Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 2/1 kur. 3-4
  • ‘Kuzaliwa Mara ya Pili’ kwa Anza Kupendwa na Watu Wengi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kuzaliwa Mara ya Pili’ kwa Anza Kupendwa na Watu Wengi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Inamaanisha Nini Kuzaliwa Tena?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kuzaliwa Mara ya Pili—Je, Ni Njia ya Kupata Wokovu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • ‘Kuzaliwa Mara ya Pili’—Sehemu ya Mwanadamu na Sehemu ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Ni Nani Wanaozaliwa Mara ya Pili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 2/1 kur. 3-4

‘Kuzaliwa Mara ya Pili’ kwa Anza Kupendwa na Watu Wengi

“KUZALIWA UPYA KWAONGEZEKA SANA.” Hicho ndicho kilichokuwa kichwa cha habari ya magazetini kutoka Los Angeles iliyoandikwa katika gazeti Post la New York la Mei 19, 1980. Habari hiyo iliendelea kusema hivi: “Zaidi ya nusu ya watu wazima Waamerika wamepitia jambo la kidini la Kikristo la ‘kuzaliwa mara ya pili’ kwa daima, ndivyo inavyoripotiwa na uchunguzi wa kupata maoni ya watu utakaotokea baadaye. Tarakimu hizo . . . zinaonyesha kwamba milioni 84 za watu wazima Waamerika wamejitoa kibinafsi kwa Yesu Kristo nao wangali wanakuona kuwa kwa maana.” Wakati fulani kabla ya hayo uchunguzi mmoja uliripoti kwamba karibu nusu ya matineja (vijana) wa Kiamerika Waprotestanti walikuwa ‘wamezaliwa mara ya pili.’ Gazeti la kila juma Parade la Julai 6, 1980, lilisema kwamba wagombezi wote watatu wa uchaguzi wa rais wa United States katika wakati huo, Carter, Reagan na Anderson, walikuwa Wakriste ‘waliozaliwa mara ya pili.’

Wakristo ‘waliozaliwa mara ya pili’ nyakati nyingine wanasema wamefanikiwa katika biashara kwa sababu ya kuzaliwa mara ya pili. Yasemekana kwamba msimamizi mmoja mwenye kufanikiwa sana wa New York alisema hivi: “Ukijitoa mwenyewe kwa Bwana, Bwana naye anakusaidia. Wakati mmoja, nilipolazimika kununua hisa ya Bonwit Teller, nilikuwa na upungufu wa dola milioni 2.5 nami sikujua jinsi ningeweza kuzipata. Ulikuwa mwujiza kabisa. Na jambo ilo hilo lilitokea niliponunua hisa ya Tiffany nami nilikuwa na upungufu wa dola milioni 1.” Katika makala yenye kichwa “Wacheza Mpira wa Mkono ‘Waliozaliwa Mara ya Pili’ Waongezeka,” habari kutoka San Francisco ilieleza juu ya wachezaji mpira wa kupiga kwa mkono waliosema kufanikiwa kwao ni kwa sababu ya kuzaliwa mara ya pili. Mmoja wao alisema hivi: “Mimi sihojiwi mara nyingi, kwa hiyo ningependa kutumia nafasi hii kumtolea sifa Yesu Kristo. Yeye ndiye wa Kwanza maishani mwangu.” Mwingine alisema kwamba ni “rahisi sana kucheza mpira wa mkono, pamoja na mchezo wa uzima, Mungu anapokuwa mwenzi wako.”

Kisha tena, ripoti moja juu ya kufanikiwa kifedha kwa ‘Dini Inayoonyeshwa katika Televisheni’ ilisema hivi: “Utangazaji wa Dini Hewani Wawa Biashara Kubwa, Wakiwa Wanasambaa United States Yote Wakristo Waliozaliwa Mara ya Pili Walipia Sehemu Kubwa ya Gharama za Maonyesho: Kufanikiwa kwa Jerry Falwell. Lengo: ‘Mioyo na Pesa.’”​—The Wall Street Journal.

Hata hivyo, wanadini wote katika Jumuiya ya Wakristo hawafurahii mtindo huo wa mambo. Kwa hivyo gazeti Times la New York lilisema kwamba ‘Wapresbiteri walitofautiana kimaoni juu ya sehemu ya evanjeli (habari njema) na kwamba uvutano wa vikundi ‘Kuzaliwa Mara ya Pili’ lilikuwa ni jambo lenye kubishaniwa na madhehebu yao.’ Wengine walieleza kwa dharau kwamba mtindo huo wa mambo ni kuongozwa na maono ya ndani tu, na profesa mmoja wa seminari alilalamika kwamba “wanafunzi wengi sana hawafundishiki kamwe” kwa sababu ya kuwa na maoni ya ‘kuzaliwa mara ya pili.’ Katika seminari moja karibu nusu ya wanafunzi walidai kuwa wamezaliwa mara ya pili.

Kwa ujumla maoni ni kwamba ‘kuzaliwa mara ya pili’ kunaenda pamoja na “kujitoa” kwa mtu atumikie Mungu na Kristo, kama ambavyo waevanjeli maarufu (wahubiri wa habari njema wanaojulikana sana) wanavyolisema jambo hilo. Jambo hilo linatokeza maulizo fulani: Yesu alisema kwamba barabara inayoongoza kwenye uzima ni nyembamba na ngumu na kwamba wachache ndio wangeipata. (Mt. 7:13, 14) Pia kwa kurudia-rudia alitaja kwamba wafuasi wake hawakuwa sehemu ya ulimwengu. (Yohana 15:19; 17:16) Maneno hayo yake yanaweza kupatanishwaje na dai la kwamba zaidi ya nusu ya watu wazima wa United States ‘wamezaliwa mara ya pili’? Wala si hayo tu. Ikiwa nusu ya watu wazima wa nchi ni Wakristo ‘waliozaliwa mara ya pili,’ sababu gani kuna uvunjaji wa sheria mwingi sana, uhalifu mwingi sana, kuepa kulipa kodi kwa wingi, udanganyifu mwingi sana katika siasa, uasherati mwingi sana, kupenda mali sana, maoni ya “mimi kwanza” kwa wingi sana? Je! Biblia inaahidi kwamba wale ‘waliozaliwa mara ya pili’ watafanikiwa katika majaribio yao ya kibiashara? Je! Mungu na Kristo wanakuwa wenzi wa wachezaji wa mpira wa mkono, na kuwasaidia washinde michezo?

Yesu alisema hivi kwa mtawala Myahudi, yule Farisayo Nikodemo: “Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa roho hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili.” (Yohana 3:5, 7) Yesu alimaanisha nini kwa kusema hivyo? Yehova Mungu anafanya wengine wazaliwe mara ya pili kwa kusudi gani? Mtu anazaliwa mara ya pili kwa kuchukua hatua gani, na wanaozaliwa mara ya pili wanakuwa na madaraka gani? Kabla ya maulizo hayo kujibiwa vizuri, ni lazima kuthibitisha mambo fulani ya msingi kuhusu kanuni za Yehova Mungu na makusudi yake kwa habari ya dunia na wanadamu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki