Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 5/15 uku. 22
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Kupata Kuwajua Wakristo wa Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Wakristo Wanaelekeana na Mateso kwa Uvumilivu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Upendo wa Kweli Unathawabisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Fuateni Njia ya Upendo Ipitayo Zote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 5/15 uku. 22

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Je! maneno ya Yesu yanayosema kwamba “upendo wa wengi zaidi utapoa” yanamaanisha kwamba jambo hilo litatukia kati ya waabudu wa kweli sasa?

Tukiwa na sababu nzuri tunaamini kwamba Yesu hakuwa akitabiri kupoteza upendo kwa kiasi kikubwa kati ya watu wa Yehova.

Mitume walikuwa wameomba ‘ishara ya kuwapo kwa Yesu na ya umalizio wa mfumo wa mambo.’ Yesu alitabiri vita, matetemeko ya ardhi, upungufu wa chakula na mateso ya Wakristo. Aliongezea hivi:“Kwa sababu ya kuongezeka kwa kutokutii sheria upendo wa wengi zaidi utapoa.”​—Mathayo 24:3-12, NW.

Mwingi wa unabii huo ulitimizwa kati ya wakati huo (33 W.K.) na dhiki kubwa iliyopata Yerusalemu kwa kusababishwa na Warumi mwaka wa 70 W.K. (Linganisha Luka 19:41-44; 21:5-28.) Wakati wa kipindi hicho cha katikati, je! upendo wa Wakristo wapakwa mafuta walio wengi ulipoa? Hapana. Wale walioanguka wakaacha Ukristo wakati wa kizazi hicho kwa wazi walikuwa wachache zaidi. Wakristo walio wengi wenye kuteswa na Wayahudi waliendelea ‘kuzitangaza habari njema za lile neno,’ wakionyesha upendo kwa Mungu, kwa wasioamini na kwa Wakristo wenzao. (Matendo 8:1-25; 9:36-42, NW) Lakini upendo ulipoa kati ya Wayahudi, ambao walidai kuwa waabudu wa kweli. Hesabu iliyo kubwa zaidi kati yao walipuuza onyo la Yesu, wakaasi Rumi na kutumia jeuri ili kukinga taifa lao.

Unabii wa Yesu unatumika kuhusu wakati wa baada ya karne ya kwanza na utimizo wake mkubwa ni leo. (Ufunuo 6:2-8) Kama ilivyokuwa kwa Wayahudi huko nyuma, watu wanaendelea kupungukiwa zaidi na upendo wenye matokeo. Mamilioni ya watu wamekuwa wasioamini kuna Mungu. Hata katika Jumuiya ya Wakristo watu wanaelekea kuonyesha upendo wa jirani ulio mpungufu zaidi, na mahudhurio ya watu kanisani na maarifa ya kujua Biblia kwa ujumla yanaendelea kupungua. Watu wengi wanaoonekana kama kwamba ni wa kidini wanajaribu kurekebisha matatizo ya kibinadamu kwa kutumia njia za kisiasa. Kwa hiyo inaonekana kwamba ni kati ya watu hao wanaodai kuwa ni waabudu wa Mungu ndimo upendo unaendelea kupoa.

Hata hivyo, ni lazima Wakristo wa kweli wasiwe na kinaya. Kwa kuwa Wakristo fulani katika karne ya kwanza waliacha upendo wao wa kwanza au wakavutwa fikira kando na matatizo, sisi tungeweza kukuta upendo wetu ukipoa. (2 Timotheo 2:16-19; Ufunuo 2:4) Ingawa kama jambo hilo lingetukia tungekuwa tofauti na watu wa Yehova walio wengi, uhakika wa kwamba lingeweza kutupata sisi mmoja mmoja unakazia uhitaji wetu wa ‘kuvumilia mpaka mwisho’ ili tuokolewe.​—Mathayo 24:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki