Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 4/15 kur. 4-6
  • Je! Wanadamu Wanaweza Kupatana Juu ya Utatuzi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wanadamu Wanaweza Kupatana Juu ya Utatuzi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Mapatano Yanadumu?
  • Alama ya Nyakati Zenye Hatari Zetu
  • Wakati Ujao Mzuri kwa Watoto Wetu
    Amkeni!—1997
  • Inawezekana Kuepuka Vita vya Nyuklia?
    Amkeni!—2004
  • Amani ya Kweli—Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Ufalme wa Mungu—Ndio Utatuzi Hakika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 4/15 kur. 4-6

Je! Wanadamu Wanaweza Kupatana Juu ya Utatuzi?

KWA KADIRI ambayo historia inaonyesha wakati wa nyuma, mapatano yamevunjwa kwa ukawaida kwa kupendelea faida za kichoyo za taifa. Zaidi ya hilo, hayajazuia vita.

“Tangu watu walipojikusanya katika makabila,” aandika Laurence W. Beilenson katika kitabu chake The Treaty Trap, “mapatano ya amani yamekamatana na vita. Lakini hayo ndiyo maajabu ya vibandiko kwamba mapatano ya amani bila kujua kabisa yanashirikishwa na amani na kutokuwapo kwayo na vita. Jambo hilo limewafanya wengine wenye kutoa maelezo wasisitize kwamba kwa kuwa vita imekuwa ya kuleta hali ya kujiangamiza zaidi, akili inasema inafaa mapatano yategemewe ili kuizuia. Lakini, maneno hayawezi kukatwa kwa jambo hilo. Vita ya nyukilia ingekuwa msiba, lakini mambo yaliyoonwa katika historia ndiyo peke yake yenye kuongoza juu ya kama mapatano yatazuia vita.”

Je! Mapatano Yanadumu?

Kumbukumbu la kihistoria linaonyesha kwamba mapatano hayazuii vita. “Mataifa yote yamekuwa ni kawaida yao kuvunja mapatano,” asema Beilenson. Na ingawa raia wa kibinafsi wanaweza kuona kutekelezwa kwa hukumu ya mahakama dhidi ya kuvunja mkataba ndani ya nchi yao, sivyo ilivyo wakati mapatano kati ya mataifa yanapovunjwa. Huenda vita ikatumiwa kuwa njia yenye matokeo ya kulipiza kisasi.

Wala mahakama za kimataifa hazijaweza kutatua magomvi na kudumisha amani ya ulimwengu. Mahakama ya Kimataifa ya Kuleta Haki (baraza la kisheria la Umoja wa Mataifa, ambalo mara nyingi linatajwa kuwa Mahakama ya Ulimwengu), kwa mfano, haiwezi kutekeleza maamuzi yake. Badala yake, inategemea maoni ya ulimwengu na ubembelezi wa kwamba jambo fulani linafaa. Mataifa mengi yamekataa kukubali mamlaka ya Mahakama hiyo kuwa yanapaswa kufuatwa ili kutatua magomvi. Na kulingana na amri za Mahakama ya Ulimwengu yenyewe, taifa linaweza kukataa kuhukumiwa nayo kwa kusema hivyo kabla kesi fulani haijapelekwa kwenye Mahakama hiyo.

Jambo lenye kuongeza tatizo hilo ni uhakika wa kwamba mataifa yanachomwa sana hasa na mambo ambayo yangehusu enzi zao. Kwa hiyo, yanajihadhari sana yanapofanya mapatano, mara nyingi yakifanya hivyo katika lugha ambayo ingeweza kuwaruhusu kuepa wakati wo wote enzi kuu yao inapowekewa vizuizi. “Kwa kawaida mapatano yanafanywa katika lugha isiyo waziwazi,” chasema kitabu The Encyclopedia Americana. “Amri za kufasiri ni nyingi sana . . . lakini hakuna zoea linalokubaliwa kwa ujumla kuwa lenye kufaa katika kutekeleza yo yote ya hizo. . . . Kwa hiyo kutokubaliana juu ya maana inayofaa kunakuwapo, na mashtaka ya kuvunja mapatano ni mengi mno.” Kama alivyosema wakati mmoja Charles de Gaulle, aliyekuwa rais wa Ufaransa, ndivyo ilivyo: “Mapatano ni kama wanawake vijana na waridi. Yanakuwapo maadamu yapo.” Halafu akitumia maneno ya Victor Hugo katika kitabu Les Orientales, akaongeza hivi: “Maskini ni wasichana wangapi vijana nimeona wakifa.”

Alama ya Nyakati Zenye Hatari Zetu

Biblia ilitabiri zamani sana kwamba wakati wetu ungejaa watu wenye kiburi na choyo wasiotaka kukubaliana au kutimiza ahadi yao. Katika 2 Timotheo 3:1-5 tunasoma: “Ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya [mapatano], wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.”

Hizi “siku za mwisho” zilianza katika karne hii​—mwaka wa 1914, na vita ya ulimwengu ya kwanza​—na zimeendelea mpaka wakati wetu huu. Ukweli wa unabii huo wa Biblia umethibitishwa kabisa na kumbukumbu la kihistoria. Kwa kushtuliwa na ukali wa ile Vita Kuu, kama ilivyokuwa ikiitwa wakati huo, mataifa yalijaribu kufanya mapatano ambayo yangezuia vita nyingine kubwa jinsi hiyo. Kabla ya vita hiyo, hakukuwako mapatano yo yote yaliyokataza vita ulimwenguni pote wala tengenezo lo lote lililokusudiwa kutekeleza amani. Kwa hiyo viongozi walitafuta kufanya mapatano kati ya mataifa ili yafanye jambo hilo na kuhakikisha amani ya ulimwengu.

Agano la Ushirika wa Mataifa lilikuwa ahadi kwamba mataifa yaliyo washiriki yangetegemezana na kulindana wala hayangepigana, isipokuwa iwe ni kujilinda, na hata ingekuwa hivyo tu baada ya kupeleka ugomvi kwenye Baraza la Ushirika huo ili upate kusuluhishwa na kuruhusu kuwe kipindi cha miezi mitatu cha kutulia. Lilianza kutenda mwaka wa 1920. Mapatano ya Locarno, yaliyoanza kutenda mwaka 1926, yalitukuzwa kuwa “ushindi kwa ajili ya amani na usalama” kati ya mataifa ya Ulaya. Mkataba wa Paris, ambao pia unaitwa Mkataba wa Kellogg-Briand, ulilaani “kutegemea vita.” Ungekuwa mkataba wa kukubalianwa na wengi ambao mataifa yote yangeruhusiwa kutia sahihi.” Ulitangazwa rasmi mwaka 1929, na hatimaye ukatiwa sahihi na mataifa 63 yaliyokubali kusuluhisha magomvi yao kwa “njia za amani” peke yake. Hesabu fulani ya mapatano mengine ilifanywa na kuanza kutenda wakati wa kipindi hicho. Jambo hilo lilifanya wengi wafikiri kwamba vita ingekuwa jambo la wakati uliopita. Lakini ilikuwa muda mfupi baadaye mataifa hayo yalipohusika katika vita nyingine ya ulimwengu.

Basi, je, wanadamu wanaweza kufanya mapatano ya amani? Kumbukumbu la kihistoria na matukio ya ulimwengu ya leo yanajibu HAPANA! Ni kama mbuni wa vitabu Beilenson anavyolisema jambo hilo: “Baada ya uharibifu wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, viongozi wa serikali walitengeneza muundo wa makaratasi wenye nguvu zaidi wa amani uliopata kufanywa. Haukuzuia madharau makubwa ya kupuuza mapatano zaidi ya wakati mwingine wo wote wa historia, au uharibifu mkubwa sana wa Vita ya Ulimwengu ya Pili, au vita vingine vidogo zaidi tangu wakati huo. Yajapokuwa mapatano ya Umoja wa Mataifa, mataifa yaliendelea kuwa bila umoja.”

Leo, kwa kuwa wanadamu ‘hawataki kufanya mapatano’ kama ilivyotabiri Biblia, hakuna mapatano ya ujumla ya amani na ulimwengu unaishi katika hali ya woga. Je! hiyo inamaanisha kwamba hakuna tumaini kwa nyakati zetu za hatari? Ikiwa kuna utatuzi, unapatikana wapi?

[Picha katika ukurasa wa 5]

“Mapatano . . . yanakuwapo maadamu yapo”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki