Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 6/15 kur. 3-4
  • Ni Nini Kilicho cha Thamani Kweli Kweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Kilicho cha Thamani Kweli Kweli?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Kilicho cha Thamani ya Kweli?
  • Unaweza Kudumishaje Maoni Yaliyosawazika Kuhusu Pesa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Pesa
    Amkeni!—2015
  • Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kuna Ubaya Gani Kuchuma Pesa?
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 6/15 kur. 3-4

Ni Nini Kilicho cha Thamani Kweli Kweli?

“Wengi wao wanaishi maisha matupu, wanashindwa kudumu na kazi yao, uhusiano wao na watu hauendelei kuwapo na wanahama-hama kutoka mahali pamoja kwenda mahali pengine bila kutegemeana na watu wengine​—na hakuna mtu anayejali. Sababu: Wao ni matajiri wa kupindukia.”​—The New York Times, Mei 15, 1984.

WEWE unajua sana kwamba pesa zinahitajiwa kwa chakula, mavazi, makao, usafiri, matibabu, na mambo mengine yaliyo ya lazima maishani. Kwa kweli, labda wewe unatambua kwamba katika jamii ya kisasa ingekuwa vigumu kuishi bila pesa, kwa maana, kama Biblia inavyosema,“fedha huleta jawabu ya mambo yote.”​—Mhubiri 10:19.

Hata hivyo, makala ya gazeti yenye maneno yaliyo juu iliyazungumza matatizo ambayo matajiri wanakuwa nayo moyoni. Kwa wazi, ingekuwa hatari ukitegemeza maisha yako juu ya kujipatia pesa na mali. Hata hivyo, watu wengi wanafanya hivyo. Nyakati nyingine, kujitakia makuu kwa pupa kunaua. Tunasikia habari za watu wenye kujisukuma mbele sana wa miaka 30 na kitu na wa miaka 40 na kitu wanaouawa na ugonjwa wa moyo. Wengine wao walihatirisha afya yao hata maisha zao ili watimize tamaa zao za kutaka makuu kuhusiana na pesa. Si lazima tuwe tunafuata sana dini ndipo tuweze kukubali kwamba ingalikuwa afadhali kama wao wangaliyathamini moyoni maneno ya Yesu Kristo: “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?”​—Mathayo 16:26.

Ni Nini Kilicho cha Thamani ya Kweli?

Hakika wewe unajua kwamba hakuna mwisho wa mambo ambayo tunaweza kushawishwa tutafute. Mashine ya ukanda wa video, nyumba yako mwenyewe, vifaa vya michezo vyenye gharama kubwa​—katika nchi nyingine hivyo ni vitu ambavyo watu wanajitahidi wavipate. Kwingineko mradi unaothaminika huenda ukawa ni wa kitu kidogo zaidi. Mwanamke kijana katika nchi moja alijitia katika umalaya ili apate pesa za mavazi mazuri zaidi.

Ingawa huenda tukatambua kwamba kuna hatari zinazohusiana na kuwa na maoni ya kufuatia vitu vya kimwili tu maishani, sisi tunaweza kujilindaje? Je! ni lazima tuipe jamii ya watu kisogo, tuwe watu wa kujitenga au wakaa-pekee-yao, kama vile wengine wamefanya? Pia, tunapofikiria ni kitu gani kilicho cha thamani kweli kweli, inatupasa tuulize, Ni jambo gani litakaloniletea mimi furaha na uradhi wa kweli wenye kudumu?

Kupata msaada mmoja katika jambo hili, acheni tufikirie mfano wa mwanamume mmoja ambaye kwa karne nyingi watu wamemheshimu na kuvutiwa na kielelezo chake. Yeye alikuwa mwalimu wa sheria na sehemu ya madhehebu ya Kiyahudi ya karne ya kwanza iliyojulikana kuwa yenye watu “wapenda fedha.” (Luka 16:14) Jina lake lilikuwa Paulo, na alikuwa na elimu na nguvu za ndani zilizohitajiwa kumwezesha ajikusanyie utajiri mwingi na kupata cheo kikubwa hata zaidi katika jumuiya.

Lakini, kwa kupatwa na tukio la kugutusha, yeye akatambua kwamba jambo fulani lililo tofauti sana ndilo lililokuwa lenye thamani kubwa zaidi maishani. Iwe au isiwe kwamba kwa sasa wewe una akili inayofanana na yake, ingekufaa ufikirie shauri lililokatwa na Paulo.

Yeye aliamua kwamba jambo la kwanza lililo lenye thamani maishani lilikuwa msimamo unaokubaliwa na Mungu akiwa mwanafunzi wa Yesu Kristo. Hilo lilikuwa jambo la thamani kubwa sana hivi kwamba Paulo, akiwa mtume wa Yesu, aliweza kuvumilia magumu na mateso. Yeye alikuwa kama mwanamume wa kabla yake aliyekuwa mashuhuri, Musa, ambaye ‘alihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri.’​—Waebrania 11:26; 2 Wakorintho 11:23-27.

Wewe pia inakupasa ujue kwamba Paulo hakusikitika kamwe kwamba kuwa mtume wa Kikristo kulikuwa kumempotezea umashuhuri katika jamii ya Kiyahudi. Baada ya kuwa amefurahia karibu miaka 25 akiwa Mkristo aliyejitoa, yeye aliandika: “Mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo.” (Wafilipi 3:7-9) Itakupasa ukubali kwamba Paulo alisadiki kwamba yeye alikuwa amepata kitu chenye thamani kweli kweli.

Wala uchaguzi wa Paulo haukumaanisha kwamba hakuwa tena na vitu vyo vyote vya kimwili. Kwa mfano, yafikirie maneno yake haya: “Katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.”​—Wafilipi 4:12.

Hata hali yako wewe iwe nini kuhusiana na Ukristo, inaelekea kwamba wewe unaweza kuona jinsi matokeo yaliyomjia Paulo yalivyokuwa yenye kuvutia. Uchaguzi wake juu, ya kilichokuwa cha thamani kubwa ulimletea uradhi usiopatikana na wanaume na wanawake wa ulimwengu walio matajiri zaidi. Jean Paul Getty, yule mmilionea mwenye mafuta ya kuuza, alikiri hivi: “Pesa sizo kwa lazima zinazoleta furaha. Labda zinaleta ukosefu wa furaha.”

Hata hivyo, mtu anaweza kuwa akidai kwamba yeye ni Mkristo na bado ashindwe kutambua ni nini kilicho chenye thamani kubwa zaidi. Ndivyo ilivyokuwa katika karne ya kwanza, kwa maana Paulo alisema hivi juu ya mshiriki mmoja: “Demasi ameniacha mimi kwa sababu aliupenda mfumo wa mambo ya sasa.” (2 Timotheo 4:10, NW) Katika wakati ambapo yeye angaliweza kumsaidia mtume huyo aliyefungwa gerezani, Demasi alichoka, akapendelea vitu ambavyo mfumo wa sasa ulimtolea.

Akionyesha hatari kubwa ambamo maoni ya kufuatia vitu vya kimwili ingeweza kuingiza Mkristo, Paulo alisema: “Hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo . . . [wamejichoma] kwa maumivu mengi.”​—1 Timotheo 6:9, 10.

Basi, wewe unaweza kuuliza, Pesa au mali zinapasa kuwa na sehemu gani katika maisha yangu? Acheni tuendelee kulichunguza jambo hilo, tuone ni jinsi gani wewe unaweza kuwa na vitu vilivyo na thamani kweli kweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki