Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 3/1 uku. 23
  • ‘Mwanamume Mwenye Kujitoa Sana Sana’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Mwanamume Mwenye Kujitoa Sana Sana’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Washiriki Wapya wa Baraza Linaloongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova Yapanuliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Maisha Yangu Katika Tengenezo la Yehova Lenye Kuelekezwa kwa Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 3/1 uku. 23

‘Mwanamume Mwenye Kujitoa Sana Sana’

William Kirk Jackson alizaliwa Septemba 16, 1901, huko Galveston, Texas. Baada ya kutumia maisha yake akimtumikia Yehova Mungu kwa kujitoa, alimaliza mwendo wake wa kidunia Desemba 13, 1981.

Tangu siku zake za mapema, William alionyesha kupendezwa sana na kweli ya Biblia. Mwaka wa 1915, akiwa na umri wa miaka 14, alijiweka wakf kwa Yehova kupitia Kristo Yesu. Sikuzote alithamini sana kuitwa kwake akiwa mmoja wa watiwa mafuta wa Bwana walio katika mwungano pamoja na Kristo. Juni 1, 1933, aliingia katika utumishi wa wakati wote amtumikie Yehova akiwa painia. Baada ya kutimiza migawo ya pekee katika Washington, D.C., na katika Chicago, Illinois, Ndugu Jackson akawa mshiriki wa daima wa jamaa ya Betheli ya Brooklyn Novemba 13, 1937. Kwa sababu alitumikia pamoja na mshauri wa mambo ya kisheria Hayden C. Covington tangu mwaka wa 1941, yeye alishiriki sana katika utetezi uliofanya Mashahidi wa Yehova wapate ushindi mara nyingi kwa njia yenye sifa katika Mahakama Kubwa Zaidi ya United States (Amerika). Yeye aliwekwa awe katika Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova Oktoba 15, 1971, na baada ya muda akapewa mgawo wa kuangalia mambo katika Halmashauri ya Utumishi na Halmashauri ya Uchapishaji pia.

Ndugu Jackson alikuwa mtu mnyenyekevu asiyejionyesha kuwa wa maana. Hakujionyesha kamwe kuwa mtu wa cheo. Alijulikana duniani kote na maelfu ya watu kama “Bill,” jina la ufupi tu. Alikuwa mtu mpole asiyekasirika upesi, mtu aliyeweza kufikiwa na watu (mwenye kuambilika) wakati wo wote. Alikuwa mtu ambaye ungeweza kufurahia na kupendezwa naye wakati wa kuwa pamoja naye; sikuzote alifanya watu wajisikie wamestarehe, wasiwe na woga. Alipokuwa akiendelea kutoa hotuba ya ukumbusho huko Betheli ya Brooklyn, F. W. Franz alisema : ‘Tunashukuru Yehova Mungu kwa sababu ya kutokeza Shahidi mzuri hivyo. Yeye amemaliza mwendo wake kwa uaminifu, na ana uhakika wa kupewa thawabu yake. Bill Jackson alikuwa mwanamume mwenye kujitoa sana sana.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki