Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 6/15 uku. 13
  • Vile Vitabu vya Injili—Uhakika au Hadithi Tu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vile Vitabu vya Injili—Uhakika au Hadithi Tu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Gospeli—Je, Ni za Kweli au Ni Hekaya Tu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kwa Nini Tumwamini Yesu Kristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Yule Yesu Halisi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Injili za Apokrifa—Je, Zina Ukweli Uliofichwa Kumhusu Yesu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 6/15 uku. 13

Vile Vitabu vya Injili​—Uhakika au Hadithi Tu?

WALE wanaoitwa wachambuzi wa hali ya juu zaidi wameshambulia kwa muda mrefu masimulizi ya Injili ya maisha ya Yesu katika pande nyingi: Wao wanadai kwamba masimulizi hayo yamejawa na habari zenye kupingana na yaliandikwa muda mrefu mno baada ya matukio yenyewe kutendeka, yasiweze kuwa historia inayofaa. Wanaipuuza ile miujiza kwa kusema ni mambo ya kutungwa tu.

Katika kitabu chake Caesar and Christ, mwanahistoria Will Durant alijaribu kuyachunguza masimulizi ya Injili kwa maoni yenye kusudi zuri kabisa​—akiyachukua kuwa ni hati za kihistoria. Ingawa aliikiri kwamba kuna habari zinazoonekana kama kwamba zinapingana, na matatizo katika masimulizi ya Injili, yeye alikata shauri hili: “Habari zenye kupingana zinahusu vijambo vidogo sana, si mambo ya maana; katika mambo yale makubwa vitabu vya Injili vilivyoandikwa kwa muhtasari vinakubaliana sana kwa njia ya kustaajabisha, na kueleza habari za Kristo kwa njia yenye upatani.”

Lakini namna gani madai yanayofanywa na wachambuzi wa hali ya juu kwamba vitabu vya Injili havifikii viwango vya kuweza kuwa historia ya kweli? Durant aliendelea kusema: “Kwa sababu ya shauku ya kuvumbua mambo, Uchambuzi wa Hali ya Juu Zaidi umechunguza-chunguza Agano Jipya vikali sana kuona kama linafaa hivi kwamba, kulingana na njia zao za kuchunguza, mamia ya watu mashuhuri wa kale​—k.m., Hammurabi, David, Socrates​—wangeonekana kuwa watu wa hadithi za mapokeo tu. Ijapokuwa kumekuwa na maoni mabaya yasiyo na msingi na mawazo yaliyotangulia kudhaniwa vibaya na wanadini juu ya waandikaji wa Injili, wao wameandika visa ambavyo wangalificha kama walikuwa watungaji wa hadithi isiyo ya kweli​—jinsi mitume walivyoshindania vyeo vya juu katika Ufalme,walivyokimbia baada ya Yesu kukamatwa, jinsi Petro alivyomkana . . . Hakuna mtu mwenye kusoma tamasha hizo anayeweza kutia shaka kwamba mwenye kutajwa katika tamasha hizo alikuwa mtu wa kweli.”

Mwanahistoria Durant alimalizia hivi: “Kama ingekuwa kwamba watu wachache wa kikawaida tu ndio waliotunga katika kizazi kimoja habari zenye uthabiti mwingi hivyo na za kuvutia kuhusu mtu mmoja, wakatunga kielelezo bora hivyo cha maadili na tazamio zuri sana la kuweza kuwa na udugu wa kibinadamu, huo ungekuwa muujiza wa kushangaza sana kuliko wo wote ulioandikwa katika vile vitabu vya Injili. Baada ya Uchunguzi wa Hali ya Juu Zaidi kuwapo kwa muda wa karne mbili, maelezo yanayohusu maisha, tabia, na mafundisho ya Kristo, yanabaki yakiwa yenye kufahamika wazi vya kutosha, na ndiyo sehemu yenye kusisimua zaidi katika historia ya watu wa Magharibi.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki