Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 5/15 kur. 12-17
  • Upendo Ukiwa “Kifungo cha Mwungano” Wathibitika Kuwa “Mkamilifu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo Ukiwa “Kifungo cha Mwungano” Wathibitika Kuwa “Mkamilifu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wameungana kwa Umoja Wakiwa “Kundi Moja”
  • “Lililo Kuu Ni Upendo”
  • Kujivika Wenyewe Upendo na Kuendelea Kuuvaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • “Roho ya Uhai Itokayo kwa Mungu Ikawaingia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • “Katika Hayo Lililo Kuu ni Upendo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Onyesha Upendo na Imani Sikuzote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 5/15 kur. 12-17

Upendo Ukiwa “Kifungo cha Mwungano” Wathibitika Kuwa “Mkamilifu”

1. Ni kwa njia gani Yehova anaweza kulinganishwa na mfua-vitu, na ni kwa njia gani kila jamaa ina deni ya jina layo kwake?

MFUA-VITU aliye mkubwa kupita wote katika ulimwengu mzima, Yehova Mungu Mwenyezi, anaweza kufua (kufanyiza) ‘kifungo cha mwungano’ kitakachoshikana mpaka milele. Vifungo vya kijamaa, hata vilivyo hapa duniani, vinaweza kuwa vyenye nguvu sana; na Yehova Mungu anatajwa kuwa ndiye Baba “ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.” (Waefeso 3:14, 15) Tangu wakati wa ile Gharika ya duniani pote ya siku za Noa mzee wa ukoo, kila jamaa ya kibinadamu imezaliwa na mwanamume huyo mwaminifu ambaye Mungu alimkubali kuwa anastahili kuhifadhiwa pamoja na jamaa yake ayapite mafuriko hayo yenye kufunika ulimwengu wote. Kwa sababu hiyo, kila jamaa ya kibinadamu iliyo duniani sasa inamwia Noa “jina” layo, yaani, imekuwa na deni kwake ya kuweza kuwa hai hata ijipatie jina ililo nalo. Zamani, Yehova Mungu amekuwa mwenye daraka la kuwapa watu fulani wa duniani majina yao, lakini yeye hakuzipa jamaa za kibinadamu majina moja kwa moja. Hata hivyo zinamwia (zina deni kwake) majina zilizo nayo, kwa maana zisingaliweza kamwe kuwako zikiwa na majina yazo kama yeye aliye Mpaji-Uzima wa ulimwengu mzima asingaliziwezesha.​—Mwanzo 5:1, 2, 32.

2. Ni kwa njia gani yule asi aliyeiasi jamaa ya Mungu akawa baba wa jamaa, na kwa hiyo inafaa kila mmoja wetu ajiulize ulizo gani?

2 Kumekuwako tendo la kibinadamu la kujitenga na jamaa ya ulimwengu mzima ya Baba wa kimbingu. Tendo hilo lilisababishwa na mwasi mwenye nguvu zipitazo za kibinadamu kwa kuipinga jamaa ya malaika za Mungu katika mbingu. Mwasi huyo alikuja kuitwa Shetani Ibilisi. Tunaweza kusema kwamba kwa kujikusanyia wafuasi wawe upande wake katika mbingu alipata kuwa baba, lakini kinachounganisha washiriki wa jamaa yake si upendo. Wakati mmoja Yesu Kristo, yule mshiriki mwaminifu aliye wa kutokeza zaidi katika jamaa ya Yehova ya ulimwengu mzima, aliwaambia hivi wapinzani wake waliokuwa wa uzao wa Kiyahudi: “Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja . . . Ninyi wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.” (Yohana 8:42, 44) Katika habari hiyo kila mmoja leo anaweza kujiuliza mwenyewe hivi: Kulingana na kiwango hicho, “baba” yangu ni nani?

3. Hali ya Shetani tangu Vita ya Ulimwengu ya Kwanza inatofautianaje na ile ya kabla ya hapo, na ni sala gani hasa inayohitaji kujibiwa kwa ajili ya wafuasi wote wenye kushikamana na tengenezo la Mungu?

3 Wakati Shetani Ibilisi alipoasi alitupwa akatolewa katika jamaa ya Yehova Mungu ya ulimwengu mzima, na baadaye mashetani zake wakatupwa pia wakiwa chini ya ubaba wake. Kwenye bustani ya Edeni alimtokea mwanadamu akiwa Mshawishi, na hata baada ya hapo aliruhusiwa kutanga-tanga katika dunia yote akiwa katika shughuli yake kubwa ya uovu na ya kuipinga kweli. (Ayubu 1:7; 2:2) Lakini sasa, tangu ile “vita” iliyotabiriwa kutokea baada ya kuzaliwa kwa Ufalme wa Mungu katika mbingu, baada ya kumalizika kwa “majira ya Mataifa” mwaka wa 1914, Shetani Ibilisi na mashetani zake wametupwa wakaondolewa katika mbingu wasiwe karibu-karibu na malaika za kimbingu. Wametelemshwa mpaka duniani. Hawatapata tena ruhusa ya kuziingia mbingu za malaika. Basi ni vyepesi kwetu kufahamu ni hasira ya kiasi gani ambayo Shetani analionea tengenezo la Yehova la ulimwengu mzima na wale washiriki washikamanifu wa tengenezo hilo. (Ufunuo 12:1-12; Luka 21:24) Basi, huu ndio wakati unaofaa kuliko nyakati zote wa kuijibu ile sala yenye upendo ya mtume Paulo, iliyoandikwa kwenye Wakolosai 1:2, kwa faida ya wafuasi walio washikamanifu kwa tengenezo la Yehova walio duniani sasa. Inasema: “Neema [fadhili zisizostahilika] na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu.” Sala hiyo ya kuomba kuwe na amani kati yao haiwezi kujibiwa ikiwa katikati yao hawana umoja. Amani inahitaji kuwe na upatano wa kindani katika tengenezo linaloonekana la Mungu apaye amani na ushikamano wa washiriki wa tengenezo.

4. Mashahidi waliounganishwa pamoja wa Yehova wanampigia asante kwa ajili ya nini, na wanahitaji kuendelea kutembea katika nini?

4 Wanaweza kuwa wakifanya vile washiriki wa kundi la Kolosai waliambiwa wafanye, wawe ‘wakimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru’ kwa sababu ya umoja wa kitengenezo unaoleta amani yenye kutofautisha tengenezo la Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote leo. (Wakolosai 1:12) Tunahitaji kuendelea kutembea katika nuru inayozidi kuongezeka, na katika hizi “siku za mwisho” za mfumo wa mambo ya kale jitihada ya pekee ni lazima ifanywe ili sisi wenyewe tuendelee ‘kustahili’ kupewa nuru zaidi ya ufahamu na urithi wo wote unaotupasa katika mfumo mpya.​—2 Timotheo 3:1.

Wameungana kwa Umoja Wakiwa “Kundi Moja”

5. Mashahidi wa Yehova leo wametolewa katika nini yajapokuwako mambo yote yanayoweza kuleta mtenganisho, lakini ni kwa sababu gani lile “kundi moja” la “mchungaji mmoja” limegandamana pamoja bila kutengana?

5 Leo Mashahidi wa Yehova wametokana na jamaa nyingi zaidi za kibinadamu kuliko ilivyokuwa kwa habari ya Wakristo wa karne ya kwanza. Wametoka katika makabila yote ya wanadamu, kutoka rangi zote za ngozi ya mwili na kutoka namna zote za maisha. Mambo hayo yenye kuonyesha wazi tofauti za watu yangaliweza kuwa kitenganishi kati ya Mashahidi wa Yehova. Lakini hayakuwatenganisha! Wanatambua kwamba wao wote wana chanzo kimoja cha kuwako kwao na cha nuru ya kweli, bila kujali ni wa kabila gani, rangi gani, lugha gani, taifa gani na cheo gani cha kijamii. Katika wakati huu ambao siku zimepita sana, kati ya Mashahidi wa Yehova kuna mabaki ya Wakristo waliozaliwa kwa roho walio na mataraja ya kuishi mbinguni, tena kuna “mkutano mkubwa” wa wale ambao yule Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, aliwaita “kondoo wengine” wake. (Yohana 10:16; Ufunuo 7:9-17; Mathayo 25:31-46) Hata hivyo, yale matabiri ya Yesu Kristo yenye kuhusu muda mrefu hayajakosa kutimia, ingawa yalisema hivi: “Kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.” Mchungaji Mwema huyo ameonyesha ustadi wake wa kufanya wafuasi wake wa kikondoo wenye kupenda amani waendelee kuwa “kundi moja,” ijapokuwa kuna tofauti kati ya matumaini yao ya wakati ujao. Wote kwa umoja wanampenda “mchungaji mmoja” wao, ambaye alitoa uhai wake wa kibinadamu uwe dhabihu kwa ajili yao wote, nao ni washikamanifu kwake.

6. Kwa sababu gani mabaki wenye tumaini la kuishi mbinguni hawakusita-sita kutangaza kweli za Biblia zinazowahusu wale “kondoo wengine”?

6 Ile “kweli” ya Kibiblia ambayo kondoo wote wa leo wanaipenda sana ina habari nyingi za kueleza juu ya tumaini la Paradiso ulio nalo ule “mkutano mkubwa” unaoongezeka daima wa “kondoo wengine” wa yule Mchungaji. Kwa hiyo, kwa kuwa mabaki ya kiroho wanaipenda “kweli” nzima ya Neno la Mungu, wao hawaoni kijicho hata wawanyime wale “kondoo wengine” kitu cho chote kinachoweza kuwafaidi. Bali, kwa upendo wamelitangaza ulimwenguni pote tumaini lile lililo zuri ajabu la kuishi duniani, hasa tangu mwaka wa 1935. Mabaki wanajua kwamba sasa wanaishi katika “nyakati za kurudishwa kwa mambo yote ambayo juu yayo Mungu alinena kupitia kinywa cha manabii watakatifu wake wa wakati wa zamani.” (Matendo 3:21, NW) Kwa mabaki, ufunuo wa kweli hiyo umekuwa sehemu ya ‘urithi wao wa watakatifu katika nuru.’ Tangu mwanzo wa kuchapishwa kwa gazeti hili, Mnara wa Mlinzi, katika Julai wa 1879 (Kiingereza), limekuwa chombo cha Mungu cha kuchochea tena tumaini hilo lililo zuri ajabu la Paradiso kwa faida ya wanadamu waliokombolewa. Vichapisho vile vingine vya Sosaiti vimejumlika pamoja kulitia nguvu na kuliimarisha tumaini hilo ambalo “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” unalifurahia sana leo, huku wakiwathamini kwa upendo wale mabaki.

7. Katika mwaka wa 1935, ni tumaini gani zaidi ya lile lao wenyewe ambalo mabaki watiwa mafuta walionyesha watu kwa upendo, na kwa sababu gani waliwaruhusu wabatizwe wale wenye tumaini hili jingine?

7 Kufikia masika ya mwaka wa 1935 mashahidi waliojiweka wakf na kubatizwa wa Yehova walikuwa wamelifurahia kwa imani ya kweli lile “tumaini moja” lililowekwa mbele yao katika Waefeso 4:4-6 kwa njia hii: “Mwili mmoja, na [roho moja], kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote.” Lakini katika mwaka huo wa 1935 unaostahili kukumbukwa, kwenye kusanyiko lililofanywa katika Washington, D.C., ule “umati mkubwa, ulioonwa katika njozi kwenye Ufunuo 7:9-17 (Authorized Version), ulitambulishwa kwamba ndani yake una wale “kondoo wengine” wa Mchungaji wanaotajwa katika Yohana 10:16. Mabaki watiwa mafuta waliokuwa wangali wanashikilia “tumaini moja” lao lililo halali walifurahi sana kwa sababu ya nuru hiyo iliyoongezeka yenye kueleza Maandiko Matakatifu kisha wakajiondokea wakawakusanye kwa moyo wote wale “kondoo wengine.” Wao hawakuwa na maoni ya kwamba “kondoo wengine” hao walikuwa wakijiingiza isivyofaa katika ule “ubatizo mmoja” ulio wapasa wao wenyewe kwa kuzamishwa katika maji, kwa maana ubatizo wa “kondoo wengine” hao ulikuwa mfano wa wakf wao pia kwa Yehova Mungu kupitia Kristo sawa na vile ule wa mabaki watiwa mafuta ulivyokuwa umekuwa. Sasa upendo waliokuwa wamejivika ulipanuka uwatie ndani hao “kondoo wengine” wenye kupendeka, wa Mchungaji wao wenyewe.

8. Upendo ulio kati ya jamii mbili hizi zilizo katika lile “kundi moja’’ unaweza kulinganishwa na upendo wa nani katika siku za Israeli wa kale?

8 Upendano wa pande mbili umesitawi, na kuwa na kina kirefu zaidi kati ya watu wote wa kikondoo wa lile “kundi moja” lililo chini ya uongozi wa Daudi Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo. Kifungo hicho cha uunganishi kinalingana na ule upendo usiovunjika na usiofifia wa Daudi, mfalme-mchaguliwa aliyetiwa mafuta wa kabila la Yuda, kumwelekea Yonathani mwenye kupendeka asiye na choyo, yaani yule mwana wa Sauli, mfalme aliyekuwa akitawala wakati huo. (2 Samweli 1:25-27) Muda mfupi kabla hawajaagana kwa mara ya mwisho, ‘Yonathani alimwapisha Daudi mara ya pili, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake; kwa maana alimpenda kama alivyoipenda [nafsi] yake mwenyewe.’ (1 Samweli 20:17) Daudi alipopata habari za kwamba Yonathani amekufa piganoni pamoja na baba yake, tukio hilo liliusukuma moyo wake kumfanya aimbe wimbo wa maombolezo na kuufikisha kwenye upeo kwa maneno haya: “Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, ulikuwa ukinipendeza sana; upendo wako ulikuwa wa ajabu, kupita upendo wa wanawake.” (2 Samweli 1:26) Upendano wao ulikuwa “kifungo kikamilifu cha mwungano.” Kifo tu ndicho kilichoweza kuwatenganisha.

9. Hapo wale “kondoo wengine” walifananishwa na nani, na ni kwa njia gani wale wa jamii hizo mbili watatenganishwa mwishowe na bado upendo ulio kati yao usipungue?

9 Yonathani alitangulia kuwa kifananishi cha “kondoo wengine” wa wakati huu. Siku fulani ya wakati ujao, baada ya “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har-magedoni, jamii ya Yonathani itakayookoka itatenganishwa na mabaki ya jamii ya Daudi. (Ufunuo 16:14, 16) Sababu moja tu itakayowatenganisha ni kwamba mabaki wapendwa watachukuliwa na kifo, twaweza kusema ‘watanyakuliwa katika mawingu, ili kumlaki Bwana hewani,’ kupitia ufufuo wao wa dakika ile ile wakiwa wamekiacha kifo kwa kuwa na umbo la kiroho. (1 Wathesalonike 4:17) Wataendelea kuwapenda “kondoo wengine” watakaowaacha duniani. Kwa kweli, upendo wao wakati huo utaonyeshwa kwa kadiri kubwa zaidi!

“Lililo Kuu Ni Upendo”

10, 11. Ni kwa njia gani imani na tumaini si mambo makubwa kama upendo, kama inavyotajwa katika 1 Wakorintho 13:13?

10 Jambo hilo linatukumbusha maneno ya Paulo yaliyo mwishoni mwa maelezo yake ya kupendeza sana yaliyo katika 1 Wakorintho sura ya 13, yaani: “Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.” (1 Wakorintho 13:13) Imekuwaje hivyo? Ebu kwanza angalia yanayosemwa katika Waebrania 11:1, NW: “Imani ni taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa, wonyesho dhahiri wa mambo ya hakika ijapokuwa hayaonwi.” Basi, kwa hakika tumaini la kutazamia mambo hayo linahusu wakati tu yanapokuwa “hayaonwi.” Kwa mfano, fikiria kisa cha Abrahamu. Yeye alionyesha imani katika Yehova Mungu na katika uwezo Wake wa kuwafufua wafu. Kwa hiyo alingojea kwa uhakika mambo ambayo hakuyaona kabla ya kifo chake. Kwa hiyo Mashahidi wa Yehova wa leo wanatumainia mambo ambayo hawajayaona bado na kuyangojea kwa sababu ya kuwa na imani yenye nguvu katika Yeye. Baadaye, wakati, watakapoyaona yale “mambo yanayotumainiwa,” hapo imani na tumaini lao kuhusu mambo hayo vitakoma, kwa maana vitakuwa vimekwisha kutimizwa. Hilo linaonyeshwa na yale ambayo Paulo anaendelea kusema katika Warumi 8:24, 25 (NW), ambapo tunasoma hivi:

11 “Kwa maana tuliokolewa katika tumaini hili; lakini tumaini linaloonekana si tumaini, kwa maana wakati mtu anapoona kitu, je! anakitumainia? Lakini ikiwa sisi tunatumainia tusichoona, sisi tunaendelea kukingojea kwa uvumilivu.”

12. Ni kwa njia gani Mashahidi wa Yehova wameona “kurudishwa kwa mambo yote,” kama inavyotajwa katika Matendo 3:21, na kwa hiyo baadaye ni sifa gani zitakazokoma lakini ni sifa gani haitakoma?

12 Vivyo hivyo, tangu ule mwaka ulioifuata vita wa 1919 Mashahidi wa Yehova walio duniani wameona “kurudishwa kwa mambo yote ambayo juu yayo Mungu alinena kupitia kinywa cha manabii watakatifu wake wa wakati wa zamani.” Wameona tengenezo la Yehova linaloonekana likiponeshwa pigo la kifo la Vita ya Ulimwengu ya Kwanza kisha wakaona likijengwa upya. Kwa mara nyingine linamwabudu Yehova Mungu, katika paradiso ya kiroho papa hapa duniani. (Isaya, sura ya 35) Ukombozi umepatikana wa kuiacha Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo. (Ufunuo 18:1-4) Mengi ya mambo yaliyotabiriwa katika Ufunuo, kitabu cha mwisho cha Biblia, yametimizwa au yanaendelea kutimizwa. Hivyo imani na tumaini vyenye kutegemea msingi wa imani hiyo ya Kibiblia vinatimiza kusudi lavyo, na wakati kusudi lavyo litakapokuwa limekwisha kutimizwa kabisa, imani na tumaini hilo vitakoma. Ah, ndiyo, namna gani juu ya upendo? Huo umebakia na utaendelea kubakia. Ijapokuwa ulimwengu uko katika hali ya kuvunjika-vunjika na sehemu asili za ulimwengu zinakaribia kuyeyuka kwa sababu ya joto kali sana, kile ‘kifungo cha mwungano’ unaotegemea upendo kutoka kwa Mungu hakiyeyuki. Kingali kimeshikana kwa uthabiti kumwelekea Mungu na tengenezo lililokubaliwa naye na kati ya mabaki ya “kundi dogo” na “mkutano mkubwa” wenye kufurahiwa, wa wale “kondoo wengine.” Kinathibitika kuwa “kikamilifu.” Upendo ukiwa ndio “kifungo” hicho ni tunda la roho ya Mungu.

13. Kwa sababu gani upendo hautakufa hata siku moja?

13 Mungu ni mfananisho wa sifa ya upendo; na kwa kuwa Mungu hafi kamwe, upendo hautakufa kamwe. Kwa usahihi inasemwa kwamba “Mungu ni upendo.”

14. Ni kweli gani inayoweza kurudiwa kutajwa juu ya uwezo wenye kuunganisha wa upendo?

14 Kwa habari ya ule uwezo wenye kuunganisha watu wa upendo, kweli iliyoongozwa na Mungu iliyotajwa kwenye 1 Yohana 4:8, 16 inaweza kurudiwa na kupanuliwa. “Mungu ni upendo, na yeye anayebaki katika upendo anabaki katika mwungano pamoja na Mungu na Mungu anabaki katika mwungano pamoja na yeye.” (NW)

15. Mungu alichochewa na nini wakati wa kuumba mtu, na kwa sababu gani mwanadamu anaweza kuithamini na kuiitikia inavyofaa hiyo kani (nguvu) yenye kuchochea?

15 Kulingana na hilo, wakati Mungu alipomtokeza kiumbe wa kwanza wa kibinadamu duniani, alifanya hivyo kwa kuchochewa na upendo. Ni kama vile Mwanzo 1:27 inavyoripoti: Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba.” Si kwamba mtu wa kwanza alikuwa na umbo la kimwili la Mungu, bali alipewa kipawa cha sifa kama za Mungu mwenyewe. Sifa hizo za kiakili, kiroho na kimoyo zilimtofautisha na viumbe wa hali ya chini walio duniani. Basi kiumbe huyo wa kibinadamu aliyepewa kipawa angeweza kuuthamini upendo ambao Muumba wake alimwonyesha na angeweza kuuitikia upendo huo kwa njia inayofaa, kama vile mwana kumwelekea baba yake. Kulikuwako kifunganishi cha kijamii kati yao kilichofanywa halisi na mawasiliano ya ukawaida kati yao ijapokuwa Baba mwenyewe alikuwa hawezi kuonwa na mwanaye wa kidunia, kwa maana hakuna mwanadamu anayeweza kumwona Mungu na bado aendelee kuwa hai. Uhakika huo ulitajwa na Mungu baadaye akimwambia Musa kwamba: “Mwanadamu hataniona akaishi.” (Kutoka 33:20) Kawaida hiyo haikubadilishwa, kwa maana miaka zaidi ya elfu moja na mia tano baadaye mtume Yohana aliwaandikia hivi Wakristo wenzake: “Hakuna mtu ambaye amemwona Mungu wakati wo wote; mungu mzaliwa wa pekee aliye mahali pa kifua pamoja na Baba ndiye ameeleza alivyo.”​—Yohana 1:18, NW.

16. Yohana na wanafunzi wenzake waliuitikia upendo wa Mungu ulio kama wa baba wakiwa na nini, na kile “kifungo cha upendo” kimethibitika kuwaje kwa habari ya mabaki watiwa mafuta na wale “kondoo wengine”?

16 Kwa kuwa mtume Yohana alikuwa mwana wa Mungu mwenye kuzaliwa kwa roho, alikuwa katika uhusiano wa kijamaa pamoja na Yehova na pamoja na Mwanaye, “mungu mzaliwa wa pekee,” Yesu Kristo. Yohana na Wakristo wenzake waliiitikia shauku ya Mungu yenye upendo kama wa baba na mwanaye. Upendo huo ulikuwa “kifungo cha mwungano” kati yao na Baba yao wa kimbingu asiyeonekana. Upendo huo uliwaunganisha kwa uthabiti mwingi pia wale waliozaliwa kwa roho wakiwa wana wa kiroho wa Mungu na wakiwa ndugu na dada wa Kikristo. Leo tunapokichunguza hicho “kifungo cha mwungano” tunaona kwamba kimethibitika kuwa “kikamilifu,” kwa maana washiriki wa mabaki waliotiwa mafuta wanagandamana pamoja wasiweze kutenganishwa wakiwa waabudu na mashahidi wa Yehova Mungu wenye kushirikiana kama wenzi. Upendo huo unawadumisha katika jamaa ya Mungu na katika udugu wa Kikristo. Jambo linalostahili kuangaliwa ni kwamba, waabudu wenzao kwenye hekalu la Mungu, ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo, wanaonyesha upendo ule ule usioweza kumaliziwa mbali unaowafunganisha Mashahidi wa Yehova wa leo kwa ukamilifu mwingi. Basi na tupige moyo konde tuwe na usadiki kama wa mtume Paulo, kwamba “kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”​—Warumi 8:38, 39.

Wewe Unajibu Namna Gani?

□ Ni kwa njia gani kila jamaa inamwia Mungu jina layo?

◻ Uhakika huo unapasa kuwa na matokeo gani juu ya wote walio katika kundi la Kikristo?

◻ Yonathani alitangulia kuwa kifananishi cha nani?

◻ Kwa sababu gani upendo ni mkubwa kuliko imani na tumaini?

◻ Upendo unatufunganishaje na Mungu?

[Picha katika ukurasa wa 15]

Ule upendo mwingi sana kati ya Daudi na Yonathani ulitangulia kufananisha upendo ulio kati ya watiwa mafuta na wale “kondoo wengine’’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki