Sala Zilizo Katika Zaburi Zinaweza Kukufariji
Ni watu wachache ambao wamepata kuzama wakajisikia namna mtu anavyojisikia anapozama majini, wakamezwa na samaki mkubwa sana kisha wakaokoka hatari hiyo waweze kueleza namna mambo yalivyokuwa. Mtu mmoja aliyepatwa na hayo ni Yona. Alijikuta katika hali ambayo ni vigumu sana kuwapata wanadamu. Hata hivyo aliweza kutumia mawazo yaliyotajwa katika Zaburi fulani zilizoongozwa na Mungu akatoa ombi la sala alipokuwa akipatwa na mambo hayo yasiyotukia kwa ukawaida. Linganisha maneno ya Yona yanayofuata pamoja na yale yaliyo katika Zaburi.
“Nalimlilia [Yehova] kwa sababu ya shida yangu, naye akaniitikia.”—Yona 2:2a.
“Katika shida yangu nalimlilia [Yehova] naye akaniitikia.”—Zaburi 120:1.
“Katika tumbo la kuzimu naliomba.”—Yona 2:2b.
“Ee [Yehova], toka vilindini nimekulilia.”—Zaburi 130:1.
“Nawe ukasikia sauti yangu.”—Yona 2:2c.
“[Yehova], uisikie sauti yangu.”—Zaburi 130:2.
“Maana ulinitupa vilindini, ndani ya moyo wa bahari; gharika ya maji ikanizunguka pande zote.”—Yona 2:3a.
“Nimefika penye maji ya vilindi, mkondo wa maji unanigharikisha.”—Zaburi 69:2.
“Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu.”—Yona 2:3b.
“Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.”—Zaburi 42:7.
“Na kwa habari ya mimi, nilisema, ‘Nimeondoshwa kufukuziwa mbali kutoka mbele ya macho yako! Nitakodoaje macho tena kutazama hekalu takatifu lako?’”—Yona 2:4, NW.
“Nami nalisema kwa haraka yangu, Nimekatiliwa mbali na macho yako.”—Zaburi 31:22.
“Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu; vilindi vilinizunguka; mwani ulikizinga kichwa changu.”—Yona 2:5.
“Maji yamefika mpaka nafsini mwangu.”—Zaburi 69:1.
“Nalishuka hata pande za chini za milima; hiyo nchi na mapingo yake yalinifunga hata milele; lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni, Ee [Yehova], Mungu wangu.”—Yona 2:6.
“O Yehova, wewe umeleta juu nafsi yangu kutoka Sheoli kwenyewe; wewe umeniweka mimi hai, kwamba nisiende chini ndani ya shimo.”—Zaburi 30:3, NW.
“[Nafsi] yangu ilipozimia ndani yangu, nalimkumbuka [Yehova].”—Yona 2:7a.
“Shida yangu nitaitangaza mbele zake. Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu.”—Zaburi 142:2, 3.
“Maombi yangu yakakuwasilia, katika hekalu lako takatifu.”—Yona 2:7b.
“Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake.”—Zaburi 18:6.
“Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo hujitenga na rehema zao wenyewe.—Yona 2:8.
“Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo; bali mimi namtumaini [Yehova].”—Zaburi 31:6.
“Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; nitaziondoa nadhiri zangu.”—Yona 2:9a.
“Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; mtimizie Aliye juu nadhiri zako.”—Zaburi 50:14
“Wokovu hutoka kwa [Yehova].”—Yona 2:9b.
“Wokovu una [Yehova].”—Zaburi 3:8.
Hata sisi tunaweza kutumia Zaburi kama hizo zilizotumiwa na Yona kwa kuzilinganisha na hali zetu wenyewe, kama yeye alivyofanya. Ndiyo sababu, hata hali yako ya sasa iwe ni ya namna gani, unaweza kupata faraja na kitia-moyo katika sala zilizoandikwa katika kitabu cha Zaburi.