Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 8/1 kur. 20-21
  • Ujumbe Mbalimbali Kutoka Mbinguni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ujumbe Mbalimbali Kutoka Mbinguni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Jumbe Kutoka Mbinguni
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Wapokea Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Elisabeti Apata Mtoto
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Apendelewa Kabla ya Kuzaliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 8/1 kur. 20-21

Maisha na Huduma ya Yesu

Ujumbe Mbalimbali Kutoka Mbinguni

KAMA ilivyo, Biblia yote ni ujumbe kutoka mbinguni, uliotolewa na Baba yetu wa kimbingu ili kutuagiza. Lakini, ujumbe wa pekee ulitolewa mara mbili karibu miaka 2,000 iliyopita na malaika mmoja ‘asimamaye mbele za Mungu.’ Jina lake ni Gabrieli. Na tuchunguze hali za ziara hizo mbili za duniani zenye maana.

Ni mwaka wa 3 K.W.K. Katika vilima vya Yudea, yaelekea si mbali sana kutoka Yerusalemu, anaishi kuhani mmoja wa Yehova mwenye jina Zekaria. Amezeeka, na mkeye Elisabeti amezeeka pia. Nao hawana watoto. Ni zamu ya Zekaria kutoa utumishi wa kikuhani katika hekalu la Mungu katika Yerusalemu. Kwa ghafula Gabrieli amtokea upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia uvumba.

Zekaria anaogopa sana. Lakini Gabrieli atuliza woga wake na kusema: ‘Mungu amesikia sala zako. Elisabeti atazaa mwana, na utamwita Yohana. Ataandalia Yehova watu waliotayarishwa.’ Lakini Zekaria anashindwa kuamini. Laonekana kuwa jambo lisilowezekana hata kidogo kwamba, katika umri wao, yeye na Elisabeti wangeweza kuzaa mtoto. Kwa hiyo Gabrieli anasema, ‘Kwa sababu hukunisadiki, hutaweza kusema mpaka mambo hayo yote yatokee.’

Wakati mambo hayo yanapoendelea, watu walio nje wanashangaa-shangaa ni kwa sababu gani Zekaria amekawia sana hekaluni. Mwishowe anapotoka, hawezi kusema isipokuwa kuonyesha ishara za mikono peke yake, nao watu wanajua ameona kitu kinachopita nguvu za kibinadamu.

Baada ya Zekaria kumaliza kipindi chake cha kutumikia hekaluni, anarudi nyumbani. Na baada ya muda mfupi yanatimia​—Elisabeti anakuwa na mimba! Anapongojea mtoto wake azaliwe, Elisabeti akaa nyumbani mbali na watu kwa miezi mitano.

Tazama! Gabrieli anatokea tena. Naye anasema na nani? Anasema na mwanamke kijana ambaye bado hajaolewa jina lake Mariamu wa mji wa Nazareti. Wakati huu anatoa ujumbe gani? Sikiliza! ‘Utakuwa na mimba na kuzaa mtoto mvulana, nawe utamwita jina Yesu,’ Gabrieli anasema. ‘Yeye atakuwa mfalme mkuu, na ufalme hautakuwa na mwisho.’

Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Gabrieli alijihesabu ana pendeleo kutoa ujumbe huo mbali-mbali. Na tusomapo mengi zaidi juu ya Yohana na Yesu katika matoleo ya wakati unaokuja ya gazeti hili, tutaona kwa uwazi zaidi ni kwa sababu gani ujumbe huo mbalimbali kutoka mbinguni ni wa maana sana. 2 Timotheo 3:16; Luka 1:5-33.

◆ Ni ujumbe gani wa maana uliotoka mbinguni mara mbili?

◆ Ni nani aliyetoa ujumbe huo, na aliyepewa ujumbe huo mbalimbali ni nani?

◆ Ni kwa sababu gani huo ujumbe mbalimbali ulikuwa mgumu sana kuamini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki