Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 6/15 kur. 3-4
  • Mashariki ya Kati Ndiyo Uwanja wa Har-Magedoni?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashariki ya Kati Ndiyo Uwanja wa Har-Magedoni?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Har–Magedoni—Si Mambo Haya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Har-Magedoni—Kwa Nini Inasemwa Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vita vya Har-Magedoni Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Har-magedoni Lini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 6/15 kur. 3-4

Mashariki ya Kati Ndiyo Uwanja wa Har-Magedoni?

“HAR-MAGEDONI”​—jina hilo la Kibiblia lina maana gani? Mfululizo wa makala zenye habari nyingi zinazohusu kichwa hicho utakuwa katika matoleo manne ya Mnara wa Mlinzi ya Juni na Julai 1985, na kila mara jalada la gazeti litapatana na habari iliyomo. Inatumainiwa kwamba mazungumzo hayo ya Kimaandiko yatakufariji kwa kukujulisha maana ya HAR-MAGEDONI hasa.

“ULIMWENGU unapopiga mbio kuelekea kwenye saa yake ya mwisho ya kupambana, mji mashuhuri wa kukazia macho si New York, Mosko, Paris, Peking, wala Kairo. Mji wa kuangalia ni Yerusalemu!” Ndivyo walivyotamka wanadini John F. na John E. Walvoord katika kitabu chao Armageddon, Oil and the Middle East Crisis (Har–Magedoni, Mafuta na Mzozo wa Mashariki ya Kati).

Watu wengi kweli wanakaza macho huko Yerusalemu na jimbo ulimo ndani yalo wakiwa na wasiwasi. Linasema gazeti Times la London, “Mashariki ya Kati inazidi kuogopesha.” Wengine wanaogopa kwamba wakati ujao hakuna budi kutokea mpambano kati ya Amerika na Urusi. Kufikia Januari 1984, uhusiano kati ya serikali hizo zenye nguvu nyingi zinazopingana ulikuwa umeharibika sana hata kichapo Bulletin of the Atomic Scientists kikasogeza ‘saa yake ya kupimia siku ya maangamizi’ (ambayo ni mfano wa namna ulimwengu ulivyo karibu na uharibifu wa nyukilia) kwenye dakika tatu kabla ya usiku wa manane. Kichapo Bulletin kilitamka hivi: “Hivyo sisi tumesimama kwenye hatua yenye msiba, kwenye ukingo wa kipindi cha mapambano, wakati ambao kuna hatari ya nguvu kutumiwa moja kwa moja badala ya namna nyingineyo yote ya mazungumzo kati ya serikali hizo zenye nguvu nyingi sana. Hilo ni taraja la kushtua sana.”

Hata hivyo, hesabu inayoongezeka ya wahubiri, walimu wa kidini na waevanjeli wa televisheni wanaoshikilia kwamba unabii unapasa kufahamika kwa njia ya uhalisi, wanashangilia matukio hayo. Misukosuko inayoongezeka katika Mashariki ya Kati imefanya ielekee kuonekana kama kwamba inathibitisha matabiri yao ya kugutusha kwamba karibuni Har–Magedoni itatokea katika ujirani huo! Na kwa kutoa onyo katika vitabu, hotuba, na vipindi vilivyotayarishwa vya televisheni, wamejikusanyia wafuasi wengi.

Waelezaji hao wanabishania mfululizo wenyewe hasa utakaofuatwa na matukio hayo. Lakini ‘mpangilio wa Har–Magedoni’ walioufanya uko namna hii: Wanasema kuanzishwa kwa Taifa la Israeli ndiko kulikuwa mwanzo wa ‘hatua za kuikaribia siku ya msiba.’ Basi wanaona kwamba Wakristo wako karibu kunyakuliwa wapelekwe hewani. Kulingana na wao, karibuni Wakristo wa kweli watatoweka kwa ghafula hapa duniani​—wanyakuliwe mbinguni. Wakati wa miaka saba itakayofuata ya “dhiki,” waevanjeli wengi hata wanatabiri kwamba taifa la Israeli litageuzwa lifuate Ukristo. Ingawa hivyo, wengi wa jamii ya kibinadamu wanasemekana watawekwa chini ya maongozi ya mtawala mtumia mabavu mwenye uvutano mkubwa juu ya watu (yule “Mpinga Kristo”) atakayeongoza muungano wa mataifa kumi ya kisiasa. Wanaamini kwamba hata Israeli itajipanga pamoja naye. Lakini mataifa ya Kiarabu na mengine yenye ushirika yatafanya shambulio la ghafula juu ya Israeli, yakiongozwa na Urusi. Mungu atakomesha kwa muujiza shambulio hilo, ndivyo wanavyosema watu hao wanaoshikilia kwamba unabii ufahamike kwa njia ya uhalisi. Lakini, baada ya muda mfupi kutakuwa na shambulio jingine kutoka kwa “Mpinga Kristo,” hilo likiifyatusha vita ya kukata maneno kabisa katika Mashariki ya Kati​—Har–Magedoni.

Labda hilo linasikika kuwa jambo la kuaminika sana na watu wengine. Ingawaje, kwa uhakika Biblia inatabiri mkusanyo wa mataifa kwa ajili ya vita kwenye “Har–Magedoni.” (Ufunuo 16:14-16) Lakini je! kweli Biblia inaonyesha kwamba tukio hilo litafanyika katika Mashariki ya Kati? Napo mahali pa pigano hilo pana maana gani?

[Picha katika ukurasa wa 3]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki