Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 6/15 kur. 3-21
  • Je! Mungu Anatunza Wakati?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Mungu Anatunza Wakati?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Sababu Gani Tuhangaikie Kutunza Wakati?
  • Kuichunguza Orodha ya Wakati ya Mungu
  • Maoni Yetu ya Wakati Yanaweza Kuharibiwa na Imani
  • Msaada wa Kuwa Wenye Kujali Wakati
  • Mtegemee Yehova—Mungu wa “Nyakati Na Majira”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova—Mungu wa Nyakati na Majira
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Mwaka wa 2000 Ni Wenye Maana Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998
  • Nyakati na Majira Mikononi mwa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 6/15 kur. 3-21

Je! Mungu Anatunza Wakati?

AKIWA ndiye Msababishi wa Kwanza wa matukio, Yehova Mungu ndiye muumba wa wakati. Uhakika huo unaweza kuonwa kwa kusoma kitabu cha kwanza cha Biblia. Kwenye Mwanzo 1:1, 14 tunasoma hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili ya majira na siku na miaka.”

Hivyo Yehova alianzisha mwendo wa madude makubwa ya kuonyesha wakati dunia yenye kujizunguka katika mpini wayo, mwezi wenye kuizunguka dunia, na vyote hivyo viwili vikawa vyenye kulizunguka jua ili kutupa sisi siku, miezi na misimu (majira). Vitu hivyo vya kimbingu vinatusaidia tujue ni saa ngapi, bila kutudai pesa wala wajibu ndipo viweze kuendelea kuzunguka au virekebishwe kwa sababu vimeharibika.

Kwa Sababu Gani Tuhangaikie Kutunza Wakati?

Yehova anahangaikia kutunza wakati na anataka sisi pia tuwe hivyo. Tumeumbwa tuwe namna hiyo. Lakini si watumishi wote wa Mungu wameonyesha hekima katika matumizi ya wakati. Wengine wamepuza kusitawisha maoni ya kutaka sana kufuata orodha ya wakati ya matukio yaliyopangwa na Mungu.

Kwa mfano, katika karne ya saba K.W.K. watu wachaguliwa wa Mungu hawakuwa na udhuru (kisababu) wa kutokujua ilikuwa ni saa ngapi. Nabii Yeremia aliandika hivi: “Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za [Yehova].” (Yeremia 8:7) Kwa silika wanyama wanajua nyakati za kutenda kulingana na mabadiliko ya misimu. Lakini ijapokuwa Waisraeli walikuwa wamesihiwa mara nyingi akilini na moyoni, wao hawakutaka kujua kwamba wakati wa Mungu wa kuwahukumu ulikuwa umefika. Tunaweza kusema hawakujali.

Namna gani sisi leo? Je! tunajua ni saa ngapi? Yehova amekuwa sikuzote na wakati uliowekwa na kuonyesha mapenzi yake na hukumu yake. Katika hotuba ambayo mtume Paulo aliwatolea Waathene, yeye alisema hivi: “Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua.” (Matendo 17:30, 31) Je! wewe unaamini kwamba tuko karibu na hiyo ‘siku ya hukumu’? Au unafikiri wakati huo uko mbali sana?

Katika karne ya kwanza wakati ulifika wa kutokea duniani kwa mtu yule ambaye Mungu angemtumia kuihukumu dunia. Kufika kwake kulikuwa tarehe ya maana sana katika orodha ya wakati ya Mungu, kama vile Biblia inavyosema: “Wakati kikomo kamili cha wakati kilipofika, Mungu alituma Mwanaye, ambaye alikuja kuwa kutoka kwa mwanamke na ambaye alikuja kuwa chini ya sheria.” (Wagalatia 4:4, NW) Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, alifika katika wakati barabara.

Kuja huko kwa Kristo katika karne ya kwanza kulionyesha mwanzo wa kipindi cha hukumu kwa mji wa Yerusalemu. Katika mwaka wa 33 W.K. Yesu aliwaonya wakaaji hao juu ya uharibifu ambao ulikuwa ukija kwa kuletwa na jeshi la maadui. Alisema hivi: “Watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiliwa kwako.” (Luka 19:44) Miaka 37 baadaye unabii huo ulitimia. Kama wewe ungalikuwa hai wakati huo, je! ungalijua ilikuwa saa ngapi? Je! ungalijua huo ulikuwa wakati wa Mungu wa kumtuma Mwanaye duniani na wa kufikiliza hukumu juu ya Yerusalemu?

Ungalijuaje? Vivyo hivyo, unaweza kujuaje ni saa ngapi leo? Unaweza kujuaje kama tuko au hatuko karibu na ile ‘siku ya hukumu’ iliyotabiriwa?

Kuichunguza Orodha ya Wakati ya Mungu

Sawa na vile tunahitaji kuchunguza orodha ya wakati yenye kuonyesha saa za kufika na kuondoka kabla hatujasafiri kwa gari-moshi au ndege, ndivyo tunavyohitaji orodha ya wakati ili tujue Mungu anataka tufanye nini na tuyafanye wakati gani. Biblia inakuwa kama orodha ya wakati ya Mungu. Kwa kuchunguza Kitabu hicho tunaweza kujua wakati uliopangwa wa kufika kwa matukio yanayohusu wanadamu. Kwa mfano, Wayahudi wote wa karne ya kwanza wangalipaswa kuwa wamejitayarishia kuja kwa Kristo. Kwa sababu gani? Kwa sababu Mungu alikuwa amekwisha kumtumia nabii wake Danieli mapema sana atabiri kwamba Masihi, au Kristo, angefika mwaka wa 29 W.K. (Danieli 9:24-27) Kwa kweli, Wayahudi katika karne ya kwanza walioujua unabii wa Danieli walikuwa wakingojea kutokea kwake mwaka huo huo. (Luka 3:1, 2, 15) Mwana chuo Myahudi Abba Hillel Silver aliandika hivi: “Masihi alitazamiwa karibu na robo ya pili ya karne ya kwanza W.K.”

Jambo lile lile linaweza kusemwa kuhusu leo. Kwa kutumia orodha ya wakati ya Biblia tunaweza kuamua kwamba sasa ndio wakati wa kuwapo kusikoonekana kwa Kristo akiwa Mfalme.a Basi, kuja kwake afikilize hukumu ya Mungu juu ya waovu na wakati wake wa miaka 1,000 ambayo ni ‘siku ya kuhukumu ulimwengu kwa haki’ uko karibu sana.​—Matendo 17:31; Danieli 4:10-17; Mathayo 24:7-31; Luka 21:24; Ufunuo 20:4-15.

Maoni Yetu ya Wakati Yanaweza Kuharibiwa na Imani

Karne kumi na tisa zilizopita watu wo wote walioshindwa kuthamini orodha ya wakati ya Mungu na wakawa na kiherehere cha kutokungojea wakati uliowekwa na Yehova wa kufika kwa Mwanaye walikosa baraka kubwa ajabu. Vivyo hivyo leo, tukiwa watu wa hala hala na kuuliza, “Iko wapi ahadi ile ya [kuwapo] kwake?” hata sisi tutakosa upendeleo wa Mungu kwa sababu ya kutokujua ni saa ngapi. (2 Petro 3:4) Namna hiyo ya roho ya wasiwasi ililikalia kundi la Kikristo la Efeso kwa sababu ya mazingira yao, nayo ilielekea kuleta hatari ya kuharibu imani yao. Je! wewe unakuta imani yako ikidhoofika kwa sababu ya kiherehere chako cha kutokungojea orodha ya wakati ya Mungu? Tunaweza kujifunza nini kutokana na shauri ambalo Paulo aliwapa Waefeso?

Wagiriki wasio Wakristo katika Efeso hakuamini kwamba wakati ulisonga upande mmoja tu ukielekea mbele bila kurudi nyuma. Shule za falsafa ya Kigiriki zilifundisha maoni ya kwamba wakati ulisonga mbele kisha ukazunguka na kurudia mahali ulipoanzia. Zilifundisha kwamba matukio yale yale yanajirudisha-rudisha na kutendeka tena na tena bila kikomo. Kama mtu aliharibu bure wakati wake katika mzingo mmoja wa maisha, angeweza kuupata tena wakati wote huo kwa kuishi mara nyingine. Namna hiyo ya kufikiri ingaliweza kuingiza katika Wakristo Waefeso maoni ya kutokujali orodha ya wakati wa Yehova wa kutokea kwa matukio, kutia ndani tukio la hukumu.

Pia, mtindo wa maisha ya kufuatia anasa hasa uliwazunguka Wakristo wa Efeso, ukawakaza sana wasiikumbuke sana orodha ya Mungu ya kuweka wakati. Kama wangeamini kwamba ni hekima kuishi kwa ajili ya wakati uliopo tu kwa kujitia katika utoshelezaji wa nyege na tamaa zao wenyewe wangekuwa sawa tu na wanyama wasio na wazo la wakati uliopita wala ujao, bali wa sasa tu. Kama walitaka kuurithi wakati ujao, walihitaji kukumbuka jambo hili la uhakika: “Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.”​—Waefeso 5:5.

Katika mistari inayofuata, Paulo anawaonya Wakristo hao wawe na fahamu kabisa ni saa ngapi. Ama sivyo, wangeweza kupumbazwa wafikiri kwamba walikuwa na wakati wa kutosha wajiingize katika mwenendo usio wa Kikristo na kuponyoka bila ya kuishiwa na hali ya kiroho. Yeye alisema: “Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu [inakuja] . . . mkihakiki ni nini impendezayo Bwana.” (Waefeso 5:6, 10) Kwa hiyo, kulingana na orodha ya wakati ya Mungu, mwenendo wetu unaonyesha wakati wetu ujao utakuwa namna gani.

Waefeso hao wangeweza kupataje kibali ya Mungu? Sisi tunaweza kuipataje? Ni kwa kuukomboa wakati.’ Kwa ‘kufahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Yehova.’ (Waefeso 5:16, 17) Jambo hilo lazima lifanywe wakati gani? Sasa Kwa sababu gani? Kwa sababu huenda tusiwe na nafasi nyingine ya kufanya hivyo. Tangu mwaka wa 1914 matukio mengi sana yaliyotabiriwa katika Biblia kwamba yangeonyesha hizi ni “siku za mwisho” yamekuwa yakitukia, na yote yameonwa na kizazi kimoja, kutuonyesha kwamba wakati umepita mbio. Hatutaki tuishiwe kabisa na wakati wa kusitawisha uhusiano mwema pamoja na Yehova na Hakimu aliyewekwa naye, au tunataka?​—Mathayo 24; Marko 13; Luka 21; 2 Timotheo 3:1-5; 2 Petro 3:10, 11.

Msaada wa Kuwa Wenye Kujali Wakati

Mungu amepanga kuwe na baraza ya watu waliojiweka wakf na waliotiwa mafuta kwa roho watusaidie tuwe wenye kujali wakati. Huyo “mtumwa mwaminifu mwenye akili” anatupakulia ‘chakula cha kiroho kwa wakati wake’ na kutuhimiza ‘tuzidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote.’ (Mathayo 24:45; 1 Wakorintho 15:58) Kwa njia hiyo tunaweza kuwa watu wenye mafaa katika utumishi wa Mungu, sasa na hata wakati ujao. Lakini tutagharimiwa kitu fulani. Ni wakati. Sisi sote tuna kipimo kile kile cha wakati wa kununua kila juma, yaani, saa 168. Je! wewe unaununua wakati wako kwa uzuri wa kadiri gani? Je! njia yako ya kufanya hivyo inaonyesha unajua kweli kweli sasa ni saa ngapi kulingana na maoni ya Mungu.

‘Mimi sina wakati,’ wengi watasema hivyo. Hiyo ndiyo sababu ni lazima uwe na nia ya kununua wakati kutokana na sehemu nyingine za maisha yako. Mambo yote, kazi za kujiburudisha tu, muziki, tafrija, kazi ya kimwili, yanashindania kuuchukua wakati wako. Tena vyombo vipya, kama sinema za televisheni zenye kutumia ukanda, vinaweza kuwa vilaji vikubwa vya wakati wako. Ingawa huenda likawa jambo la kufurahika au la uhitaji kabisa kutumia wakati fulani katika tafrija zinazofaa, je! maisha yako yanaonyesha una usawaziko wa matumizi ya unyofu ya wakati wako kulingana na yale unayoyajua juu ya orodha ya wakati ya Mungu?

Wewe unataka maneno gani ya mshairi yatumiwe kukuhusu?

Haya:

“Ati wakati wapita kasi?

Haupiti! Wapitao ndisi.”

Au haya:

“Kila siku nitakuhimidi,

Nitalisifu jina lako milele na milele.”​—Zaburi 145:2.

Unayoyataka yataamuliwa na jambo la kama kweli wewe unajua ni saa ngapi.

[Maelezo ya Chini]

a Ili upate habari zaidi, angalia kitabu “Let Your Kingdom Come,” sura ya 14, kilichochapwa na Sosalti.

[Picha katika ukurasa wa 20]

Orodha ya wakati ya kuruka kwa ndege inajulisha wasafiri saa za kufika na saa za kuondoka

Orodha ya wakati ya Biblia inatujulisha wakati matukio ya Mungu yatakapotukia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki