Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 7/15 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Habari Zinazolingana
  • Maagano Yanayohusisha Kusudi la Milele la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Agano la Mungu Pamoja na “Rafiki” Yake Tayari Lafaidi Mamilioni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Baraka Kubwa Zaidi Kupitia Agano Jipya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Yehova ni Mungu wa Maagano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 7/15 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Yale ambayo Yesu alisema katika Yohana sura ya 10 juu ya mazizi ya kondoo yanahusianaje na agano la Kiabrahamu?

Agano ambalo Yehova Mungu alifanya na Abrahamu linaeleza kusudi zuri ajabu la muda mrefu la Mungu kuwabariki watu kutoka mataifa yote kupitia uzao wa Abrahamu. Mazizi ya kondoo ambayo Yesu alizungumza juu yayo katika Yohana sura ya 10 ni sehemu-sehemu ndani ya kutimizwa kwa kusudi la Mungu lililofunuliwa katika agano la Kiabrahamu.

Alipokuwa akitoa maelezo zaidi juu ya agano lililotajwa kwanza katika Mwanzo 12:1-3, Mungu alimwambia Abrahamu hivi: “Katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.”​—Mwanzo 22:17, 18.

Lakini nasaba ya uzao huo ingelindwaje na kutunzwa ikiwa safi, na uzao ulioahidiwa ungetambulishwaje ukiisha kufika? Yehova Mungu alijiingiza akatoa agano la Torati ambalo mpatanishi walo alikuwa Musa; hilo halikuondoa agano la Kiabrahamu bali liliongezwa kwalo. (Wagalatia 3:16-18) Matakwa ya Torati yalisaidia kuendelea kulinda Israeli kutokana na uchafu wa kiroho, kiadili na wa kimwili wa mataifa yaliyowazunguka. Kwa njia hiyo Waisraeli wakawa kama kondoo ndani ya kuta zenye kulinda za zizi la kondoo lililo imara. Kuongezea hilo, kama Wagalatia 3:24 inavyosema, Torati ilikuwa kama mwalimu mwenye kuongoza kwenye “uzao” wa Kimasihi, ili kwamba wakati angefika Waisraeli wangeweza kutambua hali yao ya kuwa na dhambi na hali yao ya kumhitaji.

Yesu Kristo akawa uzao wa kwanza wa agano la Kiabrahamu, lakini bado Mungu alikusudia kuchagua wanadamu wengine wawe uzao wa pili. Kwa hiyo mtume Paulo aliandika kwamba wale ambao ‘ni wa Kristo ni uzao wa Abrahamu, na warithi sawasawa na ahadi.’ (Wagalatia 3:29) Sehemu hiyo ya agano la Kiabrahamu ingetimizwaje?

Kristo aliwatokea “kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli” akachagua wafuasi waaminifu kutoka miongoni mwa kondoo waliokuwa ndani ya zizi la kondoo la Torati ya Musa. (Mathayo 10:6) Wayahudi waliomtambua yeye kuwa Masihi, na kuwa mchungaji waliyemhitaji sana, aliwaingiza ndani ya zizi jipya, lile la Israeli wa kiroho lililotabiriwa katika “agano jipya’’ ambalo mpatanishi walo alikuwa Yesu mwenyewe. (Waebrania 8:7-13; Wagalatia 6:16) Baadaye, Wasamaria waliotahiriwa na watu wa Mataifa wasiotahiriwa waliingizwa ndani ya zizi hilo, wao pia wakawa sehemu ya uzao wa pili wa Abrahamu. Katika Yohana 10:11 Yesu alisema, “Mimi ndimi mchungaji mwema.” Na kwa hakika ndivyo alivyokuwa kwa Wayahudi na watu wa Mataifa waliokuwa Wakristo wapakwa mafuta waliokusanywa ndani ya zizi la kondoo la agano jipya.

Yote hayo yanaonyesha jinsi zizi la kondoo la Torati ya Musa kwa Israeli wa kimwili na zizi la kondoo la agano jipya pamoja na Israeli wa kiroho yalivyotumikia kwa kupatana na agano la Kiabrahamu.

Lakini namna gani juu ya “kondoo wengine” ambao hawakuwa wa “zizi hili,” zizi la Israeli wa kiroho ambao wanafanyiza uzao wa pili wa Abrahamu? (Yohana 10:16) Kondoo wengine pia wanatajwa katika agano la Kiabrahamu, kwa maana utakumbuka kwamba Mungu alimwahidi Abrahamu kwamba “na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.” (Mwanzo 22:18) Kondoo wengine hao wanaweza kusemwa wamo ndani ya zizi tofauti (zizi la pili) chini ya Mchungaji Mwema. Kwa hakika hawamo katika zizi lile lile pamoja na wanadamu wale ambao wamekuwa warithi kuhusiana na ahadi aliyopewa Abrahamu. Lakini wanafanya kazi kwa kushirikiana na uzao wa pili wa Abrahamu, na wamekuwa kundi moja chini ya yule mchungaji mmoja ambaye ndiye uzao wa kwanza wa Abrahamu. Kondoo wengine hao wana taraja zuri sana la kuwa na uzima wa milele katika Paradiso ya kidunia iliyorudishwa. Hakuna mtu anayeweza kukana aseme hawajibariki kwa njia hiyo kupitia uzao wa Abrahamu.

Basi, yale mazizi ya kondoo mbalimbali ya Yohana sura ya 10, yaani, zizi la kondoo la Torati ya Musa la Waisraeli wa kimwili, zizi la Israeli wa kiroho katika agano jipya, na mpango ulio kama zizi wa wale kondoo wengine ambao wanatoka katika “mataifa yote ya dunia,” mazizi yote hayo yanakamatana na kutimizwa kwa kusudi kuu la Mungu lililoonyeshwa katika agano la Kiabrahamu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki