Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 12/15 kur. 3-4
  • Je! Wewe Unashukuru kwa Yale Aliyofanya Yesu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unashukuru kwa Yale Aliyofanya Yesu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yale Aliyokufanyia Yesu
  • Zawadi Bora Zaidi ya Mungu​—Kwa Nini Ni Yenye Thamani Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Yesu Kristo—Ujumbe Wake Unavyokuhusu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Furaha ya Milele Yawangoja Watoaji wa Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Ni Zawadi Gani Bora Kuliko Zote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 12/15 kur. 3-4

Je! Wewe Unashukuru kwa Yale Aliyofanya Yesu?

NI NJIA gani ya kuonyesha shukrani ingekuwa rahisi zaidi na ya moja kwa moja kuliko kutumia maneno, “Asante”? Lakini si watu wote wanaosema “Asante” wanathamini kikweli kitu ambacho wamepokea. Maneno hayo yangeweza kusemwa kwa sababu nyinginezo, kama vile kufanya uungwana tu wakati wa kuitikia tendo la mtu mwingine. Inafaa kufanya hivyo, lakini inakuwa ni kufuata kawaida tu.

Lakini, baada ya kupokea zawadi, hasa yenye thamani kubwa, inafaa sana kusema maneno ya shukrani za kweli, zinazotoka moyoni. Zawadi inaweza kutufurahisha; inaweza kujaza uhitaji fulani. Inapofanya hivyo, zawadi hiyo inakuwa na thamani kubwa ajabu. Lakini, ikiwa baada ya hapo zawadi hiyo inapuuzwa tu au kutumiwa vibaya, basi maneno yo yote ya kusema asante yalikuwa ya bure tu. Basi, mara nyingi uthamini wa kitu, au ukosefu wa uthamini huo, unaonyeshwa na jinsi tunavyojisikia kuhusu zawadi na jinsi tunavyoitumia.

Muumba wa wanadamu, Yehova, alitupa sisi zawadi ya mali yake iliyo na thamani kubwa zaidi, Mwanaye. Yohana 3:16, NW inasema: “Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu sana hata akamtoa Mwana wake mzaliwa wa pekee, ili kila mtu anayejizoeza imani katika yeye asipate kuharibiwa bali awe na uzima wa milele.” Zawadi hiyo itatufurahisha na kujaza mahitaji yetu tukionyesha shukrani za kweli. Hata hivyo, kwa kuwa Yehova ndiye Mpaji, kwa sababu gani umshukuru Yesu?

Yale Aliyokufanyia Yesu

‘Yesu alinifanyia nini?’huenda ukauliza.Hata kabla hujazaliwa, Yesu alikufanyia jambo fulani. Jambo gani? Yesu alikubali kuacha maisha ya kimbingu aliyokuwa nayo kabla hajawa mwanadamu ili azaliwe na bikira Mariamu akiwa mwanadamu. (Luka 1:26-33) Hilo halikuwa jambo dogo. Je! wewe ungekuwa na nia ya kuacha makao yenye amani, usalama, na afya, ambako umezungukwa na rafiki washikamanifu, ukakae mahali ambapo ugomvi, hatari, na magonjwa ni mambo ya kawaida, kisha adui zako wanakupangia kifo? ‘Aka,’ watu wengi wangejibu hivyo. Lakini ndivyo Yesu alivyofanya,—Yohana 17:5; Wafilipi 2:5-8.

Kwa sababu Baba ya Yesu alikuwa Yehova Mungu, wala si mwanadamu ye yote, Yesu hakuwa na dhambi. (Luka 1:34, 35) Yeye hakukosea hata mara moja kwa wazo, neno, au tendo. Ijapokuwa kila upande alizungukwa na hali zenye dhambi na akalazimika kukabili upinzani, aliweza kuwaambia wapinzani wake hivi: “Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi?” Hakuna hata mmoja aliyeweza! Ni kama vile mtume Petro alivyoeleza: “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.” (Yohana 8:46; 1 Petro 2:22) Kwa kutegemea mambo hayo ya hakika, acheni tuendelee kuonyesha jinsi jambo hili linavyokuhusu wewe.

Watu wengi hawapendi sana kutembelea wagonjwa hospitali, achia mbali kuishi pamoja nao. Yesu alikuwa mkamilifu katika mwili, kwa hiyo alikuwa na afya kamilifu. Hata hivyo, yeye hakukaa mbali asiwakaribie wengine wala hakutafuta kuishi katika mazingira ya watu wenye magonjwa. Bali, kwa sababu ya upendo, Yesu alikula, akalala, na kushirikiana kwa hiari pamoja na wanadamu wagonjwa na wenye kufa.​—Mathayo 15:30-37; Marko 1:40-42.

Ndipo Yesu alipoyaachilia maisha hayo makamilifu ya kibinadamu kwa moyo wa kupenda ili afaidi wanadamu. Kwa kuwa alikuwa mkamilifu, yeye alikuwa na haki ya kupata uzima wa kibinadamu usio na mwisho, naye aliutoa dhabihu ili sisi tupate nafasi bora sana. Ni kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Mwana wa mtu alikuja, si ahudumiwe, bali kuhudumia na kutoa nafsi yake ukombozi badala ya wengi.” (Mathayo 20:28, NW) Mitume wake walishuhudia kwa njia inayofanana na hiyo: “Twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu,... ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu.” (Waebrania 2:9) Kutoa kwa Yesu uhai wake wa kibinadamu kwa ajili ya wanadamu kulikuwa ndiko wonyesho mkubwa zaidi wa upendo ambao mwanadamu ye yote angeweza kufanya. Kwa uhai huo aliandaa zawadi iliyo kubwa zaidi ambayo sisi viumbe wa kibinadamu tusio wakamilifu tungeweza kupokea, yaani, nafasi ya kupata uzima wa milele.​—Yohana 3:16; 15:13.

‘Hakika Yesu amenifanyia mengi,’ huenda wewe ukakata shauri hivyo, ‘lakini naweza kuonyeshaje kwamba ninashukuru?’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki