Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 10/1 kur. 14-17
  • Kwa Sababu Gani Barua kwa Waefeso?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Sababu Gani Barua kwa Waefeso?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mahali Pakuu pa Kidini pa Kale
  • Kurudisha Umoja na Amani
  • Kujitahidi Kuwa na Amani na Umoja
  • Kitabu Cha Biblia Namba 49—Waefeso
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • “Upendo Wako wa Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Umoja wa Kikristo Unamletea Mungu Utukufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mwungamano ni Hakika Kupitia Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 10/1 kur. 14-17

Kwa Sababu Gani Barua kwa Waefeso?

MKUU ni Artemi wa Waefeso!” Je! unaweza kuwazia uwanja wa michezo ya maonyesho, wenye nafasi ya kukaliwa na watazamaji elfu 25, ukiwa umejawa na watu wenye ghasia za hasira ya kidini wakiyasema-sema maneno hayo yaliyotajwa juu bila kuacha, kwa muda wa saa mbili? Kweli ndivyo ilivyokuwa!—Matendo 19:28, 34, NW.

Kwa sababu gani waliwaka moyo hivyo? Artemi alikuwa nani? Na zaidi, Waefeso walikuwa akina nani? Ni nani aliyewapelekea barua​—na kwa sababu gani?

Mahali Pakuu pa Kidini pa Kale

Efeso ulikuwa mmoja wa miji yenye kujulikana zaidi sana ya karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu, na mji huo ulikuwa na watu waliokadiriwa kuwa zaidi ya robo milioni. Mji wenyewe ulikuwa mahali pakuu penye biashara ya utajiri na utamaduni wa hali bora, lakini watu wengi sana hawakuvutiwa na eneo hilo kwa sababu ya utajiri tu, wala hali ya hewa yenye usawaziko mzuri na upendezi wa eneo lenyewe tu. Efeso ulikuwa mahali pakuu pa kidini pa ulimwengu wa kale na ulijivunia hekalu lililokuwa kubwa sana hata likafikia kipimo cha kuitwa moja la maajabu saba ya ulimwengu.

Yule mungu-mke Artemi, au Diana aliabudiwa katika hekalu hilo lenye mapambo ya thamani kubwa, ambapo dhahabu inasifika kuwa ilitumiwa kati ya miungano ya nguzo za marmar. Mara kwa mara, watu wafikao elfu 700 wa Efeso na wa nchi za mbali walikuwa wakijipanga kwenye barabara mbalimbali wakati huyo “mungu-mke aliye bikira” alipokuwa akipitishwa sehemu za mjini aonekane na watu. Utengenezaji na uuzaji wa sanamu za fedha za huyo mungu-mke wa uzazi mwenye maziwa (matiti) mengi ulikuwa biashara yenye kusitawi katika Efeso.​—Matendo 19:24, 25.

Yule mwanamume Paulo aliuingia mji huo ukiwa namna hiyo ili awahubirie Waefeso juu ya Ukristo. Yeye alikuwa ameagizwa na Yesu Kristo awe “mtume wa watu wa Mataifa.” (Warumi 11:13) Kundi lilianzishwa katika Efeso kisha likakua upesi-upesi. Wapya waliharibu sanamu zao na kurarua vitabu vyao vya miujiza ya kiuchawi kwa haraka. (Matendo 19:19) Kwa sababu dini hiyo mpya yenye kukua upesi-upesi ilipinga matumizi ya sanamu, Demetrio, mfua-fedha, alichochea watu wakakaribia kufanya fujo zenye ghasia, kisha wakaanza kupiga makelele wakisema, “Mkuu ni Artemi wa Waefeso!”

Paulo hasa, mwandikaji wa barua yenyewe, ndiye aliyekuwa ameweka msingi wa kuanzisha kundi la Efeso. Lilikuwa kundi lenye watu wa Mataifa sana-sana, yaani, watu wasio Wayahudi. (Waefeso 3:1) Wale waliopata kuwa Wakristo katika Efeso walikuwa wameacha namna ya ibada yenye kushusha tabia.​—Waefeso 4:17-19.

Kurudisha Umoja na Amani

Paulo aliwaandikia Waefeso akiwa Roma gerezani, karibu na mwaka wa 60 au 61 W.K. (Waefeso 1:1; 6:20) Karibu na mwanzo wa barua yenyewe anatoa taarifa ya kusudi la ajabu la Mungu la kurudisha umoja na amani, kama lilivyopangwa katika Maandiko. Kusudi hilo ndilo linalokuwa wazo kuu lenye kutegemewa na barua yote.

Paulo aliandika hivi: “[Mungu] alitujulisha sisi siri takatifu ya mapenzi yake. Ni kulingana na furaha yake njema aliyokusudia ndani yake mwenyewe kwa ajili ya usimamizi katika utimilifu wa nyakati zilizowekwa, yaani, kuvikusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni na vitu vilivyomo duniani.” (Waefeso 1:9, 10, NW) Kama inavyoonyeshwa hapo, yalikuwa ni mapenzi ya Mungu kurekebisha makosa yote ambayo yalikuwa yametukia sehemu zote za ulimwengu mzima kwa sababu ya uasi wa Shetani.

Paulo aliwataka hao Wakristo Waefeso wa Mataifa wapate umaana kamili wa pendeleo kubwa ajabu walilokuwa nalo la kuweza kuhusika kwa ndani sana katika utimizo wa mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo, mara tu baada ya salamu yake ya kuanza mazungumzo, Paulo aliwaonyesha hali yao yenye pendeleo. Wao walikuwa wamekuwa sehemu ya kikundi ambacho Mungu alikuwa amechagua “kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu” wakawe pamoja na Kristo katika Ufalme wake wa kimbingu.​—Waefeso 1:3-7.

Kwa kweli, kufurahia na Wayahudi taraja la kuwa watawala wa kimbingu pamoja na Kristo katika Ufalme wa Mungu kulikuwa pendeleo kubwa kwa Waefeso wa Mataifa, ambao hapo kwanza ‘walikuwa wametengwa mbali’ na ‘wakawa hawana Mungu katika ulimwengu’! Hiyo ndiyo ile “siri takatifu” ambayo Paulo anaitaja-taja katika barua yake, “yaani, kwamba watu wa mataifa wapaswe kuwa warithi wa ukamatano na washiriki pamoja na sisi wa ile ahadi katika mwungano pamoja na Kristo Yesu.”​—Waefeso 2:11-13; 3:3-6, NW.

Kwa hiyo barua kwa Waefeso inafunua kwamba Yehova Mungu anakusudia kurudisha umoja na amani katika ulimwengu mzima wote. Kama vile Paulo alivyoandika, Mungu ‘atavikusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni na vitu vilivyomo duniani.’ Ni kabla tu ya uasi wa Shetani kulipokuwa na umoja wa kweli katika ulimwengu mzima wote. Lakini kupitia “usimamizi” wa Mungu, yaani, kushughulikia au kusimamia mambo, umoja wa namna hiyo utakuwako tena.

Kwa kumkubali Kristo kuwa mkombozi wavyo, “vitu vilivyomo mbinguni”​—yaani, wale watu wanaochukuliwa wawe wana wa kulelewa wa kimbingu​—‘vinakusanywa tena pamoja katika Kristo.’ Lakini, kupatana na kusudi la Mungu, wakati unaofaa lazima uje wa kutimiza ile sehemu ya pili ya “usimamizi” Wake, yaani, kukusanya pamoja “vitu vilivyomo duniani.” Jambo hilo linatukia wakati wa kuwapo kwa Kristo katika mamlaka ya Ufalme anapokusanya “kondoo wengine” wake ambao wamewekewa uzima wa kukaa duniani chini ya Ufalme wa kimbingu.​—Yohana 10:16.

Akiendelea na kichwa cha habari yake, Paulo anaonyesha namna amani na umoja zinavyohitaji kufuatiwa na wote walio ndani ya “lile kundi, ambalo ni mwili [wa Kristo].” (Waefeso 1:22, 23, NW) Hivyo hakutakuwa tena na tofauti kati ya Myahudi na Mtaifa, kati ya kutahiriwa na kutokutahiriwa. Ni lazima wote wawe na nia ya kufanya kazi kwa umoja na amani.​—Waefeso 2:11.

Kwa ujumla Paulo anatumia neno “mwungano” (NW) mara 13 katika barua hii, zaidi ya mara anazolitumia katika yo yote ya barua zake. Na anatumia neno “amani” mara nane, zaidi ya mara anazolitumia katika barua nyingineyo yote isipokuwa ile waliyoandikiwa Waroma. Tunaweza kuelewa vizuri zaidi uhitaji wa kukazia umoja na amani tunapofahamu tofauti kubwa-kubwa zilizokuwa zimekuwako muda wa karne nyingi kati ya Wayahudi na Mataifa. (Matendo 10:28) Paulo anakazia daraka la maana la Kristo katika jambo hilo. “Kwa maana yeye ndiye amani yetu,” Paulo anasema, “aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza [Torati ya Musa] cha kati kilichotutenga.”​—Waefeso 2:14.

Kujitahidi Kuwa na Amani na Umoja

Sura tatu za mwisho za barua ya Paulo zinataja hali mbalimbali na kutoa mashauri ambayo yangeleta amani na umoja katika hali za wakati huo huo za Waefeso hao. Nazo amani na umoja zinaweza kupatikanaje? Kutumia upendo kunahitajiwa kabisa. Ili kutilia mkazo jambo hilo Paulo anatumia maneno “upendo,” “-napenda” na “kupenda” mara 19, mara nyingi kuliko katika yo yote ya barua zake! Hivyo anahimiza ‘kuchukuliana katika upendo, na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa roho katika kifungo cha amani.’​—Waefeso 4:2, 3.

Paulo anaendelea kueleza mipango ya Mungu ya kuleta utendaji wenye kuunganishwa kwa usawa mzuri. Kama vile anavyosema, Mungu “alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti; na wengine kuwa wachungaji na waalimu . . . hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani.” Halafu Paulo anautumia mfano wa shughuli zenye kuungana kwa usawa mzuri za mwili wa kibinadamu, ambazo “huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo.”​—Waefeso 4:11-16, NW.

Kwa hiyo ilikuwa lazima sasa mambo yenye kuchafua amani na umoja yaepukwe. Mambo hayo yangekuwa ni pamoja na kusema uongo, kuwa wenye ghadhabu au wenye uvivu, na kutamka semi zilizooza badala ya semi zilizo njema na zenye kujenga. Kusema kweli kuiba ni jambo ambalo watu walitiwa moyo wafanye katika Efeso, kwa kuwa mwivi angeweza kukimbilia hekalu la Artemi na akifika huko hangeweza kukamatwa. Lakini Paulo alisema: “Mwibaji asiibe tena.”​—Waefeso 4:25-30.

Ebu wazia namna matumizi ya onyo la upole la Paulo linalofuata yangeleta amani na umoja: “Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.”​—Waefeso 4:31, 32.

Uasherati, uchafu, pupa (kutamani), mwenendo wenye aibu, kusema mambo ya upumbavu, kufanya mizaha ya matusi, ulevi​—yote hayo yanaingiza mtu katika matata pamoja na Mungu pia, si na wanadamu wenzake tu. Kwa hiyo Paulo anahimiza hivi: “Wala msishirikiane [na watu wa mataifa katika] matendo yasiyozaa ya giza.” “Angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima . . . kwa maana zamani hizi ni za uovu.”​—Waefeso 5:1-20.

Paulo anaeleza kwamba kufuata mfano wenye upendo wa Kristo na mashauri ya Neno la Mungu kutaleta amani ndani ya jamaa za watu. Anakazia pia namna wafanya kazi na matajiri wao wanavyoweza kuchukuliana kwa kuamanika wakikumbuka wajibu ambao kila mmoja wao anapaswa kutimizia Mungu. (Waefeso 5:21–6:9) Hata hivyo inahitajiwa kabisa kujua kwamba aliyekuwa wa kwanza kuchafua amani na umoja wa ulimwengu mzima wote, Shetani Ibilisi, atapinga vikali jitihada zote za Wakristo za kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo ni lazima wao ‘wavae silaha zote za Mungu’ ili kumzuia sana Ibilisi na mashetani wake kwa njia yenye mafanikio.​—Waefeso 6:10-18.

Tunapofikiria mambo yote yaliyo katika barua ambayo Paulo aliandikia Waefeso, tunapiga asante kubwa kwa Mungu kwa sababu ya kumwongoza aiandike! Barua yake imesifiwa na wanachuo wengi, na mmoja kati yao aliitaja kuwa “inazungumza pande zote za dini ya Kikristo ingawa ni fupi.” Si kwamba tu inaeleza wazi kusudi kubwa la Mungu la kurekebisha makosa yaliyo katika ulimwengu mzima wote, bali pia inatoa mashauri mengi yenye mafaa na maonyo ya upole ya kutusaidia tumtumikie Mungu kwa njia itakayotuwezesha kupata upendeleo wake na baraka yake ya milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki