘kumwekea Mungu tumaini letu.’—1 Tim. 5:5, HNWW.

9. Je! sikuzote kufanya kazi ngumu kunaondoa upweke? Ni jambo gani linalosaidia pia?

9 Hata hivyo mjane mmoja mwanamume alisema kweli hivi: “Upweke hautuweki kwa kufanya tu kazi ngumu. Mara nyingi inakulazimu kuishi nao. Inakuwa tu lazima uuvumilie kwa msaada na nguvu kutoka kwa Yehova.” Nguvu hizo hupatikana mtu ‘anapoendelea kusali [“kusihi,” NW] na kuomba msaada usiku na mchana.’ (1 Tim. 5:5, HNWW) Kurudia kufikiria kwa njia ya sala utendaji wetu wa siku nzima, tukijua kwamba sikuzote Yehova yupo pale akisikiliza na kwamba yeye anajali kusikiliza mambo yote ya maisha yetu ni jambo lenye kufariji kweli kweli. Kumwambia yote yaliyo moyoni mwetu “usiku mchana” kunasaidia—sana sana usiku, wakati kama vile wengi wanavyoiripoti, tatizo la upweke laweza kuwa gumu sana.

KUSHINDANA NA TAMAA ZA NGONO.

10. (a) Ni wakati gani tamaa ya ngono inapoweza kuwa tatizo zito? (b) Mtu ‘anafuataje maisha ya kutosheleza tamaa za mwili,’ nako kufanya hivyo kwaweza kuongoza kwenye jambo gani?

10 Wazazi wengi wasio na mwenzi wanatamani sana ushirika mchangamfu wa ndoa pamoja na ngono katika mpango wa ndoa. Kwa hakika tamaa kama hizo zenyewe si mbaya. Tamaa ya kuoa au kuolewa ni ya asili. Tatizo linatokea wakati mtu anapoamua kutosheleza hizi ‘tamaa za maumbile [tamaa za ngono, NW]’ bila kujali hasara. Jambo hilo lilitokea wakati wa mtume Paulo. Wajane fulani vijana waliruhusu “tamaa zao za maumbile [zizidi] kuwa na nguvu zaidi kuliko kujitolea kwao kwa Kristo.” (1 Tim. 5:11, 12, HNWW) Jambo hilo lilikuwa hata kwa sababu mtu kama huyo alikuwa kwa kweli akisema hivi: ‘Uhitaji wangu wa ngono ni mkubwa sana. Lazima nifanye jambo fulani nitulize mwili wangu!” Tamaa hizo za mwili zikawa polepole jambo kubwa zaidi maishani, kubwa hata kuliko faida za kiroho. Tamaa hizo zaweza kuongezeka kufikia kiasi cha kumfanya mtu ‘aishi maisha ya anasa [‘kutosheleza tamaa za mwili,’ NW]’ na hivyo huyo “amekufa, ingawa yu hai.” (1 Tim. 5:6, HNWW) Kupendezwa kwa mtu huyo katika mambo ya kiroho kungekufa. Jambo ilo hilo laweza kumpata Mkristo ye yote (mwanamume au mwanamke) leo. Mtu anaweza ‘kujiua kiroho’ kwa kupuza Kanuni za adili za Biblia, kwa sababu ya kujitia sana katika kutosheleza “tamaa za ngono.”

11. Mtu anawezaje ‘kufisha tamaa yake ya ngono’?

11 Kwa hiyo, Biblia inasihi hivi: ‘Vifisheni viungo vyenu vya mwili kwa habari ya tamaa ya ngono.’ (Kol. 3:5, NW) Lakini namna gani? Kwa kulinda akili na moyo wako. Kama ulikuwa unajaribu kupunguza uzito wako na kuzuia hamu yako ya chakula, je! ungesoma magazeti yenye picha za chakula kizuri, au kutazama maonyesho ya televishoni juu ya kupika vyakula? Je! ungeshirikiana na watu ambao wakati wote wanaongea juu ya chakula? Hata kidogo! Ndivyo ilivyo kwa habari ya “tamaa ya ngono.” Mjane mmoja alisema kweli hivi: “Tuko katika ulimwengu ambao hauachi hata kidogo kusema juu ya ngono. Kwa hiyo mimi ni mwangalifu sana juu ya uchaguzi wangu wa tafrija na wale ninaoshirikiana nao. Kwa hakika mgonjwa mwenye ugonjwa wa sukari hangetaka kusukumia pua lake kwenye dirisha la duka la keki.”

12, 13. (a) Ili kusitawisha uhusiano wa kibinafsi pamoja na Yehova, ni nini kinachohitajiwa? (b) Kwa sababu gani maombi ya “kusihi” ni ya maana sana, naye mtu anaweza kutendaje kupatana nayo?

12 Hata hivyo, ili aendelee kushinda tamaa hizi, siku baada ya siku, lazima mtu asitawishe uhusiano wa karibu na wa kibinafsi pamoja na Mungu. Licha ya funzo la kibinafsi na kutafakari, hilo lahitaji kudumu katika “kusihi.” (1 Tim. 5:5, NW) Paulo hataji sala za kawaida tu, bali pia anasema “kusihi.” Haya ni maombi kwa Mungu yanayoonyesha uhitaji mkubwa. Ni maombi ya bidii, ndiyo, kuomba sana msaada, pengine pamoja na “kilio chenye nguvu na machozi.”—Ebr. 5:7. NW.

13 Je! sala zako kuomba msaada wa kujiweza na nguvu ni zenye nguvu jinsi hiyo? Unadumu katika kuzitoa? Je! unasali wakati ule ule tamaa hizo zinapokuwa zenye nguvu? Je! unataja mambo waziwazi, pengine ukimfunulia Baba yetu mambo ambayo hungemwambia mtu mwingine? Vilevile, je! unatenda kupatana na sala zako? Mwanamke mmoja Mkristo alisema hivi: “Usimwombe Yehova msaada wa kushinda tamaa za ngono na kisha uwe ukifiri juu ya ngono wakati wote. Ni kweli, vipindi fulani wakati wa mwezi tamaa zako za ngono huenda zikawa zenye nguvu sana. Tumia akili zako kwa kufanya jambo fulani jingine. Katembelee mtu fulani. Kwenda matembezi au ufanye jambo jingine litakaloondoa mawazo hayo. Jipe kazi nyingi iwezekanavyo wakati wa kipindi hicho cha mwezi.” Mwingine ambaye aliona faida ya kuendelea’ kuwa na shughuli nyingi katika “kila kazi njema” alikubali, akisema hivi: “Safisha madirisha yako kwa kutumia nguvu. Safisha sakafu yako kwa kutumia nguvu. Chimba katika udongo. Nimepata kufanya hivyo. Kunaleta matokeo!” Unapoona Yehova akikusaidia na tatizo hilo—si kwa kufanya mwujiza, bali angaa kwa kukupa nguvu za kushindana nalo kila siku—​utavutwa karibu zaidi naye.

14. (a) Ni jambo gani linaloweza kutokea ikiwa mtu anashindwa kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova. (b) Wazazi wasio na wenzi wanaweza kufanyaje wakati wanapongojea kumpata mwenzi Mkristo?

14 Bila huu “usiri pamoja na Yehova” wenye thamani kuu huenda mtu akaanza kutafuta mwenzi wa ndoa bila kujali hasara, pengine hata akafanya matembezi ya kirafiki na walimwengu. (Zab. 25:14, NW) Mmoja aliyefanya hivyo alikubali hivi: “Lililokuwa tatizo kweli kweli si kwamba mimi sikuwa karibu na Yehova. Nilipopata nafasi ya kuolewa, lilisikika kuwa jambo zuri sana. Nikasahau kanuni za adili nilizokuwa nimefundishwa. Ndipo siku moja nikatambua kwamba mwanamume huyo alikuwa akipendezwa na [faida] zake mwenyewe tu wala si ndoa. Ndipo nilipolazimika kuishi na dhamiri yenye hatia.” Ni kweli kwamba, kukaa bila mwenzi ni jambo gumu, walakini kama vile alivyoonya mwanamke mmoja Mkristo aliyekuwa ametalikiwa: “Kuna jambo moja baya zaidi kuliko kuwa bila mwenzi. Ni kuolewa na mtu asiyefaa!” Sikuzote kuna uwezekano wa kupata mwenzi kati ya Wakristo waliojitoa, mtu aliye “katika Bwana.” (1 Kor. 7:39) Wengine wamengoja kwa muda wa miaka mingi wapate mwenzi kama huyo. Na katika wakati huo, hawakuona uchungu au wakashindwa na hali zao. Wametumia wakati huo kwa hekima wasitawishe sifa ambazo zingewafanya kuwa wenzi walio bora. Kama vile alivyosema mzazi mmoja asiyekuwa na mwenzi: “Najiuliza, ‘Je! mimi ni mwanamke wa kiroho ambaye angechaguliwa na mtu fulani?’ Ikiwa mimi ni mwenye huzuni nyingi ninapokuwa bila mwenzi, basi pengine ningemfanya mtu fulani kuwa mwenzi mwenye huzuni.”

KUTUNZA NYUMBA NA KULEA WATOTO

15. (a) Wazazi wengine wasio na wenzi wamefanya nini ili watimize mambo ya nyumbani kwa kufaa? (b) Je! Mnayo mapendekezo yo yote ya ziada?

15 Ijapokuwa ni kazi inayotaka jitihada nyingi, wazazi wengi wasio na wenzi wameiga mwanamke anayeweza kutimiza mambo anayeelezwa katika Mithali 31. Ijapokuwa alikuwa ameolewa, yeye ndiye aliyeangalia mambo ya nyumba yake. Aliokoa fedha kwa kununua vitu kwa uangalifu, akijitengenezea vitu vyake mwenyewe kutoka kwa vitu visivyotayarishwa na kwa kutotumia vibaya chakula, kwa kuwa alitayarisha ‘sehemu iliyopangwa.’ (Mist. 13-15, 19, NW) Alianza kufanya kazi mapema akaendelea mpaka usiku, (Mist. 15, 18) Alitengeneza vitu na kuviuza. (Mst. 24) Alitumia “mikono yake mwenyewe” kufanya kazi. (Mist. 17, 19, NW) Leo, ili wajifunze namna ya kutumia ‘mikono yao wenyewe’ kwa ustadi, wazazi wengine wasio na wenzi wamesoma vitabu vinavyoeleza namna ya kufanya mambo fulani tena wameomba mashauri kwa washauri wenye ujuzi. (Mara nyingi, baada ya kueleza hali yao wamepewa maagizo na wenye ujuzi bila malipo.) Wengine wamewaeleza mashahidi wa Yehova wenzao waliokuwa na ujuzi fulani mahitaji yao, nao, walipokuwa na nafasi walitoa msaada kwa fadhili. Yote hayo yanapunguza matumizi ya fedha.

16. Sababu gani ni jambo la maana sana kumwekwa Mungu tumaini, nao ni mfano wa nani unaoonyesha uhitaji huo?

16 Hata hivyo, mjane ajapofanya yote awezayo, kadiri nyakati zinavyozidi kuwa ngumu, lazima amtumaini Mungu apate riziki ya kila siku. Mfano mzuri wa mmoja ‘aliyetumaini Mungu’ alikuwa yule mzazi asiyekuwa na mwenzi aliyeishi katika mji wa Sarepta katika siku za Eliya, nabii wa Mungu. Kwa uongozi wa Yehova, Eliya alimwomba chakula chake cha mwisho, akamwahidi kwamba Mungu angetoa riziki. Wewe ungefanya nini? Yeye alikuwa na chakula cha kutosha wakati mmoja tu. Ingawaje chakula hicho kimoja kilikuwa kitu ambacho angeweza kutumaini. Hata hivyo, kwa sababu ya imani yake, alitoa kitu cha hakika kwa ajili ya kitu kisicho cha hakika. Neno la Mungu kupitia kwa nabii huyo lilitimizwa. Yeye na mwanawe hawakukosa chakula hata kidogo. Vivyo hivyo leo, wazazi wasio na wenzi,pamoja na Wakristo wengine wote, lazima wamtumaini Mungu kwa kutafuta ufalme wake kwanza na kwa kufuata kanuni zake za haki. Ndipo watakapoona kwamba atatoa riziki.—1 Fal. 17:8-16; Luka 4:25, 26; Mt. 6:31-33.

17. Ni jambo gani ambalo haiwapasi wazazi wasio na wenzi kusahau ili waweze kulea watoto wao kwa kufaa, na sababu gani?

17 Kazi ngumu ya kuwa “mama” na “baba” ya watoto na kuwalea ifaavyo yaweza kutimizwa ikiwa tu yule mzazi hasahau kamwe jambo linalopaswa kuwa la maana zaidi katika nyumba. Angalia jibu la Biblia:

“Kuwa na mali chache pamoja na kumcha [Yehova]; ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu. Chakula cha mboga penye mapedano; ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.” (Mit. 15:16, 17)

Ubora wa kweli wa chakula si riziki yenyewe, bali yale yaliyo mioyoni mwa wale wanaokula pamoja. Upendo pamoja na kumwogopa Yehova ifaavyo ndiyo mambo yaliyo na maana kweli kweli.

18. (a) Wazazi wengine wasio na wenzi wamefanya nini ili wawe na fedha na hata hivyo wawe na wakati wa kuangalia watoto wao? (b) Wewe unaona ni jambo gani jingine linaloweza kufanywa?

18 Ili wawe na wakati wa kusaidia watoto wao wamwogope Mungu na wakati uo huo wapate fedha zinazohitajiwa, wazazi wengine wasio na wenzi, mara nyingi wakisaidiwa na watoto wao, wameuza vitu walivyotengeneza wao wenyewe nyumbani mwao au wakafanya utumishi fulani katika nyumba za watu.a Wengine wamejifaidi na msaada wo wote unaotolewa na serikali ambao wana haki ya kuupata kulingana na sheria na kanuni za mema na mabaya. Wengine wameshusha hali yao ya maisha ili mpato ya kazi ya muda yawatoshe, kama vile alivyofanya mwanamke mmoja Mkristo ambaye ana watoto wanne. Alisema hivi: “Nilitaka kuwa pamoja na watoto kadiri iwezekanavyo. Ilitosha kuwa bila baba pasipo kuwanyima mama pia.” Kwa wazi, si kila mtu anayeweza kupata kazi kama hiyo inayofaa. Walakini, kwa kuzungumza na watoto waziwazi, na kuwaeleza sababu gani inakuwa lazima kufanya kazi ya kimwili na kwa kutumia wakati mwingi iwezekanavyo pamoja nao, wazazi hawa wanaweza kuendeleza hali yenye uchangamfu na ya upendo nyumbani.

19. (a) ‘Kupenda watoto wao’ kunamaanisha nini kwa wazazi? (b) Ni kwa sababu gani jambo hilo haliwi jepesi sikuzote kwa wazazi wasio na wenzi?

19 ‘Kuwapenda watoto wao,’ jambo linalotia ndani kuwapa adabu inayohitajiwa, ni kwa lazima. (Tito 2:4; Mit. 13:24) Kunasaidia kuzuia watoto, ambao wamekwisha mpoteza mzazi mmoja, wasijione kutokuwa salama. Kwa sababu wanawake wengine wana maelekeo ya kuvutwa sana na maono ya moyoni, huenda wakahitajiwa kujitahidi kweli kweli ili watoe adabu. Lakini kumbuka, adabu, ambayo huenda ikatia ndani kuadhibu, inamwambia mtoto kwamba unampenda vya kutosha usiweze kuruhusu aingie katika taabu.

20. (a) Wengine wamefanya nini ili waendelee kuwa karibu na watoto wao? (b) Kuna baraka gani za namna mbili zinazopatikana kwa kukaa karibu na watoto na kuwalea ifaavyo?

20 Wazazi wasio na wenzi ambao wamekaa karibu na watoto wao wanapendekeza hivi:

“Weka kando wakati wa pekee wa kuwa pamoja na watoto wala usiruhusu jambo lo lote liuingilie. Sikuzote kazi ya nyumbani itakuwapo; lakini si watoto. Kaza akili zako katika kujenga watoto kiroho.” “Ilikuwa lazima kuchanganya adabu yangu pamoja na ufahamu kwa sababu ya mshtuko waliokuwa nao kwa kumpoteza mama yao. Nilizungumza nao kila nilipokuwa na nafasi, hata uwe wakati gani mchana ama usiku. Tunakuwa na vipindi vyenye furaha sana tunapotayarisha chakula. Huo ndio wakati wanapozungumza nami kwa wazi kweli kweli.”

Upendo wa namna hiyo unafikia mioyo ya watoto. Wanaweza kuusikia na kuuona. Ijapokuwa mengi yanatakiwa na jitihada hizo za kulea watoto, mzazi anaridhika sana kwa kuona watoto wakikua na kuwa wasifaji wa Yehova wenye kutumainika. Vilevile, kazi kama hiyo ni ulinzi wa kiadili kwa mzazi.—1 Tim. 2:15.

SULUHISHO KAMILI—ILE TARATIBU MPYA

21. (a) Je! matatizo ya wazazi wasio na wenzi yanaondolewa kwa urahisi? (b) Mwendo wa uaminifu unatimiza jambo gani?

21 “Nashiriki kazi ya kuhubiri karibu kila siku. Najifunza na kusali nyakati zote,” akasema mjane mmoja, aliyekiri hivi: “Hata hivyo, kila usiku ninalala nikilia.” Ndiyo, matatizo ambayo mzazi asiye na mwenzi analazimika kushindana nayo ni magumu sana kutatua. Mara nyingi inakuwa vita ya kila siku. Hata hivyo, kila siku ambayo Mkristo anaonyesha uvumilivu, Shetani anaaibishwa tena, kwa kuwa alishtaki kwamba watu wangeacha kumtumikia Mungu wakati hali zinapokuwa ngumu. (Ayubu 1:9-11; Mit. 27:11) Tambua kwamba hakuna mtu asiyeona matatizo katika maisha ya sasa. “Ushirika mzima wa ndugu [zako]” unataabika (1 Pet. 5: 9, NW) Matatizo ya mwingine yaweza kuwa tofauti na yako, lakini ni magumu kadiri ile ile kwa mtu huyo. Hata matatizo yako yaweje, hali zingeweza kuwa mbaya zaidi kuliko zilivyo. Kwa hiyo jaribu kuendelea kuwa na maoni yanayofaa juu ya maisha yako kadiri uwezavyo.

22. (a) Inatupasa kukaza macho yetu juu ya nini na sababu gani? (b) Ni jambo gani litazungumzwa katika makala inayofuata?

22 Na zaidi ya yote, lazima tukaze macho yetu kwenye tumaini lenye uzima taratibu inayokuja itakayoleta uradhi mkamilifu. Kama vile asemavyo mtume Paulo: “Tusiviangalie vinavyoonekana [dhiki inayoweza kututatiza na kututupa chini], bali visivyoonekana [tumaini la uzima wa milele]. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.” Ndiyo, mikazo ya taratibu ya leo yenye kutatiza mwishowe itakoma. Baraka za Taratibu Mpya, inayokaribia sana, hazitakuwa na mwisho. Zitazame sana hizo kwa macho yanayoona waziwazi nawe ‘hutakata tamaa.’ (2 Kor. 4:8, 9, 16-18) Lakini wengine wanaweza kufanya nini wasaidie wazazi wasio na wenzi? Hilo litazungumzwa katika makala inayofuata.

[Maelezo ya Chini]

a Kupata mapendekezo, angalia Awake! la Agosti 22,1975, kurasa 9-11, na Septemba 22, 1975, kurasa 9-12.

[Sanduku katika ukurasa wa 9]

NAMNA YA KUSHINDA MATATIZO

□ Mtumaini Mungu sasa na kutarajia tumaini la uzima wa milele aliouahidi

□ Endeleza uhusiano wa karibu na wa kibinafsi pamoja na Mungu

□ Jishughulishe katika kazi yenye kufaidi

[Picha katika ukurasa wa 5]

Wazazi wasio na wenzi waweza kuzoeza watoto wao wasaidie kufanya kazi za nyumbani

[Picha katika ukurasa wa 8]

‘Weka wakati wa pekee wa kuwa pamoja na Watoto . . . Zungumza nao kila unapokuwa na nafasi’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki