Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 8/15 uku. 22
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Msijifunge Nira Pamoja na Wasioamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Amri ya Kuoa au Kuolewa “Katika Bwana Tu”—Je, Imepitwa na Wakati?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Mwongozo wa Mungu Katika Kuchagua Mwenzi wa Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 8/15 uku. 22

Maswali kutoka kwa Wasomaji

◼ Wakristo mmoja mmoja na kundi lote kwa ujumla wanapaswa kuwa na maoni gani juu ya shauri la Biblia kuoa au kuolewa “katika Bwana tu”?

Kwa habari ya mwanamke ambaye mume wake amekufa, mtume Paulo alishauri hivi: “Yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39) Hilo si shauri la kibinafsi la maoni ya mwanadamu fulani tu. Paulo aliliandika kwa kuongozwa na Mungu; kwa hiyo shauri hilo lenye hekima na upendo limetokana na Mungu. Kwa hiyo, Wakristo wanapaswa kulichukua kwa uzito, si kuliona kama jambo la kupuzwa au kuchukuliwa vivi hivi tu. Maandishi ya kihistoria yaliyo katika Biblia yanakazia jambo hilo.

Wakati Abrahamu alipochagulia Isaka mke, hakuchagua mwanamke kati ya wazoeaji wa dini ya uongo, Wakanaani waliokuwa jirani. Bali, alijipa kazi nyingi ya kutafuta mke, katika nchi ya mbali, kati ya watu wa ukoo wake waliomtambua yule Mungu wa kweli. Vivyo hivyo, Isaka alimwambia Yakobo hivi: “Usitwae mke wa binti za Kanaani.” (Mwanzo 28:1; 24:1-67) Abrahamu na Isaka walitambua kwamba ndoa haikuwa mshikamano wa kimahaba tu. Kujitolea utumishi wa Yehova kulihusika, kwa maana kuoa au kuolewa na mtu asiye mwamini kungeweza kuleta matatizo mazito na hata kumwondoa mtu katika ibada safi.

Hata hivyo si Waebrania wote waliojitenga kwa uthabiti na watu wasiomwabudu Yehova. Kwa mfano, Dina alishirikiana na vijana wa ujirani wao ambao hawakumtumikia yule Mungu wa kweli. Halafu ikawaje? Mmoja wa wanaume vijana aliamka nyege kisha akamnajisi. Inaonekana kwamba kwa muda Yuda aliiacha jamaa yake akatwaa mke Mkanaani. Matokeo yakawa namna gani? Wana watatu walizaliwa kutokana na mwungano huo usiolingana, lakini ikambidi Yehova aangamize wawili kati yao kwa sababu ya ubaya wao. Simeoni pia alizaliwa mwana na mwanamke Mkanaani. Ni wazi hilo lilionekana kuwa ajabu kubwa sana au kuwa jambo baya sana hata likafikia kipimo cha kuweza kutajwa katika orodha ya wazao wa Yakobo.​—Mwanzo 34:1, 2; 38:1-10; 46:8-10.

Wakati Mungu alipotoa sheria za kuongoza Israeli, aliwaonya wasifanye mapatano ya ndoa na mtu asiyemwabudu Yehova. (Kumbukumbu la Torati 7:2-4) Hekima ya jambo hilo ilikaziwa na msiba uliompata Sulemani. Labda yeye alidhani kwamba, kwa sababu alikuwa na hekima isiyopatikana na watu wa kawaida, angeweza kukabiliana na tatizo au jaribu lo lote ambalo lingetokana na kuoa wanawake wasiomtumikia Yehova. Lakini Sulemani alipopuza shauri la Mungu, hata yeye alipatwa na kihoro.​—1 Wafalme 11:1-6.

Mwishowe, katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, Mungu alirudia shauri hili: Usioe wala kuolewa na mtu asiyemtumikia Bwana. Shauri lenye kuongozwa na Mungu halikuwa, ‘Ukipata mtu safi, mwenye tabia nzuri, inaruhusika kuchumbiana na kuoana naye ukiwa na tumaini la kwamba yeye atakuwa Mkristo hatimaye.’ Bali Neno la Mungu linasema hivi waziwazi: “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini.” (2 Wakorintho 6:14) Kuoa au kuolewa na mtu ambaye si Mkristo aliyekwisha kubatizwa kungekuwa ni tendo la kulipuza shauri hilo zito.

Kwa sababu kundi lote la Mashahidi wa Yehova linalichukua jambo hilo kuwa la hekima na zito, wao hawataki kusaidia mtu ye yote atende kinyume chalo. Kwa mfano, ikiwa ndugu au dada wa kiroho anaanza kuchumbiana au kufanya matembezi na mtu asiye shahidi wa Yehova, wengine kundini wasingepaswa kumtia moyo aendelee hivyo kwa kushirkiana kirafiki na yule asiyeamini. Wao wanakubaliana na Biblia kwamba huyo asiye Mkristo si mshirika mwema. (1 Wakorintho 15:33) Lakini wanapaswa waendelee kuonyesha wanapendezwa na huyo ndugu au dada yao. Huenda wakaweza kumpa onyo la upole lenye busara na la kutia moyo ili kumsaidia Mkristo huyo mwenye kuacha njia aepuke pito lililofuatwa na Sulemani.​—Linganisha 2 Wathesalonike 3:14, 15, NW.

Lakini namna gani Shahidi akipanga kupuza shauri la Mungu kisha aoe au aolewe na asiye Shahidi aliyebatizwa? Kusipokuwa na sababu pekee sana ya kufanya hivyo, kina ndugu kundini wasingepaswa kufungamanisha nira hiyo isiyopatana. Wala jumba la Ufalme lisingeruhusiwa kwa matumizi ya arusi iyo. Linaruhusiwa kutumiwa kwa ndoa za Wakristo wawili waliobatizwa wanaooa “katika Bwana tu.” Au nyakati nyingine huenda likatumiwa na watu wawili wanaotumikia Mungu kwa ukawaida wakiwa sehemu ya kundi na ambao karibuni watabatizwa. Kwa kutokuruhusu Jumba la Ufalme litumiwe na Shahidi anayepanga ‘kufungwa nira moja na asiyeamini,’ wazee wa kundi wanaweza kukazia uzito wa shauri la Mungu la kuoa au kuolewa “katika Bwana tu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki