Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 5/15 uku. 23
  • Maswali Kutoka Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Mfano wa Ngano na Magugu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Shamba Lenye Kuzaa Ngano na Magugu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • “Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • “Tazama! Mimi Nipo Pamoja Nanyi Siku Zote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 5/15 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Kama kweli Musa alikuwa mpole na mwenye kiasi, angewezaje kuandika katika Hesabu 12:3 kwamba ‘Musa alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote’?

Ingawa huenda ikawa haikuwa vyepesi kufanya hivyo, Musa aliweza kuandika maelezo hayo sahihi chini ya uongozi wa Mungu.

Alama moja inayoonyesha Biblia iliongozwa na Mungu ni kwamba waandikaji wake walisema mambo waziwazi. Musa na watu wengine waliotumiwa na Mungu kuandika visehemu vya Maandiko waliandika mambo kwa kuyasema wazi isivyo kawaida.

Kwa mfano, Musa aliandika visa vya hali za kupungukiwa na dhambi zilizotendwa na watu wake, kutia ndani zile za ndugu na dada yake mwenyewe. (Kutoka 16:2, 3; 17:2, 3;32:1-6; Mambo ya Walawi 10:1, 2) Wala Musa hakujiondoa asijitaje kati ya waliokosa; alisimulia waziwazi makosa yake mwenyewe, hata yale yaliyofanya akaripiwe na Mungu. (Hesabu 20:9-12; Kumbukumbu la Torati 1:37) Kwa hiyo lilikuwa jambo lenye kupatana na hali hizo nyingine Musa kuandika wazi habari ya uhakika ambayo inaonekana Yehova alitaka itiwe ndani​—kwamba Musa mwenyewe alikuwa mpole isivyo kawaida. Hali inayohusika katika kisa cha kuandikwa kwa maneno hayo inaonyesha vizuri jambo hilo. Badala ya Musa kuchukizwa sana wakati Miriamu na Haruni walipotokeza mwito wa ushindani juu ya mamlaka yake, yeye aliruhusu Yehova asahihishe hali hiyo.

Musa alitangulia kufananisha Masihi. (Kumbukumbu la Torati 18:15-19) Kwa hiyo Yehova Mungu alipoelekeza fikira kwenye upole wa Musa, Yeye alikuwa akitoa uhakikisho wa kwamba sifa hiyo ya kutamanika ingepatikana katika Masihi. Wakati tunaposoma yale masimulizi mbalimbali ya Injili, je! hatuoni upole wa Yesu ukituvuta, ukitufanya tutake kumkaribia na kutupa sababu ya kumtegemea?​—2 Wakorintho 10:1; Waebrania 4:15, 16.

◼ Katika mfano wa Yesu wa ngano iliyokuwa kati ya magugu, je! “magugu” yanatia ndani wale ambao hivi majuzi wamekuwa waasi-imani?

Hapana, kwa maana ikisemwa kulingana kabisa na jinsi mambo yalivyo, wao si “magugu.”

Mfano huo na maelezo ambayo Yesu aliutolea unapatikana kwenye Mathayo 13:24-30, 37-43. Katika “shamba,” (NW) ambalo ni ulimwengu, “Mwana wa Adamu” alipanda ile “mbegu njema,” inayofananisha “wana wa ufalme,” Wakristo wa kweli wapakwa mafuta. Halafu Ibilisi akapanda “magugu” ambayo huenda yakaonekana kama kwamba ni “ngano,” lakini kwa kweli ni “wana wa yule mwovu,” kwa wazi wakiwa ni Wakristo wa kusingizia tu wanaokuwako wakati mmoja na Wakristo wa kweli walio mfano wa ngano. Jambo hilo IiIisitawi hasa baada ya mitume kufa. (2 Wathesalonike 2:6, 7) Muda wote wa karne zilizopita wamekuwako wengi waliodai tu kuwa ni Wakristo, kutia ndani viongozi wa kidini ambao wameeneza mafundisho ya uongo.

Yesu alisema kwamba wakati wa kipindi cha mavuno, “umalizio wa mfumo wa mambo,” “magugu” yangekusanywa yatoke miongoni mwa wengine na “kuchomwa motoni “Huenda wengine wakaiona hesabu ndogo ya watu waliogeuka hivi majuzi wakawa waasi-imani kuwa ni “magugu” yanayokusanywa yatoke miongoni mwa wengine. Lakini Yesu hakusema kwamba wakati mmoja “magugu” yalikuwa “ngano” kisha yakageuka yakawa mabaya. Hayo yalipandwa yakiwa “magugu” na ndivyo yalivyobaki yakiwa, kupatana na sheria ya urithi wa tabia za uzazi kwamba majani ya shambani yanazaa “kwa jinsi yake.” (Mwanzo 1:11, 12) Hata hivyo, tunahitaji kukumbuka kwamba kwa kutaja “magugu,” Yesu alikuwa akitabiri namna fulani ya pekee ya Wakristo wa uongo, au wa kusingizia tu, ambao wangetokea. Hakuwa akizungumza juu ya watu mmoja mmoja wa jamii ya “ngano” ambao wangeweza kugeuka wawe wabaya, wawe kama vishina vya ngano vilivyooza.

Waasi-imani wa siku za mitume na wafanani wao wa kisasa hawafananishwi na “magugu.” Hata hivyo Biblia inaonyesha kwamba waasi-imani hao si “wa kwetu,” wanakosa kibali ya Mungu na wanapasa kuepukwa na Wakristo washikamanifu. Wo wote wanaoasi imani wasitubu kufikia mwisho wa huu mfumo wa mambo watapatwa na jambo lile lile litakalopata “magugu,” ‘wachomwe motoni’ au waharibiwe kabisa.​—Tito 3:10; 1 Yohana 2:18, 19; 2 Yohana 9-11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki