Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 4/15 kur. 3-4
  • Kizazi Chetu cha Kukatisha Tamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kizazi Chetu cha Kukatisha Tamaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wanadamu Wanaweza Kuleta Amani na Usalama Wenye Kudumu?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Ni Nani Wanaosababisha Tisho la Vita vya Nyuklia?
    Amkeni!—2004
  • Tisho la Nyukilia—Laondolewa Milele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Tisho la Nyuklia Halijaisha
    Amkeni!—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 4/15 kur. 3-4

Kizazi Chetu cha Kukatisha Tamaa

NINGEPENDA kuona amani ya ulimwengu katika siku za maisha yangu,” akasema mwanafunzi wa chuo aliye kijana, “lakini najua hiyo ni ndoto tu kwa sababu ya chuki yote iliyomo ulimwenguni.” Je! wewe pia unahisi hivyo? Je! hali ya ulimwengu inaonekana kuwa isiyo na tumaini kwako?

Maoni hayo yasiyo na tumaini yana msingi mzuri. Hali ulimwenguni ni zenye hatari zikiangaliwa kutoka pande nyingi. Kuwapo kwenyewe kwa wanadamu kunahatirishwa. Hewa, chakula na maji ya dunia yanachafuliwa kwa kadiri yenye kushtua sana. Hali za kiuchumi zinakuwa mbaya zaidi na uhalifu unaongezeka sana, na kuwafanya wengi daima wawe wakiogopa kwa ajili ya maisha zao na mali zao. Mchafuko na wasiwasi wa ulimwengu ni wa kadiri isiyopata kufikiwa tena hapo mbele.

Jambo lenye kuhangaisha hata zaidi ni tisho la kuangamizwa na silaha za nyukilia ambalo linaelea juu ya dunia kama kitambaa cha kufunika jeneza huku vita na maasi yanapoendelea bila kukoma. Akiwakilisha wengi kwa aliyosema juu ya kukata tamaa, mwanafunzi mwingine alisema: “Inaonekana hakuna lo lote hata ambalo mtu binafsi anaweza kufanya juu ya suala la vita vya nyukilia.”

Hata ikiwa maangamizi ya silaha za nyukilia yangeweza kuepukwa, kuwapo kwa wanadamu kunahatirishwa na wingi wenyewe tu wa wanadamu. “Hesabu ya watu duniani inaongezeka daima na kwa kadiri kubwa ajabu kwamba kufikia mwaka 2000—miaka 16 [hivi] kutoka sasa​—ulimwengu, pamoja na mabilioni yake yaliyoongezwa, hautaweza kutoa chakula cha kutosha na nishati, achilia mbali kazi, nyumba, elimu na utunzaji wa afya,” ndivyo linavyoripoti gazeti Parade. “Na kinachoweza kutokea kufikia katikati ya karne ya 21 (wakati watoto wanaozaliwa katika kumi hilo la miaka watakapokaribia uzee) ni jambo lisilowazika.”

Kila mwaka, mamilioni wanakufa kwa ajili ya hali yenye kuogopesha sana ya ukosefu wa chakula kinachofaa iliyopo katika nchi nyingi changa. Mtaalamu mmoja kwenye U.S. Census Bureau’s Center for International Research anasema: “Isipokuwa tendo la mataifa yote lichukuliwe haraka sana kuzuia ongezeko la watu, naona kuvunjika kwa mifumo ya serikali.” Yanayotangulia kuonwa, ni kumalizwa kwa mali za asili za msingi pamoja na ukosefu wa chakula kinachofaa wenye kuenea sana na maradhi, uhamaji wa watu wengi, njaa kubwa-kubwa zaidi, mchafuko kati ya raia na hata vita.

Hata hivyo, uadui wenye kuongezeka wa kibinadamu pamoja na choyo vinaondoa tumaini lo lote kwamba watu watasuluhisha matatizo na tofauti zao kwa njia ya akili na ya kirafiki. Utumiaji wa nguvu unakuwa ndio mwongozo unaofuatwa kila mahali huku jeuri ikiwa njia ya kawaida ya kueleza malalamiko, ya kweli au ya kuwazia. Adili “za kizamani” za udugu​—kuhangaikia na kuheshimu wengine​—zaonekana ni kama karibu hazipo kabisa katika ulimwengu wetu wa kisasa. Kweli kweli, kama Biblia ilivyotabiri, kuna “huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea . . . , huku wanadamu wakizimia moyo kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.”​—Luka 21:25, 26, NW.

‘Lakini, bila shaka, wanadamu wanapokomaa wanatambua maangamizi yanayokaribia ya nyakati zetu za hatari, wanaweza kufanya mapatano ili kuhakikisha kuwapo kwa amani na ufanisi wa ulimwengu,’ huenda ukasema. Ingawa hilo laonekana kuwa jambo la kutamanika, je, kweli ni tumaini la kweli? Maandishi ya kihistoria yanaonyesha nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki