Je! Wakumbuka?
UMEFURAHIA kusoma matoleo kadha ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Basi inaelekea utakumbuka baadhi ya mambo ya kuvutia yafuatayo yaliyozungumzwa:
◼ Tunawezaje kujifanyia “jina zuri” pamoja na Mungu?
Kwa kufikiria yaliyo mema na yaliyo mabaya machoni pa Mungu. Lazima tuache kufanya yaliyo mabaya tuanze kufanya yaliyo mema. (Warumi 12:2, NW) Ili kufikia mradi huo ni lazima tujifunze Neno la Mungu halafu sisi wenyewe tutumie maarifa hayo tuliyopata. (Warumi 2:21, 22) Hiyo inatia kufuata hatua za Yesu na kushiriki katika kuhubiri “habari njema” za ufalme. (Mathayo 24:14; 1 Pet. 2:21)—7/15 kur. 11, 13, 15.
◼ “Mtumwa mwaminifu mwenye akili” anawezaje kutambuliwa leo?
Yesu alidokeza kwamba “mtumwa” huyo angejulikana kwa sababu ya kulinda na kwa kutoa chakula cha kiroho kinachohitajiwa na wote katika kundi la Kikristo. (Mathayo 24:45-47) Mambo ya hakika yanaonyesha kwamba tangu miaka ya mapema kuanza na wa 1870 jamii ya Wanafunzi wa Biblia (sasa wanajulikana kuwa Mashahidi wa Yehova) walitambua uhitaji wa kufanya uchunguzi wa Maandiko usio wa kimadhehebu. Matokeo yakawa ni kurudishwa kwa kweli nyingi za Biblia zilizochapishwa na kutolewa na wale waliotamani kuwa tayari kwa ajili ya kurudi kwa Bwana. Hilo limetokeza kukusanywa kwa kundi la wanafunzi watiwa mafuta wa Kristo, ambao wakiwa mtu mmoja mmoja wamelishwa na wako macho kiroho. Wakiwa wamemtambua “mtumwa” huyo mwaminifu, “mkutano mkubwa” wa wafanyi kazi wenzi sasa unatumikia pamoja naye kwa ushikamanifu. (Ufunuo 7:9, 15)—8/1 kur. 19, 21, 22.
◼ Matatizo katika maisha ya Mkristo yanawezaje yakawa kitia-moyo kwake?
Mkristo anapokabili matatizo ya kila siku kama infuleshoni, uchafuzi wa mazingira na magonjwa akitumia mashauri ya Biblia yasiyolinganika, ataona jinsi yanavyofanya kazi hasa. Biblia ni chanzo kikuu cha kutia moyo na inamfundisha kutegemea sikuzote hekima ya Mungu badala ya ile yake mwenyewe. (Zaburi 119:105)—10/1 uku. 7.
◼ Ni maulizo gani yanayoweza kuijaribu imani yetu katika serikali ya Ufalme ya Mungu?
Sisi binafsi tunauonaje ulimwengu huu? Je! tunajichukua wenyewe kama ‘wageni’ na ‘wakaaji wasio wa nchi’ ndani yake? Je! wengine katika mtaa wetu wanatuona sisi kuwa tofauti? Je! tunaweza kujiona tukiwa wenye kutarajia kuwa raia wa serikali ya Mungu? Je! tunawatangazia wengine kwa ushikamanifu juu yayo?—10/15 kur. 8, 18.
◼ Kwa sababu gani ni jambo la hekima kujiendesha wenyewe kama watu wadogo zaidi?
Biblia inaonyesha kwamba mwendo huo wa hekima unaleta uhusiano mwema na Yehova Mungu, na Wakristo wenzetu na washiriki wa jamaa zetu wenyewe. Tena, kuwapa wengine mapendo yao na faida kunaongeza fufaha yetu maishani. (Matendo 20:35)—11/1 uku. 24.