Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 8/1 uku. 21
  • Ukweli wa Biblia Unaleta Umoja na Furaha ya Kijamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ukweli wa Biblia Unaleta Umoja na Furaha ya Kijamaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Maisha ya Jamaa—Namna Unavyoweza Kufanikiwa
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 8/1 uku. 21

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Ukweli wa Biblia Unaleta Umoja na Furaha ya Kijamaa

MWANAMUME mmoja na mkeye katika India waliokuwa washiriki wa kanisa moja la Jumuiya ya Wakristo walikuwa wakigombana mara nyingi. Mara nyingi yule mume alimpiga mke wake. Hata walijaribu kuuana! Katika pindi moja mke alichemsha samli akamletea mumeye kama kwamba anampelekea chai, kumbe akammwagia mumeye samli hiyo usoni. Mwishowe, mke aliamua kujiua.

Je! jambo lo lote lingeweza kuletea mume na mke huyo umoja na furaha? Wengi wangesema hapana. Lakini kabla ya kujiua, mke alienda kutembelea bintiye na mume wa binti huyo. Wao walikuwa wakijifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Yeye aliamua kusikiliza, na moyo wake ukavutwa sana na mambo aliyosikia. Baada ya funzo lile, aliwaambia Mashahidi juu ya matatizo yake. Wao wakamwonyesha kutokana na Biblia madaraka yake hasa akiwa mke. Mume wake alifikiwa pia kisha akaanza kufunzwa Biblia. Matokeo yakawa nini? Mume na mke huyo walipotumia kanuni za Biblia wote wawili, waliyashinda matatizo yao ya kijamaa. Sasa hao wawili wamefanya maendeleo kufikia hatua ya kuweka wakfu maisha zao kwa Yehova, na wamebatizwa.

Waume wengine wengi wasiohesabika pamoja na wake zao wamekuta kwamba Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho yake ndilo lenye utatuzi wa matatizo ya kijamaa. Kwa kutumia mashauri yalo, kama yale yanayopatikana kwenye Wakolosai 3:12-14 na Waefeso sura ya 5, wanayashinda matatizo hayo na kupata umoja na furaha.

◻ Mfano mwingine wa jinsi ukweli wa Biblia unavyoweza kuunganisha jamaa unatoka katika Lebanoni. Mwaka 1973 mmoja wa Mashahidi wa Yehova alianzisha funzo la Biblia pamoja na jamaa moja katika kijiji kidogo. Wasichana wawili, waliokuwa mtu na dada yake, wa kutoka ujirani huo walihudhuria pia funzo hilo. Lakini wakati padri wa pale alipolipinga funzo hilo, jamaa ile iliacha kujifunza. Wasichana wale wawili waliendelea kujifunza kwa barua, wakitumia anwani ya shemeji wao wa kike. Baada ya wao kujifunza barua walizoandikiwa na Shahidi yule, walimpa shemeji wao azisome, ingawa kufikia hapo mume wake alikuwa akipinga. Walipokuwa na maulizo, walimwuliza Shahidi kwa barua.

Lakini, ndugu yao aliendeleza upinzani wake. Alirarua vichapo vya Biblia vya dada zake na mkeye na hata akazichoma Biblia zao Ijapokuwa jamaa yao, padri, na wengine kijijini waliwakemea vikali, wasichana hao, waliendelea kujifunza.Baada ya muda fulani, walibatizwa. Watu wengine wa ukoo walianza pia kujifunza Biblia na kubatizwa. Yule ndugu mpinzani wa wasichana hao alijifunza ukweli pia akabatizwa. Yeye sasa anatumikia akiwa mtumishi wa huduma katika kundi, na ni painia-msaidizi wa kawaida. Kufikia mwishoni mwa mwaka 1985, washiriki 23 wa jamaa hiyo walikuwa wamejifunza ukweli na kubatizwa!

Jinsi walivyo wenye furaha dada wawili hao kwa kushikamana na ukweli kujapokuwa na upinzani! Ni furaha kama nini kwao kuona umoja na furaha katika jamaa yao kwa sababu ya wao kuukubali ukweli wa Biblia! Hiyo inayathibitisha maneno ya mtunga zaburi alipotangaza hivi: “Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova! ”—Zaburi 144:15, NW.

◻ Bado jambo jingine lililoonwa linatoka katika Mji wa New York, U. S. A. Mtu huyu alianza kutumia dawa za kulevya akiwa na umri wa miaka 13 na akawa mzoelevu sana hata akawa hawezi kula mpaka kwanza avute kasumba! Zoea lake la kutumia kokeni lilimgharimu dola 100 kila siku, na alipokuwa akienda kuuza dawa za kulevya sikuzote alikuwa na bunduki za kwenda nazo. Alioa akazaa watoto wanne. Mke wake alipokuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, yeye alimpinga. Lakini mwishowe alichoshwa na mtindo wake wa maisha ya kulevywa na dawa na kuwa mtembezi, akifanya uzinzi.

Kwa kuendelea kutiwa moyo na mkeye na kusaidiwa na wazee kwa upendo, alikubali kujifunza Biblia mwaka mmoja baada ya ubatizo wa mkeye. Kufanya hivyo kulimsaidia akabiliane na matatizo makubwa yaliyohisiwa na mwili wakati wa kuziacha dawa zile, kutia na kuona vitu visivyo vya kweli. Alifanya maendeleo kufikia ubatizo na sasa ana furaha ya kuona jamaa yake ikiwa imeungana kwa furaha na watoto wake wanne wakifanya maendeleo katika ukweli. Kwa kuwa yeye ana kazi yenye uthabiti na mapato mazuri, yeye na mkeye wanatazamia kushiriki utumishi wa painia msaidizi.

[Blabu katika ukurasa wa 21]

“Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova! ”—Zaburi 144:15, NW

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki