Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Je! andiko la 2 Yohana 10, linalosema mtu asikaribishe nyumbani au kusalimu watu fulani, lilihusu wale peke yao waliofundisha uwongo?
Kulingana na vifungu vinavyozunguka mstari huo shauri hili lilihusu “wadanganyaji wengi” waliokuwa wametokea, “wasiokiri ya kuwa Yesu Kristo [alikuja] katika mwili.” (2 Yohana 7) Mtume Yohana alitoa mielekezo juu ya jinsi Wakristo huko nyuma walipaswa kumtendea mtu aliyekana kwamba Yesu alikuwa amekuwako au kwamba alikuwa ndiye Kristo na Mkombozi. Yohana alielekeza hivi: “Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.” (2 Yohana 10,11) Lakini kwingine Biblia inaonyesha kwamba hili lilikuwa na matumizi mapana zaidi.
Wakati mmoja kati ya Wakristo katika Korintho, mwanamume mmoja alikuwa akizoea mwenendo usio wa adili, na mtume Paulo aliwaandikia waache ‘kuchangamana na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.’ (1 Wakorintho 5:11) Basi, je, hilo lilihusu waliokuwa ndugu hapo kwanza waliokuwa wamefukuzwa kwa ajili ya makosa mazito tu yaliyoorodheshwa hapo?
Hapana. Andiko la Ufunuo 21:8 linaonyesha pia kwamba watu kama wauaji wasiotubu, wachawi, na waongo wanatiwa kati ya wale wanaostahili kifo cha pili, Kwa hakika shauri katika 1 Wakorintho 5:11 lingehusu pia kwa mkazo ule ule wale waliokuwa wamekuwa Wakristo hapo kwanza wenye hatia ya makosa hayo. Kuongezea hayo, Yohana aliandika kwamba wengine “walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.” (1 Yohana 2:18, 19) Yohana hakusema kwamba walikuwa wamefukuzwa kwa ajili ya dhambi nzito. Labda wengine wao waliacha tu, wakaamua kwamba hawakutaka tena kuwa ndani ya kundi kwa sababu hawakukubaliana na fundisho fulani. Huenda wengine wakawa walichoka wakaacha.—1 Wakorintho 15:12; 2 Wathesalonike 2:1-3; Waebrania 12:3, 5.
Bila shaka, kama ndugu alikuwa ameanza kwenda kwenye njia mbaya ya dhambi, Wakristo waliokomaa wangejaribu kumsaidia. (Wagalatia 6:1; 1 Yohana 5:16) Hata kama alikuwa na mashaka, wangejaribu ‘kumnyakua katika moto.’ (Yuda 23) Hata kama alikuwa amekuwa asiyetenda, asiende kwenye mikutano au katika huduma ya peupe, wenye nguvu kiroho wangejitahidi kumrejeza. Huenda akawa aliwaambia hakutaka kusumbuliwa juu ya kuwa ndani ya kundi, kuonyesha imani yake ilidhoofika na hali ya kiroho ilishuka. Hawangemsukuma-sukuma, lakini pindi kwa pindi wangemtembelea kirafiki. Jitihada hizo za upendo, subira, na rehema zingeonyesha kupendezwa kwa Mungu kwamba ye yote asipotee,—Luka 15:4-7.
Tofauti na hilo, maneno ya Yohana yanaonyesha kwamba wengine walichukua hatua inayozidi kuwa dhaifu kiroho na kutotenda; kwa kweli walikana kundi la Mungu. Huenda mtu akawa alijitokeza waziwazi kupinga watu wa Mungu, akitangaza kwamba hakutaka tena kuwa ndani ya kundi. Hata huenda akawa alikataa imani yake ya kwanza kwa njia rasmi, kama kwa njia ya barua. Bila shaka, kundi lingekubali uamuzi wake wa kujitenga mwenyewe. Lakini sasa wangemtendeaje?
Yohana anasema: “Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia. Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.” (2 Yohana 9, 10) Bila shaka maneno hayo yangehusu mtu aliyekuwa mwasi-imani kwa kujiunga na dini ya uwongo au kwa kueneza fundisho la uwongo. (2 Timotheo 2:17-19) Lakini namna gani wale ambao Yohana alisema “walitoka kwetu”? Kwa kuwa Wakristo katika karne ya kwanza walijua kwamba hawapaswi kushirikiana na mkosaji aliyefukuzwa au na mwasi-imani, je, walitenda vivyo hivyo kuelekea mtu ambaye hakufukuzwa bali aliyekana kwa makusudi njia ya Kikristo?
Kitabu Aid to Bible Understanding kinaonyesha kwamba neno “uasi-imani” iinatoka kwa neno la Kigiriki linalomaanisha kwa halisi ‘“kusimama mbali na’ lakini lina maana ya ‘kuondoka, kuacha au uasi.’”a Kitabu Aid kinaongeza hivi: “Kati ya visababisho vya uasi-imani mbalimbali vilivyoonyeshwa kwenye maonyo ya mitume kulikuwa: kukosa imani (Ebr. 3:12), kukosa uvumilivu wakati wa kuteswa (Ebr. 10:32-39), kuacha viwango vya adili (2 Pet. 2:15-22), kusikiliza ‘maneno ya bandia’ ya walimu wa uwongo na ‘semi zilizoongozwa na roho zenye kupoteza’ ( . . . 1 Tim. 4:1-3) . . . Watu hao kwa kuacha makusudi kundi la Kikristo wanakuwa sehemu ya ‘mpinga Kristo.’ (1 Yohana 2:18,19)”
Mtu ambaye kwa makusudi na kwa njia rasmi alijitenga mwenyewe na kundi angefaa maelezo hayo. Kwa kukanusha makusudi kundi la Mungu na kwa kukana njia ya Kikristo, angejifanya mwasi-imani. Mkristo mshikamanifu hangetaka kushirikiana na mwasi-imani. Hata kama walikuwa wamekuwa marafiki, mtu alipokana kundi, akawa mwasi-imani, alikataa msingi wa ukaribu pamoja na ndugu. Yohana alionyesha wazi kwamba yeye mwenyewe hangekaribisha nyumbani mwake mtu ambaye ‘hakuwa na Mungu’ na ambaye ‘hakuwa wa kwetu.’
Kulingana na Maandiko, mtu aliyekanusha kundi la Mungu allkuwa mwenye lawama zaidi ya wale walio katika ulimwengu. Kwa sababu gani? Paulo alionyesha kwamba Wakristo katika eneo la Roma walikutana kila siku na waasherati, wanyang’anyi, na waabudu-sanamu. Hata hivyo alisema kwamba Wakristo wanapaswa Ruacha ‘kuchangamana na mtu aitwaye ndugu’ aliyerudia njia zisizo za kimungu. (1 Wakorintho 5:9-11) Hali moja na hiyo Petro alisema kwamba mtu ‘aliyekwisha kuyakimbia machafu ya ulimwengu’ lakini tena arudie maisha yake ya kwanza alikuwa kama nguruwe mwenye kurudi katika matope. (2 Petro 2:20-22) Kwa hiyo, Yohana alikuwa akitoa shauri la kupatana kwa kuelekeza kwamba Wakristo hawakupaswa ‘kukaribisha nyumbani mwao’ mtu ambaye kwa makusudi ‘alitoka kwao.’—2 Yohana 10.
Yohana aliongeza hivi: “Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.” (2 Yohana 11) Hapa Yohana alitumia neno la Kigiriki la salamu khai’ro badala ya neno a.spa’zo.mai linalopatikana katika mstari 13.
Khai’ro lilimaanisha kufurahi. (Luka 10:20; Wafilipi 3:1; 4:4) Pia lilitumiwa kama salamu, ya kusemwa au kuandikwa. (Mathayo 28:9; Matendo 15:23; 23:26) Aspa’zo-mai lilimaanisha “kukumbatia kwa mikono, kwa hiyo kusalimu, kukaribisha.” (Luka 11:43; Matendo 20:1, 37; 21:7,19) Lo lote la maneno hayo lingeweza kuwa salamu, lakini huenda aspa’zo-mai likawa lilidokeza mambo mengi kuliko salamu ya “jambo” au “habari” iliyosemwa kwa uungwana tu. Yesu aliwaambia wale wanafunzi 70 wasi-a.spa’se.sthe mtu ye yote. Kwa njia hiyo akaonyesha kwamba kazi yao yenye kutaka hatua ya haraka haikuruhusu wakati wa kusalimiana kwa mtindo wa Mashariki wa mabusu, makumbatiano, na maongezi marefu. (Luka 10:4) Petro na Paulo walisihi: ‘Salimianeni [aspa’sasthe] kwa busu la upendo, au busu takatifu.’—1 Petro 5:14; 2 Wakorintho 13:12,13; 1 Wathesalonike 5:26.
Kwa hiyo huenda Yohana alitumia kwa makusudi khai’ro katika 2 Yohana 10, 11 badala ya aspa’zomai (2Jo mstari 13). Ikiwa ndivyo, basi Yohana hakuwa akisihi Wakristo waache tu kusalimu kwa uchangamfu (kwa kukumbatia, busu, na maongezi) mtu aliyefundisha uwongo au aliyekana kundi (akaasi imani). Badala yake, Yohana alikuwa akisema kwamba hawapaswi hata kusalimu mtu kama huyo kwa salamu ya khai’ro, salamu ya kawaida ya “habari.”b
Uzito wa shauri hilo unaonekana wazi katika maneno ya Yohana: “Yeye ampaye salamu—azishiriki kazi zake mbovu.” Hakuna Mkristo wa kweli ye yote angalipenda Mungu amwone kuwa mshiriki katika kazi mbovu kwa kushirikiana na mkosaji aliyefukuzwa au mtu aliyekana kundi Lake. Ni vema zaidi kama nini kuwa mshiriki katika udugu wa Kikristo wenye upendo, kama alivyoandika Yohana: “Hilo tuliloliona na kulisikia, [twaripoti kwenu]; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.”—1 Yohana 1:3.
[Maelezo ya Chini]
a Kamusi Webster’s New Collegiate Dictionary inasema “uasi-imani” ni “1: kukana imani ya kidini 2: kuondoa ushikamanifu katika mahali pa kwanza.”
b Kuhusu matumizi ya khai’ro katika 2 Yohana 11, R. C. H. Lenski anaeleza hivi: “[Neno hilo] lilikuwa salamu ya kawaida wakati wa kukutana au kuachana. . . . Hapa maana ni: Hata msimpe mwasi-imani salamu hiyo! Tayari hilo linakufanya kuwa mshiriki katika kazi mbovu ambazo amekuja ili azifanye. Yohana [anazungumza] . . . juu ya salamu ya aina yo yote.”