Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 6/15 kur. 20-22
  • Msimamo wa Mtume wa Kupinga Uasi wa Imani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msimamo wa Mtume wa Kupinga Uasi wa Imani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Kristo Alikuja Katika Mwili?
  • Je! Yesu Siye Kristo?
  • Je! Sisi Ni Watenda Dhambi?
  • Ni Nini Kilichochochea Uasi wa Imani?
  • Mambo ya Kuzuia Utendaji wa Dhambi na Uasi wa Imani
  • Kitabu cha Biblia Namba 62—1 Yohana
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Endelea Kutembea Katika Nuru ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Onyesha Upendo na Imani Sikuzote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kataa Uasi wa Imani, Ambatana na Ile Kweli!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 6/15 kur. 20-22

Msimamo wa Mtume wa Kupinga Uasi wa Imani

Ili upate faida zote kabisa kutokana na makala hii, tunapendekeza usome kitabu cha Biblia kinachoitwa Yohana wa Kwanza. Kina kurasa chache tu.

KUELEKEA mwisho wa karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu, hatari kubwa yenye kujificha ilikuwa inakaribia kulipata kundi la Kikristo la kwanza. Je! hatari hiyo ilikuwa mateso kutoka kwa watu wale waliokuwa nje ya jamii ya Kikristo? Hapana, hatari iliyo kuu zaidi ilikuja kutokea ndani. Adui huyo mwenye kuotea-otea alikuwa uasi wa imani.

Kufikia mwaka wa 98 W.K. mtume mmoja alibaki awe kama boma la mwisho la kuzuia kile ambacho baadaye kingekuja kuwa wimbi kubwa la mafundisho ya uongo na hatua ya kukubali kuacha yaliyo haki kwa kufuata mambo yasiyofaa ya kidini na ya kisiasa. Huyo alikuwa ndiye mtume Yohana mzee-mzee, mwana wa Zebedayo na ndugu ya mtume Yakobo, ambaye aliuawa kwa sababu ya imani miaka karibu 54 kabla ya hapo. Alipokuwa kijana, Yohana alikuwa ametumikia pamoja na Yesu wakati wa huduma yake fupi ya kidunia. Labda Yesu alimwita Yohana ‘Mwana wa Radi’ (‘Mwana wa Ngurumo,’ UV) kwa sababu ya utu wake wenye matendo ya uthabiti mwingi sana. Sasa akiwa mwanamume mzee, alijianzisha kuandika barua yenye nguvu nyingi ya kuonya na kushauri makundi ya Kikristo. Anayosema yangali ni ya maana kabisa kwetu sisi leo.​—Marko 3:17; Luka 9:51-56, NW.

Yohana alijua vizuri sana kwamba uasi wa imani ulikuwa ukiendelea kupenya kwa kujificha kati ya waamini wenzake. Mtume Paulo alikuwa ametangulia kutabiri anguko hilo. (Matendo 20:29, 30) Kwa maneno yaliyo wazi kabisa Yohana aliwafichua wadanganyifu hao, akisema hivi: “Hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi.” Uhakika wa kwamba Yohana anataja “wapinga Kristo” kwa wingi unaonyesha kwamba uasi wa imani haukuhusu mtu mmoja tu, bali ulitia ndani watu wengi walioyakataa maoni ya Kristo ambayo yameonyeshwa katika Maandiko.​—1 Yohana 2:18, 19.

Wapinga Kristo hao walikuwa akina nani? Nao walikuwa wakijaribuje kudanganya waamini wenzao? Yohana anatoboa mambo wazi kabisa anapowafichua waasi wa imani waliokuwa wakipinga Kristo. Yeye anawashambulia juu ya makosa matatu: (1) kukana kwamba Kristo alikuja katika mwili, (2) kukana kwamba Yesu alikuwa ndiye Kristo na Mwana wa Mungu na (3) kukana kwamba wao wenyewe walikuwa watenda dhambi.

Je! Kristo Alikuja Katika Mwili?

Lakini huenda wewe ukauliza, ‘Waamini fulani wangewezaje kukana kwamba Yesu alikuwa amekuja katika mwili?’ Ni wazi kwamba kufikia mwisho wa karne ya kwanza Wakristo wengine walikuwa wameharibiwa na falsfa (elimu) ya Kigiriki, kutia ndani ufuasi wa watu wa siku hizo za kwanza waliodai kwamba wao pekee ndio waliokuwa na ufahamu wa kutambua mafumbo. Waasi-imani hao walishikilia maoni ya kwamba vitu vyote vya kimwili vilikuwa vyenye uovu, kutia ndani mwili wenye nyama. Hivyo, kulingana na maoni ya wapinga Kristo hao waasi-imani, Yesu hakuwa amekuja katika mwili wenye uovu, bali alikuja akiwa roho. Yohana anaonyesha wazi kwamba yeye hashiriki katika mawazo hayo ya elimu ya kidini ambayo yalikana kwamba dhabihu ya ukombozi ya Kristo ilikuwa na matokeo mazuri. Hivyo anaandika habari ya “Yesu Kristo mwenye haki” ambaye alikuwa “kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.”​—1 Yohana 2:1, 2.

Baadaye, Yohana anatumia maelezo ya moja kwa moja kulionyehsa wazi zaidi jambo lililohusika, akisema: “Kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu.”​—1 Yohana 4:2, 3.

Je! Yesu Siye Kristo?

Inaonekana kwamba watu wengine wenye kujiita Wakristo ambao walizaliwa wakiwa Wayahudi walikuwa wameanza kukana kwamba Yesu alikuwa ndiye Kristo na Mwana wa Mungu. Yohana anaupinga ukosefu huo wa imani kwa dharau, akisema: “Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana.” (1 Yohana 2:22) Maneno ya Yohana yenye kulenga kabisa jambo linalohusika hayawaachii nafasi watu wenye kutia mashaka.

Baadaye Yohana anatokeza ulizo jingine kutegemeza njia yake ya kuwaza: “Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu? . . . Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu.”​—1 Yohana 5:5, 13.

Je! Sisi Ni Watenda Dhambi?

Ijapokuwa linaelekea kuwa jambo lisiloweza kuaminiwa, wengine wa wapinga Kristo walikuwa wakisema kwamba wao hawakuwa na dhambi au labda walikuwa hawawezi kutenda dhambi (kwa kuwa walijiona kuwa wameokoka). Basi Yohana anagonga kwa nguvu wazo hilo lenye kosa katika sehemu zote za barua yake. Kwa mfano, yeye anasema: “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. . . . Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye [Mungu] kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.”​—1 Yohana 1:8-10.

‘Lakini dhambi ni nini?’ huenda wewe ukauliza hivyo. Neno la Kigiriki ha.marti’a linamaanisha kwa uhalisi “kuikosa shabaha.” Lakini akiwa chini ya uongozi wa Mungu Yohana anatupa sisi ufafanuzi wa maelezo mapana zaidi: “Kila [azoeaye, NW] atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi [Kigiriki, anomia, maana yake kudharau sheria na kuivunja, ukosefu wa kutenda haki, uovu]... Atendaye [anayeendeleza, NW] dhambi ni wa Ibilisi... Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi.”​—1 Yohana 3:4, 8, 9.

Ni kweli kwamba sisi sote ni watenda dhambi. Lakini jambo ambalo Yohana anataka kufanya ni kulaumu mtenda dhambi au mvunja-sheria wa kukusudia, yule ‘anayeendeleza dhambi,’ anayeizoea. Baadaye, anafunua wazi uzito wa hali ya mzoeaji wa dhambi kwa kusema hivi: “Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.” (1 Yohana 3:10; 5:18) Basi, na tuepuke uzoeaji wa dhambi usio wa Kikristo.

Ni Nini Kilichochochea Uasi wa Imani?

Ni nini ambacho labda ndicho kilichokuwa kichocheo kisichoonekana wazi cha mafundisho hayo mbalimbali ya uasi wa imani? Uwezekano mmoja unaonyeshwa na William Barclay, mwanachuo Mgiriki wa karne ya 20, ambaye anaandika kwamba matatizo ambayo Yohana anajaribu kupambana nayo yalitokana na watu “ambao lengo lao lilikuwa kufanya Ukristo uonekane kuwa wenye kuheshimika kwa upande wa maarifa ya kielimu . . . , ambao waliyajua maelekeo ya kielimu ya siku hizo, na ambao walitaka kuufuata Ukristo kulingana na mawazo ya falsafa iliyokuwako wakati huo. Yalitokana na watu waliokuwa na maoni ya kwamba wakati ulikuwa umefika Ukristo upatanishwe na falsafa ya kilimwengu na mawazo ya wakati huo.”

Maoni yanayofanana na hayo, yenye kushambulia imani ya kweli kwenye misingi yake, yamefuatwa na watu fulani katika nyakati za kisasa. Wabishani hao wanataka kupunguza uzito wa fundisho la Kikristo na kulifanya liwe lenye kukubalika zaidi kwa waheshimiwa wenye akili nyingi ya masomo ya mfumo huu. Kama maoni hayo yenye kushikiliwa na wengine yangalifuatwa, kwa uhakika Mashahidi wa Yehova wangalikuwa wamepoteza sifa zao na nguvu zao za kuwa watendaji zisizo na kifani ambazo zinasemwa kuwa ni za “Ukristo wa kishamba.”

Basi, shauri la Yohana linafaa sana hata leo: “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.” Amri hizo zinatia ndani kuzihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu na kuendelea kujitenga na ulimwengu na kutokuwamo katika mizozo yake, huku tukifanya yote tuwezayo tutakase jina la Yehova na kuzoea upendo wa kweli.​—1 Yohana 5:3; Marko 13:10; Yohana 17:16; Mathayo 6:9; 1 Yohana 3:23.

Mambo ya Kuzuia Utendaji wa Dhambi na Uasi wa Imani

Je! kuna kizuizi cha kuzoea dhambi? Jibu la Yohana ni kwamba: “Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, KWA MAANA MUNGU NI UPENDO.” Hivyo, Yohana anatumia njia nyepesi sana ya kueleza maana yake, Upendo ndio ufunguo. Na upendo wa Mungu ulioonyeshwa kupitia Mwana wake ndio kizuizi cha matokeo ya dhambi. “Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.” Maarifa ya kujua hivyo yawe na matokeo gani juu yetu? Yohana anajibu hivi: “Wapenzi, ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.”​—1 Yohana 4:8-11.

Ikiwa tunapenda Mungu na jirani kweli kweli, basi tutazipinga sana njia za kuingia katika dhambi na uasi wa imani. Upendo hautendi kinyume cha sheria na kanuni za Mungu kwa makusudi. Hata hivyo, Yohana anaonya hivi: “Iko dhambi iliyo ya mauti.” Kwa uhakika waasi wa imani wasiotubu wangehesabiwa katika fungu moja na wale wanaostahili uharibifu.​—1 Yohana 5:16, 17; Mathayo 12:31; Luka 12:10; Waebrania 6:4-6; 10:23-27.

Ikiwa dhambi na uasi wa imani unasikika kuwa habari isiyo ya kupendeza iliyo katika sehemu zote za barua ya Yohana, upendo unatajwa-tajwa katika barua yote kwa njia yenye uzuri mwingi. Ingawa barua yake ina onyo lenye uzito, bado inatiwa uchangamfu na vichwa vitatu vya habari zinazorudiwa-rudiwa​—upendo, nuru na uzima. Yohana anasema, ‘Epukeni waongo, wapinga Kristo, waasi wa imani. Tupilieni mbali giza, tembeeni katika nuru. Kataeni chuki kisha mzoee upendo. Pingeni sana dhambi, mkijua kwamba kama mnatenda dhambi mna msaidiaji au wakili-mteteaji kwa Baba, Yesu Kristo.’ Ndiyo, “huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.”​—1 Yohana 5:11; 2:1, 2.

Katika shauri lake la mwisho, Yohana anaonya hivi: “Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Katika ulimwengu wa Roma ya kale, shauri hilo lilifaa sana. Na kwa wale wanaotaka leo kuzoea Ukristo wa kweli na kuepuka uasi wa imani lingali ni la maana sana kama lilivyokuwa zamani hizo. Basi, sisi na tutii mashauri ya Yohana yaliyoongozwa na Mungu. Yatatusaidia kupinga sana dhambi, kuzoea upendo wa kweli we Kikristo, kutembea katika kijia cha ukweli na kuendelea kuwa na msimamo usiotikisika wa kupinga uasi wa imani.

[Picha katika ukurasa wa 21]

Falsafa ya Kigiriki iliongoza kwenye uasi wa imani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki