Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 11/15 kur. 4-5
  • Msingi wa Imani Iliyohakikishwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msingi wa Imani Iliyohakikishwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • YALIYO MAKUBWA SANA​—YALIYO MADOGO SANA
  • Je! Kuna faida ya Kumwamini Mungu?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Maagizo Yalitoka Wapi?
    Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
  • Kuchunguza Chembe kwa Hadubini
    Amkeni!—1999
  • Chembe Zako​—Maktaba Iliyo Hai!
    Amkeni!—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 11/15 kur. 4-5

Msingi wa Imani Iliyohakikishwa

WATU wengine wanaodhani kwamba imani haifai hawajapata kufikiria kwa uzito juu ya kama kuna msingi thabiti wa imani. Je! wewe umekwisha kufanya hivyo?

Kama ungetaka kuchunguza jambo hilo, ungeanza wapi nao ushuhuda wa kuunga mkono jambo hilo ungekuwa nini? Unaweza kuchunguza mambo mengi juu ya ulimwengu unaokuzunguka na kuona mambo ya hakika yanayohusiana na jambo hilo.

YALIYO MAKUBWA SANA​—YALIYO MADOGO SANA

Ni haki kusema: Unaweza kuchunguza yaliyo makubwa sana—ulimwengu wa anga za juu unaoelekea kutokuwa na kipimo. Au unaweza kuchunguza yaliyo madogo sana​—hata vitu vidogo sana visivyoonekana kwa macho yetu vilivyo sehemu yetu na sehemu ya ulimwengu wetu. Vyo vyote iwavyo, utapata sababu ya kumwamini Muumba.​—Mwa. 1:1; 2:1-4.

Miaka 3,000 iliyopita, katika Mashariki ya Kati, mwanamume mmoja ambaye aliitwa jina lake Elihu alisema hivi: “Tazama juu angani kisha utafakari.”‏ (Ayubu 35:5, The New English Bible) Yeye aliona kwamba ushuhuda juu ya Muumba ulikuwa unaonekana katika mbingu zilizo juu. Bila shaka, bila msaada wa chombo cha kusaidia kuona mbali, Elihu angeweza kuona kwa macho yake nyota zinazopungua 5,000 kati ya zile nyota zaidi ya 100,000,000,000 za taratibu ya vikundi vya nyota iliyo jirani yetu. Yeye asingaliweza kujua kwamba kuna maelfu ya mamilioni ya vikundi vya nyota, kila kimoja kikiwa na mabilioni ya nyota zake. Walakini kama angaliweza kujua hivyo, kama sisi sasa, je! unadhani hilo lingedhoofisha imani yake kwa Mungu? Au, maarifa hayo yangalitia nguvu imani yake? Wakati fulani baadaye, mtunga zaburi Daudi alisema: “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, na anga laitangaza kazi ya mikono yake.”‏​—Zab. 19:1.

Sasa wanasayansi wamekwisha kutumia viruka-angani wakachunguza jua na nyota zinazohusiana nalo, na wakachunguza anga za juu kwa darubini na kusikiliza sauti zinazotoka mbali kule-e-e katika ulimwengu mkubwa mno kwa njia ya darubini zenye kunasa sauti. Maarifa hayo yaliyoongezeka yanatoa sababu zaidi za kumwamini Mungu.

Mtaalamu wa maumbile Wernher von Braun, aliyekuwa kiongozi wa makao makuu ya kuruka angani ya NASA (Shirika la Taifa la Urukaji wa Ndege na Usimamizi wa Anga za Juu) wa United States, aliandika hivi: “Watafutaji wa mali wa karne ya kumi na tisa na warithi wao wa karne ya ishirini wenye kufuata maongozi ya Marx, walijaribu kutuambia kwamba, kwa kadiri ambavyo sayansi inavyotupa maarifa zaidi juu ya uumbaji, ndivyo tungeweza kuishi pasipo kumwamini Muumba. Hata hivyo kufika sasa, tunapopata kila jibu jipya, tunagundua maulizo mapya. Kwa kadiri tunavyofahamu vizuri zaidi . . . upangaji wa ustadi wa vikundi vya nyota, ndivyo tumepata sababu zaidi ya kustaajabia uzuri wa uumbaji wa Mungu.”

Tunaweza kukata maneno vivyo hivyo tukigeuka kutoka ulimwengu mkubwa mno na kuchunguza sehemu ndogo-ndogo za miili yetu wenyewe. Daudi alichochewa akasema hivi juu ya Mungu: “Uliumba kila sehemu yangu; na ukanikusanya pamoja katika tumbo la uzazi la mama yangu. . . . yote unayofanya ni ya kushangaza na ya ajabu.” (Zab. 139:13, 14, Today’s English Version) Wakati wa kutumika miaka mingi akiwa daktari wa upasuaji wa mishipa ya fahamu, Profesa Robert J. White, M.D., amepata nafasi ya kuchunguza akili ya kibinadamu kwa uangalifu. Anasimulia hivi:

“Mambo ambayo nimeona nikitibu wagonjwa wangu, na wakati wa kufanya uchunguzi wa ushipa ya fahamu nikijaribu kufunua waziwazi ni za ubongo, yamenifanya nistaajabie sana ubongo kuliko wakati mwingineo wote. Nami sina uchaguzi mwingine ila kukubali kuwapo kwa Mtu Mkuu Zaidi Mwenye Akili, ambaye amebuni na kutengeneza uhusiano ulio kati ya ubongo na akili—jambo linalozidi uwezo wa wanadamu wa kuweza kufahamu.”

Hata kama ungeweza kuchunguza namna ambavyo chembe ya mwili wa kibinadamu imetengenezwa, ungeona sababu ya kutosha kumwamini Muumba. Chembe ndiyo asili ya kitu kilicho hai duniani. Mwili wako umefanyizwa kwa chembe ndogo 100,100,000,000,000. Walakini kila chembe ina sehemu nyingi zenye kushangaza na ambazo zimebuniwa vizuri.

Kwa mfano, katika kila chembe ya mwili wako kuna makumi ya maelfu ya vinakili tabia na kichukua tabia (DNA) ambacho kinajulikana sana, ambacho huongoza namna chembe itakavyofanya kazi na itakavyojigawanya. Ndicho kilichoamua rangi ya nywele zako, namna ukuzi wako ulivyokuwa wa haraka na mambo mengine mengi yasiyohesabika. Jiulize hivi: Inawezekanaje kwamba habari yote hiyo ingeweza kuwa ndani ya kichukua tabia katika kila chembe yangu?

Katika kitabu chake Whence and Wherefore (1978), Dakt. Zev Zahavy anasimulia juu ya mazungumzo yaliyokuwapo katika darasa la elimu ya viumbe na dawa katika Shule ya Kuhitimu ya Sayansi za Kitiba ya Chuo Kikuu cha Cornell. Profesa huyo alikuwa akizungumza juu ya “visehemu vilivyopangwa kwa utaratibu vya kichukua tabia.” Twasoma hivi:

“Darasa hilo lilikuwa la wanafunzi vijana ambao walikuwa wamekulia katika kipindi cha ufundi wa kompyuta, na, kwa hiyo, walikuwa na ujuzi mwingi juu ya sehemu ya lazima inayotimizwa na mwenye kupanga utaratibu utakaofuatwa na kompyuta. Ulizo linalofaa liliulizwa na mwanafunzi mmoja wakati ‘visehemu vilivyopangwa’ vilipotajwa.

“‘Ikiwa kinakili tabia (RNA) na kichukua tabia (DNA) vinapangwa vifanye kazi na kutengeneza tabia kulingana na namna zilizokusudiwa,’ akauliza, ‘mipango yenyewe inatoka wapi?’

“Profesa huyo akajibu kwa kutabasamu, ‘Si kwa mwingine ila Mtokezaji wa Utofautiano Mwingi’ (kwa Kiingereza: ‘Generator of Diversity’).

“Mwanafunzi huyo mwenye kuduwaa akauliza hivi kwa mshangao, ‘Mtokezaji wa Utofautiano Mwingi (kwa Kiingereza: ‘Generator of Diversity)? Huyo ni nani?’

“Nafikiri Yeye anajulikana vizuri zaidi kwa herufi zake za kwanza,’ mshauri huyo mwenye urafiki akajibu.”‏

Bila shaka, profesa huyo alimaanisha herufi G O D (yaani, Mungu kwa lugha ya Kiingereza).

Ndiyo, kuchunguza sehemu zilizo kubwa sana au zilizo ndogo sana za uumbaji kunatupa msingi thabiti wa kumwamini Mungu kwa uhakika. Hata hivyo, huenda ikawa ungali unataka kujua, Je! inafaa kuwa na imani hiyo siku hizi na katika kizazi hiki?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki