Sababu Gani Uuzuie Ulimi Wako?
Je! wewe wamjua mtu ambaye husema-sema sana? Mithali 10:19 hutoa sababu ya kujilinda na jambo hilo. Inasema: “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.
Yakobo ndugu mzazi mmoja na Yesu alithibitisha kwamba kuna uhitaji wa kujilinda tusikwaze wengine kwa ulimi, kwa sababu kushindwa kuuzuia kwaweza kufanya ibada ya mtu kuwa ya bure. (Yak. 1:26) Hakuna ye yote kati yetu anayeweza kuuzuia ulimi kwa ukamili, walakini bila shaka tunaweza kufanya maendeleo.—Yak. 3:2-8.
Hiyo haituhitaji tukae kimya, pasipo kushiriki kamwe mazungumzo. Walakini sababu gani usifanye jaribio hili? Fikiria maelekeo yako kwa muda fulani. Uone kama, katika mazungumzo ya kikundi, unajisikia kusukumwa useme zaidi katika kila habari inayozungumzwa. Katika mazungumzo ya habari mbalimbali juu ya maisha je! yanamalizika ukiwa kila wakati umezungumza zaidi kuliko wengine katika kikundi? Ikiwa ndivyo, huenda kutafakari juu ya Mithali 10:19 kukakulinda.