Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 5/1 kur. 22-24
  • Wenye Kazi za Ustadi Waliopata Kazi ya Maisha Yote ya Kweli Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wenye Kazi za Ustadi Waliopata Kazi ya Maisha Yote ya Kweli Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ustadi wa Kazi na Kujitoa kwa Kazi
  • Kazi Yake Ilikuwa Maisha Yake
  • Alitaka Kutajirika Upesi
  • Biashara Yake Ilimchukulia Wakati Wake Wote
  • Kazi Yake Ilimsaidia Kumpata Mungu
  • Walipata Kitu Kilicho Bora
  • Biblia Inabadili Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Waweza Kuacha—Sisi Tuliacha!”
    Amkeni!—1998
  • Biblia Inabadili Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Unakadiriaje Mafanikio?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 5/1 kur. 22-24

Wenye Kazi za Ustadi Waliopata Kazi ya Maisha Yote ya Kweli Kweli

HEWA ya usiku ilikuwa baridi na maji yalikuwa baridi kama barafu. Vijana 200 wa kiume na kike, wakiwa wamevaa kanzu ndefu na kushika mishumaa juu sana ya vichwa vyao, walitembea ndani ya maji yaliyowafikia kifuani. Je! hiyo ilikuwa desturi ya dini ya kifumbo yenye kuwaingiza jandoni? Au, labda ulikuwa mchezo wa kitoto tu?

Vijana hao wenye kuhitimu masomo ya juu na chuo kikuu walikuwa wakijiunga na maelfu ya wengine wa umri wao katika ile inayoweza kuonwa kuwa desturi ya kuingia kazi ya kistadi ya maisha kwenye shirika kubwa katika Japani. Ubatizo huo wa umati ndani ya maji yaliyokuwa baridi kama barafu ulikusudiwa kung’oa ndani ya hao waliotazamiwa kuwa wafanya kazi maelekeo yo yote ya kujitegemea ambayo labda walijipatia shuleni na hivyo waimarishe kifungo na ushikamifu wao kwa shirika.

Ustadi wa Kazi na Kujitoa kwa Kazi

“Katika Japani kazi ndiyo watu. Watu ndiyo kazi,” anaandika Frank Gibney katika kitabu chake Japan: The Fragile Superpower. Maana ya maneno hayo ni kwamba mtu akisha kuingia shirika fulani, maisha yake yote yanalitegemea. “Ikiwa anafanya kazi kwa kampuni ya Mitsubishi, yeye ni mtu wa Mitsubishi. Walio wengi kati ya rafiki zake ni watu wa Mitsubishi. Yeye anakunywa pamoja nao, anacheza mipira ya vijiti pamoja nao, na kushiriki nao taabu zake. Na hakika anashindana nao, lakini hakuna anayefikiria kuwaacha wenzake kama vile wasivyoachana watu wa jamaa moja wenye kushindana waliotokana na mzazi mmoja. Isipokuwa watu wa ukoo wake, na labda rafiki kadha wa shule yao, walio wengi kati ya washirika wake—na mara nyingi wale wa jamaa yao—wanaendelea kuwa kiunzi cha shirika hilo.”

Kwa sababu ya kujitoa na kujidhabihu kwa njia hiyo, wafanya kazi wanahakikishiwa usalama kwa kuandikwa kazi ya maisha yote. Hii inatia ndani mazoezi yasiyokoma, marekebisho ya kikazi, kuhamishwa- hamishwa, bila shaka hata kupandishwa cheo.

Vijana walio wengi katika Japani wanaikubali upesi njia hiyo ya kupata mafanikio na kuwa sehemu ya mfumo huo. Wengine, ingawa hawatafuti vyeo katika mashirika, wanang’ang’ana sana kusonga mbele katika shughuli za kikazi. Lakini je! mfumo wa namna’ hiyo unaleta furaha na uradhi? Je! kazi ya kuajiriwa maisha yote inamaanisha furaha? Wengi zaidi na zaidi wanakuta kwamba kuna jambo lililo bora na lenye kuthawabisha zaidi ya kutafuta vyeo katika mashirika au kung’ang’ania kuwa na utajiri na sifa za binafsi.

Kazi Yake Ilikuwa Maisha Yake

Junichi alihitimu Chuo Kikuu cha Keio cha Somo la Biashara mwaka 1961. Kwa kufuata hatua za wanachuo wengine wo wote waliomtangulia, yeye alijiunga na shirika lililo kubwa zaidi la magari katika Japani, lililokuwa na wafanya kazi 4,700 wakati huo. Kupanda kwake cheo katika shirika kulitokea polepole. Hatimaye, akawa mkuu katika idara yake. Ingawa kazi yake, ambayo mara nyingi ilikuwa ikianza asabuhi mpaka usiku wa manane, ni kama haikumpa wakati wo wote wa kuwa pamoja na mkeye na watoto 5, yeye aliona ilikuwa lazima ajidhabihu hivyo, ili awe na wakati ujao salama.

Lakini jambo fulani lilitukia Oktoba mwaka 1974. Junichi alikuta kwamba mkeye na watoto wake walikuwa wakijifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova wakawa wakihudhuria mikutano ya Kikristo. Alijaribu yote aliyoweza kuwakomesha, hata akawa akiwahama, lakini ilikuwa kazi bure tu.

Siku moja aliporudi nyumbani kutoka kazini, jamaa yake ilikuwa imeenda mikutanoni. “Nikakuta meza imetandikwa tayari kwa chakula cha jioni, na hapo nilikuwa nimeachiwa barua,” akasema Junichi. “Katika barua, jamaa yangu iliniambia kwamba wasingeweza kuuacha ukweli kamwe, kwamba ulikuwa kwa faida yangu, pia, na kwamba siku moja ningefahamu.” Jambo hilo lilikaa sana akilini mwa Junichi. “Mimi nikawaza kwamba labda huu ulikuwa ndio ukweli, na nikaacha kuwapinga.”

“Kadiri wakati ulivyoendelea kupita, Mashahidi walikuwa wakija na kunitembelea wakinitia moyo nijifunze Biblia. Hapo ndipo nilipoanza kuona kazi yangu ya maisha ikiniingilia. Mimi nilikuwa mwenye shughuli sana kazini hivi kwamba nilijisikia nisingeweza kamwe kuweka wakati wa kujifunza Biblia na kuhudhuria mikutano. Halafu nikajua kwamba nikijifunza, ningelazimika kuyaacha yale mazoea ya udanganyifu na vitumbuizo vilivyokuwa vikifanyika mara kwa mara usiku sana kuhusiana na kazi. Kwa kuwa kuiacha kungeleta hasara kwenye kazi hiyo, nilisita-sita kujifunza.”

Lakini kwa kutiwa moyo na Mashahidi, Junichi alianza kujifunza na baada ya muda mfupi akafanya maendeleo kufikia hatua ya kuweka maisha yake wakfu kwa Mungu na kubatizwa. Ingawa angali na kazi yake ya wakati wote, Junichi ameipata ile anayoihesabu kwa uhalisi kuwa ndiyo kazi ya maisha yote. Tangu Machi wa mwaka wa 1978, amekuwa akitumikia akiwa painia msaidizi, akitumia saa 60 kwa mwezi katika kazi ya kuhubiri.

Je! Junichi amefaidika kutokana na njia yake ya maisha? “Ndiyo, nimefaidika. Nakuta kwamba ninafanya kazi yenye mazao zaidi wakati wa mchana ili nyakati za jioni ziwe huru kwa kufuatia faida za Ufalme pamoja na jamaa yangu. Nimepata nafasi nyingi za kuwapa ushuhuda wa wafanya kazi wenzangu na kujifunza Biblia pamoja na wanaume wengine ambao wamekuwa na kazi za kimwili zenye kuwashughulisha kama mimi hapo kwanza. Wawili wamebatizwa, nami najifunza na watatu wengine. Namshukuru Yehova kwa subira alinionyesha mimi.”

Alitaka Kutajirika Upesi

Akiwa mmoja wa watoto 6 katika jamaa, Takafu aliyaponya mashambulizi yaliyofanya kutoka angani juu ya mji wa Nagoya wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili akiwa na shati alilovaa mgongoni na falsafa ya kutaka kutajirika upesi. Kwa kuhimizwa na mjomba wake, aliingia shule ya kuzoeza kufanya kazi ya uendeshaji wa baiskeli akiwa na umri wa miaka 15. Kufikia wakati alipokuwa na umri wa miaka 22, alikuwa amefaulu kuwa mwendeshaji hodari sana wa baiskeli, akawa akionekana-onekana katika mashindano nchini pote. Alikumbuka kwamba alimwona mama yake akiweka zawadi za ushindi wake mbele ya madhabahu ya jamaa ziwe kama sadaka za kuonyesha shukrani. Ilionekana kama kwamba Takafu alikuwa ametimiza mradi wake maishani na kwamba alikuwa akisonga mbele katika mambo yote.

Ndipo mmisionari wa Mashahidi wa Yehova alipozuru nyumba yake na kumtolea Takafu mambo ya kufikiria. Maneno kama haya yaliyonenwa na Yesu yalikwama katika akili na moyo wake: “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? ” (Mathayo 16:26) Baada ya muda fulani, Takafu akafanya maendeleo katika kupata maarifa ya Biblia na kutambua kwamba ingempasa kufanya mabadiliko fulani.

“Nikiwa mtu aliyesomea undeshaji wa baiskeli, nilijua kwamba kwendesha baiskeli na kuchezakamari ni mambo yanayoambatana pamoja,” akasema Takafu. “Lakini bado uamuzi wenyewe haukuwa rahisi. Nilikuwa nimetumia miaka saba ya maisha yangu kwenye mchezo huo, na ilielekea kuwa kwamba mapato yangu yalihitajiwa sana kwa masilahi ya jamaa yetu. Lakini nimejifunza kutokana na Biblia kwamba Musa na Paulo walikuwa wamekabiliwa na maamuzi yanayofanana na huo nao wakachagua mwendo ulio bora. Ndivyo mimi nilivyofanya.” Takafu alianza mbio ya namna mpya—mbio ya uzima—naye ameendelea kuipiga mpaka leo hii, akatumika miaka kadha akiwa mwangalizi mwenye kusafiri.

Biashara Yake Ilimchukulia Wakati Wake Wote

Satoshi alikuwa katika biashara ya mavazi ya wanawake. Alikuwa na usalama wa kifedha kwa sababu ya kuwa na maduka manne yeye kusitawi ya mitindo ya mavazi. Lakini shughuli za mwanamume huyo katika ulimwengu wa kibiashara zilimwongoza akate shauri kwamba uchafuzi, upungufu wa vyakula, na vita ulimwenguni pote vingekomesha kuwako kwa wanadamu baada ya muda mfupi. Hivyo, wakati shahidi alipomfikia akiwa na karatasi yenye kutoa uhakikisho wa kwamba Mungu hangeruhusu jambo hilo lifanyike, kupendeza kwa Satoshi kuliamshwa.

Lakini biashara yake ilimzuia. “Kwa sababu ya kuwako mashidano makali ya kibiashara, kupunguza mwendo kungemaanisha mtu angepoteza biashara yake,” akasema Satoshi. “Ni shauri la ‘kula au uliwe.’. Usemi ulio katika biashara hiyo ni kwamba ikiwa hujishughulishi kweli kweli huna budi kufilisika.” Kwa hiyo ilichukua miaka miwili, kuongeza na jitihada kubwa sana, kabla Satoshi hajaamua mwishowe kuwa na funzo la Biblia.

Alipokwisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, aliuza mawili ya maduka yake naye ana ‘wakubwa wa maduka’ wa kuangalia yale mengine mawili. Ingawa Satoshi sasa anafanya kazi siku mbili au tatu tu hivi kwa mwezi akiwa mhasibu na mtu wa kufikiwa kwa mashauri, yeye anasema: “Ningali na mapato ya kutosha. Ninataka kutanguliza utumishi wangu wa Yehova Mungu.” Sasa anafuatia kazi yake ya maisha iliyo ya kweli katika huduma ya wakati wote, akitumika kama painia. Yeye na jamaa yake wanafanya maendeleo mazuri ya kiroho.

Kazi Yake Ilimsaidia Kumpata Mungu

Hiroshi alikuwa akifanya kazi katika duka la mabati la jamaa yake. Lakini jambo hasa lililompendeza lilikuwa upigaji picha wa viumbe. Alipata ustadi mwingi sana katika kazi hiyo hivi kwamba baadhi ya picha zake za wadudu zikachapishwa. Kufikia wakati alipokuwa na umri wa miaka 29, alikuwa amekwisha ingia katika kazi ya kistadi ya kupiga picha viumbe.

“Kutokana na uchunguzi wangu wa wadudu,” Hiroshi anakumbuka, “niliwaza kwamba kama kuna Mungu, bila shaka yeye anapenda ucheshi. Jambo hilo liliniongoza kutilia shaka ile nadharia ya mageuzi, nami nikaanza kidogo kupendezwa na Biblia.”

Siku moja ya majira ya baridi, Mashahidi wawili walimtembelea Hiroshi. “Nilipokubali kutoka kwao magazeti mawili yaliyokuwa na makala juu ya wanyama, walijitolea kujifunza Biblia pamoja nami nyumbani kwangu,” akasema Hiroshi. “Niliwaza kwamba kwa kuwa haikuwa lazima niende kanisani ili nijifunze, haikuwa lazima niwe mshiriki. Kwa hiyo nikakubali.” Ingawa alishangaa alipojua yanayosemwa na Biblia juu ya Muumba, aliyakubali upesi. Kupenda kwake kwa viumbe kukawa kwa pili kwa kumpenda Mungu.

Sasa Hiroshi anaruzuku jamaa yake akiwa mpiga picha wa kujiandika. Lakini kazi yake ya kweli ni kuwa mhudumu wa wakati wote.

Walipata Kitu Kilicho Bora

Orodha ni ndefu ya watu waliokuwa wakifanya kazi za ustadi katika Japani ambao wamebadili maisha zao—na, nyakati nyingine, kazi zao—walipopata kumjua Yehova na kusudi lake. Baadhi yao ni kutia na matabibu, madaktari wa meno, wachoraji ramani za mijengo, wenye kutayarisha progamu za kompyuta na wabuni wa mifumo hiyo, walimu, wenye kutunza afya za mifugo, wapamba nywele, wakuu wa mashirika, na kadhalika.

Wakati mmoja, wastadi hao wote wa kikazi walikuwa wemejitoa kabisa wafanye kazi yao. Walipojua kwamba mfumo huo wa mambo unakaribia mwisho, walifanya uamuzi kuhusu kazi zao. Waliziweka kazi zao mahali panapozipasa wakaanza kuwa, kufuatia kitu kilicho bora—Ufalme wa Mungu na baraka zao zilizoahidiwa. (Mathayo 6:33) Kwa kuachilia mbali ile waliokuwa wamewaza ingekuwa ndiyo kazi yao ya maisha yote, wamekuwa wastadi katika shughuli mpya. Wao wameanza kazi ya maisha yote wakiwa watumishi mapainia wa yule Aliye Juu Zaidi, Yehova Mungu.

[Picha katika ukurasa wa 23]

Bingwa wa Kuendesha Baiskeli Takafu Yamaguchi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki