Maswali kutoka kwa Wasomaji
● Katika ule mfano wa wanawali 10 (Mathayo 25:1-13), ni nani aliyepiga kelele akisema: “Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki”?
Yesu hakumtaja aliyesema hivyo. Katika arusi ya Kiebrania, yenye kuwa kama ile ambayo Yesu alikuwa akiitumia kutoa mfano huo, labda bwana-arusi alikuwa akifuatwa na watumishi wa kiume au marafiki. (Yohana 3:29) Hao wangeweza kuwajulisha watu wo wote wenye kungoja wawe macho kwa sababu bwana-arusi na kundi lake walikuwa wanakuja. Walakini, hakukuwa na uhitaji wa Yesu kutaja watumishi wa namna hiyo. Wala kusingekuwa na matumizi ya kimfano juu ya watu hao. Jambo la maana ni kwamba kulikuwa na kelele iliyowafanya macho wale wanawali, ikawachochea kuchukua hatua.