Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 8/1 kur. 8-13
  • “Wakisongamana Pamoja Katika Mpango wa Vita”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Wakisongamana Pamoja Katika Mpango wa Vita”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Askari za Kristo Yesu’
  • Uchaguzi wa Uufalme​—Zamani na Sasa
  • Ni Nani Wanaostahili Kuwa Vitani?
  • Ushindi Umeahidiwa kwa Uhakika
  • Kulitatua Daima Suala la Ulimwengu Wote Mzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Utawala wa “Mwana-Mfalme wa Amani” Katikati ya Maadui
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Maoni ya Mungu Kuhusu Vita Katika Nyakati za Kale
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Maoni ya Mungu Kuhusu Vita Katika Karne ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 8/1 kur. 8-13

“Wakisongamana Pamoja Katika Mpango wa Vita”

“Wote hao walikuwa wanaume wa vita, wakisongamana pamoja katika mpango wa vita; kwa moyo kamili wakaja Hebroni kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli wote.”​—1 MAMBO YA NYAKATI 12:38, NW.

1. Ni hali gani yenye uharaka leo inayofanya kuwa macho kuhitajiwe?

PA-A-A-ZE-NI sauti ya vita! Mashahidi wote hodari wa Yehova na wajikusanye waje kazini! Kupigana na adui kunakaribia hatua yenye hatari. Hizi ni siku zenye uharaka. Hatuwezi kuwa na nia za kujistarehesha au kulala usingizi wa kudhani vita imepungua. Hivyo ndivyo adui anavyotaka tudhani, maana anajua wakati wake ni mfupi. Basi, tunaweza kumtazamia adui afyatushe shambulio la ghafula akitumainia kuwavamia wenye kupigania kweli wakiwa katika hali ya kutokufahamu.

2. Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova hawahitaji kuogopa maadui wao? (Zaburi 24:8)

2 Yehova anawaona mashahidi wake waaminifu leo kuwa wapiganaji walio katika vita ya kiroho inayokwenda mbio-mbio ikafikie upeo. Kunapokuwa na uhitaji, Yehova huwa “mtu wa kiume wa vita” ambaye mkono wake wa kuume unaweza kuponda-ponda maadui na kuwabwaga chini. (Kutoka 15:3, 6, 7) Ahadi aliyowapa Israeli wa kale waliopaswa kuongozwa na malaika wake ingali inafanya kazi: “Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao.”​—Kutoka 23:20-22.

3. (a) Eleza cheo cha Yesu tangu mwaka wa 1914 W.K (b) Yeye amekuwa katika vita gani? (c) Kwa sababu gani wafuasi watiwa mafuta wa Yesu wanashambuliwa leo?

3 Kweli ya kiunabii inafunulia macho yetu ya imani kwamba, tangu vuli ya mwaka wa 1914 Kristo Yesu aliyetukuzwa amewekwa na Yehova kuwa Amiri-Jeshi wa vikosi vya kimbingu vya malaika walio askari wa vita. (Zaburi 110:1, 2; Mathayo 25:31) Yeye ameyaongoza mbio majeshi haya dhidi ya (kupigana) Ibilisi na malaika zake, yakafagia mbingu ziondokwe na uchafu wa kuwapo kwao kisha akawabana katika ujirani wa Dunia-sayari. Na sasa, akiwa anangojea kiishara cha mwisho kutoka kwa Yehova ili awaharibu maadui, Kristo Yesu anaendesha utendaji wa duniani pote wenye kuonekana ambao pia unahusu vita. (Ufunuo 12:7-9) Shetani na vikosi vyake vya kishetani, kwa kutambua wakati wao ni mfupi, wanapiga vita kwa ghadhabu pamoja na mabaki ya wale wafuasi watiwa mafuta wa Yesu. Kwa sababu gani? Kwa sababu hao wanautangaza kwa utii ule Ufalme wa Mungu wao na Kristo wake.​—Ufunuo 12:17.

‘Askari za Kristo Yesu’

4. Eleza ni nini kinachofanya mtu astahili kuwa ‘‘askari mwema wa Kristo Yesu.”

4 Basi inakuwa kwamba wote wanaoshirikiana na kuunga mkono mabaki ya watiwa mafuta wa Mungu duniani na kuwaunga mkono katika kazi waliyopewa na Mungu wanakuwa pia shabaha ya vita hii kali sana. Kwa hiyo, kila mmoja anayetumikia hivyo leo akiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova anapewa kitia-moyo hiki cha Paulo chenye kuchochea: “Ukiwa askari mwema wa Kristo Yesu chukua fungu lako la kupatwa na uovu. Hakuna mwanamume anayetumikia akiwa askari ajitiaye mwenyewe katika shughuli za kibiashara za maisha, ili kwamba aweze kupata ukubali wa yule aliyemwandika orodhani awe askari.” (2 Timotheo 2:3, 4, NW) Lazima kila utendaji mwingine wa maisha uchukue mahali pa pili, utumishi wetu kwa Amiri-Jeshi mkuu wa Yehova uwe ndio wa kwanza.

5. (a) Paulo anaielezaje vita ya kiroho ya Mkristo? (b) Askari Wakristo wamekaza nia kufanya nini, na ni nini kitakachowasaidia katika shindano hilo?

5 Akili zetu zinapata kuuona uhakika wa vita hii ya kiroho tunapofikiria kwa uzito makumbusha haya ya mtume Paulo: “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; . . . tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia.” (2 Wakorintho 10:3-6; angalia pia Waefeso 6:12.) Sisi askari za Kristo Yesu tunataka kuonyesha watu wote kwamba tunatii maagizo yake ya pigano na tuko tayari nyakati zote kushiriki na kutimiza maarifa yote ya kivita anayochagua. Basi, ili kututia moyo katika uwanja wa shindano la kiroho, na tuangalie kurasa za Neno la Mungu kuhusu tukio la huko nyuma katika Israeli wa kale. Hapo tunaweza kuona vifano vya kiunabii vya mambo yanayoendelea kutukia sasa.​—Warumi 15:4; 1 Wakorintho 10:11.

Uchaguzi wa Uufalme​—Zamani na Sasa

6. Eleza matukio yaliyofuatana mpaka Daudi akaja kukubaliwa kuwa mfalme na namna jambo hilo lilivyohusu watu mmoja mmoja.

6 Ifikirie hali iliyokuwako wakati wa Mfalme Daudi, chaguo la Mungu la kuwa mfalme wa Israeli wote. Baada ya kufa kwa Sauli, wanaume wa Yuda ndio waliokuwa wa kwanza kukubali kuchaguliwa kwa Daudi na Mungu awe mfalme wao. Yale makabila mengine yote yalimchagua Ish-boshethi mwana wa Sauli awe mfalme wao, basi ugomvi ukawa ukiendelea. (2 Samweli 2:1-11; 3:1) Ish-boshethi alipouawa yapata miaka miwili baadaye, njia ikawa wazi makabila yale mengine yaungane na Yuda. Kwa wakati wake Daudi akatiwa mafuta awe mfalme juu ya Israeli wote. (2 Samweli 4:5-12; 5:1-3) Lakini katikati ya kipindi hicho ilikuwa lazima watu wengi mmoja mmoja wakate kauli wangetumikia nani. Ilikuwa lazima wafikirie vitambulishi vya kumstahilisha huyu kijana Daudi. Je! kweli yeye alikuwa mtiwa mafuta wa Mungu? Je! ndiye angebarikiwa na Yehova badala ya kukataliwa na Mungu kama Sauli? Je! Daudi angeongoza majeshi ya Israeli yafanikiwe kushinda maadui waliowazunguka?

7. Ni nini kilichohusika katika kuukubali uufalme wa Daudi?

7 Ni wazi kwamba Waisraeli fulani walifanya uamuzi wa kupendelea nyumba ya Sauli iliyolaaniwa. Wengine walifanya uamuzi wao kwa kutegemea faida zao binafsi. Na bado wengine wakabaki wakizubaa-zubaa. Lakini baada ya muda fulani ikawa lazima watu wafanye uchaguzi wao, na wenye furaha ni wale waliochagua kuunga mkono kwa moyo wote uufalme wa Daudi! Hao hawakuwa wachoyo au wenye woga wa kupambana na matatizo. Hawakuwa watu wa kauli mbili. Badala yake, tendo lao la kumwunga mkono mfalme wa Yehova liliwaongoza wajibidiishe kuwa raia na askari za Daudi. Ni kama vile andiko la 1 Mambo ya Nyakati 12:22 (NW) linavyotaarifu: “Siku kwa siku watu waliendelea kumjia Daudi wamsaidie, mpaka ikawa kama kambi kubwa, kama kambi ya Mungu.”

8. Wale wenye kuukubali uufalme wa Daudi wanatambulishwaje?

8 Kutokana na mapana na marefu ya maandishi yenyewe tunaona kwamba kati ya umati huo kulikuwa na wale “wenye maarifa ya jinsi ya kuzifahamu nyakati za kujua linalopasa Israeli kufanya.” (1 Mambo ya Nyakati 12:32, NW) Hawakuwa na uvuguvugu kuhusu utii wenye ushikamano kwa mfalme. Walikuwa na silaha za kutosha ili wajitokeze mbele yake kama watu walio tayari kukubali uongozi wa Daudi vitani. Hawakutazamia maisha ya starehe tu. ‘Walizifahamu nyakati’ na wakajua kwamba ufalme huo ulikuwa umezungukwa na maadui waliokuwa tayari kuimeza Israeli na kufutilia mbali ibada ya Yehova. Wale wa kutoka mashariki ya Mto Yordani walikuwa “wanaume wa vita, wakisongamana pamoja katika mpango wa vita,” tayari kutumikia chini ya Daudi “kwa moyo kamili.”​—1 Mambo ya Nyakati 12:38, NW.

9. (a) Je! tunapata ulinganifu wa kisasa kuhusu hali iliyokuwako siku za Daudi? (b) Ni ulizo gani linalowaelekea watu wote leo?

9 Inasisimua sana sasa kuona mbele yetu kifananisho cha kisasa cha hali hiyo kikiendelea kujitokeza? Yule Daudi Mkubwa Zaidi, Kristo Yesu, amechaguliwa na Yehova na sasa anatawala akiwa Mfalme wa kimbingu. Mataifa ya ulimwengu yanapinga uufalme wake. Yanatisha kufutilia mbali raia za Mfalme huyo watoke duniani. (Zaburi 2:1-3) Basi, ulimwenguni pote watu mmoja mmoja wanaombwa wachukue msimamo wao upande mmoja lile suala, upande huu au ule. Suala lenyewe ni hili: Je! wao wanautetea au wanaupinga ufalme wa Mwana wa Yehova? Umati wa watu ungali haujaamua. Wengine wanaamua msimamo watakaochukua kwa kufuatia faida zao tu, kwa kufikiria usalama na mafaa watakayojipatia wao wenyewe tu.​—Sefania 2:2,3; Yoeli 3:14.

10. (a) Kwa sababu gani watu wengi wanazubaa-zubaa (hawajaamua) kukubali uufalme wa Kristo? (b) Ni daraka gani ambalo sasa linawakalia Mashahidi Yehova?

10 Wakati sifa ya umashuhuri wa wajumbe wa kifalme wa Mungu walio duniani inapoendelea kuenea kwa mapana na marefu, watu zaidi na zaidi wanawezeshwa kufanya uchaguzi wa akili. (Mika 4:1-3; Zekaria 8:23) Wengi wamekosa kufanya uamuzi kwa sababu tu hawana maarifa ya kuyajua mambo ya hakika; hawana busara ya kutambua maana ya nyakati hizi na hawaoni uhitaji wa kufanya haraka wasimame kwa imara upande wa Ufalme wa Mungu. Basi halaiki za watu wangali chini ya mavutano ya porojo za Shetani na wako katika hatari ya kukokotwa wakapate uharibifu pamoja na Shetani na washirika wake. Kwa hiyo, mwito wa haraka ni wa kwamba Mashahidi wa Yehova wote wajikusanye upande wa Daudi Mkubwa Zaidi, Kristo Yesu, wakiwa na silaha na vifaa vya kupiga vita pamoja na adui​—Linganisha Mathayo 12:30.

Ni Nani Wanaostahili Kuwa Vitani?

11. Eleza namna Yesu alivyoonyesha kwamba utii wetu kwa Kristo unaweza ‘kutimizwa kwa ukamili.’

11 Katika vita yao ya kiroho, ni lazima askari wote wa Kristo watimize matakwa fulani ya maana sana. Kwa mfano, Paulo alionyesha namna ilivyo lazima utii wao wenyewe kwa Kristo ‘utimizwe kwa ukamili.’ (2 Wakorintho 10:5, 6, NW) Tunaweza kuamuaje kama utii huo unaonekana katika mwendo na nia yetu wenyewe? Maulizo yanayofuata yatatusaidia sisi mmoja mmoja tupige moyo konde (tujikaze):

Je! kweli tumeweka utumishi wetu kwa Mungu na Kristo mbele sana ya uhusiano wote wa kibinadamu? (Mathayo 10:37)

Je! tumetupa mbali tamaa yo yote kali ya kutaka utajiri wa vitu vya kimwili au kusifiwa katika mambo ya kilimwengu? (Luka 6:20-26)

Je! sisi tunahangaikia sana kupendeza Kiongozi na Amiri wetu badala ya kuhangaikia vitu ambavyo Yehova ameahidi kutupa​—chakula, mavazi na makao? (Mathayo 6:25-32)

Je! sisi tumeacha kuhukumu na kulaumu-laumu askari wenzetu wa Kristo ili tusilete mafarakano na mtengano kati ya kundi hilo la askari watakatifu? (Luka 6:37; Zaburi 133:1-3)

Je! tunapenda ndugu zetu kikweli na kutafuta masilahi (hali njema) ya wote walioandikwa katika hii vita ya kiroho dhidi ya maadui wa Mungu? (Yohana 13:35; 1 Petro 4:8)

Hayo ni maulizo yenye kuchunguza moyo ambayo ni lazima wafuasi wote wa Kristo wajijibie mmoja mmoja.

12. Marafiki na maadui wa ufalme wa Mungu wanaweza kutambuliwaje?(Mathayo 25:31-46)

12 Jambo jingine la maana kufikiriwa katika vita yetu ya Kikristo ni kuwa na maono yaliyo wazi juu ya tofauti kubwa inayotenganisha tengenezo safi la Mungu na matengenezo yenye wendekevu na ufisadi ya ulimwengu. (Mwanzo 3:15; Zaburi 97:10) Majeshi ya kila upande vitani lazima yaweze kutofautisha wazi kati ya rafiki na adui. Jambo hilo linawezekana kwa sababu ya kuvaa mavazi tofauti na silaha za kuwatambulisha. Sisi tumefundishwa habari za matunda ya roho ya Mungu. Tumejulishwa tujihadhari na kazi za mwili, ambazo hata hizo zinaonekana wazi kama matunda. (Wagalatia 5:19-24) Kwa hiyo hakuna jambo lisilopambanuliwa wazi kabisa kati ya tengenezo la Mungu na tengenezo la Shetani.

13. Mikutano ya ukawaida inatimiza kusudi gani katika vita ya kiroho yetu?

13 Tena, je! tunaonyesha kwa mwendo wetu kwamba ‘tunaujua uhitaji wetu wa kiroho’? (Mathayo 5:3, NW; Waebrania 10:25) Katika vita ya kimwili maafisa na askari wengine wanahitajiwa kabisa wawe na vipindi vya kupashwa habari ili wajue habari za sasa hivi katika uwanja wa pigano na pia wajue maarifa yanayotumiwa sasa hivi na maadui wao. Vivyo hivyo, mikutano yetu kwenye Jumba la Ufalme au kwingineko ni ya maana kwa kila mmoja wetu ili tutiwe nguvu kwa ukawaida na Neno la Mungu na roho takatifu yake, na vilevile kujulishwa daima miendo ya adui.​—1 Petro 5:8.

14. Maneno ya Zekaria kwenye Luka 1:74, 75 yanaweza kuonyeshaje vizuri maoni tuliyo nayo?

14 Inatupasa sisi sote tumshukuru sana Yehova na Mwanaye kwa kutuweka tayari sana kwa vita ya kiroho! Kama Zekaria, baba yake Yohana Mbatizaji, tunajisikia tukilazimika kumsifu Yehova kwa kutupatia, “baada ya sisi kuwa tumekombolewa kutoka mikono ya adui, lile pendeleo la kumtolea yeye utumishi mtakatifu bila woga tukiwa na ushikamanifu na uadilifu mbele zake siku zetu zote.” (Luka 1:74, 75, NW) Tumeokolewa kutoka Babeli Mkuu. Na sasa, baada ya kutimiza matakwa ya Kiongozi na Amiri wetu, tuko katika hali ya kuweza kusongamana katika mpango wa vita tupigane na maadui wa Mungu na Kristo.

15, 16. (a) Shetani ametia “mawazo” gani na ‘mambo yaliyo imara kama ngome’ katika akili za watu? (b) Ni kwa njia gani moja tu yanaweza ‘kupinduliwa,’ na hilo linatukia kwa kadiri gani?

15 Silaha zote na majeshi yenye silaha ya ulimwengu huu ni vibaramwezi vya kitoto tu vikilinganishwa na falsafa na mapokeo ya uongo ya wanadamu, yanayochochewa na Shetani na majeshi yake ya kishetani. Shetani amewaka tamaa akitaka kuwa kama Mungu katika adhama na uweza kwa kueneza porojo za mafundisho yake ya uongo kote kote. Yeye anampinga yule Mungu wa kweli na kudai kwa udanganyifu kwamba yeye mwenyewe ndiye chemchemi ya maarifa. Anafundisha kwamba mwanadamu hamhitaji Yehova, kwamba mwanadamu anaweza kujitegemea mwenyewe mpaka akawe kama Mungu. Ibilisi anakataa kukubali kwamba Mungu ndiye aliyeumba vitu, kwa kupokeza wanadamu kwa udanganyifu lile wazo la kwamba mwanadamu alitokea kwa mageuzi. Yeye amefaulu kuaminisha umati mkubwa wa watu kwamba watu hawafi kabisa kabisa, kwamba kile kinachoonekana kuwa kifo ni badiliko tu la kuingia katika namna nyingine ya maisha. Yeye ameendeleza namna mbalimbali za serikali ya kibinadamu, na mizizi na misingi ya zote imekuwa ni choyo. Hayo na mengine mengi ndiyo ‘mawazo na vitu vilivyoinuka ambavyo vimeinuliwa juu ya elimu ya Mungu.’​—2 Wakorintho 10:5.

16 ‘Mawazo hayo yaliyo imara kama ngome’ yanahitaji kupinduliwa, kufunuliwa wazi yaonekane hayafai, ili waliotekwa nyara na mambo ya udanganyifu wakombolewe kiakili na kiroho. (2 Wakorintho 10:4) Sisi tuna silaha na mavazi ya kujikinga tunayohitaji​—imani ikiwa ngao, kweli ikiwa mshipi wa kutia nguvu kiuno, uadilifu ukiwa ulinzi wa moyo tumaini la wokovu likiwa ni kofia ya kukinga kichwa, Neno la Mungu likiwa upanga na zile habari njema za amani, za kusaidia wale wanaotaka kunyenyekea Mfalme aliyechaguliwa na Yehova. (Waefeso 6:14-17, NW) Kwa kutumia silaha za kiroho za namna hiyo mashahidi Wakristo wa Yehova wanaweka huru mateka wengi sana!

Ushindi Umeahidiwa kwa Uhakika

17. Andiko la Zaburi 45:3, 4 linaelekeza kwenye matokeo gani yatakayopatikana Kristo akiwatia adui katika ile vita ya mwisho?

17 Wakati unazidi kukaribia ambapo Yehova atamtolea kiishara Mfalme aliyemchagua akapigane na adui katika vita ya mwisho. Akimwambia huyo Kiongozi wa majeshi ya kimbingu, Yehova atapaza mwito kwa kutumia maneno ya Zaburi 45:3, 4: “Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, utukufu ni wako na fahari ni yako. Katika fahari yako usitawi uendelee kwa ajili ya kweli na upole na haki. Na mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.” Matokeo ya hatua hiyo ni hakika. Tengenezo lote la Shetani, lenye kuonekana na lisiloonekana, litaondolewa, uondolewe kabisa duniani utawala wote mbovu ulio na uonezi. Hiyo itakuwa siku ya furaha gani kwa waokoaji, siku ambayo waonezi, waongo, washerati na waharabu wote wa dunia watakuwa wametokomea kale na kale!​—Ufunuo 11:16-18; 19:11-21.

18. Tangu mwaka wa 1914 W.K., kumekuwaje na tendo la ‘kusongamana pamoja katika mpango wa vita’?

18 Ni vizuri kama nini kuona hali za kutazamisha zilizoandikwa katika Maandiko zikitimia sasa! Katika siku zetu, ndugu watiwa mafuta wa kiroho wa Kristo Yesu ndio waliokuwa wa kwanza kumkubali yeye kuwa Mfalme wao, baada ya kutawazwa kwake mwaka wa 1914 W.K. Wote ‘wamesongamana pamoja katika mpango wa vita.’ Halafu “mkutano mkubwa” umekitambua chanzo cha kweli cha fanaka na baraka kisha ‘ukasongamana pamoja’ hasa tangu mwaka wa 1935, wakati ambao nuru ilimulika andiko la Ufunuo 7:9-17 likafahamiwa. Hao wamejiunga na Waisraeli wa kiroho wa sasa. Wote kwa ujumla wametokea kwa kusongamana pamoja katika mpango Wa vita, wakiwa tayari kuyashiriki mateso na magumu yanayotokana na upigaji vita wa waziwazi pamoja na tengenezo zima la Shetani​—kwa heshima na utukufu wa Yehova.​—Zekaria 2:11.

19. Basi, inampasa kila shahidi wa Yehova aliye hodari apige moyo konde kufanya nini?

19 Basi, ni wazi kwamba hizi ni siku zenye uharaka. Huu sio wakati wa kudhani vita ya kiroho imekwisha. Adui asije kamwe akatuvamia bila sisi kujua, katika hatua ile hatari inayokaribia ya utumishi mtakatifu wetu. Kama sisi ni mabaki ya Waisraeli wa kiroho au ni “mkutano mkubwa” wa wenzi wao, acheni ‘tusongamane pamoja katika mpango wa vita, tukiwa na moyo kamili.’ Acheni tuendelee kuipaza sauti ya vita kwa ujasiri kwa sababu Yehova anatuhakikishia tutashinda!—2 Mambo ya Nyakati 20:15.

Kwa Muhtasari

□ Kwa sababu gani sasa kuna uhitaji wa kufanya haraka ‘kusongamana pamoja katika mpango wa vita’?

◻ Mashahidi wa Yehova wanapiga vita ya namna gani?

◻ Watu wote leo wanaelekeana na ulizo gani la maana sana?

◻ Ni nani anayestahili kuwa ‘askari wa Kristo Yesu’?

◻ Sasa ni ahadi gani ya ushindi hakika ambayo imetolewa?

[Picha katika ukurasa wa 11]

Kukutana kwa ukawaida kwenye Jumba la Ufalme (1) Kunatutia nguvu kwa ajili ya vita ya kiroho, (2) Kunatusaidia “kuzifahamu nyakati” na (3) kunatuonyesha namna ya kutumikia kwa “moyo kamili”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki