Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 10/15 kur. 11-15
  • Waliotiwa Nguvu Zinazopita za Kawaida

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waliotiwa Nguvu Zinazopita za Kawaida
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maandalizi Mazuri Ajabu ya Yehova
  • Elimu ya Kimungu
  • Mfalme na Wakuu Wake
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Ona Baraka za Umoja wa Ufalme!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • ‘Mdogo Awa Taifa Hodari’
    Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 10/15 kur. 11-15

Waliotiwa Nguvu Zinazopita za Kawaida

“Uwezo unaopita ulio wa kawaida [ni] wa Mungu na si ule unaotokana na sisi wenyewe.”​—2 WAKORINTHO 4:7, NW.

1. Yehova alitangulia kujua nini juu ya kipindi chetu cha wakati huu wa historia, na yeye aliwaonyaje watumishi wake juu ya kipindi hiki?

ZAMANI za kale Yehova alitangulia kujua nyakati zenye hatari ambazo zingekuja juu ya mataifa ya dunia. Yeye alitangulia kujua kwamba choyo na uovu wa wanadamu mwishowe ungetokeza mavuno mabaya sana ya uharibifu na jeuri. Mtume Paulo alisukumwa na roho ya Yehova atoe Onyo hili lililo wazi: “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake.” (2 Timotheo 3:1-5) Hakika hayo ni mazingira yenye hatari kwa wale wenye kutafuta kumtumikia Mungu wa ukweli!

2. Je! ingekuwa rahisi kwa mashahidi wa Yehova kutimiza kusudi lake alilowapa, na wao wangehitaji nini ili wafaulu?

2 Lakini ilikuwa katikati ya hali hizo Yehova alikusudia jina lake na Ufalme utangazwe duniani pote. Wa nani wangefanya hivyo? Ni watu ambao alifunulia jina na kusudi lake lenye maana​—Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10-12, NW) Yeye alitangulia kujua kwamba wangekabili upinzani kutoka kwa watawala ambao wangeuona Ufalme wa Mungu kuwa tisho na adui. (Zaburi 2:2, 3) Pia alijua kwamba mashahidi wake wangepatwa na matatizo na mateso yanayowapata watu wote. Wangehitaji uwezo unaopita ule ambao wao wenyewe wangeweza kujipa. Je! Mungu wao alifanya uandalizi kwa ajili ya uhitaji huo?

3. Uandalizi wa Yehova kwa ajili ya watumishi wake wakati huu wa hatari ni sawa na uandalizi gani aliofanyiwa Paulo?

3 Mambo yaliyompata mtume Paulo yanatoa jibu la ulizo hilo. Nyingine za hatari zilizomwelekea zimepangwa kwa ajili yetu katika 2 Wakorintho 11:23-27. Kwa kuwa Paulo aliagizwa na Yehova awe mtume na mwalimu wa mataifa, yeye alikaza fikira zake kwanza juu ya kazi hiyo ya kufundisha. (Warumi 11:13) Lakini yeye aliwezaje kuokoka hatari zote hizo na kumaliza kazi aliyokuwa amepewa afanye? Yehova aliendelea kumwangalia mtumishi wake mshikamanifu na kumwokoa, mara nyingi katika dakika ya mwisho, kwenye kila upeo wa hatari. Ili Paulo aweze kufanya huduma yake ya Kikristo kwa kufanikiwa, Mungu alimpa “uwezo unaopita ulio wa kawaida.” (2 Wakorintho 4:7, NW) Uwezo huo ulimwezesha mtume huyo avumilie mateso na ukosefu mkubwa wa vitu vya lazima maishani. Paulo alikubali waziwazi msaada huo wa kimungu alipoandika hivi: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”​—Wafilipi 4:13.

4. Je! Paulo alitambua msaada huo wa kimungu, na ulikuwa na matokeo gani juu yake?

4 Kwa hiyo inaonekana kwamba pamoja na matendo ya kimuujiza ya Mungu ya kujiingiza kwa ajili ya Paulo, Mungu ‘alimtia nguvu.’ Mambo hayo yalimwezesha mtume huyo afaulu kuvumilia na kutimiza huduma yake. Kwa hiyo, yeye aliandika: ‘Sionei haya habari njema; kwa sababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu, kwa kila aaminiye.’ (Warumi 1:16) Kupitia maana na utimizo wa unabii mwingi wa nyakati za kale, habari njema zilifunuliwa kwa Paulo, naye akasadikishwa juu ya ukweli wazo. Bila shaka, maarifa ya ukweli na kuuthamini pia yalikuwa vyanzo vya kumtia nguvu.

Maandalizi Mazuri Ajabu ya Yehova

5. Je! Yehova amekuwa haangalii sana mahitaji ya mashahidi wake waliopo duniani wakati huu?

5 Lakini namna gani watumishi wa Yehova duniani katika hizi siku za mwisho? Je! Mungu amefanya uandalizi kwa ajili yao? Ndiyo, hakika amefanya hivyo! Kama vile mtume Paulo, tuna unabii mwingi mzuri ajabu katika Maandiko Matakatifu Kwa kuwa Yehova alikuwa na maarifa ya kimbele ya mahitaji ya watu wake, kwa ukarimu yeye aliandaa maandishi hayo ili kuwapa uhakikisho na faraja. Unabii huo mbalimbali ungeelezwa wazi wakati siku za utimizo wake zingefika.

6. Unabii ambao Mungu alimpa Isaya umefarijije na kutiaje nguvu watu wa Yehova leo?

6 Mmoja wa unabii huo uliandikwa na Isaya mwana wa Amozi miaka 700 hivi kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. (Isaya 1:1) Isaya aliandika hukumu kali si juu ya taifa lake mwenyewe la Israeli tu bali pia juu ya mataifa mengi jirani, makubwa kwa madogo. Katikati ya ujumbe huo wa hukumu nabii huyo pia alitoa habari njema kwa waabudu washikamanifu wa Yehova​—habari ambazo zingewapa faraja katika dhiki zao zote. Na kama vile tu Wayahudi waaminifu walivyotiwa uwezo na tumaini na habari njema za Yehova, vivyo hivyo leo washikamanifu wanafarijiwa, kutiwa nguvu na kubarikiwa kwa utimizo wa ahadi nzuri sana za Yehova juu yao.

7, 8. (a) Maneno ya lsaya 32:1, 2 yalitiaje nguvu na kitia-moyo Wayahudi watawa wa wakati wa Isaya, na hasa kwa sababu ya hali gani? (b) Maneno ayo hayo yanatimiaje kati ya Mashahidi wa Yehova wakati huu?

7 Katika Isaya sura ya 32 tunapata kitia-moyo cha namna hiyo. Mistari ya kwanza miwili inatoa ahadi ambayo hata sasa inatimizwa: “Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu [“wana wa kifalme,” NW] watatawala kwa hukumu. Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.” Lazima hizo ziwe zilikuwa habari njema kama nini kwa waabudu wa Yehova wenye moyo mnyofu katika wakati wa Isaya, baada ya kuwa chini ya wafalme na wana wa kifalme wasio na imani kwa muda mrefu!

8 Lakini hizo ni habari njema kama nini kwa Mashahidi wa Yehova leo! Hasa tangu mwaka wa 1919, Mfalme Yesu Kristo aliyekalishwa juu ya kiti cha ufalme amesitawisha hali nzuri miongoni mwa wafuasi wake duniani. Ameweka katikati yao “wana wa kifalme” (Kiebrania, sarim) ambao kweli kweli wanatoa uangalizi wa haki na upendo. Tofauti na watawala wenye kuonea na wenye kujitumikia ambalo ndilo jambo la kawaida ulimwenguni pote, Mfalme huyo katika tengenezo la Mungu ameinua wanaume wenye madaraka ambao hawaabudiwi kama viongozi wa kidini au wengine kama hao. Mahali pake, wao ni watumishi wanyenyekevu, wanaume ambao kweli kweli wanahangaikia hali njema ya wote wenye mfano wa kondoo ambao Yehova amekusanya katika kikundi kimoja. Usimamizi wa wanaume hao, ambao pia wanatarajia kuwa “wana wa kifalme” wa Utaratibu Mpya, ni wenye kuburudisha kweli kweli.a

9. Ni badiliko gani limetokea kati ya watu wa Yehova?

9 Lo! hilo limeleta badiliko kama nini katika tengenezo la watumishi wa kidunia wa Yehova! Ni kama tu inavyosemwa katika Isaya 32:3: “Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.” Kwa sababu ya tamaa yao nyingi ya kuheshimu na kutumikia Yehova, yeye amefungua macho ya mioyo yao na masikio yao ya ufahamu. Amewapa ufahamu wenye kusisimua kuhusu mapenzi yake kwao. Mashahidi washikamanifu hawaegemei kwenye nia na njia za kidemokrasi. Wanauona kabisa uhakika wa kwamba wanatumikia katika tengenezo la kitheokrasi, tengenezo ambalo katika hilo mtu anahakikisha ni nini mapenzi ya Mungu halafu kuyafanya. Sifa inamwendea Theokrati Mkuu kwa ajili ya kufunulia watumishi wake wenye nia wa cheo cha chini walio wa kidunia makusudi yake.

10. Ni baraka gani nyingine nzuri ajabu ambazo watu wa Yehova walioangaziwa maarifa wanafurahia?

10 Ebu hesabu baraka ambazo watumishi wa Yehova wamepokea. Kati ya mambo mengine, wanafurahia maarifa sahihi kuhusu kuwapo kwa kifalme kwa Yesu Kristo tangu mwaka wa 1914; tofauti iliyo wazi kati ya tengenezo la Mungu linaloonekana na lile la Shetani; namna kazi yao ya kuhubiri ilivyo ya kufanywa mpaka ifike mbali kabla ya mwisho wa ulimwengu wa Shetani; utakatifu wa damu; na umaana wa kumpa Mungu vitu vilivyo vya Mungu. Katika tengenezo la Mashahidi wa Yehova kumekuwako kurudishwa kwa usimamizi kama ule uliokuwa kati ya Wakristo wa karne ya kwanza. Pia, baraka kubwa sana ni hali ya sasa ya kiparadiso katikati ya waabudu wa kweli. Zawadi hiyo pamoja na nyinginezo nyingi kutoka kwa Yehova inatia si uwezo tu bali pia amani, umoja na uradhi wa watu wake, hata wakati huu wa hatari katika historia.

11. Yehova ametiaje nidhamu au kufundisha wawakilishi wake wa kidunia, na ni maandiko gani yanayoonyesha kwamba jambo hilo lilikuwa la lazima?

11 Watumishi wa Yehova wamepewa dhamiri yenye msingi wa Biblia, hata kwamba wanasikia na kutii vikumbusho vyake, na kuvifuata katika maisha yao ya kila siku. (Zaburi 25:10) Wamekwisha kuonywa juu ya mazoea yaliyo najisi na machafu ambayo Mungu anachukia. Mambo ya kichoyo, yasiyo ya uadilifu, yaliyo haramu ambayo wengine wao walifanya wakati uliopita sasa wanayaacha nyuma, wakiwa wamekwisha kuyakataa kabisa. (1 Petro 4:3) Ni lazima iwe hivyo kwa wote wanaotaka kuendelea kushiriki katika baraka za Ufalme. Wote lazima wawe safi kiakili, kiadili na kimwili ili wafurahie pendeleo la kumtolea Yehova dhabihu ya sifa, “dhabihu katika haki.” (Malaki 3:3; Isaya 52:11) Lo! Mashahidi wote washikamanifu wanajiona ni wenye usalama kama nini wanaposhirikiana na umati mkubwa ambao ni wenye umoja kweli kweli katika utumishi wenye furaha ya Muumba!

Elimu ya Kimungu

12. Andiko la Isaya 32:4 limetimiaje kati ya watumishi wa kisasa wa Yehova?

12 Andiko la Isaya 32:4 linaendelea kusema: “Tena moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu maarifa, na ndimi zao wenye kigugumizi zitakuwa tayari kunena sawa-sawa.” Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, mabaki watiwa mafuta wa Yehova hawakuwa na ufahamu unaofaa, walikuwa wangali na madoa-doa ya mawazo ya Kibabuloni na njia ya kufanya mambo ya kitheokrasi haikuwa ikitenda kazi kati yao. Lakini mwaka wa 1919 Mungu aliwafungua kutoka utumwa wa Kibabuloni akawapa maarifa mengi zaidi ya kweli zake. Kupitia kweli hizo wamejifunza kuwa wenye kiasi, si wenye hamaki. Sasa wanaisema imani yao kwa uhakika, wala hawasemi kwa kigugumizi wakiogopa na bila uhakika. Na je, tunawezaje sisi binafsi kuwa wahubiri wakomavu wenye ujasiri wa habari njema? Ni kwa kutumia kwa faida kabisa maagizo ya kimungu, ambayo mengi yayo yanatolewa wakati wa mikutano kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Kwa mfano, hakuna shaka kwamba Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ni njia moja ambayo kwayo Yehova amebariki watumishi wake na kuwatia nguvu waseme ukweli kwa ujasiri na kwa uwazi.

13. Twapaswa tujihadhari na maneno ya namna gani?

13 Hali moja na hiyo, elimu ya kimungu imefunza watumishi wa Mungu wasitoe ahadi ambazo hawakusudii kutimiza na wasiseme maneno ya kuchongea wala ya kumuumiza mtu mwingine. Kwa hakika baraka ya Mungu iko pamoja na wale wanaotii shauri hilo, lililoandikwa katika Mhubiri 5:2: “Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, kwa hiyo maneno yako na yawe machache.” Ni jambo la maana sana kutolaumu kwa uchungu kamwe tengenezo la Bwana wala wawakilishi walo waliowekwa rasmi. Yehova ndiye Hakimu mkuu sana ambaye mbele zake hesabu itatolewa kwa ajili ya kusema maneno hayo na mengine yasiyofaa.​—Mathayo 12:36, 37; Mambo ya Walawi 19:16; Yuda 8.

14. Ni onyo gani linalotolewa hapa kwa ajili ya watu wa Yehova, na andiko la Mithali 29:20 linakaziaje hilo?

14 Wanaodharau mafundisho ya Yehova ni kutia na watu mmoja mmoja ambao wanalaumu-laumu na kunung’unika juu ya tengenezo safi la Yehova na amri zalo za kudumisha amani na utaratibu mzuri. Kuna tofauti ndogo tu kati yao na wale wanaoasi waziwazi. Kora na wenye kumuunga mkono walitambua hivyo na kupatwa na maangamizi kabisa walipothubutu kufanya hamaki katika kusema mambo ya kumpinga mtumishi wa Mungu, Musa. (Hesabu 16:1-40) Kuhusu habari iyo hiyo, andiko la Mithali 29:20 linasema: “Je! umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.”

15. Maneno ya Isaya 32:5, 6 yametimiaje kwa watumishi wa Yehova leo?

15 Pia Yehova amewabariki watu wake kwa hekima watambue yaliyo mema na yaliyo mabaya. Wanajihadhari na wo wote wanaowajia kwa maneno matamu-matamu na usemi wenye kuvutia, na labda hata wakija na zawadi, wakiwa na kusudi la kudanganya mioyo ya wasiojihadhari. (Linganisha 1 Timotheo 6:20, 21; Yuda 16.) Huenda wanadini wakajaribu kuwapelekea habari njema zilizo tofauti na zile ambazo tayari wamepokea kutoka kwa Yesu Kristo na mitume wake. Zaidi ya hilo, watu mmoja mmoja wapumbavu na wasioongozwa na kanuni wanakataliwa wasiwekwe rasmi kuwa watumishi katika tengenezo la Yehova. Hilo linapatana na maneno haya: “Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala ayari [mtu asiyeongozwa na kanuni] hatasemwa kwamba ni karimu. Maana ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli [yaliyopotoka, NW] juu ya [Yehova], ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.”​—Isaya 32:5, 6.

16. (a) Mengine kati ya mawazo ambayo waasi imani wametokeza ni yapi? (b) Kwa habari hiyo, ni mambo gani yanayosemwa katika Isaya 32:7?

16 Je! si kweli kwamba wale ambao wametoka kwetu katika miaka iliyopita kwa sababu ‘si wa kwetu,’ na wanaojaribu kushawishi wengine wafuate mwendo uo huo wenye kuhatirisha maisha, wamejitenga na chanzo cha chakula kigumu cha kiroho na maji ya kiroho yenye kuburudisha? (1 Yohana 2:19) Na wapumbavu hao badala ya kuwa wakarimu na wasio wanyimivu kuelekea wanadamu wenye njaa na kiu ya uadilifu, hawaoni uhitaji wo wote wa haraka wa kazi ya kuhubiri yenye kufanywa kitengenezo katika wakati wetu. Wanasema kila mtu anapaswa kuongozwa na usomaji na ufasiri wake wa kibinafsi wa Biblia badala ya kuwe umoja wa watu waliozoezwa kuishi na kutenda kupatana na kanuni za juu na vikumbusho vya Neno la Mungu. (Zaburi 133:1-3; 1 Wakorintho 1:10) Wangependa kudanganya wengine wasadiki kwamba Yehova ataendelea kusamehe wakosaji kwa wakati usiojulikana maadamu tu wanaonyesha toba ya kinje-nje. Yenye kupendeza kuhusiana na hilo ni yanayosemwa katika Isaya 32:7 juu ya waasi imani wa Israeli ya kale: “Tena vyombo [njia za kutimiza kusudi lake] vyake ayari [mtu asiyeongozwa na kanuni] ni vibaya; hutunga hila mbaya, ili kuwaangamiza wanyonge kwa maneno ya uongo, mtu mhitaji ajaposema maneno yenye haki.”

17. (a) Yesu amechagua nani wawe wafuasi wake? (b) Ni maulizo gani yanayotokea kuhusu utendaji wao wa wakati ujao katikati ya hali zenye kuwa mbaya zaidi za ulimwengu huu mbovu?

17 Wafuasi wa kweli wa Yesu, ambao amechagua kwa sababu wanatambua uhitaji wao wa kiroho, kwa uhakika ‘wanasema maneno yenye haki.’ Lakini wapinzani wapumbavu hawapendezwi na hali njema halisi ya wale wanaotafuta ukweli. Wana nia ya kuwavuta wafuasi wawafuate wao wenyewe, hata iwe wanajiingiza wao wenyewe na wengine katika hatari ya namna gani. Lakini, je, Yehova ataruhusu wenye mioyo minyofu wategwe na mawazo ya uongo? Je! yeye ametoa uandalizi kwa ajili ya baraka za watumishi wake mwenyewe na utumishi wao wa kuhubiri ulimwenguni pote?

[Maelezo ya Chini]

a Tafadhali ona Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Desemba 1, 1951, kurasa 716-29.

Wewe Ungejibuje?

◻ Yehova ametiaje nguvu mashahidi wake leo?

◻ Maneno ya Isaya 32:1,2 yanatimiaje kati ya Mashahidi wa Yehova?

◻ Nyingine za baraka wanazofurahia watu wa Mungu walioangaziwa maarifa ni zipi?

◻ Andiko la Isaya 32:5, 6 linahusuje leo?

[Picha katika ukurasa wa 14]

Je! wewe unakataa kusikiliza wenye kulaumu-laumu kwa uchungu tengenezo la Yehova? Unapaswa kukataa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki