Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 3/15 uku. 30
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • “Tukio la Mfano” Ambalo Ni Muhimu Kwetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Mwanamke Aliye Huru
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • “Tukio la Mfano” Linalotuelimisha
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Agano la Mungu Pamoja na “Rafiki” Yake Tayari Lafaidi Mamilioni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 3/15 uku. 30

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Yerusalemu ulikuwaje “mtumwa pamoja na watoto wake,” kama mtume Paulo alivyoandika katika Wagalatia 4:25, (HNWW)?

Sana-sana, Yerusalemu na watu wake katika siku za Paulo ulikuwa katika utumwa kwa Torati ya Musa.

Katika Wagalatia sura ya 4 mtume alionyesha kwamba Wakristo walio katika agano jipya walikuwa wamenunuliwa na Kristo na hivyo walikuwa huru. Jambo hilo lilitofautiana na hali ya Wayahudi chini ya agano la Torati. Paulo alifananisha jambo hilo na mke wa Abrahamu (Sara) na suria wake (Hagari), akisema: “Wanawake hao wanamaanisha maagano mawili, moja la kutoka Mlima Sinai, ambalo linazaa watoto kwa ajili ya utumwa, na ambalo ni Hagari. Sasa Hagari huyo anamaanisha Sinai, mlima ulio katika Arebia [ambako Yehova aliwapa Israeli Torati kupitia Musa], naye analingana na Yerusalemu wa leo, kwa maana yeye yuko katika utumwa pamoja na watoto wake. Lakini Yerusalemu wa juu yuko huru, naye ni mama yetu.“—Wagalatia 4:24-26, NW.

Paulo aliposema kwamba “wanawake hao wanamaanisha maagano mawili,” alikuwa akisema kwa ufupi tu. Yehova hakuoa kwa njia ya mfano agano fulani lisilo na utu bali ameoa watu waliofanywa tengenezo katika agano hilo. Mapema alikuwa amewafikiria Israeli chini ya agano la Torati kuwa kama mke wake. (Linganisha Isaya 54:1, 6.) Lakini, mwanamke aliye huru (Sara) alisimamia Yerusalemu wa juu, tengenezo la Yehova la ulimwengu wote, ambalo ni kama mke kwake.

Lakini Wayahudi wangeweza kufikiriwaje kuwa katika utumwa kwa Torati, kwa kuwa Torati hiyo ilikuwa kamilifu na iliandaliwa na Mungu mwenyewe?

Ni kweli kwamba ‘Torati yenyewe ilikuwa takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.’ (Warumi 7:12) Lakini Waisraeli wasio wakamilifu waliokuwa chini ya Torati hawakuweza kuishika kwa ukamilifu, hata walipojaribu sana. (Warumi 7:14-16) Mtume Petro alielekeza kwenye uhakika huo alipouliza ulizo linalofuata mbele ya baraza linaloongoza la Kikristo: “Sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua?” (Matendo 15:10) Vivyo hivyo, katika Wagalatia 4:4, 5 Paulo alisema kwamba Kristo alikuja “kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria.” Mtu yeyote ambaye angesisitiza kwamba Wakristo wana wajibu wa ‘kushika siku, na miezi, na nyakati, na miaka,’ kama ilivyoagizwa na Torati, angewafanya wawe tena utumwani.​—Wagalatia 4:9, 10.

Bila shaka, kama ilivyoonyeshwa katika ukurasa 25 wa Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1,1985, Wayahudi wa karne ya kwanza walikuwa watumwa kwa njia kadha. Kisiasa walikuwa katika utumwa wa Waroma. Walikuwa watumwa wa dhambi. (Yohana 8:34) Tena walikuwa wamefungwa na maoni yenye makosa ya kidini. Lakini utumwa mkubwa zaidi ambao Paulo aliutaja katika Wagalatia 4:25 ni utumwa wa Wayahudi kwa agano la Torati ya Musa, Iililotolewa Sinai na kuwakilishwa na Hagari suria kijakazi wa Abrahamu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki