Tatizo Linalohusu Kukopa Pesa
“Tatizo la kukopa pesa ni kwamba mara mtu akiisha kuzipata, hawezi kuepuka kuzifikiria kuwa zake mwenyewe. Anazizoea, anazitendea kama kwamba ni jamaa yake na huenda hata akasahau au akaja kuchukia wazo la kwamba siku moja ni lazima pesa zote hizo ziondoke zikatembelee mtu mwingine. Kukopa ni rahisi. Kulipa ni matanga.” Ndivyo lilivyosema Parade, gazeti la siku ya Jumapili, kuhusu tatizo linalopata maoni ya akilini mtu anapokopa pesa.
Lakini, halihusu maoni ya akilini tu. Pia kuna lile jambo la kiadili—wajibu wa kulipa kile kilichokopwa. Basi, ingefaa tuzingatie akilini maoni ya Yehova juu ya mtu asiyelipa kile anachokopa. Neno la Mungu linasema: “Asiye haki hukopa wala halipi.”—Zaburi 37:21.