Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 2/15 uku. 7
  • Papa na Ufunuo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Papa na Ufunuo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Ufunuo Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ufunuo—Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Je, Tisho la Nyuklia Limekwisha?
    Amkeni!—1999
  • Ni Nani Wanaosababisha Tisho la Vita vya Nyuklia?
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 2/15 uku. 7

Papa na Ufunuo

KUIEPUKA HAR-MAGEDONI ndicho kichwa ambacho maripota wawili walikipa kitabu chao cha 1984 juu ya siasa za hivi majuzi za Papa. Gordon Thomas na Max Morgan-Witts wamekuwa wakiripoti juu ya shughuli za makao ya papa kwa miaka zaidi ya 17. Tunaweza kujipatia ufahamu gani kutokana na ripoti zao kuhusu jinsi ufunuo unavyohangaikiwa na wenye vyeo vya juu katika Kanisa Katoliki?

Kulingana ripota hao, Monsinya Emery Kabongo, aliye katibu wa kibinafsi wa John Paul wa Pili, alisema: “Papa ni kama mbabe Hercules kwa njia ya kiroho anapojaribu kuyaamua yale mataifa mawili makubwa zaidi ili yasitokeze Har–Magedoni ya silaha za nyukilia.”

Inaonekana kwamba viongozi wa kanisa ndio hasa wanaohangaishwa na uharibifu wa duniani pote wenye kuletwa na matendo ya wanadamu badala ya kuhangaikia ile hatua ya Mungu ya kujitia katika mambo ya wanadamu​—ufunuo ambao Biblia inatabiri. Hivyo, kitabu Averting Armageddon (Kuepuka Har–Magedoni) kinasema: “Kati ya wale wanaohusika na Kabongo, hakuna ishara ya nje-nje kuonyesha kwamba wanajikaza sana kujaribu kuuondosha ufunuo wanaohisi utatokea. . . . Lakini shughuli hiyo inaleta mkazo ambao umetokana moja kwa moja na lile Baraza la Maaskofu wa mataifa yote. Lilikuwa limekata maneno juu ya makusudio yenye kuonyesha maelekeo ya kutokea kwa maangamizi, likasikitishwa sana na ‘uchokozi wa kutaka vita, jeuri na uharamia, kuongeza mabohari ya silaha za kawaida na hasa zile za nyukilia, na biashara yenye sifa mbaya ya silaha zote za vita.’” Hata papa anahusika. Thomas na Morgan-Witts wanaripoti kwamba katika rafu za chumba chake cha uchunguzi ameweka vitabu kama International Defense Review (Marudio ya Ulinzi wa Kimataifa), The Problems of Military Readiness (Matatizo ya Utayari wa Kijeshi), na Surprise Attack: Lessons For Defense Planning (Shambulio la Ghafula: Masomo ya Kupanga Ulinzi). Wanaongeza hivi:

“Karibu na barua za papa pana vitabu vinavyohusu habari ambayo sasa inachukua fikira nyingi za papa: eskatolojia, uchunguzi wa mafundisho ya Kibiblia yanayoshikilia ya kwamba Mungu ataanzisha Ufalme Wake duniani kupitia mfululizo wa ‘matukio’ ya kumaliza kizazi. John Paul anaamini sana . . . kwamba, kabla ya mwisho wa karne hii, huenda jambo fulani ‘la kukata maneno’ likaukumba ulimwengu. Je, lingeweza kuwa ni ugonjwa wa kipuku, kutokea tena kwa tauni inayofurisha-furisha mwili na kuua watu kama mainzi? Au ukame au njaa kubwa kwa kadiri isiyowazika? Au vita ya nyukilia? Sasa yeye anaogopa-ogopa kwamba jambo hilo la mwisho linaweza kutokea; imesemwa kuwa yeye amepata kufikiria sana kwamba huenda ikawa ametupwa katika daraka la kuwa kichwa cha Kanisa katika ule ambao ungeweza kuwa ndio mwongo wa mwisho wa ulimwengu kabla haujateketezwa kabisa na uharibifu wenye kuletwa na silaha za nyukilia.”

Kitabu Averting Armageddon kinavuta fikira pia kwenye ile “saa ya siku ya maangamizi” inayosemwa sana kwa ukawaida katika Bulletin of the Atomic Scientists. “Saa” hiyo ilipochapishwa mara ya kwanza katika Desemba 1947, mikono yayo ilisogezwa kwenye dakika saba kabla ya usiku wa manane kuonyesha “jinsi ulimwengu ulivyokuwa karibu na Har–Magedoni yenye kuletwa na silaha za nyukilia.” Baada ya mapatano ya kupunguza silaha mwaka 1972, mikono ya saa hiyo ilirudishwa nyuma kwenye dakika 12 kabla ya usiku wa manane. Mwaka 1984 Thomas na Morgan-Witts waliandika hivi: “Sasa ile saa inaonyesha dakika tatu tu kabla ya usiku wa manane. Katika muda wa miaka thelathini, sasa ndipo imeikaribia zaidi siku ya maangamizi.”

Papa ajapofanya jitihada zo zote ‘kuepuka Har–Magedoni yenye kuletwa na silaha za nyukilia,’ katika Novemba 1985, mikono ingali ilionyesha kwamba dakika 3 tu ndizo zimebaki. Ingawa hivyo, fikira zetu zisiondoshwe kando kwa kuhangaika juu ya kama mataifa yataangamiza wanadamu. Badala ya kujaribu kuuepuka ufunuo wa maangamizi, tutakuwa wenye hekima tukiitafuta njia ya Mungu ya kuokoka ufunuo huo, kwa maana ni hakika kwamba huo ‘utakuja juu ya dunia nzima inayokaliwa na watu.’​—Ufunuo 3:10, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki