Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 5/15 uku. 3
  • Jina la Mungu Katika “Agano Jipya”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Katika “Agano Jipya”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Jina Yehova Linapaswa Kuwa Katika Agano Jipya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • “New World Translation” ya Utaalamu na Yenye Kufuatia Haki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jina la Mungu na “Agano Jipya”
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 5/15 uku. 3

Jina la Mungu Katika “Agano Jipya”

TAFSIRI zilizo nyingi za “Agano Jipya” hazitumii jina lo lote la pekee katika kumtaja Mungu Mweza Yote. Kwa sababu gani? Je! sababu ni kwamba zinafuata kwa uangalifu sana maandishi ya kwanza ya Kigiriki? Katika visa vingi ni wazi kwamba hazijali sana uangalifu huo, kwa sababu hazitumii jina Yehova hata katika “Agano la Kale.” Hata hivyo katika Kiebrania cha kwanza kabisa, zaidi ya kuwako kwa maneno ya kusema Bwana na Mungu, jina la pekee la Mungu linaonekana mara karibu 7,000.

Walakini, watafsiri fulani wametambua kwamba jina la kimungu linastahili kwa haki kuwa katika “Agano Jipya.” Sababu iliyo kubwa zaidi ya ustahili huo ni kwamba “Agano Jipya” lina maneno yaliyotokana moja kwa moja na Maandiko ya Kiebrania ambayo katika hayo jina hilo limetumiwa. Kwa hiyo inapendeza kuona kwamba katika lugha ya Wajeremani, kuna tafsiri zisizopungua tano za “Agano Jipya” zenye jina la kimungu.

Moja ya tafsiri hizo, ile iliyofanywa na Dominikus von Brentano katika mwaka wa 1976, ambayo inalitumia jina la kimungu mara mbili katika maandishi yake makuu ya kwanza kabisa, imetajwa-tajwa katika vitabu vya zamani vya Watch Tower. Tafsiri nyingine mbili zinatumia jina hilo kwenye Marko 12:29—moja ni tafsiri ya Stolz, iliyochapishwa katika Zurich, Uswisi, mwaka wa 1781, na ile nyingine ni tafsiri ya Profesa Dakt. Johann Babor, iliyochapishwa katika Vienna, Austria, mwaka wa 1805. Kuna ile pia inayoitwa Biblia ya Bonner, iliyotafsiriwa na Profesa D. P. Dausch na ikachapishwa katika Bonn, Ujeremani, katika mwaka wa 1932, nayo inatumia jina “Jahve” kwenye Luka 20:37.

Tafsiri nyingine ya Kijeremani inalitumia jina hilo, Yehova, mara kumi katika “Agano Jipya.” Hiyo ni tafsiri yenye vitabu viwili ya New Testament of the Holy Scriptures iliyotokea Munich, Ujeremani, katika mwaka wa 1789 na 1790. Ingawa jina la mtafsiri halionyeshwi, kitabu Die Bibel in Deutschland (Biblia Katika Ujeremani), katika ukurasa wa 281, kinasema hivi: “Tafsiri hiyo imefanywa na [Sebastian] Mutschelle. Yeye alizaliwa Januari 18, 1749, katika Allershausen bei Freising, na alijiunga na ushirika wa Wayeswiti akiwa na umri mdogo.”

Jina la kimungu linaonekana katika tafsiri za “Agano Jipya,” si katika Kijeremani tu bali pia katika lugha nyingine zipatazo 50, kutia ndani Kiebrania.

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Sababu Linakuhusu Wewe

’Lakini kuna tofauti gani tukitumia jina la Mungu au tusipolitumia?’ huenda mtu akauliza. Kuna tofauti kubwa! Fikiria jambo hili: Katika “Agano Jipya” inasemwa kwamba Mungu ‘angeangalia mataifa ili achague watu kati yao kwa ajili ya jina lake.’ (Matendo 15:14)

Ikiwa wewe hulijui wala hulitumii jina hilo, kweli unaweza kuhesabiwa kuwa mmoja wa watu ambao Mungu anachagua wawe wake mwenyewe? Zaidi ya kulijua jina la Mungu, inatupasa pia tulisifu mbele ya wengine, kama Yesu Kristo alivyofanya alipokuwa duniani.​—Mathayo 6:9; Yohana 17:6, 26.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki