Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/1 kur. 22-23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • “Lori” Ndogo za Mwili Wako
    Amkeni!—2001
  • Chembe Nyekundu za Damu Zenye Kustaajabisha
    Amkeni!—2006
  • Waebrania 4:12—“Neno la Mungu Liko Hai na Linatenda Kazi”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/1 kur. 22-23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Ikiwa mtoto wa mzee wa kundi ana hatia ya kosa zito, je! jambo hilo linafanya moja kwa moja baba huyo asistahili kuwa mzee?

Ndugu ‘hawi moja kwa moja asiyestahili’ kutumikia akiwa mzee ikiwa mwanaye au bintiye mdogo ana ugumu fulani mzito. Mambo yote yanayohusika yanahitaji kufikiriwa katika kuamua kama anastahili.

Andiko la Tito 1:6 (NW ) linasema kwamba mzee ‘asiwe na shtaka,’ awe “mwenye watoto wanaoamini ambao hawakushtakiwa kuwa na ufisadi wala utundu.” (Linganisha 1 Timotheo 3:4.) Mashahidi wa Yehova wanashikilia kiwango hicho.

Kwa hiyo, gazeti The Watchtower la Septemba 1, 1983, lilikazia kwamba mzee anahitaji kutia jitihada yenye usawaziko aipe jamaa yake, mkeye na watoto wo wote walio nao, mahitaji ya moyoni na ya kiroho. Mwanamume akikosa kujali jambo hilo inaelekea jamaa yake itapatwa na madhara. Mahitaji ya kumtunza mtoto kiroho na kumtia nidhamu yasipotimizwa, huenda akashindwa kufanya maendeleo kiroho kisha akahusika katika kosa zito. Jambo hilo lingefanya baba huyo asiyejali aache kustahili kutumikia kundi akiwa mzee aliyewekwa, kwa maana, kama vile 1 Timotheo 3:5 (NW ) linavyosema: “Ikiwa kweli mwanamume ye yote hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, yeye ataliangaliaje kundi la Mungu?”

Mazungumzo marefu zaidi juu ya jambo hilo yanapatikana katika kurasa 23, 24 za Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 1978. Ulionyesha sababu gani mambo yote yanayohusika lazima yafikiriwe. Kwa mfano, mzee mmoja alijifunza Biblia kwa ukawaida pamoja na watoto wake watano, akashiriki katika tafrija, akawapeleka kwenye mikutano ya Kikristo kisha katika njia zile nyingine zinazofaa akajitahidi kutimiza madaraka yake akiwa baba Mkristo. Wanne kati ya watoto hao waliendelea vizuri sana, lakini mwana mmoja alikuwa akiwatatiza daima, na baadaye akaingia katika dhambi. Jambo hilo lisingeleta lazima ya kufanya baba huyo aache kustahili kuwa mzee ikiwa bado aliheshimiwa na kundi.

Huenda kundi likawa linajua kwamba ndugu alifanya yote yanayaweza kutazamiwa kwa kiasi kutokana na baba Mkristo katika kutunza jamaa yake, awe alikuwa ana mtoto mmoja au wengi. Kwa hiyo ikiwa mtoto aliharibika, huenda wasiwe na maoini ya kwamba ni kosa la baba. Huenda wakathamini kwamba hali za kupotoka kwa Yuda Iskariote na malaika aliyekuja kuwa Shetani hazipasi kutumiwa kuweka lawama juu ya Yesu au Yehova. Ni jambo la maana ndugu anayetumikia akiwa mzee aendelee kuheshimiwa sana na kundi, ili wote waweze kukubali mashauri yake yanayotegemea Biblia na wakiisha kuona namna mwenendo wake kwa ujumla ulivyo, waweze kuiga imani yake.—Waebrania 13:7

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki