Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 5/15 kur. 15-20
  • “Timiza kwa Ukamili Huduma Yako”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Timiza kwa Ukamili Huduma Yako”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya kuitimiza Huduma kwa Ukamili Zaidi
  • Kitia-Moyo Kinahitajiwa
  • Geuka Kutoka Waliko Waasi-Imani
  • Baraka Kutokana na Ushirika wa Kikristo
  • Kazi ya Mwevanjeli
  • Kutimiza Kazi Hiyo
  • Ni Nini Kinachoweza Kutusaidia Kutumia Neno la Kweli Sawasawa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kitabu cha Biblia Namba 55—2 Timotheo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Timotheo Anapata Mashauri kwa Mwanamume Mzee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 5/15 kur. 15-20

“Timiza kwa Ukamili Huduma Yako”

“Mimi nakuamuru kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, aliyekusudiwa kuhukumu walio hai na waliokufa, . . . timiza kwa ukamili huduma yako.”​—2 TIMOTHEO 4:1, 5, NW.

1. Uhusiano kati ya Paulo na Timotheo ulikuwa nini?

WAKATI mtume Paulo alipoandika barua yake ya pili kwa Timotheo, Paulo alikuwa amefuatia mradi wake akiwa mhudumu wa Mungu kwa miaka 30 hivi. Alikuwa amepokea baraka nyingi kutoka kwa Yehova. (2 Timotheo 1:2) Paulo alikuwa amemchagua Timotheo afanye kazi kwa ushirikiano wa karibu pamoja naye katika kazi ya kusafiri, wakitumikia makundi. Walifurahia miaka ya visa tele wakiwa pamoja.​—Matendo 16:1-5.

2. Ni nini umaana wa maneno ya Paulo kwenye 2 Timotheo 4:6-8?

2 Sasa wakati ulikuwa umekaribia huduma ya Paulo iishe. Aliandika hivi: “Sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.” (2 Timotheo 4:6-8) Hilo lilidokeza kwamba kifo cha Paulo kilikuwa kimekaribia. Inafahamika kwamba Paulo alipatwa na kifo chini ya mateso ya Nero mwaka wa 66 W.K. Akiwa anakabiliwa na kifo ni mawazo gani yangepita akilini mwake? Labda haya: Je! nilifanya utumishi wangu vizuri? Je! nilimaliza huduma yangu kwa kufanikiwa? Ndiyo, Paulo angaliweza kusema usadikisho wake kwamba alikuwa amefanya hivyo? Imani yake ilikuwa yenye nguvu sana, naye alikuwa na uhakika kwamba angepata zawadi ya mwito wa juu. Lazima awe alikuwa na uradhi kama nini kwa sababu hakuuacha kamwe mgawo wake!

3. Kabla ya kifo chake, ni jambo gani jema ambalo Paulo angeweza kumfanyia Timotheo?

3 Paulo angali alikuwa amebaki na wakati mchache wa kufanya jambo jema Kabla hajalala katika kifo, Paulo angeweza kumfanyia Timotheo jambo gani jema? Chini ya uongozi wa roho ya Mungu alitoa mashauri yenye maana. Tunasoma mawazo na maneno yake katika kitabu cha Timotheo wa Pili. Hayo ndiyo maandishi yake ya mwisho katika Maandiko kwa ajili ya faida yetu pia.

4. Ni onyo gani ambalo Paulo alimpa Timotheo?

4 Timotheo alikuwa bado hajamaliza mgawo wake katika huduma, kwa hiyo Paulo aliandika hivi: “Mimi nakuamuru kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, aliyekusudiwa kuhukumu walio hai na waliokufa, na kwa wonyesho wake na ufalme wake, lihubiri neno, fanya hivyo kwa haraka kwa majira yanayofaa, kwa majira yenye taabu, karipia, kemea, tia moyo, kwa ustahimili wote na ustadi wa kufundisha. Kwa maana kutakuwako kipindi cha wakati ambapo hawatakubali fundisho linalofaa, bali, kwa kulingana na tamaa zao wenyewe, watajikusanyia kwa wingi walimu kwa ajili yao ili watekenywe masikio; na watayageuza masikio yao mbali na ukweli, ambapo watageuzwa kando kwenye hadithi za uongo. Lakini, wewe, tunza akili zako katika mambo yote, vumilia ovu, ifanye kazi ya mwevanjeli, timiza kwa ukamili huduma yako.”​—2 Timotheo 4:1-5, NW.

5. Ni kwa nini shauri la Paulo ni lenye kutupendeza kipekee?

5 Shauri hilo jema lazima liwe lilimfaidi Timotheo sana, lakini je, sisi, pia, tutafaidika nalo? Tunaishi katika “siku za mwisho” ambazo Paulo aliandika juu yake. Watu wengi leo wana “mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake.” (2 Timotheo 3:1-5) Watu hao wana maelekeo ya kusikiliza “walimu” wale tu watakaotekenya masikio yao. Hata hivyo, kuongezea kuhubiri lile neno katika kikao cha kundi, Wakristo wa kweli wana daraka la kuhubiria wote peupe, wakitafuta wale watakaoitikia “neno.” Kwa hiyo shauri hilo linahusu leo kwa mashahidi Wakristo wa Yehova.

Jinsi ya kuitimiza Huduma kwa Ukamili Zaidi

6. (a) Ni kwa nini tunapaswa ‘kulihubiri neno’? (b) Ni faida gani zinazoletwa na kukaza fikira juu ya jinsi tunavyoifanya huduma yetu?

6 Huduma hiyo ina sehemu zenye kutofautiana; kuna mambo mengi anayopaswa kufanya mhudumu. Kwanza, Paulo alitaja, “lihubiri neno.” Hilo ni neno ambalo Yehova amechagua kufunulia watumishi wake. Ndilo neno la ukweli ambalo juu yake Yesu alisema. Yehova anajulisha ujumbe wake ni nini kwa wanadamu kwa wakati uliopo, akihakikisha mashahidi wake duniani wanasema juu ya upande wake wa suala. Njia ya Yehova ni kutoa ujumbe wa onyo kabla hajachukua hatua. (2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16; Isaya 42:9; 43:12; Yona 3:2-4) Ujumbe wake utatokeza faida kwa wale wanaousikiliza; wanaweza kupata mahali pa usalama. Wale wasiosikiliza watakiona wakati Yehova atakapochukua hatua ya kutekeleza hukumu yake. Ni lazima wabebe daraka lao wenyewe. (Matendo 20:20, 21, 26, 27) Hata hivyo, mwendo wa hekima kwa mhudumu wa Mungu ni huu: “Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.”​—1 Timotheo 4:16.

7. Ni kwa nini hiyo ni kazi ya uharaka hata ikiwa hali zinaonekana kuwa si nzuri?

7 Kazi ya kuhubiri inafanywa chini ya hali zenye kutofautiana, lakini ni lazima isonge mbele. “Uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa,” Paulo aliandika. Ujumbe huo unaweza kumaanisha uzima kwa watu. Kwa hiyo, mhudumu mwaminifu hata ajikute katika hali gani, yeye anauona ujumbe huo kuwa wenye kutaka hatua ya haraka na anatafuta njia za kusikizisha neno, hata ikiwa upinzani fulani unatokea juu ya kazi ya kuhubiri. Tunaweza kuona hilo waziwazi kupitia mfano wa Yesu na maandishi katika kitabu cha Biblia cha Matendo.

8. (a) Ni nini linaloweza kumsaidia mhudumu ahubiri neno? (b) Ni kwa nini kukaripia kwaweza kuwa sehemu ya huduma?

8 Ili kulihubiri neno, iwe ni ndani au nje ya kundi, ni lazima mhudumu afahamiane na Neno la Mungu, yeye akiwa mwanafunzi walo. Ni lazima atumie wakati kujifunza, kufikiria na kutafakari, akitafuta kulielewa vizuri. Kuhubiri ni lazima kutegemee msingi wa kufahamiana na mafundisho ya ukweli. Paulo alimwambia Tito kwamba mwangalizi ni lazima awe “mwenye kushikamana kwa imara na neno la uaminifu kwa habari ya ustadi wake wa kufundisha, apate kuweza kutia moyo kwa fundisho ambalo ni lenye afya na kukaripia pia wale wanaopinganisha.” (Tito 1:9, NW) Neno la Mungu linatumika likiwa njia ya kutoa karipio kwa wale wasiopatana na anayotaka Yehova, likimsahihisha mkosaji kwa faida yake mwenyewe. Hiyo yote ni sehemu ya kutimiza huduma kwa ukamili.

Kitia-Moyo Kinahitajiwa

9. Ni kwa nini onyo la Kikristo linahitajiwa?

9 Nyakati nyingine vikumbusho vinahitajiwa kwa ajili ya wale ambao huenda wakawa hawafanyi kila jambo wanalopaswa kufanya au ambao wanakosa kuthamini na kukosa kuwa na bidii kwa ajili ya ibada ya Yehova. Kitia-moyo cha Kikristo kinathaminiwa sana na wale wenye upendo kwa ajili ya Yehova. Wanafurahi kusikia anayosema Yehova na wanayaona kuwa chakula cha kiroho kinono. (Isaya 55:3; Waebrania 12:5, 6) Kwa hiyo ni utumishi mzuri kwa wafanyi kazi wenzetu​—na pia kwa watu wenye maelekeo ya kumwabudu Yehova​—kuwatia moyo kwa Neno la Mungu. Paulo mwenyewe alitoa vitia-moyo vingi,—Warumi 15:30; 16:17; 1 Wakorintho 1:10, 11; 1 Timotheo 4:13; 6:11, 12; Waebrania 10:24.

10. Ni kwa nini ustahimilivu unatakwa kwa kukamatana na kutoa onyo?

10 Mhudumu aliye wakfu pia anapaswa kujua jinsi ya kusitawisha matunda ya roho ya Mungu. Huenda ikachukua saburi na uvumilivu mwingi kujaribu kutia moyo wale wasioitikia mara moja. Huenda wengine hata wakaonyesha ukosefu wa kuthamini jitihada zinazofanywa za kuwatia moyo na kuwahimiza. Hata hivyo, ni lazima hilo lifanywe, hasa na wazee Wakristo wote. Ustadi wa kufundisha unahusika. Kwa kadiri mtu anavyotumia Neno la Yehova zaidi, ndivyo anavyokuwa stadi zaidi katika kulitumia. Wakati mwalimu anapomjua mwanafunzi, anapaswa aweze kumpa maarifa huyo. Paulo anasimulia vizuri njia inayofaa katika 1 Wathesalonike 5:14: “Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.”

Geuka Kutoka Waliko Waasi-Imani

11. Tunapaswa kufanya nini kuhusu waasi-imani?

11 Paulo alitaka Timotheo aweze kudumisha usawaziko wake, au kutunza akili zake katika mambo yote. Hakupaswa ajiruhusu awe kama wale wasioendelea katika mafundisho yenye afya na kugeuza masikio yao kutoka uliko ukweli. Mhudumu wa kweli wa Mungu leo hana wasiwasi usiofaa wala kuhangaishwa katika utendaji wake anapoona kwamba wengine wanageuka mbali kutoka kwa Neno la Mungu na mafundisho yalo yenye afya. Tumekwisha kutangulia kuonywa kwamba kungekuwako waasi-imani na watu ambao wanapenda kutekenywa masikio yao tu. Mashauri kama kwenye 2 Yohana 9-11, 1 Wakorintho 5:11-13 na 2 Timotheo 3:5 hayaruhusu hata kidogo kushirikiana na wale wanaogeuka mbali kutoka kwa ukweli Wala hatununui wala kusoma maandishi yao. Kuna wengine wengi wanaopenda kuusikia ukweli, na wao ndio tunakuwa na ushirika wa Kikristo nao.​—1 Timotheo 6:20, 21.

12. Kwa nini mhudumu Mkristo anakuwa na msimamo imara huo?

12 Paulo alishauri hivi: “Watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.” (2 Timotheo 3:13) Kwa msaada wa onyo hilo la kimbele, mhudumu Mkristo hafuatani na watu wa namna hiyo. Yeye anatii shauri zuri la mtume: “Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu. Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” (2 Timotheo 3:14-17) Funzo la kawaida la Neno la Mungu ni msaada kwa wale wanaotafuta kutimiza huduma yao.

Baraka Kutokana na Ushirika wa Kikristo

13. Kufanya kazi katika huduma pamoja na Paulo kulikuwaje kwenye faida kwa Timotheo, na tunaweza kufaidikaje?

13 Ilikuwa baraka kweli kweli kwa Timotheo kuwa na miaka ya ushirikiano pamoja na Paulo, akaweza kuona jinsi mhudumu mwaminifu, aliyekomaa wa Mungu anavyojiongoza mwenyewe. Paulo alitumia mambo waliyoona kuwa kikumbusho kizuri kwa ajili ya Timotheo: “Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili; naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.” (2 Timotheo 3:10-12) Ingawa sisi leo hatushirikiani moja kwa moja na Paulo, maandishi mengi ya njia zake yanayopatikana katika Biblia yanatusaidia sisi pia.

14. Ni kwa nini tunapaswa kuwa tayari kupatwa na ovu?

14 Paulo alitaja mateso na taabu zake, na shauri lake kwa mhudumu Mkristo ni awe na nia ya kupatwa na ovu. (2 Timotheo 4:5) Mara nyingi ni lazima kupitia aina fulani ya mateso katika kutimiza huduma yetu kwa ukamili. Ni pendeleo kuendelea kushika ukamilifu chini ya jaribu na kufurahisha moyo wa Yehova. (Mithali 27:11) Ushuhuda unaweza kutokeza sifa iwe kwa Yehova!

Kazi ya Mwevanjeli

15. Ni kwa nini kueneza evanjeli ni lazima kufanywe tunapotimiza kwa ukamili huduma yetu?

15 Kueneza evanjeli kunachukua sehemu kubwa ya wakati wa mhudumu Mkristo mwaminifu. Yesu alisema: “Sharti injili ihubiriwe kwanza katika mataifa yote.” (Marko 13:10) Alionyesha wazi kwamba mwisho hautakuja mpaka habari njema ziwe zimehubiriwa vya kutosha. Paulo alipendelewa kushiriki habari njema pamoja na waamini wengi katika Milki ya Roma yote. Matokeo yalikuwa kuanzishwa kwa makundi mapya na kuwekwa kwa waangalizi. Wao, nao, walishiriki pamoja na ndugu na dada zao Wakristo katika kazi ya kueneza evanjeli na kwa hiyo wakapanua kazi ya kuhubiri kwa mapana na marefu. Nyingi ya kazi inafanywa kama alivyoeleza Paulo, ‘kufundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba.’ (Matendo 20:20) Wakati huo kulikuwako matokeo mazuri, na kuna matokeo bora sana leo wakati ambapo kuhubiri kwa Kikristo kunafanywa ulimwenguni pote.​—Yohana 14:12.

16. Ni ushuhuda gani unaoonyesha kwamba wengi wanafuata shauri la Paulo kwenye 2 Timotheo 4:5?

16 Kwa imani, wengi wanatumia nafasi ili kupanua utendaji wao katika kazi ya kueneza evanjeli. Maelfu wameingia katika shamba la umisionari, na mamia ya maelfu wanashiriki katika namna namna za utumishi wa painia. Katika nchi 205 sasa kuna zaidi ya 2,650,000 wanaotumikia wakiwa waeneza evanjeli katika makundi zaidi ya 46,000, na hesabu zinaongezeka. Mambo hayo mazuri ajabu ni ushuhuda kwamba watumishi walio wakfu wa Yehova wanaweka moyoni daraka lao la kimungu na ‘kutimiza kwa ukamili’ huduma yao.

Kutimiza Kazi Hiyo

17. Yehova anataka kuona watumishi wake wakifanya nini kuhusiana na kazi waliyogawiwa leo?

17 Yehova amewapa mgawo wa huduma wapakwa mafuta wake, na “mkutano mkubwa” unafanya kazi pamoja nao kando kwa kando. Kwa njia ya unabii, katika Ezekieli sura ya 9, kazi hiyo inafananishwa na kuweka alama juu ya vipaji vya nyuso za wale wanaopiga kite na kulia. Tunajua kutokana na unabii huo kwamba wakati utakuja ambapo yule mtu mwenye kidau cha wino cha mwandishi atakaposema: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.” Yehova anapendezwa na watumishi wake wanapofanya kama anavyowaamuru.​—Ezekieli 9:4, 11; Mwanzo 6:22; 1 Wakorintho 4:2.

18, 19. Ni zipi baadhi ya njia ambazo katika hizo unaweza sasa kufuata onyo la Paulo kwenye 2 Timotheo 4:1-5?

18 Tunapotazama hali za ulimwengu zikisitawi kwa kupatana na unabii mbalimbali unaohusu hizi siku za mwisho, tunalazimika kuona hatua ya haraka inayotakiwa ya kazi ya kuhubiri tuliyogawiwa. Maisha yanahusika. Kukusanya kunaendelea na Yehova anakuharakisha kwa wakati wake. (Isaya 60:22) Kwa hiyo, hata daraka lako liwe nini ukiwa mtumishi wa Yehova aliye wakfu, tia jitihada ya kulifanya ili umpendeze kwa ukamili. (Wakolosai 1:10; 3:23, 24) Kumbuka kazi uliyopewa ufanye na kujaribu kuitimiza kwa ukamili. Ikiwa unaangalia kazi fulani kwenye Jumba la Ufalme, fanya kazi hiyo kwa ukamilifu. Ikiwa umegawiwa utendaji mbalimbali pamoja na Funzo la Kitabu la Kundi, fanya kazi kwa ukaribu nalo na kuonyana na kutiana moyo. Ikiwa wewe ni painia au misionari, hakikisha kufanya kazi kwa bidii ili utimize miradi yako ya utumishi.​—Warumi 12:6-9.

19 Pia unaweza kujiuliza mwenyewe, Je! ningeweza kuwa nikifanya jambo fulani zaidi ili kusaidia Wakristo wengine, hasa wapya katika kundi, niwe mwenye kuwajenga? Ikiwa sehemu ya huduma yako ni kuwa mzee katika kundi, lijue “kundi” lako linavyoonekana na watunze vizuri wale wanaoshirikiana nalo. Kaza fikira ili ye yote asiwe asiyetenda au asiyezaa matunda kuhusiana na maarifa sahihi ya Bwana Yesu Kristo. (2 Petro 1:5-8) Zaidi ya yote, uwe macho kuona unayofanya katika kazi ya kueneza evanjeli mpaka ufikie ‘kutimiza huduma yako kwa ukamili.’​—Kutoka tcl2/15/84.

Mambo ya Kukumbuka

◻ Hali ya Paulo ilikuwa nini alipoandika Timotheo wa Pili?

◻ Ni kwa nini ni jambo la maana sana kuhubiri lile neno?

◻ Ni kwa nini onyo ni la maana?

◻ Walimu wa uongo wanapaswa kushughulikiwaje?

◻ Ni kwa nini kueneza evanjeli ni kwa maana sana leo?

[Picha katika ukurasa wa 16, 17]

Barua ya pili ya Paulo aliyomwandikia Timotheo ilimsaidia ‘atimize kwa ukamili huduma yake’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki