Je! Unakumbuka?
Umefurahia matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Basi ona kama unaweza kukumbuka:
◻ Kitabu cha Mambo ya Walawi kinaweza kuwaje na matokeo mazuri juu ya ibada yetu?
Wakristo leo hawaishi chini ya Torati. Hata hivyo, kitabu cha Mambo ya Walawi kinatupa ufahamu juu ya maoni ya Yehova kuhusu mambo mbalimbali, na kwa hiyo, kinaweza kuwa na matokeo mazuri juu ya ibada yetu. Kwa mfano, kinakazia kwetu uhakika wa kwamba Yehova anatazamia utakatifu kwa watumishi wake. Hiyo inaonyesha kwamba ni lazima Wakristo watunze jina lake likiwa takatifu kwa kujitahidi daima kuepuka dhambi, kumpa Yehova vilivyo bora zaidi na kudumisha usafi na utakatifu katika utumishi wanaomtolea.—9/1/84, kurasa 22, 23.
◻ Tarehe ya 1914 ina umaana gani?
Katika mwaka wa 1914 matukio yalianzishwa ambayo yatatokeza badiliko kamili katika tamasha ya ulimwengu. Yesu alianza kutawala katika Ufalme wake wa kimbingu, baada ya hapo Shetani alitupwa kutoka mbinguni. Karibuni Ufalme wa Mungu utavunja-vunja mifumo inayotawala. (Danieli 2:44)—10/2/84, kurasa 5-7.
◻ Kitabu cha Hesabu kina thamani gani kwa Wakristo leo?
Kinatoa kiunganishi cha thamani katika maandishi ya kimungu yanayoongoza kwenye kusimamishwa kwa Ufalme wa Mungu. Dhabihu za wanyama zinaelekeza kwenye dhabihu ya Yesu Kristo. (Hesabu 19:2-9; Waebrania 9:13, 14) Pia, kitabu hicho kinawasaidia Wakristo waepuke ibada ya sanamu na ngono zisizo za adili, na kinawatahadharisha na hatari ya kunung’unika juu ya Mungu, watu alioweka rasmi na maandalizi yake.—10/15/84, ukurasa 24.
◻ Makumbusha ya Yehova yanaweza kutufaidije leo?
Makumbusha ya kimungu yanatusukuma tumtafute Yehova kwa moyo wetu wote. Jambo hilo linatuletea furaha nyingi, na kutuzuia tusiende kombo au kufuata mwendo fulani wa aibu machoni pa Mungu. (Zaburi 119:2, 31, NW)—11/15/84, kurasa 19-23.