Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 1/1 uku. 3
  • Kuthamini Kumeenda Wapi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuthamini Kumeenda Wapi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakiwa “Wamekosa Kuthamini Kabisa”
  • Kwa Nini Uwe Mwenye Shukrani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Kwa Nini Uonyeshe Uthamini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Kwa Nini Uonyeshe Shukrani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • ‘Wale Tisa Wako Wapi?’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 1/1 uku. 3

Kuthamini Kumeenda Wapi?

MVULANA huyo wa miaka kumi na miwili alikuwa akikausha vyombo, bila kutaka. Ghafula, sahani kubwa likateleza likaanguka na kuvunjika-vunjika juu ya sakafu ya jikoni. Unyamavu mfupi uliofuata ulionekana kama hauna mwisho. Halafu mamaye akasema: “Wajua, Robert, kati ya mara zote ambazo umenikaushia vyombo, hii ndiyo mara ya kwanza umeangusha kimoja. Nafikiri umeweka rekodi ya namna fulani.”

Ule wasiwasi uliokuwa usoni pa mvulana huyo ukaondoka na akamtabasamia (akamchekelea) mamaye kwa upendo. Maneno machache ya mama ya kuthamini kwa wakati unaofaa yalikuwa yameifanya siku hiyo iendelee kuwa nzuri kwa mwanaye na kwake. Maneno ya mtu mwenye hekima Sulemani, ni ya kweli kama nini! “Neno linenwalo wakati wa kufaa, Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.”​—Mithali 25:1, 11.

Wakiwa “Wamekosa Kuthamini Kabisa”

Inachangamsha moyo kweli kweli kuambiwa maneno machache ya sifa au kuthamini. Lakini kuthamini kumeenda wapi? Katika ulimwengu wa leo wenye kupenda rnali, maneno ya kuthamini kwa moyo mweupe yanapotea! Mahali pa kuthamini panachukuliwa na nia ya “mimi kwanza.” Katika maneno ya wengi mnakosekana usemi “Asante sana!” Hali hiyo inatimiza maneno ya mtume Paulo: “Lakini lazima utambue kwamba katika siku za mwisho nyakati zitakuwa zimejaa hatari. Watu watajifikiria wenyewe kabisa . . . Watakuwa wamekosa shukrani kabisa.”​—2 Timotheo 3:1-5, Phillips.

Wakati uo huo, mahali pa kuthamini pamechukuliwa na kupiga kilemba cha ukoka (kusifu-sifu kiuongo). Semi za kuthamini za kweli zinatoka moyoni bila wazo lo lote la kujipatia faida ya kibinafsi. Hata hivyo, kupiga kilemba cha ukoka, wakati mwingi si kwa moyo mweupe na ni kwa kutia chumvi, na kunatokana na kusudi jingine la kufanikiwa au kupata faida fulani za kibinafsi. (Yuda 16) Ni nani anayetaka kupigwa kilemba cha ukoka kwa moyo usio mweupe? Lakini kuthamini kwa kweli ni jambo tofauti!

Mwandikaji Mark Twain alisema hivi wakati mmoja: “Naweza kutafakari sifa nzuri kwa miezi miwili kabisa.” Wengi wetu tunajisikia vizuri mtu anapotusifu kwa weupe wa moyo. Kwa kweli, kusifiwa au kuthamini kikweli kunaweza kutuchochea tuendelee kujitahidi tuwezavyo na vilevile kusifu au kuthamini wengine tunapokuwa na nafasi ya kufanya hivyo.

Semi nyingi katika Biblia zinaonyesha kwamba kuthamini kutoka moyoni ni wema wa kimungu. Kwa mfano, zaburi nyingi zina maneno ya kuthamini. Kwa mfano: Mtunga zaburi Daudi alisali kwamba akae katika nyumba ya ibada ya Yehova Mungu maisha yake yote na kuiona ‘kwa kuthamini.’ (Zaburi 27:4, NW) Asafu, mtunga zaburi mwingine, alitangaza hivi: “Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru.” (Zaburi 75:1) Kwa hiyo inafaa kwamba tuchunguze habari hii ya kuonyesha kuthamini.

Hata hivyo, tunawezaje kuwaonyesha wengine kuthamini? Na namna gani juu ya kumwonyesha kuthamini Yule aliyefanya vitu vyote?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki