Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 3/15 uku. 3
  • Ni Nani Wanaosema Katika Lugha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Wanaosema Katika Lugha?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Kusema Katika Lugha Leo—Kunatoka kwa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je! Zawadi ya Ndimi Ni Sehemu ya Ukristo wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kusema kwa Lugha?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 3/15 uku. 3

Ni Nani Wanaosema Katika Lugha?

“SIKU moja, hapa katika chumba changu cha mezani, nilikuwa nimepiga magoti nikitoa sala. Ghafula nikajiona kuwa mwenye furaha tele tena isiyozuilika. Nikaanza kumsifu Mungu katika Kiingereza, kisha nikasema katika lugha nyingine. Hilo lilikuwa jambo zuri kweli kweli.”​—Mwanamke Mbaptisti katika Texas.

“Ikawa kwamba ulimi wangu ukakamatwa, na mara moja nikawa sijui lo lote, nikawa sijui kitu kabisa, walakini nilipata kichocheo cha kusema. Nilitaka kuacha kusema, walakini ulimi wangu ulikuwa umesukumwa useme. . . . kisha ninasikia maneno yangu mwenyewe, nami siyafahamu, walakini naendelea tu kuuona ulimi wangu ukisukumwa useme.”​—Mshiriki mwanamume wa kundi la Kimtume katika Mexico.

“Jambo hilo linaeleza kitu kinachotendeka moyoni mwangu.”​—Mwanamume Mkatoliki katika Michigan.

Ni kitu gani wanachosimulia? Kusema katika lugha (ndimi), au glossolalia.a Wakati wa muongo mmoja au miwili iliyopita (makumi ya miaka), kwa halisi mamilioni ya watu wanadai kuwa wamepokea kutoka kwa Mungu karama ya kimwujiza ya kusema katika lugha. “Karama” hiyo inapatikana katika makanisa ya Kipentekoste “yaliyo bora” na pia katika dini zote zinazofuata wazo la kwamba zina karama ya kusema lugha ngeni (katika kiingereza charismab)—Katoliki ya Roma, Baptisti, Methodisti, Lutheri na Presbiteri. Kulingana na Uchunguzi wa maoni ya watu wa Christianity Today, kati ya watu wazima Waamerika milioni 29 wanaojiona kuwa Wapentekoste au wenye kukirimiwa, karibu milioni tano wanadai wamepokea karama ya kusema katika lugha.

“Karama” hiyo mara nyingi inaonyeshwa kwa kubwata-bwata kwa shauku nyingi maneno na semi zisizofahamika. Kwa mtu anayesikiliza, huenda, ukasikika kuwa usemi usio na maana, walakini kwa Mpentekoste au mwenye kukirimiwa mnyofu, “ndilo jambo zuri zaidi Mkristo analoweza kupata,” kama ambavyo msemaji mmoja katika lugha alivyosema. Kwa sababu gani wengi wanatia mkazo juu ya karama ya kusema katika lugha?

“Kwanza kabisa,” ndivyo anavyoeleza Felisitas D. Goodman katika kitabu chake Kusema katika lugha, “kunaonyesha kuwapo kwa Roho Takatifu katika mfu. . . . Pili, kusema katika lugha ni namna ya sala, inayoongozwa na kuwapo kwa Roho Takatifu.” Kwa hiyo kwa mtu mnyofu anayesema katika lugha, karama yake ni ishara ya kuwa amepokea roho takatifu. Huenda akawa anaona kwamba maneno yake hayatoshi kueleza shukrani zake kwa Mungu. Basi, kusema katika lugha kunaonwa kuwa “karama ya Roho inayomruhusu mtu asali kwa matokeo zaidi” katika “namna ya usemi isiyo na vizuizi, asiyoifahamu,” ndivyo anavyosema Clark H. Pinnock, profesa mshiriki wa theologia (elimu ya dini) yenye utaratibu katika Shule ya Dini ya McMaster katika Ontario, Kanada.

Lakini, kwa kweli, je! karama ya kusema katika lugha ‘inaonyesha kuwapo kwa roho takatifu katika mtu’? Je! unapaswa kutafuta karama hiyo ili ikusaidie ‘usali kwa matokeo zaidi’ kwa Mungu?

[Maelezo ya Chini]

a Neno “glossolalia” linatokana na maneno mawili ya Kigiriki, glossa, linalomaanisha “ulimi” (“lugha”), na lalia, linalomaanisha “kusema.”

b Neno “charisma” linatokana na neno la Kigiriki charismata, linalomaanisha “karama.” Mara nyingi neno hilo linatumiwa kumaanisha watu wale waliomo katika dini zenye kufuatia mambo ya kale zaidi walio na maoni kwamba kusema katika lugha na karama nyinginezo zisizo za kawaida ni sehemu ya kawaida ya Ukristo leo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki